Friday, October 20, 2017

MAHAFALI YA 14 SHULE YA SEKONDARI BWAWANI

Naibu kamishna wa huduma za urekebishaji Magereza Tusekile Mwaisabila akimkabidhi cheti na fedha tasilimu mwanafunzi alie fanya vizri katika mitahani wa kujipima kidato cha nne Elizabert Victor katika mahafali ya 14 yalio fanyika katika viwanja vya shule ya Sekondari bwawani mkoa wa Pwani.
Naibu kamishna wa huduma za urekebishaji magereza Tusekile Mwaisabila akiangalia maktaba ya shule ya sekondari bwawani inayo milikiwa na Jeshi la Magereza katika mahafali ya 14 ya shule hiyo yalio fanyika jana katika viwanja vya shule hiyo mkoani Pwani
Naibu kamishna wa huduma za urekebishaji magereza Tusekile Mwaisabila akipata maelekeokutoka kwa mwanafunzi wa shule ya bwawani sekondari kuhusiana na matengenezo ya komputa katika mahafali ya 14 ya shule hiyo yaliofanyika jana.
Wahitimu wa kidato cha nne wa shule ya sekondari Bwawani wakitumbuiza hadhira iliyo hudhuria katika mahafali ya 14 ya shule hiyo jana ambapo mgeni rasmi katika mahafali hayo alikuwa Naibu kamishna wa huduma za urekebishaji Tusekile Mwaisabila kutoka Makao Makuu ya Magereza
Naibu kamishna wa huduma zaurekebishaji magereza Tusekile Mwasabila akiwa kaitka picha ya pamoja na hitimu wa kidato cha nne katika mahafali ya 14 ya shule hiyo yalio fanyika katika jana mkoani Pwani 

NA: CPL. MFAUME

Naibu kamishna wa huduma za urekebishaji magereza amepongeza walimu na bodi ya shule kwa ushirikiano mzuri kwa kujidhatiti  katika kuimasha na kuboresha  miundombinu  katika Shule yasekondari Bwawani kama vile madarasa, maabara ya kisasa, mabweni na afya bora ya mwanafunzi aliyasema hayo alipokuwa akitoa hutuba yake kwa niaba ya kamishna jenerali wa magereza katika mahafali ya 14 shulen I hapo jana.

Aidha aliwasihi wazazi waweze kulipa ada kwa wakati na kuwaruhusu mapema wanafunzi kurudi shuleni pindi wamalikazo likizo zaoili walimu waweze kwenda na muhutasari iliopo.