Mojawapo ya Jukumu la Jeshi la Magereza ni kuwapeleka mahakamani mahabusu na kuwarudisha magerezani.

Gadi ya askari Wanawake na Wanaume wa Jeshi la Magereza katika Maadhimisho ya Sherehe za Kitaifa.

Ng'ombe bora wa Nyama na Maziwa ni sehemu ya miradi ya Uzalishaji inayoendeshwa na kusimamiwa na Jeshi la Magereza nchini.

Sehemu ya Mashamba makubwa yanayoendeshwa na Jeshi la Magereza: Shughuli za Kilimo cha Mashamba makubwa, madogo na bustani za mboga mboga ni moja ya shughuli za Magereza katika kuwafunza wafungwa namna ya kujitegemea mara wamalizapo vifungo vyao.

Baadhi wa wafungwa katika Kiwanda cha Ushonaji nguo cha Gereza Kuu Ukonga wakiwa kazini: Shughuli za Ushonaji wa nguo ni moja ya eneo ambalo wafungwa hupata huduma za urekebishwaji kwa vitendo.

Tuesday, August 29, 2017

VYOMBO VYA ULINZI NA USALAMA NCHINI VYAITIKIA WITO WA RAIS MAGUFULI KUNUNUA BUTI KATIKA KIWANDA CHA VIATU KARANGA, MOSHI

Mkuu wa Divisheni ya Huduma za Urekebishaji, Naibu Kamishna wa Magereza, Tusekile Mwaisabila akisalimiana na Maafisa Waandamizi wa Jeshi la Magereza mara baada ya kuwasili katika ziara Maalum ya kukagua maboresho mbalimbali katika Kiwanda cha Viatu cha Gereza Kuu Karanga Moshi leo Agosti 29, 2017(wa kwanza kulia) ni Mkuu wa Gereza Kuu Karanga – Moshi, Kamishna Msaidizi wa Magereza, Leonard Mushi.
Mkuu wa Divisheni ya Huduma za Urekebishaji, Naibu Kamishna wa Magereza, Tusekile Mwaisabila akiongea na Maafisa Waandamizi wa Jeshi la Magereza Mkoani Kilimanjaro katika Kiwanda cha viatu cha Karanga Moshi(kushoto) ni Mkuu wa Magereza Mkoa wa Kilimanjaro, Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Magereza, Hassan Mkwiche.
Naibu Kamishna wa Magereza, Tusekile Mwaisabila akiangalia Buti la Jeshi lililotengenezwa katika Kiwanda cha Viatu Karanga Moshi.
Viatu aina ya Buti za Jeshi zinazotengenezwa katika Kiwanda cha Viatu Karanga Moshi.
Naibu Kamishna wa Magereza, Tusekile Mwaisabila akikagua eneo la mradi wa Ubia kati ya Jeshi la Magereza na Mfuko wa hifadhi ya jamii wa PPF ambapo katika eneo hilo kutajengwa mradi wa Kiwanda kipya cha viatu na bidhaa za ngozi katika eneo hilo.
Mkuu wa Divisheni ya Huduma za Urekebishaji, Naibu Kamishna wa Magereza, Tusekile Mwaisabila akifyatua tofali zitakazotumika kujengea nyumba za askari katika Gereza Kuu Karanga, Moshi kama inavyoonekana katika picha.

(Picha zote na Lucas Mboje wa Jeshi la Magereza).

Monday, August 28, 2017

WAZIRI MWIGULU NCHEMBA AZINDUA NYUMBA ZA MAKAZI YA ASKARI MAGEREZA, GEREZA KUU ARUSHA

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe. Mwigulu Nchemba(Mb) akisalimiana na Maafisa Waandamizi wa Jeshi la Magereza Mkoani Arusha alipowasili katika viwanja vya Gereza Kuu Arusha katika ziara Maalum ya uzinduzi wa nyumba za makazi ya askari wa Gereza Kuu Arusha leo Agosti 28, 2017 ambapo nyumba hizo zimejengwa hivi karibuni na Uongozi wa Jeshi hilo kwa kutumia fedha iliyopatikana katika miradi ya Shirika la Magereza. Kushoto kwa Waziri ni Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza nchini Dkt. Juma Malewa.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe. Mwigulu Nchemba akikata utepe kuashiria uzinduzi rasmi wa nyumba za makazi ya askari wa Gereza Kuu Arusha, leo Agosti 28, 2017(Wa pili kulia) ni Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza nchini Dkt. Juma Malewa(wa tatu toka kulia) ni Mbunge wa Jimbo la Arusha Mjini, Mhe. Gobless Lema.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe. Mwigulu Nchemba(katikati) akikagua nyumba za askari Magereza zilizojengwa kwa kutumia fedha iliyopatikana katika miradi ya Shirika la Magereza(kushoto) ni Mkuu wa Magereza Mkoa wa Arusha, Khamis Nkubasi.
 Muonekano wa nyumba zilizozinduliwa za makazi ya askari wa Gereza Kuu Arusha.
Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza nchini Dkt. Juma Malewa akitoa maelezo mafupi kabla ya kumkaribisha Mgeni rasmi kutoa hotuba fupi ya uzinduzi wa nyumba za makazi ya askari wa Gereza Kuu Arusha.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe. Mwigulu Nchemba(Mb) akitoa hotuba mbele ya Maofisa na askari wa Magereza Mkoani Arusha katika hafla ya uzinduzi wa nyumba za makazi ya askari wa Gereza Kuu Arusha.
Baadhi ya Maafisa na Askari wa Magereza Mkoani Arusha waliohudhuria hafla ya uzinduzi wa nyumba za makazi ya askari wa Gereza Kuu Arusha.
Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza nchini Dkt. Juma Malewa akimpongeza Mkuu wa Magereza Mkoa wa Arusha, Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Magereza, Khamis Nkubasi mara baada ya uzinduzi wa nyumba hizo(katikati) ni Naibu Kamishna wa Magereza, Tusekile Mwaisabila.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe. Mwigulu Nchemba(Mb) akisalimiana na Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mhe. Mrisho Gambo(kulia) alipomtembelea ofsini kwake leo kabla ya uzinduzi rasmi wa nyumba za makazi ya askari wa Gereza Kuu Arusha.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe. Mwigulu Nchemba(katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Maafisa na Askari ambao ni mafundi ujenzi waliojenga nyumba hizo(waliosimama) mara baada ya hafla ya uzinduzi wa nyumba hizo. Wengine walioketi ni Kamishna Jenrerali wa Magereza, Dkt. Juma Malewa(wa tatu toka kushoto), wa pili kushoto ni  Mbunge wa Jimbo la Arusha Mjini, Mhe. Gobless Lema

(Picha zote na Lucas Mboje wa Jeshi la Magereza).

Friday, August 11, 2017

BURIANI MSTAAFU SACP OMARI MTIGA

Kamishna Mkuu Mstaafu wa Jeshi la Magereza, Kamanda Simon A. Mwanguku akiweka saini kwenye kitabu cha maombolezo nyumbani kwa marehemu.
Kamishna Mstaafu wa Huduma za Urekebishaji, Kamanda Deonis Chamulesile akimpokea Kamishna Mkuu mstaafu, Kamanda Alhaj Jumanne  Mangara aliyeambata na Naibu Kamishna  Mstaafu Green E. Mwaibako.
Kamishna Mkuu Mstaafu wa Jeshi la Magereza, Kamanda Alhaj Jumanne  Mangara akiweka saini kwenye kitabu cha maombolezo nyumbani kwa marehemu.
Kamishna mstaafu wa Huduma za Urekebishaji wa Jeshi la Magereza,Kamanda Deonis Chamulesile akiweka saini kwenye kitabu cha maombolezo nyumbani kwa marehemu.
Naibu Kamishna wa Jeshi la Magereza,aliyemwakilisha Kamishna Jenerali wa Magereza, mama Tusikile Mwaisabila, akiweka saini kwenye kitabu cha maombolezo nyumbani kwa marehemu.
 
Naibu Kamishna wa Magereza ambaye ni Mkuu wa Magereza Mkoa wa Dar es Salaam,Augustino Mboje akiweka saini kitabu cha maombolezo.
Naibu Kamishna Mstaafu wa Magereza, Green E.Mwaibako akiweka saini kwenye kitabu cha maombolezo nyumbani kwa marehemu.
Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Magereza,ambaye ni Mnadhimu wa Jeshi, Deogratius Lwanga, akiweka saini kwenye kitabu cha maombolezo.
Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Magereza ambaye ni Mkuu wa Magereza Mkoa wa Pwani, Boyd P. Mwambingu, akiweka saini kwenye kitabu cha maombolezo.
Mwili wa Marehemu Kamishna Msaidizi Mwandamizi mstaafu wa Magereza Omari Mtiga ukiwasili nyumbani kwake Segerea.
Mke wa Marehemu Kamishna Msaidizi Mwandamizi mstaafu wa Magereza Omari Mtiga akiwa na wanae,wakiomba dua kwenye jeneza lenye mwili wa marehemu.
Mama wadogo na shangazi wa marehemu wakiomba dua mbele ya mwili wa marehemu Omari Mtiga.
Paredi maalum la Makamishna Wasaidizi Waandamizi wa Jeshi la Magereza likitoa heshima ya saluti mbele ya mwili wa marehemu.
Naibu Kamishna Mstaafu, John Nyoka akitoa salamu za maombolezo kwa wafiwa na waombolezaji kwenye msiba.
 Naibu Kamishna Tusikile Mwaisabila akitoa salamu kwa niaba ya Kamishna Jenerali wa Magereza.
Naibu Kamishna Tusikile Mwaisabila akitoa rambirambi kwa niaba ya Kamishna Jenerali wa Magereza kwa motto mkubwa wa Marehemu.
 Sehemu ya umati wa waombolezaji waliohudhuria msiba huo nyumbani kwa marehemu Segerea.
Waombolezaji wakipata chakula cha mchana kabla ya kwenda kumzika Kamishna Msaidizi Mwandamizi mstaafu wa Magereza Omari Mtiga.
Sehemu ya waombolezaji wakina mama  wakiwa na majonzi kwenye msiba huo huko Segerea nyumbani kwa marehemu.
Kamishna Msaidizi Mwandamizi mstaafu wa Magereza, Dk. Rajabu Mbiro(wan ne toka kulia) akiwa na Mkuu wa Gereza la Keko, Kamishna Msaidizi Abdalah Kiangi na makamanda wengine, wakizungumza mawili matatu kwenye msiba.
Makamishna Wakuu wastaafu,pamoja na makamnda wengine wakipita kwenye jeneza la marehemu kutoa heshima zao za mwisho.
Viongozi wa dini ya kiislam na baadhi ya waumini wa dini hiyo wakimsalia marehemu na kumuombea dua kwa Mwenyezi Mungu.
Paredi maalum la Makamishna Wasaidizi Waandamizi wa Jeshi la Magereza likitoa heshima ya saluti mbele ya mwili wa marehemu kabla ya kuupeleka kwenye kaburi.
Mwili wa Marehemu Kamishna Msaidizi Mwandamizi msaafu wa Magereza Omari Mtiga ukipelekwa kwenye sehemu ya kaburi lililoandaliwa kwa ajili ya mazishi hayo.
Shughuli za kumzika Kamishna Msaidizi Mwandamizi mstaafu Omari Mtiga zikiendelea makaburini.
Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Magereza ambaye ni Mkuu wa Magereza Mkoa wa Morogoro , Afande Ramadhan Nyamka akiweka udongo juu ya kaburi.
Paredi maalum lililoanda kwa mazishi ya Kamishna Msaidizi Mwandamizi msaafu wa Magereza ,Marehemu Omari Mtiga, liktoa heshima ya mwisho ya kijeshi.
Sehemu ya kikosi cha paredi maalum la mazishi kikitoa heshima ya marehemu,kamanda Kamishna Msaidizi Mwandamizi mstaafu wa Magereza Omari Mtiga, kwa kulipua risasi baridi hewani.
Sehemu ya Makamanda na waombolezaji waliohudhuria makaburini wakitoa heshima zao za mwisho baada ya kumzika kamanda Kamishna Msaidizi Mwandamizi mstaafu wa Magereza Omari Mtiga.



Kamishna Msaidizi wa Mwandamizi wa Magereza (SACP) Mstaafu  Mtiga Hussein Omari aagwa na kuziwa rasmi katika makaburi ya Kijitonyama Jijini Dar es salaam.

SACP Mtiga Omari alifariki tarehe 07. 08. 2017 katika Hosiptali ya Taifa Muhimbili alipokuwa amelazwa kwa matibabu.

Marehemu SACP Mtiga alizaliwa tarehe 25.09.1956 katika kijiji cha Chumbi Kata ya Rusembe Tarafa ya Muhoro wilaya ya Rufiji Mkoani Pwani.

Alijiunga na Jeshi la Magereza mwaka 1979 akitokea Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) alilojiunga nalo kwa mujibu wa sheria baada ya kuhitimu elimu ya kidato cha sita (VI) katika shule ya sekondari ya wavulana Tabora (Tabora Boy’s)

Marehemu Mtiga alipata mafunzo ya ndani na nje ya kwa ngazi na nyakati tofauti ikiwa ni pamoja na Mafunzo ya Uongozi Dara la Pili na la Juu kutoka Chuo cha Maafisa  wa Magereza Ukonga (kwa sasa Chuo cha Taaluma ya Urekebishaji Tanzania, Stashahada ya Uandishi wa Habari kutoka TSJ na Stashahada ya Uhusiano wa Kimataifa katika chuo cha Diplomasia Kurasini.

Mafunzo mengine ni Intelligence Security kutoka chuo cha Galilee nchini Israel na mafunzo mafupi kama vile Correctional Intelligence Management,Diplomatic Security Services nakadhalika.

SACP Mtiga ndani ya Jeshi la Magereza alifanya kazi katika vituo tofauti tofauti ikiwa ni pamoja na Singida, Iringa,Uyui Tabora,Tarime na Musoma Mara na Makao Makuu kwa nyakati tofauti. Marehemu Mtiga nakumbukwa zaidi akiwa Mkuu wa Kitengo cha Intelijensia na Operesheni, Habari na Msemaji wa Jeshi la Magereza.

Marehemu alistaafu kazi rasmi mwezi 07.2016 akiwa Mkuu wa Magereza wa Mkoa wa Kagera (RPO). Ameacha na watoto watano.Wakiume watatu na wakike 2.

Kamishna Jenerali wa Magereza kwa niaba ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania anatoa pole kwa familia, ndugu, jamaa, marafiki na wote walioguswa na msiba huu.
BWANA ALITOA NA BWANA AMETWAA JINA LAKE LIBARIKIWE.

 

Saturday, August 5, 2017

APPLICATION FOR ADMISSION IN THE CERTIFICATE PROGRAMME IN CORRECTIONAL SCIENCE (NTA LEVEL 5), ACADEMIC YEAR, 2017/2018.

APPLICATION FOR ADMISSION IN THE CERTIFICATE PROGRAMME IN CORRECTIONAL SCIENCE (NTA LEVEL 5), ACADEMIC YEAR, 2017/2018.
The Commandant of Tanzania Correctional Training Academy wishes to invite application to pursue Technician Certificate Programme in Correction Science (NTA Level 5) for Academic year 2017/2018. The programme will be conducted in one Academic year of 34 weeks. Eligible applicants should possess the following qualifications:

1.    An employee of Prison Service of the rank of Warder/wardress to Staff Sergeant.
2.  A person of good character whom for the past three years has not been convicted of any disciplinary offence.
3.    Who have served in the Prisons Service for not less than three (3) years.
4.    Approved by Government chemist to be physically fit to undergo studies.
5.  A holder of form six certificates (ACSEE) with a minimum of one principal Pass and Two subsidiary Passes; OR
6.    A holder of form four certificates (CSEE) should have at least (5) pass of “D” in non religious subjects with possession of any Basic Technician Certificate (NTA level 4) or a certificate in any field related to prisons/correction works from any recognized college.

Application Forms are available at “www.magereza.go.tz
Application form and copies of relevant certificates should be SCANNED and send to the TCTA Commandant through the following E-MAIL below:
E-Mail address:  tcta@magereza.go.tz
The deadline for receiving application will be not later than 18th August, 2017.
NB:
      For any inquiry please contact the TCTA – REGISTRAR/ADMISSION OFICER
      Mobile: 0787 829750
      Email:  peter.ndunguru@gmail.com
THE COMMANDANT,
TANZANIA CORRECTIONAL TRAINING ACADEMY,
P.O. BOX 4283,
DAR ES SALAAM.


Issued by;

The Commandant,
Tanzania Correctional Training Academy (TCTA)
Dated: 4th August, 2017