Mojawapo ya Jukumu la Jeshi la Magereza ni kuwapeleka mahakamani mahabusu na kuwarudisha magerezani.

Gadi ya askari Wanawake na Wanaume wa Jeshi la Magereza katika Maadhimisho ya Sherehe za Kitaifa.

Ng'ombe bora wa Nyama na Maziwa ni sehemu ya miradi ya Uzalishaji inayoendeshwa na kusimamiwa na Jeshi la Magereza nchini.

Sehemu ya Mashamba makubwa yanayoendeshwa na Jeshi la Magereza: Shughuli za Kilimo cha Mashamba makubwa, madogo na bustani za mboga mboga ni moja ya shughuli za Magereza katika kuwafunza wafungwa namna ya kujitegemea mara wamalizapo vifungo vyao.

Baadhi wa wafungwa katika Kiwanda cha Ushonaji nguo cha Gereza Kuu Ukonga wakiwa kazini: Shughuli za Ushonaji wa nguo ni moja ya eneo ambalo wafungwa hupata huduma za urekebishwaji kwa vitendo.

Monday, September 27, 2021

TANGAZO LA AJIRA JESHI LA MAGEREZA

 Bofya hapa kupakua tangazo la ajira

Thursday, March 11, 2021

WAFUNGWA, MAHABUSU KUNUFAIKA NA BIMA YA AFYA ILIYOBORESHWA (CHF).


 DODOMA. Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza Meja Jenerali Suleimani Mzee Leo Tarehe 11 Machi 2021 amekutana na kufanya mazungumzo na Dkt. Francis Lutalala, ambaye ni Mratibu wa Bima ya Afya ya Jamii iliyoboreshwa(CHF) Jijini Dodoma kwa lengo la kuona  uwezekano wa  kuboresha afya ya Watumishi wa Jeshi hilo pamoja na Wafungwa na Mahabusu waliopo Magerezani.


Jenerali Mzee amesema kuwa amefurahishwa na ujio wa Dkt. Lutalala, kwakuwa umetoa mwangaza kuelekea mpango wa kupunguza gharama za matibabu kwa Wafungwa kutokana na bima hiyo kuchukua watu Sita kwa gharama nafuu ya Shilingi Elfu 30 kwa mwaka, huku akiweka wazi nia yake ya kujenga Hospitali kubwa katika eneo la Msalato yalipo Makao Makuu ya Jeshi Hilo.

''Niseme tu nimefurahishwa na ujio wako, hii bima nimekubaliana nayo na Nina mpango wakujenga hospitali kubwa kwahiyo ninaimani Mambo yataenda vizuri na tutaboresha zaidi Afya za watu wetu"

Kwaupande wake Mganga Mfawidhi wa Zahanati ya Gereza Msalato Dkt. Mpamba Juma amesema, wamejipanga vizuri kuhakikisha wanatoa huduma nzuri kwa wananchi wa maeneo ya jirani pamoja na Wafungwa kwa kushirikiana na CHF.

''Sisi tumejipanga vizuri Sana katika kutoa huduma, hivyo kuja kwa CHF kutapelekea huduma kuwa Bora zaidi kwakuwa wanachi wengi Sasa wenye bima hii wataanza kuja katika Zahanati yetu'' alisema Mpamba.

Akizungumzia mafanikio ya ujio wake Dkt. Lutalala mratibu wa CHF amesema, anashukuru kukutana na Jenerali Mzee na kufanya nae mazungumzo chanya, ambapo amemueleza namna walivyo itangaza Zahanati ya Gereza Msalato na Mafanikio yanayoanza kuonekana kwa muda mfupi, huku akiahidi kulichukua wazo la kujenga Hospitali kubwa zaidi na kulifikisha kwa Mkuu wa Mkoa ili kupata msaada zaidi.

Monday, February 22, 2021

MKURUGENZI MKUU WA TBC DR. RYOBA AFANYA ZIARA MAKAO MAKUU YA JESHI LA MAGEREZA.

 Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Utangazaji la Tanzania (TBC) Dkt Ayubu
Rioba, leo tarehe 22,February,2021 amefanya ziara katika Makao Makuu
ya Jeshi la Magereza yaliyoko Msalato Jijini Dodoma.
Akizungunza muda mfupi baada ya kuwasili ofisini hapo Rioba amesema,
madhumuni ya ziara hiyo ni kujifunza namna  Jeshi la Magereza
limefanikiwa kujenga Makao yake Makuu kwa muda mfupi na kwa gharama
nafuu huku akisisitiza kuwa kilichofanywa na Jeshi hilo kinafaa
kuigwa.
‘‘ Hakika ziara yangu hii katika Makao Makuu ya Jeshi la Magereza
imenifanya kujifunza na kunipa mwanga zaidi wa namna ya kujipanga
kwani hata sisi TBC tunao mpango  wa kujenga ofisi zetu za shirika
hapa Dodoma. Pia nashauri taasisi nyingine hazina budi kuja kujifunza
mahali hapa.’’ Amesema mkurugenzi huyo.
Awali akimpokea mkurugenzi mkuu wa TBC kwa niaba ya Kamishna Jenerali
wa Magereza, Naibu Kamishna wa Magereza  Jeremiah Katungu amesema kuwa
amefurahi kwa ujio wake hivyo awe huru kujifunza na kuuliza pale
anapohitaji ufafanuzi.
Aidha Naibu Kamishna wa Magereza  Jeremiah Katungu Katungu amesema,
mafanikio ya ujenzi wa Makao Makuu ya Jeshi la Magereza yametokana na
mpango kabambe wa Kamishna Jenerali wa Magereza Meja Jenerali Suleiman
Mzee.
‘‘Kimsingi tunamshukuru Kamishna Jenerali wa Magereza kwa juhudi
alizozionyesha mpaka kufanikisha ujenzi wa ofisi hizi kwa muda
mfupi.’’
Pia Katungu amesema kuwa rasilimali zilizotumika kukamilisha ujenzi
huu ni za ndani tu kwani waliotumika ni maafisa na askari pamoja na
wafungwa.
Aidha amesema kuwa ujenzi huo ulianza mwezi wa tano mwaka jana hadi
kufikia mwezi Disemba mwaka jana ulikuwa umekamilika kwa kiasi kikubwa
na gharama ya ujenzi huo uligharimi kiasi cha milioni 900 taslimu.

Mkurugenzi Mkuu wa Shirika l Utangazaji Tanzania (TBC)Dr.
Riyoba akiangalia akiangalia eneo la Makao Makuu Ya Magereza alipo
fanya ziara yake akiongozana na Naibu Kamishna Wa magereza Jeremia
Katungu, Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Magereza Justine Kaziulaya na
Mandarasi wa mradi wa jengo La Makao Makuu ya Jeshi Mkaguzi wa
Magereza Belela
 
Mkurugenzi  mkuu wa Shirika la utangazaji Tbc Dr. Rioba
akiangalia Ramani ja majengo ya makao makuu ya jeshi la Magereza alipo
tembelea makao makuu hayo
 

                           Mkurugenzi wa TBC akiangalia Bustani ya maua ya Makao makuu ya
                                                                       Jeshi la Magereza

 

Mkurugrenzi Kuu wa Shirika la Utangazaji la Taifa TBC Dr. Rioba
akiangalia baadhi ya ofisi akiongozana na Naibu kamishna wa Jeshi la
Magereza Jeremiah  Katungu.
 

 

Friday, February 19, 2021

TANGAZO


 

Thursday, February 4, 2021

RAIS MAGUFULI AFURAHISHWA NA UTENDAJI KAZI WA KAMISHNA JENERALI WA MAGEREZA SULEIMAN MZEE

 

 Rais wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania Mh.Dkt John Pombe Magufuli (wa pili kushoto) akiwasili katika viwanja vya nyumba 20 Gereza Isanga kabla ya kuzizindua leo tarehe 4 Februari,2021. Wa tatu toka kulia ni Kamishna Jenerali wa Magereza Mej. Jen Suleiman Mzee

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh. Dkt, John Pombe Magufuli (wa tatu toka kushoto) akizindua nyumba 24 zilizopo katika viwanja vya Gereza Isanga Jijini Dodoma leo tarehe 4 Februari,2021.

Injinia wa Mradi wa Kiwanda cha samani kilichopo Msalato, Mrakibu Bonaza Malata(wa pili kulia) akitoa maelezo mafupi ya ujenzi wa kiwanda hicho kwa Rais Magufuli.

Rais wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania Mh.Dkt John Pombe Magufuli(wa tatu kushoto) akikata utepe katika uzinduzi wa ofisi ya Makao Makuu ya Magereza,Msalato Jijini Dodoma.Wa kwanza kushoto ni Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Mh. George Simbachawene na wa pili kulia ni Kamishna Jenerali wa Magereza Mej. Jen Suleiman Mzee.





Wednesday, January 20, 2021

TANZIA: NAIBU KAMISHNA WA MAGEREZA JULIUS SANG'UDI AFARIKI DUNIA JIJINI DODOMA.

 

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI

(Jeshi la Magereza)

TANZIA

 

 

 

Kamishna Jenerali wa Jeshi Magereza Mej. Jen Suleiman M. Mzee anasikitika kutangaza kifo cha Naibu Kamishna wa Magereza Julius Mayenga Sang’udi kilichotokea Hospitali ya Benjamin Mkapa, Jijini Dodoma leo tarehe 20 Januari, 2021.

Aidha anatoa pole kwa Familia ya Marehemu, Watumishi wote wa Jeshi la Magereza Nchini, Ndugu, Jamaa na Marafiki wote walioguswa na msiba huu.

Jeshi  la Magereza kwa kushirikiana na familia ya Marehemu inaendelea kuratibu taratibu za Mazishi nyumbani kwake Kisasa nyumba 300, Dodoma.

Mwili wa Marehemu unatarajiwa kusafirishwa Ijumaa tarehe 22 Januari,2021 na Mazishi yatafanyika Mkoani Simiyu Kijiji cha Ikulilo – Mwandete Jumamosi tarehe 23 Januari,2021.

Mwenyezi Mungu ailaze Roho ya Marehemu mahala pema peponi, Amen.

 

Imetolewa na Msemaji wa Jeshi la Magereza,

Kitengo cha Habari na Mawasiliano ya Umma,

Dodoma.

Saturday, January 16, 2021

MAGEREZA WAOKOA BILIONI 11 ZA CHAKULA CHA WAFUNGWA.


Na Mwandishi Wetu


Jeshi la Magereza nchini limeokoa jumla ya Shilingi Bilioni 11, ikiwa
ni gharama ya chakula cha wafungwa tangu lianze kujitegemea kwa
chakula ikiwa  ni maelekezo ya Rais  Dkt. John Pombe Magufuli ya
kulitaka jeshi hilo litumie nguvu kazi ya wafungwa ilionao kuzalisha
chakula.

Akizungumza leo katika ziara ya Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya
Nchi,iliyofanyika katika Makao Makuu Mapya ya Jeshi hilo ,Msalato
jijini Dodoma, Kamishna Jenerali wa Magereza, Suleiman Mzee amesema
walikuwa wanatumia Shilingi Bilioni Moja kila mwezi kulipa wazabuni wa
chakula waliokuwa wanaliuzia chakula  jeshi hilo.

“Sasa hivi tunajitegemea asilimia kubwa kwa chakula, Serikali kabla ya
mwezi wa tatu mwaka jana kila mwezi kulikua kuna deni la Bilioni Moja,
lakini baada ya mwezi huo wa tatu sasa tunaokoa kiasi hicho cha fedha
shilingi bilioni moja na mpaka sasa tuna miezi kumi na moja
tunajilisha wenyewe kupitia shirika la magereza” alisema CGP Mzee

Akizungumza wakati wa ziara hiyo, Naibu Waziri, Khamis Hamza Chilo
alilipongeza Jeshi la Magereza kwa kutekeleza vyema agizo la Rais
Magufuli ikiwa sambamba na ujengaji wa kiwanda kikubwa cha samani
ambapo mpaka kukamilika kwake kitagharimu shilingi Bilioni
1,101,743,123/=

“Niwapongeze kwa hatua mbalimbali za maendeleo ambazo zingine
nimeshuhudia mwenyewe,lakini kubwa kuweza kujitegemea kwa chakula cha
wafungwa hali iliyopelekea kuokoa kiasi kikubwa cha fedha ambacho
kinabaki humu humu ndani na mnakitumia kwa shughuli zingine za
maendeleo hongereni sana” alisema Naibu Waziri Chilo

Kamishna Jenerali wa Magereza Mej. Jen. S.M Mzee akielezea jambo kwa Naibu Waziri wa mambo ya ndani  ya Nchi Mh. Khamis Hamza Chilo (MB) wakati wa Ziara ya Kikazi Makao Makuu ya Jeshi la Magereza  Jijini Dodoma jana tarehe 15 Jan, 2021.

Kamishna Jenerali  Suleiman M. Mzee (kushoto  akimpa taarifa fupi Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani Mh. Khamis Hamza Chilo  alipotembelea Makao Makuu ya Magereza Jijini Dodoma.

Naibu waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Mh. Khamis Hamza Chilo (MB) akipanda Mti mbele ya Ofisi ya Ofisi ya  Makao Makuu Ya Magereza eneo la Msalato Jijini Dodoma.

Naibu waziri wa Mambo ya Ndani Mh. Khamis Chilo akitoa maelekezo alipotembelea Makao Makuu ya Magereza sehem ya Kiwanda cha Samani Msalato jijini Dodoma.

Mrakibu msaidizi wa Magereza Malima akifafanua jambo mbele ya Naibu waziri wa Mambo ya ndani ya Nchi Mh. Khamis Chilo katika Mashine za Kiwanda cha Samani Msalato jijini Dodoma.

Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Mh. Khamis Chilo (kushoto,mbele) akipokewa na Mwenyeji wake Kamishna Jenerali wa Magereza Mej. Jen. Suleiman Mzee ( kulia, mbele) alipotembelea Makoa Makuu ya Magereza katika ziara ya kikazi jijini Dodoma jana.

Naibu waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Mh. Khamis Chilo akikagua gwaride la heshima lilioandalia kwa ajili yake wakati  wa Ziara ya kikazi Makao makuu ya Magereza Jijini Dodoma.