Mojawapo ya Jukumu la Jeshi la Magereza ni kuwapeleka mahakamani mahabusu na kuwarudisha magerezani.

Gadi ya askari Wanawake na Wanaume wa Jeshi la Magereza katika Maadhimisho ya Sherehe za Kitaifa.

Ng'ombe bora wa Nyama na Maziwa ni sehemu ya miradi ya Uzalishaji inayoendeshwa na kusimamiwa na Jeshi la Magereza nchini.

Sehemu ya Mashamba makubwa yanayoendeshwa na Jeshi la Magereza: Shughuli za Kilimo cha Mashamba makubwa, madogo na bustani za mboga mboga ni moja ya shughuli za Magereza katika kuwafunza wafungwa namna ya kujitegemea mara wamalizapo vifungo vyao.

Baadhi wa wafungwa katika Kiwanda cha Ushonaji nguo cha Gereza Kuu Ukonga wakiwa kazini: Shughuli za Ushonaji wa nguo ni moja ya eneo ambalo wafungwa hupata huduma za urekebishwaji kwa vitendo.

Tuesday, February 5, 2019

WAZIRI MKUU WA TANZANIA MH. KASSIM MAJALIWA ATEMBELEA BANDA LA MAGEREZA KATIKA WIKI YA SHERIA JIJINI DODOMA TAR. 02 FEB,2019


Waziri Mkuu wa Tanzania Mh. Khasim Majaliwa akihutubia katika ufunguzi wa wiki ya Elimu ya Sheria ambapo kitaifa yanaendelea kufanyika  Jijini Dodoma, kaulimbiu ni utoaji haki ni jukumu la mahakama na wadau.
Waziri Mkuu wa Tanzania Mh. Khasim Majaliwa akiwa na Jaji Mkuu wa Tanzania  Mh.Profesa Ibrahim Juma Jaji Mkuu wa Tanzania , Mh. Tulia Akson Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,  Dr.B. Mahenge Mkuu wa Mkoa wa Dodoma wakiwa katika matembezi ya ufunguzi wa  wiki ya Sheria yaliofanyika   asubuhi ya tarehe 02 Feb, 2019  Jijini Dodoma ambapo yalianzia katika viwanja vya Mahakama Kuu na kuishia katika viwanja vya Nyerere Squire.
Maafisa wa Jeshi la Magereza kutoka Makao Makuu ya Magereza , Ofisi ya Mkuu wa Magereza Mkoa wa Dodoma na Gereza Kuu Isanga  wakiwa katika matembezi ya wiki ya elimu ya sheria jijini Dodoma kutoka  kushoto ni Kamishna  wa Magereza anayesimamia Fedha na Mipango  (CP) Gideon Nkana , Mkuu wa Magereza Mkoa wa Dodoma Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Magereza (SACP) Salum Hussein, Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Magereza (SACP) Rajabu Nyange, Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Magereza(SACP) Mzee Ramadhan Nyamka, Kamishna Msaidizi Mwandamizi (SACP) Chacha Jackson Bina,  Mkuu wa Gereza Kuu Isanga Kamishna Msaidizi wa Magereza(ACP) Keneth Mwambije.
Msemaji wa Jeshi la Magereza nchini Mrakibu wa Magereza (SP) Amina Kavirondo akimpa ufafanuzi  Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Khasim Majaliwa kuhusu masuala ya haki na ulinzi wa watoto walioko Magerezani kutokana na Mama zao kukinzana na sharia.
Baadhi ya Maafisa na askari wa jeshi la Magereza wakishiriki katika matembezi ya maadhimisho ya wiki ya sheria Dodoma.( picha na Cpl Mfaume Ally- Jeshi la Magereza)

KAMISHNA JENERALI WA MAGEREZA, PHAUSTINE KASIKE ATEMBELEA GEREZA KUU LA WANAWAKE TANZANIA - KINGOLWIRA, MOROGORO

Kamishna Jenerali wa Magereza nchini, Phaustine Kasike(kushoto) akisalimiana na Mkuu wa Gereza Kuu la Wanawake Tanzania - Kingolwira, ACP. Loyce Ruhembe alipotembelea alipotembelea Gereza hilo jana februari 4, 2019 katika ziara yake ya kikazi Mkoani Morogoro

Mkuu wa Gereza Kuu la Wanawake Tanzania, Kingolwira, ACP. Loyce Ruhembe akitoa taarifa fupi ya uendeshaji wa Gereza Kuu la Wanawake Tanzania – Kingolwira kwa Kamishna Jenerali wa Magereza nchini, Phaustine Kasike(kushoto meza kuu) jana februari 4, 2019 alipotembelea Gereza hilo.

Kamishna Jenerali wa Magereza nchini, Phaustine Kasike(katikati) akikagua maeneo mbalimbali ya Gereza Kuu la Wananwake(kulia) ni Mkuu wa Gereza Kuu la Wanawake Tanzania, Kingolwira, ACP. Loyce Ruhembe. Kushoto ni Mkuu wa Chuo cha Udereva cha Magereza – Kingolwira, ACP. Lazaro Nyanga.

Askari wa Gereza Kuu la Wanawake Kingolwira wakiwa timamu kazini wakati Kamishna Jenerali wa Magereza nchini(hayupo pichani) akizungumza na Wafungwa wa Gereza hilo jana februari 4, 2019 alipotembelea Gereza hilo.

Kamishna Jenerali wa Magereza nchini, Phaustine Kasike(kulia) akiangalia mradi wa kuku wa mayai katika Gereza Kuu la Wanawake Tanzania – Kingolwira alipotembelea jana februari 4, 2019.

Ujenzi wa nyumba kwa njia ya ubunifu katika Kambi mojawapo ya Gereza Mtego wa Simba, Morogoro ukiendelea katika hatua awali za ujenzi.

Kamishna Jenerali wa Magereza nchini, Phaustine Kasike akiangalia mashine kufunga majani ya malisho ya mifugo katika mradi wa ng’ombe wa maziwa Gereza Mtego wa Simba.

Mkuu wa Chuo cha Udereva cha Magereza – Kingolwira, ACP. Lazaro Nyanga akimuongoza Kamishna Jenerali wa Magereza nchini, Phaustine Kasike(kushoto) kukagua majenego mbalimbali yanayokarabatiwa katika chuo hicho kwa kutumia ubunifu (Picha na Jeshi la Magereza).