Mojawapo ya Jukumu la Jeshi la Magereza ni kuwapeleka mahakamani mahabusu na kuwarudisha magerezani.

Gadi ya askari Wanawake na Wanaume wa Jeshi la Magereza katika Maadhimisho ya Sherehe za Kitaifa.

Ng'ombe bora wa Nyama na Maziwa ni sehemu ya miradi ya Uzalishaji inayoendeshwa na kusimamiwa na Jeshi la Magereza nchini.

Sehemu ya Mashamba makubwa yanayoendeshwa na Jeshi la Magereza: Shughuli za Kilimo cha Mashamba makubwa, madogo na bustani za mboga mboga ni moja ya shughuli za Magereza katika kuwafunza wafungwa namna ya kujitegemea mara wamalizapo vifungo vyao.

Baadhi wa wafungwa katika Kiwanda cha Ushonaji nguo cha Gereza Kuu Ukonga wakiwa kazini: Shughuli za Ushonaji wa nguo ni moja ya eneo ambalo wafungwa hupata huduma za urekebishwaji kwa vitendo.

Friday, March 17, 2017

WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI AFUNGUA MKUTANO WA MAAFISA WAANDAMIZI WA JESHI LA MAGEREZA, JIJINI DAR

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe. Mwigulu Nchemba (Mb) akiwasili leo Machi 17, 2017 katika Bwalo Kuu la Maafisa Magereza Ukonga jijini Dar es Salaam tayari kwa ufunguzi  wa Mkutano wa Maafisa Waandamizi wa Jeshi la Magereza(wa kwanza kushoto) ni Kamishna Jenerali wa Magereza, Dkt. Juma Malewa.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe. Mwigulu Nchemba akisaini katika kitabu cha wageni kama inavyoonekana katika picha.
Kamishna Jenerali wa Magereza, Dkt. Juma Malewa(wa pili kushoto) akiwa meza kuu na  Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe. Mwigulu Nchemba(wa pili kulia) kabla ya ufunguzi wa Mkutano huo. Wa kwanza kushoto ni Kamishna wa Fedha na Utawala wa Magereza, Gaston Sanga (wa kwanza kulia) ni Naibu Kamishna wa Magereza, Edith Mallya.
Kamishna Jenerali wa Magereza, Dkt. Juma Malewa akitoa maelezo mafupi kabla ya kumkaribisha mgeni rasmi Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe. Mwigulu Nchemba kufungua rasmi Mkutano huo.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe. Mwigulu Nchemba akiwasilisha hotuba yake kwenye Mkutano wa Maafisa Waandamizi wa Jeshi la Magereza.
Baadhi ya Maafisa Waandamizi wa Jeshi la Magereza wakifuatilia kwa makini hotuba fupi ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe. Mwigulu Nchemba (hayupo pichani).
Kamishna Mkuu Mstaafu wa Magereza Simon Mwanguku akiwasilisha mada katika Mkutano wa Maafisa Waandamizi wa Jeshi la Magereza. Mkutano huo umefanyika leo Machi 17, 2017 katika Bwalo Kuu la Maafisa Magereza Ukonga jijini Dar es Salaam.
Kikundi cha Brass Band ya Jeshi la Magereza kikitumbuiza kwenye ufunguzi wa huo.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya nchi, Mhe. Mwigulu Nchemba(wa pili toka kulia) akiwa katika picha ya pamoja na Wakuu wa Jeshi la Magereza Wastaafu(waliosimama mstari wa nyuma).Wa pili kushoto ni Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza, Dkt. Juma Malewa, wa kwanza kushoto ni Kamishna wa Fedha na Utawala wa Magereza, Gaston Sanga na wa kwanza kulia ni Naibu Kamishna wa Magereza, Edith Mallya mara baada ya ufunguzi wa Mkutano wa Maafisa Waandamizi wa Jeshi la Magereza 

(Picha zote na ASP  Deodatus Kazinja).

Wednesday, March 15, 2017

KAMISHNA JENERALI WA MAGEREZA DKT. JUMA MALEWA AONGOZA KIKAO KAZI CHA SHIRIKA LA MAGEREZA, JIJINI DAR

Kamishna Jenerali wa Magereza, Dkt. Juma Malewa akiongoza Kikao kazi cha Shirika la Uzalishaji mali la Magereza ambapo katika Kikao hicho cha siku mbili Wakuu wa miradi watapata fursa ya kuelezea maendeleo ya miradi mbalimbali ya shirika hilo. Kikao hicho kimeanza leo Machi 15, 2017 katika Ukumbi wa Bwalo Kuu la Maafisa Magereza Ukonga – Dar es Salaam.
Baadhi ya Wakuu wa miradi mbalimbali ya Shirika la Magereza wakifuatilia kwa makini maelekezo kutoka kwa Kamishna Jenerali wa Magereza, Dkt. Juma Malewa katika Kikao kazi cha Shirika la Uzalishaji Mali la Magereza(hayupo pichani).
Kamishna Jenerali wa Magereza, Dkt. Juma Malewa akimkaribisha Mkurugenzi wa Manunuzi wa Wizara ya Mambo ya ndani ya nchi, Bw. David Mwangosi ambaye alimwakilisha Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya nchi katika ufunguzi wa Kikao kazi hicho.
Meza Kuu ikiongozwa na Kamishna Jenerali wa Magereza, Dkt. Juma Malewa(kulia) akitolea ufafanuzi wa hoja mbalimbali(kushoto) ni Mdhibi Mkuu wa Shirika la Magereza, ACP. Joel Bukuku(katikati) ni Kamishna wa Fedha na Utawala wa Magereza, Gaston Sanga.
Mkuu wa Magereza Mkoa Mara, ACP. Goleha Masunzu akichangia hoja katika Kikao hicho.
Mkurugenzi wa Manunuzi wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya nchi, Bw. David Mwangosi ambaye alimwakilisha Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya nchi katika ufunguzi wa Kikao kazi cha Shirika la Magereza (wa pili toka kulia) akiwa katika picha ya pamoja na Wakuu wa Miradi ya Shirika la Magereza(wa pili toka kushoto) ni Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza, Dkt. Juma Malewa(wa kwanza kushoto) ni Kamishna wa Fedha na Utawala wa Magereza, Gaston Sanga (wa kwanza kulia) ni Naibu Kamishna wa Magereza, Edith Mallya 

(Picha zote na Jeshi la Magereza).

Tuesday, March 14, 2017

JESHI LA MAGEREZA KUPOKEA MAGARI 450 AINA YA ASHOK LEYLAND KWA SHUGHULI ZA UENDESHAJI MAGEREZANI


Na Lucas Mboje, Dar es Salaam
KAMISHNA Jenerali wa Magereza nchini, Dkt. Juma Malewa(pichani) ameipongeza Serikali ya Awamu ya Tano chini ya Rais Dkt. John Pombe Magufuli kwa kufanikisha mchakato wa ununuzi wa magari 450 ya Jeshi hilo ambayo yanatarajiwa kupokelewa muda wowote kuanzia sasa.

Kamishna Jenereli Malewa ameyasema hayo leo katika ufunguzi rasmi wa mkutano wa wakuu wa  magereza yote Tanzania Bara unaofanyika kwa siku moja katika Bwalo kuu la Maafisa magereza, ukonga jijini Dar es Salaam.

Jenerali Malewa amesema kuwa upatikanaji wa magari hayo utapunguza tatizo kubwa la uhaba wa magari kwa ajili ya shughuli za uendeshaji na utawala pamoja uboreshaji wa utekelezaji wa majukumu ya Jeshi hilo.

“Nichukue nafasi hii kumshukuru kwa dhati Mhe. Rais Dkt. John Pombe Magufuli pamoja na serikali yote kwa ujumla kwa namna inavyoshughulikia utafutaji wa ufumbuzi wa changamoto tulizonazo,” alisema Jenerali Malewa.

Aidha kuhusu madeni ya Watumishi wa Jeshi hilo na wazabuni, Kamishna Jenerali Malewa amesema serikali imetoa kiasi cha zaidi ya Bilioni 8 za pesa ya kitanzania kwa ajili ya kulipa madeni hayo ambapo madeni yote yaliyokwisha kuhakikiwa tayari yameanza kulipwa na wahusika wamekwishaanza kupata fedha wanazodai Jeshi hilo.

Kwa upande wake Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani, Mhe. Mhandisi Hamad Yusuph Masauni akizunguza katika ufunguzi wa Mkutano huo ametoa rai kwa jeshi hilo kutumia vyema fursa zilizopo katika katika maeneo mbalimbali ya jeshi hilo kwa kuanzisha na kuimarisha viwanda vidovidogo vilivyopo ili kuongeza uzalishaji hivyo kuchangia pato la taifa.

Masauni amesema kuwa Jeshi la Magereza linazo fursa nyingi sana za uzalishaji yakiwemo maeneo makubwa yanayofaa kwa kilimo, miradi ya ufugaji na miradi mengineyo ya kiuchumi.

“Nisisitiza kwamba wekeni mikakati yenye lengo la kuongeza uzalishaji katika maeneo yenu kwani nataka kila mmoja wenu katika gereza alilopo aweke malengo ya kuongeza uzalishaji kulingana na fursa zilizopo,” alisema Mhe. Masauni.

Mkutano huu wa Wakuu wa Magereza yote Tanzania Bara unajumuisha Maafisa Waandamizi kutoka Makao Makuu ya Magereza na Wakuu wa vituo vya Magereza yote nchini ambapo lengo kuu ni kujadiliana kwa kina hali halisi ya utendaji kazi magerezani na kuweka mikakati ya kukabiliana na changamoto zilizopo ili kuongeza tija na ufanisi. Kauli mbiu ya mkutano huo ni JESHI LA MAGEREZA KATIKA JITIHADA ZA KUFANIKISHA KUELEKEA TANZANIA YA UCHUMI WA VIWANDA.

MASAUNI AWATAKA MAAFISA MAGEREZA KUONGEZA KASI YA UZALISHAJI NCHINI, AFUNGUA MKUTANO WA WAKUU WA VITUO VYA MAGEREZA TANZANIA BARA, JIJINI DAR ES SALAAM LEO

Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni (aliyevaa suti) akiongozwa na Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza nchini, (CGP) Dkt. Juma Malewa (mbele), kuingia ukumbini kwa ajili ya kufungua Mkutano wa Maafisa Waandamizi kutoka Makao Makuu ya Jeshi la Magereza pamoja na Wakuu wa Vituo vya Magereza Tanzania Bara, uliofanyika Bwalo Kuu la Maafisa wa Jeshi hilo, Ukonga, jijini Dar es Salaam leo. Katika hotuba yake ya ufunguzi, Masauni aliwataka Maafisa wa Jeshi hilo, kuongeza kasi zaidi ya kuzalisha katika kilimo, miradi ya ufugaji pamoja na vyanzo vingine ili kulilitea mapato zaidi Jeshi hilo. Aidha, alisema kwa Maafisa watakaozembea katika uzalishaji wataondolewa katika nyadhifa zao. 
Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni akizungumza na Maafisa Waandamizi kutoka Makao Makuu ya Jeshi la Magereza naWakuu wa Vituo vya Magereza yote Tanzania Bara (hawapo pichani) katika Mkutano uliofanyika katika Ukumbi wa  Bwalo Kuu la Maafisa wa Jeshi hilo, Ukonga, jijini Dar es Salaam leo. Katika hotuba yake ya ufunguzi wa mkutano huo, Masauni aliwataka Maafisa wa Jeshi hilo, kuongeza kasi zaidi ya kuzalisha katika kilimo, miradi ya ufugaji pamoja na vyanzo vingine ili kulilitea mapato zaidi Jeshi hilo. Aidha, alisema kwa maafisa watakaozembea katika uzalishaji wataondolewa katika nyadhifa zao. 
Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza nchini, (CGP) Dkt. Juma Malewa akitoa hotuba yake ya kumkaribisha mgeni rasmi Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni (kulia) kwa ajili ya kuja kuufungua Mkutano wa Wakuu wa Vituo vya Magereza Tanzania Bara ambao pia ulihudhuriwa na Maafisa Waandamizi wa Jeshi hilo kutoka Makao Makuu, ulifanyika Bwalo Kuu la Maafisa wa Jeshi hilo, Ukonga, jijini Dar es Salaam leo. Hata hivyo, Dkt Malewa katika hotuba yake alimshukuru Rais John Magufuli kwa kutatua kwa kiasi kikubwa changamoto ya uhaba wa nyumba za Makazi ya Askari wa Jeshi hilo pamoja na juhudi za Serikali yake za ununuzi wa  magari 450 kwa awamu ya kwanza ambapo jeshi hilo linatarajia kuyapata. Katikati ni Naibu Kamishna wa Jeshi hilo, Edith Mallya.
Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni akizungumza na Maafisa Waandamizi kutoka Makao Makuu ya Jeshi la Magereza naWakuu wa Vituo vya Magereza yote Tanzania Bara katika Mkutano uliofanyika katika Ukumbi wa  Bwalo Kuu la Maafisa wa Jeshi hilo, Ukonga, jijini Dar es Salaam leo. Katika hotuba yake ya ufunguzi wa mkutano huo, Masauni aliwataka Maafisa wa Jeshi hilo, kuongeza kasi zaidi ya kuzalisha katika kilimo, miradi ya ufugaji pamoja na vyanzo vingine ili kulilitea mapato zaidi Jeshi hilo. Aidha, alisema kwa maafisa watakaozembea katika uzalishaji wataondolewa katika nyadhifa zao. 
Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni (wapili kulia waliokaa), Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza nchini, (CGP) Dkt. Juma Malewa (wapili kushoto waliokaa), Kamishna wa Fedha na Utawala wa Jeshi hilo, Gaston Sanga (kulia waliokaa), Naibu Kamishna wa Jeshi hilo, Edith Mallya (kushoto) wakiwa katika picha ya pamoja na Maafisa wa Jeshi hilo, mara baada ya Naibu Waziri huyo, kuufungua Mkutano wa Maafisa Waandamizi wa Makao Makuu ya Jeshi hilo pamoja na Wakuu wa Vituo vya Magereza Tanzania Bara, uliofanyika Bwalo Kuu la Maafisa wa Jeshi hilo, Ukonga, jijini Dar es Salaam leo. 

Picha zote na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.

Monday, March 13, 2017

MKUTANO MKUU WA MWAKA WA NNE WA MAGEREZA SACCOS WAFANYIKA BWALO KUU LA MAAFISA MAGEREZA, UKONGA - DAR ESALAAM

Kamishna Jenerali wa Magereza, Dkt. Juma Malewa ambaye pia ni Mlezi wa Chama cha Akiba na Mikopo cha Watumishi wa Jeshi la Magereza(TPS SACCOS LTD) akitoa maelezo mafupi kabla ya kumkaribisha Kaimu Mrajis wa Vyama vya Ushirika afungue rasmi Mkutano Mkuu wa Nne wa TPS SACCOS Ltd leo Machi 13, 2016 uliofanyika kwa siku moja katika Ukumbi wa Bwalo Kuu la Maafisa Magereza Ukonga – Dar es Salaam.
Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Magereza, Tusekile Mwaisabila ambaye ni Mkuu wa Magereza Mkoa wa Lindi akitoa hoja ya kuthibitisha Notisi ya Mkutano Mkuu mbele ya Wajumbe wa Mkutano Mkuu wa Nne uliofanyika kwa siku moja katika Ukumbi wa Bwalo Kuu la Maafisa Magereza Ukonga – Dar es Salaam
Kaimu Mrajis wa Vyama vya Ushirika, Bw. Colin Nyakunga akitoa salaam ya Ushirika kabla ya kutoa Hotuba ya Ufunguzi wa  Mkutano Mkuu wa Nne wa TPS SACCOS Ltd leo Machi 13, 2016 uliofanyika kwa siku moja katika Ukumbi wa Bwalo Kuu la Maafisa Magereza Ukonga – Dar es Salaam.
Wajumbe wa Mkutano Mkuu ambao ni Maafisa, Askari na Watumishi raia wa Jeshi la Magereza wenye vyeo mbalimbali ambao ni Wanachama wa TPS SACCOS LTD kutoka Mikoa yote Tanzania Bara wakisikiliza hotuba ya Mgeni rasmi katika Mkutano huo.
Meza Kuu wakiwa wameketi wakifuatilia zoezi la Utambulisho wa Wajumbe wa Mkutano Mkuu wa nne wa TPS SACCOS Ltd leo Machi 13, 2016 uliofanyika kwa siku moja katika Ukumbi wa Bwalo Kuu la Maafisa Magereza Ukonga – Dar es Salaam (katikati) ni Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza, Dkt. Juma Malewa(Kulia) ni Kaimu Mrajis wa Vyama vya Ushirika, Bw. Colin Nyakunga(kushoto) ni Mwenyekiti wa TPS SACOSS LTD, SACP. Gideon Nkana.
Sekretarieti ya Mkutano Mkuu wa Nne wa TPS SACCOS Ltd wakiwajibika kama inavyoonekana katika picha.
Mwenyekiti TPS SACCOS Ltd, Kamishna Msaidizi  Mwandamizi wa Magereza, Gideon Nkana akiteta jambo na Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza, Dkt. Juma Malewa(Kulia).
Baadhi ya Watendaji wa Chama cha Akiba na Mikopo cha Watumishi wa Jeshi la Magereza wakiwajibika katika Mkutano huo kama inavyoonekana katika picha.
Kaimu Mrajis wa Vyama vya Ushirika, Bw. Colin Nyakunga(wa nne toka kulia) akiwa katika picha ya pamoja na Wajumbe wa Mkutano Mkuu wa Nne wa TPS SACCOS Ltd uliofanyika katika Ukumbi wa Bwalo Kuu la Maafisa Magereza Ukonga – Dar es Salaam(wa nne toka kushoto) ni Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza, Dkt. Juma Malewa(wa tatu kulia) ni Kamishna wa Fedha na Utawala wa Magereza, Gaston Sanga (wa pili kulia) ni Naibu Kamishna wa Magereza, Edith Mallya(wa pili kushoto) ni Mwenyekiti TPS SACCOS Ltd, Kamishna Msaidizi  Mwandamizi wa Magereza, Gideon Nkana

(Picha zote na Lucas Mboje wa Jeshi la Magereza).