JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI
(Jeshi
la Magereza)
TANZIA
Kamishna Jenerali wa Jeshi Magereza Mej. Jen
Suleiman M. Mzee anasikitika kutangaza kifo cha Naibu Kamishna wa Magereza Julius
Mayenga Sang’udi kilichotokea Hospitali ya Benjamin Mkapa, Jijini Dodoma leo tarehe
20 Januari, 2021.
Aidha anatoa pole kwa Familia ya Marehemu, Watumishi
wote wa Jeshi la Magereza Nchini, Ndugu, Jamaa na Marafiki wote walioguswa na msiba
huu.
Jeshi la
Magereza kwa kushirikiana na familia ya Marehemu inaendelea kuratibu taratibu za
Mazishi nyumbani kwake Kisasa nyumba 300, Dodoma.
Mwili wa Marehemu unatarajiwa kusafirishwa Ijumaa
tarehe 22 Januari,2021 na Mazishi yatafanyika Mkoani Simiyu Kijiji cha Ikulilo
– Mwandete Jumamosi tarehe 23 Januari,2021.
Mwenyezi Mungu ailaze Roho ya Marehemu mahala pema
peponi, Amen.
Imetolewa
na Msemaji wa Jeshi la Magereza,
Kitengo
cha Habari na Mawasiliano ya Umma,
Dodoma.