Mojawapo ya Jukumu la Jeshi la Magereza ni kuwapeleka mahakamani mahabusu na kuwarudisha magerezani.

Gadi ya askari Wanawake na Wanaume wa Jeshi la Magereza katika Maadhimisho ya Sherehe za Kitaifa.

Ng'ombe bora wa Nyama na Maziwa ni sehemu ya miradi ya Uzalishaji inayoendeshwa na kusimamiwa na Jeshi la Magereza nchini.

Sehemu ya Mashamba makubwa yanayoendeshwa na Jeshi la Magereza: Shughuli za Kilimo cha Mashamba makubwa, madogo na bustani za mboga mboga ni moja ya shughuli za Magereza katika kuwafunza wafungwa namna ya kujitegemea mara wamalizapo vifungo vyao.

Baadhi wa wafungwa katika Kiwanda cha Ushonaji nguo cha Gereza Kuu Ukonga wakiwa kazini: Shughuli za Ushonaji wa nguo ni moja ya eneo ambalo wafungwa hupata huduma za urekebishwaji kwa vitendo.

Friday, October 20, 2017

MAHAFALI YA 14 SHULE YA SEKONDARI BWAWANI

Naibu kamishna wa huduma za urekebishaji Magereza Tusekile Mwaisabila akimkabidhi cheti na fedha tasilimu mwanafunzi alie fanya vizri katika mitahani wa kujipima kidato cha nne Elizabert Victor katika mahafali ya 14 yalio fanyika katika viwanja vya shule ya Sekondari bwawani mkoa wa Pwani.
Naibu kamishna wa huduma za urekebishaji magereza Tusekile Mwaisabila akiangalia maktaba ya shule ya sekondari bwawani inayo milikiwa na Jeshi la Magereza katika mahafali ya 14 ya shule hiyo yalio fanyika jana katika viwanja vya shule hiyo mkoani Pwani
Naibu kamishna wa huduma za urekebishaji magereza Tusekile Mwaisabila akipata maelekeokutoka kwa mwanafunzi wa shule ya bwawani sekondari kuhusiana na matengenezo ya komputa katika mahafali ya 14 ya shule hiyo yaliofanyika jana.
Wahitimu wa kidato cha nne wa shule ya sekondari Bwawani wakitumbuiza hadhira iliyo hudhuria katika mahafali ya 14 ya shule hiyo jana ambapo mgeni rasmi katika mahafali hayo alikuwa Naibu kamishna wa huduma za urekebishaji Tusekile Mwaisabila kutoka Makao Makuu ya Magereza
Naibu kamishna wa huduma zaurekebishaji magereza Tusekile Mwasabila akiwa kaitka picha ya pamoja na hitimu wa kidato cha nne katika mahafali ya 14 ya shule hiyo yalio fanyika katika jana mkoani Pwani 

NA: CPL. MFAUME

Naibu kamishna wa huduma za urekebishaji magereza amepongeza walimu na bodi ya shule kwa ushirikiano mzuri kwa kujidhatiti  katika kuimasha na kuboresha  miundombinu  katika Shule yasekondari Bwawani kama vile madarasa, maabara ya kisasa, mabweni na afya bora ya mwanafunzi aliyasema hayo alipokuwa akitoa hutuba yake kwa niaba ya kamishna jenerali wa magereza katika mahafali ya 14 shulen I hapo jana.

Aidha aliwasihi wazazi waweze kulipa ada kwa wakati na kuwaruhusu mapema wanafunzi kurudi shuleni pindi wamalikazo likizo zaoili walimu waweze kwenda na muhutasari iliopo.


Friday, October 13, 2017

MAGEREZA YAPIGWA "JEKI" VIFAA TIBA au MAREKENI YAMWAGA VIFAA TIBA KWA MAGEREZA

Kamishna Jenerali wa Magereza Dkt. Juma Malewa akisalimiana na Mkurugenzi, Ofisi ya Afya ya Shirika na Misaada la Marekani (USAID) Bi. Laurel Fain (wa pili kulia) mara baada ya kuwasili katika viwanja vya Gereza la Mahabusu Segerea tayari kwa hafla ya makabidhiano ya vifaa Tiba leo tarehe 13.10.2017
Kamishna Jenerali wa Magereza Dkt. Juma Malewa akipokea hati ya makabidhiano ya Vifaa Tiba kutoka kwa Mkurugenzi wa Ofisi ya Afya ya Shirika la Misaada la Marekani (USAID) Bi. Laurel Fain katika hafla fupi ya makabidhiano ya vifaa hivyo iliyofanyika leo tarehe 13.10.2017 katika viawanja vya Gereza la Mahabusu Segerea Jijini Dar Es Salaam.
Mwonekano wa sehemu ya vifaa tiba vya aina tofauti tofauti vilivyokabidhbiwa leo kwa Jeshi la Magereza Tanzania Bara na Chuo cha Mafunzo Zanzibar kutoka serikali ya Marekeni kupitia Asasi ya JSI/AIDSFree. Vifaa hivyo vyenye thamani ya dola za Kimarekani milioni 1.3 ambazo ni zaidi ya shilingi bilioni 2 fedha za Kitanzania vitasambazwa katika Zahanati za Magereza nchini, Vyuo vya Mafunzo Zanzibar na hospitali Mpya ya Jeshi la Maagereza inayojengwa sasa eneo  la Ukonga jijini Dar es Salaam.
Afisa Muuguzi Staff Sajin wa Magereza Recho Komakoma (kushoto) akitoa maelezo mafupi kwa mgeni rasmi Kamishna Jenerali wa Magereza Dkt. Juma Malewa (wa pili kulia) jinsi kitanda cha kisasa cha kujifungulia (delivery kit) kinavyofanya kazi. Kitanda hicho ni sehemu ya vifaa mbalimbali vya tiba vilivyokabidhiwa leo tahere 13.10.2017 kutoka Serikali ya Marekani kupitia USAID chini ya Mradi wa JSI/AIDSFree. Wa kwanza kulia ni Naibu Kamishna wa Mafunzo Zanzibar Haji Omar.
Mkaguzi wa Magereza Dr. Abdilatif Mkingule (kushoto) ambaye ni daktari kutoka Zahanati ya Chuo cha Taaluma ya Urekebishaji Ukonga akitoa maelezo ya matumizi ya mashine ya uchunguzi (surgical microscope) wa magonjwa ya koo,pua masikio na macho  katika hafla fupi ya makabidhiano ya vifaa hivyo iliyofanyika leo tarehe 13.10.2017 katika viawanja vya Gereza la Mahabusu Segerea Jijini Dar Es Salaam.
Kamishna Jenerali wa Magereza Dkt. Juma Malewa akiwahutubia wageni waalikwa pamoja na maofisa na askari wa Jeshi la Magereza katika hafla ya makabidhiano ya vifaa tiba kutoka serikali ya Marekani kupitia Asasi ya misaada ya USAID, JSI/AIDSFree iliyofanyika leo tarehe 13.10.2017 katika viwanja vya Gereza la Segerea jijini Dar es salaam. Kamishna Malewa alizishukuru serikali ya Marekani kupitia Asasi ya USAID, AIDSFree, Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi na Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa ushirikiano wanaoutoa katika kuboresha huduma za Afya ndani ya Jeshi la Magereza.
Mkurugenzi Mkaazi wa JSI/AIDSFree Dr. Beati Mboya akitoa maneno mafupi ya ufunguzi katika hafla ya Makabidhiano ya vifaa tiba kwa Jeshi la Magereza na Vyuo vya Mafunzo Zanzibar. Dr. Mboya Ameiambia hadhira kuwa Asasi yake imekuwa nchini Tanzania tangu mwaka 2015 ikivijengea uwezo vituo vya Afya katika Jeshi la Magereza na Polisi kwa kuimarisha ubora wa huduma zao hasa katika magonjwa ya Ukimwi na Kifua Kikuu.Kwamba walengwa ni wafanyakazi katika taasisi hizi, familia zao, wafungwa,mahabusu na jamii nzima inayozunguka maeneo hayo.
Baadhi ya Maofisa wa Jeshi la Magereza kutoka vituo mbalimbali wakifuatilia hotuba ya Mgeni rasmi Kamishna Jenerali wa Magereza (hayupo picha) wakati wa hafla ya makabidhiano ya vifaa tiba kutoka Serikali ya Marekani kupitia Asasi ya USAID JSI/AIDSFree. Hafla hiyo imefanyika leo tarehe 13.10.2017 katika viwanja vya Gereza Segerea Jijini Dar es salaam.
Mkurugenzi,Ofisi Ya Afya Bi. Laurel Fain kutoka USAID akitoa hotuba katika hafla ya makabidhiano ya Vifaa Tiba kwa Jeshi la Magereza kutoka Serikali ya Marekeni kwa Jeshi la Magereza nchini.
Baadhi ya askari wa gereza la Mahabusu Segerea waliohudhuria hafla fupi ya kukabidhiana vifaa tiba kutoka serikali ya Marekani kupitia Asasi ya USAID JSI/AIDSFree iliyofanyika leo tarehe 13.10.2017 jijini Dar es salaam.
Kamishna Jenerali wa Magereza Dkt. Juma Malewa (katikati) katika picha ya pamoja na Watendaji wakuu wa Asasi ya JSI/AIDSFree waliosimama. Waliokaa kutoka kuli ni Naibu Kamishna wa Magereza Uwesu Ngarama na Naibu Kamishna wa Mafunzo Haji Omar kutoka Zanzibar. Kushoto ni Mkurugenzi Mkaazi wa JSI/AIDSFree Dr. Beati Mboya na Mkurugenzi, Ofisi ya Afya wa USAID Bi. Laurel  Fain.