Monday, September 10, 2018
WADAU JITOKEZENI KUTOA MISAADA KWA MAGEREZA: CGP KASIKE
9:48 AM
Na
Deodatus Kazinja
Wito
umetolewa kwa Asasi mbalimbali za kiraia kujitokeza kushirikiana na Jeshi la
Magereza nchini katika kukabiliana na
baadhi ya changamoto zinazoweza kulikwamisha katika kutoa huduma muhimu za
wafungwa kutokana na ufinyu wa bajeti.
Hayo
yamesemwa leo na Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza nchini Phaustine Kasike
katika hafla ya kupokea msaada wa Kibinadamu uliotolewa na Asasi ya Kidini ya
New Life In Christ iliyofanyika katika
viwanja vya Gereza Kuu Karanga mjini Moshi leo Septemba 8, 2018.
“Ni
ukweli usiopingika kuwa Jeshi la Magereza limekuwa likishindwa kutekeleza kwa
ukamilifu utoaji wa baadhi ya huduma muhimu kwa wafungwa kutokana na ufinyu wa
bajeti” Amesema Kamishna Jenerali Kasike
Na
kuongeza “ natoa wito kwa Asasi nyingine kuiga mfano uliooneshwa na New Life in
Christ na Dorcas Aid International Tanzania zinavyoshirikiana na Jeshi la
Magereza”
Asasi
ya Kidini ya New Life In Christ pamoja
na Dorcas Aid International Tanzania kwa miaka 14 sasa tangu 2005 zimekuwa
zikishirikiana na Jeshi la Magereza kwa kutoa misaada ya Kibinadamu na Kiroho
yenye thamani ya zaidi ya shilingi bilioni 1.7.
Kwa
kipindi chote hicho Asasi hizi zimekuwa zimekuwa zikitoa huduma mbalimbali
ikiwa ni pamoja na uwezeshaji wa semina za ushauri pamoja na mafunzo ya ufundi
stadi kwa wafungwa na maafisa wa magereza.
Huduma
nyingine ni kuwa na vituo vidogo vidogo vya kujifunza kufanya jambo ambavyo
tayari linafanyika ndani ya magereza kama vile uokaji mikate, ushonaji na
kudarizi, ushonaji wa viatu, ukinyozi,useremala na uchomeleaji mchanganyiko.
Katika
hafla hiyo Asasi ya Kidini ya New Life In Christ imekabidhi msaada wenye
thamani ya zaidi ya shilingi milioni 200.2. Na kuahidi kuendelea kutoa misaada
ya namna hiyo kwa kadiri Mungu atakavyowajali.
Misaada
ya Kibinadamu iliyotolewa leo imewalenga zaidi wafungwa walioko mkoani
Kilimanjaro, Tanga, Arusha na Mwanza. Ambapo Kamishna Kasike amewaagiza
wakuu wa magereza yote ambayo vifaa
hivyo vitapelekwa kuhakikisha wanavitunza na kuvitumia kwa uadilifu kama
ilivyokusudiwa.
KAMISHNA JENERALI WA MAGEREZA PHAUSTINE KASIKE APOKEA MISAADA YA KIBINADAMU YA WAFUNGWA GEREZA KUU KARANGA, MOSHI
9:47 AM
Kamishna Jenerali wa Magereza (CGP) Phaustine Kasike akisalimiana na Meneja Miradi
wa Asasi ya Kidini ya New Life In Christ Ndg. Charles Shang’a mara baada ya
kuwasili katika viwanja vya Gereza Kuu Karanga Moshi kwa ajili ya hafla fupi ya
kupokea Misaada ya Kibinadamu iliyotolewa na Asasi hiyo kwa ajili ya wafungwa
leo Septemba 8, 2018
Wageni wa meza kuu wakiongzwa na Kamishna
Jenerali wa Magereza (CGP) Phaustine
Kasike (katikati) wakiimba wimbo wa
Taifa la Tanzania ikiashiria ufunguzi wa hafla fupi ya kupokea misaada ya
Kibinadamu kwa ajili ya wafungwa iliyotolewa na Asasi ya Kidini ya New Life In
Christ. Tukio hilo limefanyika leo Septemba 8, 2018 katika viwanja vya Gereza
Kuu Karanga Moshi.
Mkurugenzi wa Asasi ya Dorcas Aid International
Tanzania Bi. Lilian Urasa akitoa maelezo
mafupi kabla ya kukabidhi msaada wa Kibinadamu kwa ajili ya Wafungwa nchini.
Dorcas Aid International Tanzania hushirikiana na Asasi ya Kidini ya New Life
In Christ katika kutoa misaada ya namna hiyo.
Kamishna Jenerali wa Magereza (CGP) Phaustine Kasike akipokea msaada wa vyerehani uliotolewa na Asasi ya Kidini ya New Life In Christ leo Septemba 8, 2018 kwa ajili ya wafungwa. Hafla ya upokeaji wa misaada hiyo imefanyika katika gereza Kuu Karanga Moshi
Kamishna
Jenerali wa Magereza (CGP) Phaustine
Kasike (wa pili kushoto) akipokea msaada wa vifaa vya kuchomelea akiwa ni
sehemu ya vifaa vilivyotolewa na Asasi ya Kidini ya New Life In Christ kwa
ajili ya wafungwa vitakavyotumika kuwafundisha stadi mbalimbali za ufundi
magerezani.
Mwenekano wa baadhi ya misaada ya
Kibinadamu iliyotolewa Asasi ya Kidini
ya New Life In Christ iliyokabidhiwa kwa Jeshi la Magereza leo Septemba 8, 2018
katika viwanja vya Gereza Kuu Karanga Moshi. Misaada iliyotolewa leo kwa ujumla
wake ina thamani ya zaidi ya milioni 200.2.
Kamishna
Jenerali wa Magereza (CGP) Phaustine
Kasike (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya askari wa magereza
mkoani Kilimanjaro wakati wa hafla ya kupokea misaada ya Kibinadamu kutoka kwa
Asasi ya Kidini ya New Life In Christ leo Septemba 8, 2018. Kutoka kulia ni Miradi
wa Asasi ya Kidini ya New Life In Christ Ndg. Charles Shang’a, Mkurugenzi wa
Asasi ya Dorcas Aid International Tanzania
Bi. Lilian Urasa na Mkuu wa Magereza Mkoa wa Kilimanjaro Kamishna Msaidizi
Mwandamizi wa Magereza (SACP) Dkt. Hasan Mkwiche. Kutoka kushoto ni Kaimu Mkuu
wa Magereza Mkoa wa Tanga Kamishna Msaidizi wa Magereza (ACP) Emmanuel Lwinga,
Kaimu Mkuu wa Magereza Mkoa wa Arusha Kamishna Msaidizi wa Magereza (ACP)
Anderson Kamtiaro na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kilimanjaro Kamishna Msaidizi wa
Polisi (ACP) Hamis Isaya.
Kamishna
Jenerali wa Magereza (CGP) Phaustine
Kasike akitoa hotuba kwa wageni mbalimbali (hawapo pichani) waliohudhuria hafla
fupi ya kupokea msaada wa Kibinadamu kwa ajili ya wafungwa kutoka kwa Asasi ya Kidini ya New Life In
Christ leo Septemba 8, 2018 katika
viwanja vya Gereza Kuu Karanga Moshi.
Kikundi
cha Sanaa cha Mama Jusi Anglikan cha mjini Moshi kilikonga nyoyo za wageni
waalikwa katika hafla ya kupokea msaada wa Kibinadamu uliotolewa na Asasi ya
Kidini ya New Life In Christ leo Septemba 8, 2018.
KAMISHNA JENERALI KASIKE AFANYA ZIARA YA KIKAZI MKOANI TANGA
9:09 AM
Kamishna Jenerali wa Magereza (CGP) Phaustine
Kasike akifuatilia kwa makina taarifa ya mkoa wa Tanga kutoka kwa Kaimu Mkuu wa
Magereza wa Mkoa huo Kamishna Msaidizi wa Magereza (ACP) Emmanuel Lwinga
alipofanya ziara ya kikazi ya siku moja mkoani humo leo Septemba 7,2018.
Kamishna Jenerali wa Magereza (CGP) Phaustine
Kasike (mwenye miwani) akisalimiana na baadhi ya maafisa wa ofisi ya Mkuu wa
Magereza mkoa wa Tanga, Gereza Kuu Maweni na gereza la Mahabusu Tanga mara alipowasili katika viwanja vya Gereza
Kuu Maweni jijini Tanga akiwa katika
ziara ya kikazi ya siku moja mkoani humo
leo Septemba 7, 2018.
Kamishna Jenerali wa Magereza (CGP) Phaustine
Kasike akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya askari wa Kikosi Maalum cha
Kutuliza Ghasia Magerezani (KMKGM) walioko mkoani Tanga alipofanya ziara ya
kikazi ya siku moja mkoani humo leo Septemba 7, 2018.
Kamishna
Jenerali wa Magereza (CGP) Phaustine Kasike (mwenye “microphone” ) akizungumza
na maafisa na askari wa vituo vya ofisi ya Mkuu wa Magereza Mkoa wa Tanga,
Gereza Kuu Maweni na Gereza la Mahabusu Tanga (hawapo pichani) kwa pamoja
katika bwalo la Gereza Kuu Maweni Tanga alipofanya ziara ya siku moja ya kikazi
mkoani humo. Wa kwanza kulia ni Kaimu Mkuu wa Magereza Mkoa wa Tanga Kamishna
Msaidizi wa Magereza (ACP) Emmauel Lwinga, wa tatu kulia ni Mkuu wa Gereza Kuu
Maweni Kamishna Msaidizi wa Magereza (ACP) Felichism Masawe na wa kwanza
kushoto ni Afisa Mnadhimu wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Tanga Marakibu Mwandamizi
wa Magereza (SSP) Hamis Mbwana.
Baadhi
ya maafisa na askari wa vituo vya ofisi ya Mkuu wa Magereza mkoa wa
Tanga, waliokusanyika kwa pamoja katika
bwalo la gereza Kuu Maweni wakifuatilia
kwa makini hotuba ya Kamishna Jenerali wa Magereza Phaustine Kasike (hayupo
pichani) alipofanya ziara ya kikazi
mkoani humo leo Septemba 7, 2018. Katika
hotuba yake CGP ametilia mkazo suala la kubadili mtazamo wa kiutendaji, kuacha
kufanya kazi kwa mazoea ili kufanikisha majukumu yetu kama serikali na jamii
nzima inavyotarajia kutoka kwetu.
Kamishna Jenerali wa Magereza (CGP) Phaustine
Kasike akiwa katika picha ya pamoja na baadhi askari wa magereza wa kike mkoani
Tanga alipofanya ziara ya siku moja mkoani humo leo Septemba 7, 2018.
Picha zote na Jeshi la Magereza.