Mkuu wa Jeshi la Magereza nchini CGP Jeremiah Yoram Katungu,leo Julai 11, 2025 amewavisha vyeo vipya maafisa 29 wa Magereza Makao Makuu, ikiwa ni miongoni mwa maafisa 839 waliopandishwa vyeo kwa kada mbalimbali katika Jeshi la Magereza Tanzania bara, kwa mwaka 2024/2025.
Akizungumza katika hafla hiyo ya uvalishaji vyeo CGP. Katungu amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Dkt.Samia Suluhu Hassan, kwa kuliwezesha Jeshi la Magereza kutekeleza majukumu yake na kutoa kibali cha upandishaji vyeo kwa Maafisa hao.
Aidha, CGP. Katungu amewapongeza maafisa wote walio panda vyeo nchi nzima na kuwataka kufanya kazi kwa uweledi,uadilifu huku akieleza kuwa ni matarajio ya Jeshi na Serikali kwaujumla kuwa watatekeleza majukumu yao kwa ufanisi mkubwa na kutanguliza mbele maslahi na ustawi wa Jeshi la Magereza na Taifa kwaujumla.
Kwaupande wake Kamishna wa Sheria na Uendeshaji wa Magereza CP. Nicodemus Tenga, amewapongeza Maafisa wote waliopandishwa vyeo na kuwataka wakatafute suluhisho la matatizo yaliyopo katika sehemu zao za kazi ili kuleta ufanisi wakiutendaji katika Jeshi.
Akitoa neno la shukrani kwaniaba ya wote waliopandishwa vyeo, Kamishna Msaidizi wa Magereza (ACP) Elmas Mgimwa, amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuridhia kibali cha upandishaji vyeo pamoja na Tume ya Utumishi wa Jeshi la Polisi, Magereza, Zimamoto na Uokoaji na Uhamiaji na uongozi mzima wa Jeshi la Magereza kwa kuwapendekeza.
Maafisa hao wamepandishwa vyeo kuanzia Julai 07, 2025 kwa mujibu wa Muundo wa Maendeleo ya Utumishi wa Jeshi la Magereza wa mwaka 2015 na kuzingatia Ikama ya Jeshi.