Mojawapo ya Jukumu la Jeshi la Magereza ni kuwapeleka mahakamani mahabusu na kuwarudisha magerezani.

Gadi ya askari Wanawake na Wanaume wa Jeshi la Magereza katika Maadhimisho ya Sherehe za Kitaifa.

Ng'ombe bora wa Nyama na Maziwa ni sehemu ya miradi ya Uzalishaji inayoendeshwa na kusimamiwa na Jeshi la Magereza nchini.

Sehemu ya Mashamba makubwa yanayoendeshwa na Jeshi la Magereza: Shughuli za Kilimo cha Mashamba makubwa, madogo na bustani za mboga mboga ni moja ya shughuli za Magereza katika kuwafunza wafungwa namna ya kujitegemea mara wamalizapo vifungo vyao.

Baadhi wa wafungwa katika Kiwanda cha Ushonaji nguo cha Gereza Kuu Ukonga wakiwa kazini: Shughuli za Ushonaji wa nguo ni moja ya eneo ambalo wafungwa hupata huduma za urekebishwaji kwa vitendo.

Wednesday, October 22, 2014

Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza akabidhi zawadi ya basi dogo Bwawani Sekondari katika mahafali ya kumi na moja ya kidato cha nne yaliyofanyika mkoani Pwani

Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza, John Casmir Minja(kulia) akikabidhi funguo za Basi dogo kwa Kaimu Mkuu wa Shule ya Sekondari Bwawani, Mrakibu Mwandamizi wa Magereza, Emmanuel Lwinga(kushoto). Basi hilo litatumiwa na Wanafunzi katika ziara mbambali za Mafunzo hivyo kuondoa kero kubwa ya Usafiri shuleni hapo.
Kaimu Mkuu wa Shule ya Sekondari Bwawani Sekondari, Mrakibu Mwandamizi wa Magereza, Emmanuel Lwinga akijaribisha kuwasha gari jipya lililokabidhiwa na Kamishna Jenerali wa Magereza, John Casmir Minja(hayupo pichani) katika Mahafali ya Kumi na moja ya Kidato cha Nne Bwawani Sekondari yaliyofanyika leo Oktoba 22, 2014.
Muonekano wa Basi dogo lenye Na. MT. 0341 lililokabidhiwa leo Oktoba 22, 2014 na Kamishna Jenerali wa Magereza, John Casmir Minja(hayupo pichani) katika Mahafali ya Kidato cha Nne ya Shule ya Sekondari Bwawani, Mkoani Pwani. Basi hilo litatumiwa na Wanafunzi wa Bwawani Sekondari katika ziara mbalimbali za Mafunzo.
Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza, John Casmir Minja(aliyevaa skafu) akiwa meza Kuu amesimama na Viongozi mbalimbali Waalikwa wakati Wahitimu Wakiimba Wimbo Maalum wa Shule katika Mahafali ya Kumi na Moja ya Kidato cha Nne Bwawani Sekondari leo Oktoba 22, 2014(wa pili kushoto) ni Kamishna wa Fedha na Utawala wa Jeshi la Magereza, Gaston Sanga(wa kwanza kushoto) ni Mkuu wa Magereza Mkoani Morogoro, Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Magereza, Kato Rugainunula (wa kwanza kulia) ni Kaimu Mkuu wa Shule ya Bwawani Sekondari, Mrakibu Mwandamizi wa Magereza, Emmanuel Lwinga.
Kamishna Jenerali wa Magereza Nchini, John Casmir Minja akikabidhi cheti kwa Mhitimu wa Kidato cha Nne katika Mahafali ya Kidato cha Nne Bwawani Sekondari leo Oktoba 22, 2014. Jumla ya Wahitimu 95 wametunukiwa cheti cha kuhitimu Elimu ya Kidato cha Nne katika Shule hiyo inayomilikiwa na Jeshi Magereza, Mkoani Pwani.
Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza John Casmir Minja akitoa hotuba yake fupi katika Mahafali ya Kumi na Moja ya Kidato cha Nne Bwawani Sekondari yaliyofanyika leo Oktoba 22, 2014 Mkoani Pwani.
Sehemu ya Wahitimu katika Mahafali ya Kumi na Moja ya Kidato cha Nne, Bwawani Sekondari wakisikiliza hotuba ya Mgeni rasmi, Kamishna Jenerali wa Magereza, John Casmir Minja(hayupo pichani).
Kikundi cha Wasanii kinachoundwa na Wanafunzi wa Bwawani Sekondari kikijiandaa kutumbuiza mbele ya Mgeni rasmi katika Mahafali ya Kumi na Moja ya Kidato cha Nne Shule ya Bwawani Sekondari, Mahafali hayo yamefanyika leo Oktoba 22, 2014, Mkoani Pwani.
Mama mzazi wa Mhitimu wa Kidato cha Nne kutoka familia ya Kifugaji ya Kimasai akimbusu mkono Mtoto wake ambaye amehitimu Elimu ya Kidato cha Nne katika Shule inayomilikiwa na Jeshi la Magereza, Bwawani Sekondari iliyopo Mkoani Pwani. Mahafali hayo yamefanyika leo Oktoba 22, 2014.
Kamishna Jenerali wa Magereza Nchini, John Casmir Minja(katikati) akiwa na Wahitimu wa Kidato cha Nne katika Mahafali ya Kumi na moja ya Kidato cha Nne ya Shule ya Sekondari Bwawani inayomilikiwa na Jeshi la Magereza. Mahafali hayo yamefanyika leo Oktoba 22, 2014 katika Bwalo la Bwawani Sekondari, Mkoani Pwani

(Picha na Lucas Mboje wa Jeshi la Magereza).

Monday, October 20, 2014

Kamishna Jenerali wa Magereza Minja awaongoza waombolezaji kuuaga mwili wa aliyekuwa afisa mnadhimu mkuu msaidizi wa Jeshi la Magereza, Jijini Dar es Salaam

Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza, John Casmir Minja akisaini katika Kitabu cha Maombolezo nyumbani kwa aliyekuwa Afisa Mnadhimu Mkuu Msaidizi wa Jeshi la Magereza, Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Magereza, Stephen Nzawila ambaye amefariki Jumapili tarehe 19 Oktoba, 2014 katika Hospitali ya Taifa Muhimbili, Dar es Salaam.
 
Mwili wa aliyekuwa Afisa Mnadhimu Mkuu Msaidizi wa Jeshi la Magereza, Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Magereza, Stephen Nzawila ukiwa umebebwa na Maafisa Waandamizi wa Jeshi la Magereza kabla ya kuagwa rasmi leo Oktoba 20, 2014 nyumbani kwake, Ukonga Dar es Salaam.
Kamishna Jenerali wa Magereza, John Casmir Minja(suti nyeusi) akiwa amesimama wakati mwili wa aliyekuwa Afisa Mnadhimu Mkuu Msaidizi wa Jeshi la Magereza, Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Magereza, Stephen Nzawila ulipowasili tayari kwa kuuagwa rasmi nyumbani kwake Ukonga, Dar es Salaam leo Oktoba 20, 2014(wa kwanza kushoto) ni Kamishna Mkuu Mstaafu wa Magereza, Nicas Banzi(wa pili kushoto) ni Kamishna Mkuu Mstaafu wa Magereza, Jumanne Mangara(wa kwanza kulia) ni Kamishna wa Fedha na Utawala, Gaston Sanga(wa pili kulia) ni Kamishna wa Sheria na Uendeshaji wa Magereza, Dkt. Juma Malewa
 Mchungaji wa Kanisa la Moravian lililopo Ukonga, Banana Relini Hansi Mwakijoja akiwaongoza Waombolezaji kwa sala kabla ya kuuaga rasmi mwili wa aliyekuwa Afisa Mnadhimu Mkuu Msaidizi wa Jeshi la Magereza ambaye amefariki Jumapili Oktoba 19, 2014 katika Hospitali ya Taifa Muhimbili, Dar es Salaam.
 Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza, John Casmir Minja akitoa heshima za mwisho kwa aliyekuwa Afisa Mnadhimu Mkuu Msaidizi wa Jeshi la Magereza ambaye amefariki Jumapili Oktoba 19, 2014 katika Hospitali ya Taifa Muhimbili, Dar es Salaam.
 Baadhi ya Maofisa na Askari wa Jeshi la Magereza wakiwa wamejipanga katika mstari tayari kuuaga mwili wa aliyekuwa Afisa Mnadhimu Mkuu Msaidizi wa Jeshi la Magereza leo Oktoba 20, 2014 Ukonga, Jijini Dar es Salaam. Mwili wa Marehemu unatajiwa kusafirishwa kesho kuelekea Tutuo Wilayani Sikonge, Mkoani Tabora kwa Mazishi.
 Mke wa Aliyekuwa Afisa Mnadhimu Mkuu Msaidizi wa Jeshi la Magereza akiwa na majonzi makubwa na waombolezaji kabla ya kuuaga rasmi mwili wa mume wake ambaye amefariki Jumapili Oktoba 19, 2014 katika Hospitali ya Taifa Muhimbili, Dar es Salaam.
 Sehemu ya Waombolezaji waliojitokeza kuuaga mwili wa aliyekuwa Afisa Mnadhimu Mkuu Msaidizi wa Jeshi la Magereza wakisikiliza kwa makini wasifu wa Marehemu kabla ya kuuaga rasmi leo Oktoba 20, 2014 Ukonga, Dar es Salaam.
 Bendi ya Jeshi la Magereza ikitumbuiza katika hafla fupi ya kuuaga mwili wa aliyekuwa Afisa Mnadhimu Mkuu Msaidizi wa Jeshi la Magereza, Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Magereza, Stephen Nzawila ambaye amefariki Jumapili Oktoba 19, 2014 katika Hospitali ya Taifa Muhimbili, Dar es Salaam

(Picha zote na Lucas Mboje wa Jeshi la Magereza).

TANZIA

  JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI
(Jeshi la Magereza)

TANZIA
Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza, John Casmir Minja anasikitika kutangaza kifo cha aliyekuwa Afisa Mnadhimu Mkuu Msaidizi wa Jeshi, Makao Makuu ya Jeshi la Magereza, Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Magereza, Stephen J.K. Nzawila kilichotokea Jijini Dares Salaam tarehe 19 Oktoba, 2014.

Jeshi la Magereza kwa kushirikiana na Familia ya Marehemu linaratibu mazishi yake ambapo mwili wa marehemu utaagwa rasmi leo tarehe 20 Oktoba, 2014 saa 10:00 jioni nyumbani kwake Magereza Ukonga, Dar es Salaam kabla ya kusafirishwa kuelekea nyumbani kwao Tutuo Wilayani Sikonge, Mkoani Tabora kwa mazishi.

          Mwenyezi Mungu ailaze roho ya marehemu mahali pema peponi;
AMINA

Tuesday, October 7, 2014

President of the Asian Injury Prevention Foundation (AIP)/ Global Helmet Vaccine Initiative holds official talks with the permanent secretary in the Prime Minister’s office in Dar es Salaam

 The Permanent Secretary in the Prime Minister's Office, Dr. Florens Turuka(centred) and the President of Assian Injury Prevention Foundation, Creig Craft(third right) during the Official talks held in Prime Minister's Office this afternoon concerns about the support of government to the Helmet factory project expected to take off at Ukonga Central Prison in Dar es Salaam.
 President of Assian Injury Prevention Foundation, Creig Craft(third right) in conversation with his host The Permanent Secretary in the Prime Minister's Office, Dr. Florens Turuka(not in picture). The first right is the Agro Economist, Superitendent of Prisons, Uswege Mwakahesya(centered) is the Chief Executive Officer of the Helmet Vaccine Inniciative Tanzania, Mr. Alpherio Nchimbi.
 The Permanent Secretary in the Prime Minister's Office, Dr. Florens Turuka held talks concerns the support of government to the Helmet factory project expected to take off at Ukonga Central Prison in Dar es Salaam.
 The Chief Executive Officer of Tanzania Prisons Cooperation Sole, Senior Assistant Commissioner of Prisons, John Masunga(right) listens a comment from the The Permanent Secretary in the Prime Minister's Office, Dr. Florens Turuka(left) is Mr. Asanterabi Sang'enoi, Assistant Director in the Prime Minister's Office.
 The Permanent Secretary in the Prime Minister's Office, Dr. Florens Turuka(right) shares a light moment with the  Chief Executive Officer of Tanzania Prisons Cooperation Sole, Senior Assistant Commissioner of Prisons, John Masunga(left)after an Official talks about the support of government to the Helmet factory project expected to take off at Ukonga Central Prison in Dar es Salaam.
 The Permanent Secretary in the Prime Minister's Office, Dr. Florens Turuka(centred) in a group photo with the President of Assian Injury Prevention Foundation, Creig Craft(third right) during the Official talks held in Prime Minister's Office in Dar es Salaam this afternoon. Others are Senior Prisons Officers' who accompanied the President.
The Permanent Secretary in the Prime Minister's Office, Dr. Florens Turuka(right) accompany the President of Assian Injury Prevention Foundation, Creig Craft(left) after the Official talks held in Prime Minister's Office this afternoon concerns about the support of government to the Helmet factory project expected to take off at Ukonga Central Prison in Dar es Salaam.

Thursday, October 2, 2014

Kamishna Jenerali wa Magereza Nchini Tanzania afunga rasmi mafunzo ya ulinzi wa amani kwa maafisa magereza toka nchi za SADC, mkoani Kilimanjaro


 Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza, John Casmir Minja(katikati meza Kuu) akisikiliza maelezo mafupi toka kwa Mratibu wa Mafunzo ya Ulinzi wa Amani, Kanali Sambulo Ndrovu(hayupo pichani) kabla ya kufunga rasmi Mafunzo hayo leo Oktoba 02, 2014. Mafunzo hayo yamefanyika kwa wiki mbili katika Chuo cha Maafisa Uhamiaji, Moshi Mkoani Kilimanjaro(wa pili kushoto) ni Mkuu wa Kituo cha Mafunzo cha SADC, Bregedia Jenerali Christopher Chellah(wa pili kulia) ni Mratibu Msaidizi wa Mafunzo hayo Kamishna Msaidizi wa Magereza toka Nchini Zimbabwe, Didmas Chimvura(wa kwanza kulia) ni Mkuu wa Magereza Mkoani Kilimanjaro, Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Magereza, Venant Kayombo.
 Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza Tanzania, John Casmir Minja akitoa hotuba fupi ya ufungaji wa Mafunzo ya Ulinzi wa Amani ambayo yamefanyika kwa wiki mbili katika Chuo cha Maafisa Uhamiaji, Moshi Mkoani Kilimanjaro ambapo jumla ya Maafisa Magereza 27 toka Nchi za SADC ikiwemo Tanzania, Botswana, Afrika Kusini, Mauritius, Swaziland na Zimbabwe wameshiriki kikamilifu Mafunzo hayo.
 Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza, John Casmir Minja akikabidhi cheti kwa Mmoja wa Washiriki wa Mafunzo ya Ulinzi wa Amani, Mkaguzi wa Magereza Nchini Tanzania, Pendo Kazumba. Mafunzo hayo yamefanyika kwa wiki mbili na yameendeshwa na Kituo cha Mafunzo cha SADC kwa kushirikiana na Jeshi la Magereza Tanzania(kushoto) ni Mkuu wa Kituo cha Mafunzo cha SADC Bregedia Jenerali Christopher Chellah.
 Wakufunzi wa Mafunzo hayo wakisikiliza hotuba fupi ya ufungaji wa Mafunzo ya Ulinzi wa Amani kwa Maafisa Magereza toka Nchi za SADC. Jumla ya Wahitimu 27 toka Nchi za SADC wameshiriki Mafunzo hayo kikamilifu katika Chuo cha Uhamiaji, Moshi Mkoani Kilimanjaro(wa kwanza kulia) ni Mratibu wa Mafunzo hayo, Kanali Sambulo Ndlovu toka Zimbabwe(wa pili kulia) ni Mkufunzi toka Tanzania, Kamishna Msaidizi wa Magereza, Charles Novart(wa tatu kushoto) ni Mkufunzi toka Tanzania, Ahmad Mwidadi(wa pili kulia) ni Mkufunzi toka Zambia, Mrakibu wa Polisi Nchini Zambia, Edward Njovu.
Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza Tanzania, John Casmir Minja akifanya mahojiano Maalum na Waandishi wa Habari toka Vyombo vya TBC1 na ITV Mkoani Kilimanjaro mara tu baada ya kufunga rasmi Mafunzo ya Ulinzi wa Amani kwa Maafisa Magereza toka Nchi za SADC leo Oktoba 2, 2014 Chuo cha Maafisa Uhamiaji, Moshi Mkoani Kilimanjaro.


Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza Nchini Tanzania, John Casmir Minja(wa sita kulia) na Mkuu wa Kituo cha Mafunzo cha SADC, Bregedia Jenerali Christopher Chellah(wa tano kulia) wakiwa katika picha ya pamoja na Maafisa Magereza Wanawake toka Nchi za SADC ambao wameshiriki kikamilifu Mafunzo ya wiki mbili ya Ulinzi wa Amani katika Chuo cha Maafisa Uhamiaji, Moshi Mkoani Kilimanjaro
Mkuu wa Kituo cha Mafunzo cha SADC, Bregedia Jenerali Christopher Chellah(kushoto) akiteta jambo na Kamishna Jenerali wa Magereza Nchini Tanzania, John Casmir Minja(kulia) mara tu baada ya kufunga rasmi Mafunzo ya Ulinzi wa Amani kwa Maafisa Magereza toka Nchi za SADC(katikati) ni Mmoja wa Washiriki wa Mafunzo hayo toka Nchini Tanzania, Mkaguzi wa Magereza, Pendo Kazumba.

Kamishna Jenerali wa Magereza, John Casmir Minja(katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Maafisa Magereza toka Nchi za SADC(waliosimama) walioshiriki Mafunzo ya Ulinzi wa Amani ambayo yamefanyika kwa wiki mbili katika Chuo cha Uhamiaji, Moshi Mkoani Kilimanjaro. Mafunzo hayo yamefungwa leo na Kamishna Jenerali wa Magereza ambapo jumla ya Maafisa Magereza 27 toka Nchi za SADC ikiwemo Tanzania, Mauritius, Afrika Kusini, Swaziland, Botswana, Namibian na Zimbabwe wamehitimu Mafunzo hayo Maalum ya Ulinzi wa Amani(Picha na Lucas Mboje wa Jeshi la Magereza).