Mojawapo ya Jukumu la Jeshi la Magereza ni kuwapeleka mahakamani mahabusu na kuwarudisha magerezani.

Gadi ya askari Wanawake na Wanaume wa Jeshi la Magereza katika Maadhimisho ya Sherehe za Kitaifa.

Ng'ombe bora wa Nyama na Maziwa ni sehemu ya miradi ya Uzalishaji inayoendeshwa na kusimamiwa na Jeshi la Magereza nchini.

Sehemu ya Mashamba makubwa yanayoendeshwa na Jeshi la Magereza: Shughuli za Kilimo cha Mashamba makubwa, madogo na bustani za mboga mboga ni moja ya shughuli za Magereza katika kuwafunza wafungwa namna ya kujitegemea mara wamalizapo vifungo vyao.

Baadhi wa wafungwa katika Kiwanda cha Ushonaji nguo cha Gereza Kuu Ukonga wakiwa kazini: Shughuli za Ushonaji wa nguo ni moja ya eneo ambalo wafungwa hupata huduma za urekebishwaji kwa vitendo.

Monday, September 10, 2018

WADAU JITOKEZENI KUTOA MISAADA KWA MAGEREZA: CGP KASIKE


Na Deodatus Kazinja

Wito umetolewa kwa Asasi mbalimbali za kiraia kujitokeza kushirikiana na Jeshi la Magereza  nchini katika kukabiliana na baadhi ya changamoto zinazoweza kulikwamisha katika kutoa huduma muhimu za wafungwa kutokana na ufinyu wa bajeti.

Hayo yamesemwa leo na Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza nchini Phaustine Kasike katika hafla ya kupokea msaada wa Kibinadamu uliotolewa na Asasi ya Kidini ya New Life In Christ  iliyofanyika katika viwanja vya Gereza Kuu Karanga mjini Moshi leo Septemba 8, 2018.

“Ni ukweli usiopingika kuwa Jeshi la Magereza limekuwa likishindwa kutekeleza kwa ukamilifu utoaji wa baadhi ya huduma muhimu kwa wafungwa kutokana na ufinyu wa bajeti” Amesema Kamishna Jenerali Kasike

Na kuongeza “ natoa wito kwa Asasi nyingine kuiga mfano uliooneshwa na New Life in Christ na Dorcas Aid International Tanzania zinavyoshirikiana na Jeshi la Magereza”

Asasi ya Kidini ya New Life In Christ  pamoja na Dorcas Aid International Tanzania kwa miaka 14 sasa tangu 2005 zimekuwa zikishirikiana na Jeshi la Magereza kwa kutoa misaada ya Kibinadamu na Kiroho yenye thamani ya zaidi ya shilingi bilioni 1.7.

Kwa kipindi chote hicho Asasi hizi zimekuwa zimekuwa zikitoa huduma mbalimbali ikiwa ni pamoja na uwezeshaji wa semina za ushauri pamoja na mafunzo ya ufundi stadi kwa wafungwa na maafisa wa magereza.

Huduma nyingine ni kuwa na vituo vidogo vidogo vya kujifunza kufanya jambo ambavyo tayari linafanyika ndani ya magereza kama vile uokaji mikate, ushonaji na kudarizi, ushonaji wa viatu, ukinyozi,useremala na uchomeleaji mchanganyiko.

Katika hafla hiyo Asasi ya Kidini ya New Life In Christ imekabidhi msaada wenye thamani ya zaidi ya shilingi milioni 200.2. Na kuahidi kuendelea kutoa misaada ya namna hiyo kwa kadiri Mungu atakavyowajali.

Misaada ya Kibinadamu iliyotolewa leo imewalenga zaidi wafungwa walioko mkoani Kilimanjaro, Tanga, Arusha na Mwanza. Ambapo Kamishna Kasike amewaagiza wakuu  wa magereza yote ambayo vifaa hivyo vitapelekwa kuhakikisha wanavitunza na kuvitumia kwa uadilifu kama ilivyokusudiwa.




KAMISHNA JENERALI WA MAGEREZA PHAUSTINE KASIKE APOKEA MISAADA YA KIBINADAMU YA WAFUNGWA GEREZA KUU KARANGA, MOSHI

Kamishna Jenerali wa Magereza (CGP)  Phaustine Kasike akisalimiana na Meneja Miradi wa Asasi ya Kidini ya New Life In Christ Ndg. Charles Shang’a mara baada ya kuwasili katika viwanja vya Gereza Kuu Karanga Moshi kwa ajili ya hafla fupi ya kupokea Misaada ya Kibinadamu iliyotolewa na Asasi hiyo kwa ajili ya  wafungwa  leo Septemba 8, 2018

Wageni wa meza kuu wakiongzwa na Kamishna Jenerali wa Magereza (CGP)  Phaustine Kasike (katikati)  wakiimba wimbo wa Taifa la Tanzania ikiashiria ufunguzi wa hafla fupi ya kupokea misaada ya Kibinadamu kwa ajili ya wafungwa iliyotolewa na Asasi ya Kidini ya New Life In Christ. Tukio hilo limefanyika leo Septemba 8, 2018 katika viwanja vya Gereza Kuu Karanga Moshi.

Mkurugenzi wa Asasi ya Dorcas Aid International Tanzania  Bi. Lilian Urasa akitoa maelezo mafupi kabla ya kukabidhi msaada wa Kibinadamu kwa ajili ya Wafungwa nchini. Dorcas Aid International Tanzania hushirikiana na Asasi ya Kidini ya New Life In Christ katika kutoa misaada ya namna hiyo.

Kamishna Jenerali wa Magereza (CGP)  Phaustine Kasike akipokea msaada wa vyerehani uliotolewa  na Asasi ya Kidini ya New Life In Christ leo Septemba 8, 2018 kwa ajili ya wafungwa. Hafla ya upokeaji wa misaada hiyo imefanyika katika gereza Kuu Karanga Moshi


Kamishna Jenerali wa Magereza (CGP)  Phaustine Kasike (wa pili kushoto) akipokea msaada wa vifaa vya kuchomelea akiwa ni sehemu ya vifaa vilivyotolewa na Asasi ya Kidini ya New Life In Christ kwa ajili ya wafungwa vitakavyotumika kuwafundisha stadi mbalimbali za ufundi magerezani.

Mwenekano wa baadhi ya  misaada ya Kibinadamu  iliyotolewa Asasi ya Kidini ya New Life In Christ iliyokabidhiwa kwa Jeshi la Magereza leo Septemba 8, 2018 katika viwanja vya Gereza Kuu Karanga Moshi. Misaada iliyotolewa leo kwa ujumla wake ina thamani ya zaidi ya milioni 200.2.


Kamishna Jenerali wa Magereza (CGP)  Phaustine Kasike (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya askari wa magereza mkoani Kilimanjaro wakati wa hafla ya kupokea misaada ya Kibinadamu kutoka kwa Asasi ya Kidini ya New Life In Christ leo Septemba 8, 2018. Kutoka kulia ni Miradi wa Asasi ya Kidini ya New Life In Christ Ndg. Charles Shang’a, Mkurugenzi wa Asasi ya Dorcas Aid International Tanzania  Bi. Lilian Urasa na Mkuu wa Magereza Mkoa wa Kilimanjaro Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Magereza (SACP) Dkt. Hasan Mkwiche. Kutoka kushoto ni Kaimu Mkuu wa Magereza Mkoa wa Tanga Kamishna Msaidizi wa Magereza (ACP) Emmanuel Lwinga, Kaimu Mkuu wa Magereza Mkoa wa Arusha Kamishna Msaidizi wa Magereza (ACP) Anderson Kamtiaro na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kilimanjaro Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP) Hamis Isaya.

Kamishna Jenerali wa Magereza (CGP)  Phaustine Kasike akitoa hotuba kwa wageni mbalimbali (hawapo pichani) waliohudhuria hafla fupi ya kupokea msaada wa Kibinadamu kwa ajili ya wafungwa  kutoka kwa Asasi ya Kidini ya New Life In Christ  leo Septemba 8, 2018 katika viwanja vya Gereza Kuu Karanga Moshi.

Kikundi cha Sanaa cha Mama Jusi Anglikan cha mjini Moshi kilikonga nyoyo za wageni waalikwa katika hafla ya kupokea msaada wa Kibinadamu uliotolewa na Asasi ya Kidini ya New Life In Christ leo Septemba 8, 2018.

KAMISHNA JENERALI KASIKE AFANYA ZIARA YA KIKAZI MKOANI TANGA



Kamishna Jenerali wa Magereza (CGP) Phaustine Kasike akifuatilia kwa makina taarifa ya mkoa wa Tanga kutoka kwa Kaimu Mkuu wa Magereza wa Mkoa huo Kamishna Msaidizi wa Magereza (ACP) Emmanuel Lwinga alipofanya ziara ya kikazi ya siku moja mkoani humo leo Septemba 7,2018.


Kamishna Jenerali wa Magereza (CGP) Phaustine Kasike (mwenye miwani) akisalimiana na baadhi ya maafisa wa ofisi ya Mkuu wa Magereza mkoa wa Tanga, Gereza Kuu Maweni na gereza la Mahabusu Tanga  mara alipowasili katika viwanja vya Gereza Kuu Maweni jijini Tanga  akiwa katika ziara ya kikazi ya siku moja  mkoani humo leo Septemba 7, 2018.
Kamishna Jenerali wa Magereza (CGP) Phaustine Kasike akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya askari wa Kikosi Maalum cha Kutuliza Ghasia Magerezani (KMKGM) walioko mkoani Tanga alipofanya ziara ya kikazi ya siku moja mkoani humo leo Septemba 7, 2018.

Kamishna Jenerali wa Magereza (CGP) Phaustine Kasike (mwenye “microphone” ) akizungumza na maafisa na askari wa vituo vya ofisi ya Mkuu wa Magereza Mkoa wa Tanga, Gereza Kuu Maweni na Gereza la Mahabusu Tanga (hawapo pichani) kwa pamoja katika bwalo la Gereza Kuu Maweni Tanga alipofanya ziara ya siku moja ya kikazi mkoani humo. Wa kwanza kulia ni Kaimu Mkuu wa Magereza Mkoa wa Tanga Kamishna Msaidizi wa Magereza (ACP) Emmauel Lwinga, wa tatu kulia ni Mkuu wa Gereza Kuu Maweni Kamishna Msaidizi wa Magereza (ACP) Felichism Masawe na wa kwanza kushoto ni Afisa Mnadhimu wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Tanga Marakibu Mwandamizi wa Magereza (SSP) Hamis Mbwana.

Baadhi ya maafisa na askari  wa  vituo vya ofisi ya Mkuu wa Magereza mkoa wa Tanga,  waliokusanyika kwa pamoja katika bwalo la gereza Kuu Maweni  wakifuatilia kwa makini hotuba ya Kamishna Jenerali wa Magereza Phaustine Kasike (hayupo pichani)  alipofanya ziara ya kikazi mkoani humo leo  Septemba 7, 2018. Katika hotuba yake CGP ametilia mkazo suala la kubadili mtazamo wa kiutendaji, kuacha kufanya kazi kwa mazoea ili kufanikisha majukumu yetu kama serikali na jamii nzima inavyotarajia kutoka kwetu.

Kamishna Jenerali wa Magereza (CGP) Phaustine Kasike akiwa katika picha ya pamoja na baadhi askari wa magereza wa kike mkoani Tanga alipofanya ziara ya siku moja mkoani humo leo Septemba 7, 2018.
Picha zote na Jeshi la Magereza.