Mojawapo ya Jukumu la Jeshi la Magereza ni kuwapeleka mahakamani mahabusu na kuwarudisha magerezani.

Gadi ya askari Wanawake na Wanaume wa Jeshi la Magereza katika Maadhimisho ya Sherehe za Kitaifa.

Ng'ombe bora wa Nyama na Maziwa ni sehemu ya miradi ya Uzalishaji inayoendeshwa na kusimamiwa na Jeshi la Magereza nchini.

Sehemu ya Mashamba makubwa yanayoendeshwa na Jeshi la Magereza: Shughuli za Kilimo cha Mashamba makubwa, madogo na bustani za mboga mboga ni moja ya shughuli za Magereza katika kuwafunza wafungwa namna ya kujitegemea mara wamalizapo vifungo vyao.

Baadhi wa wafungwa katika Kiwanda cha Ushonaji nguo cha Gereza Kuu Ukonga wakiwa kazini: Shughuli za Ushonaji wa nguo ni moja ya eneo ambalo wafungwa hupata huduma za urekebishwaji kwa vitendo.

Monday, December 23, 2019

KAMISHNA JENERALI WA MAGEREZA NCHINI, PHAUSTINE KASIKE AHIMIZA WAFUASI WAKE KUZINGATIA NIDHAMU JESHINI

Kamishna Jenerali wa Magereza nchini Phaustine Kasike akizungumza katika kikao na Maafisa na askari wa vituo vya Magereza Mkoa wa Dar es Salaam ambapo kikao hicho kilijadili masuala mbalimbali ikiwemo masuala ya utendaji kazi, maadili ya kazi, nidhamu na mikakati mbalimbali ya Jeshi ikiwemo ya Kilimo, viwanda na ufugaji. Kikao kazi hicho kimefanyika Bwalo Kuu la Maafisa Magereza, Ukonga jijini Dar es Salaam.

Baadhi ya Maafisa Waandamizi wa Jeshi la Magereza kutoka vituo vya Magereza Mkoa wa Dar es Salaam wakimsikiliza Kamishna Jenerali wa Magereza nchini, Phaustine Kasike(hayupo pichani) kikao hicho kilijadili masuala mbalimbali ikiwemo masuala ya utendaji kazi, maadili ya kazi, nidhamu na mikakati mbalimbali ya Jeshi ikiwemo ya Kilimo, viwanda na ufugaji.

Askari wa vyeo mbalimbali wa Jeshi la Magereza kutoka katika vituo vya Magereza Mkoa wa Dar es Salaam wakifuatilia mazungumzo ya kikao kazi na Kamishna Jenerali wa Magereza nchini Phaustine Kasike Desemba 20, 2019 (Picha zote na Jeshi la Magereza).

Saturday, December 14, 2019

UTEKELEZAJI WA ZOEZI LA KUWAACHILIA HURU WAFUNGWA WANUFAIKA WA MSAMAHA WA RAIS WAKAMILIKA NCHI NZIMA


Na ASP. Lucas Mboje, Dar es Salaam

JUMLA ya Wafungwa 5,533 katika magereza mbalimbali nchini walionufaika na msamaha wa Rais wakati wa  maadhimisho ya miaka 58 ya Uhuru wameachiliwa huru magerezani.
Akizungumza na wanahabari leo jijini Dar es Salaam, Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza, Phaustine Kasike amesema kuwa utekelezaji wa zoezi la kuwaachiliwa huru wafungwa wote walionufaika na msamaha wa Rais umekamilika nchi nzima.

“Ni matarajio yangu kuwa wafungwa walioachiliwa wamejutia makosa yao na wataacha kutenda uhalifu hivyo kujihusisha na shughuli halali kwa maendeleo yao, familia zao, jamii na taifa kwa ujumla”, amesisitiza Jenerali Kasike.

Aidha, Kamishna Jenerali Kasike ameelezea manufaa mbalimbali ya msamaha huo; mosi kupungua kwa msongamano magerezani, pili, wanufaika wa msamaha kujumuika na familia zao, tatu, kichocheo cha urekebishaji magerezani kwani msamaha huo utasaidia kuimarika kwa nidhamu na kurejesha matumaini kwa wanaobakia magerezani pamoja na wanufaika wa wamsamaha huo kupata fursa ya kujishughulisha na shughuli za maendeleo uraiani.

“Zipo changamoto zilizojitokeza katika utekelezaji wa zoezi hili ambapo baadhi ya wafungwa walionesha kuwa hawako tayari kuungana na jamii zao pamoja na waliosamehewa kurejea kutenda makosa mara baada ya kuachiwa huru. Hata hivyo nitoe wito kwa jamii nchini kuwapokea wafungwa hao na kuacha kuwanyanyapaa”, amesema Jenerali Kasike. 

Wakati huo huo, Kamishna Jenerali Kasike amemshukru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama, Dkt. John Pombe Magufuli kwa kutoa msamaha huo ambao ni wa kihistoria hapa nchini. Pia amewapongeza wanahabari wote nchini kwa namna walivyoshiriki kutoa habari za zoezi la msamaha huo katika ngazi ya Mkoa na wilaya.

Kwa mujibu wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ibara ya 45(1) (d) imempa mamlaka Rais kutoa msamaha kwa wafungwa waliopo magerezani. Kwa kutumia Ibara hiyo Rais Dkt. John Pombe Magufuli alitoa msamaha kwa wafungwa wakati wa maadhimisho ya miaka 58 ya Uhuru ambapo kilele chake kilifanyika Mkoani Mwanza Desemba 9, 2019.

Wednesday, December 11, 2019

WAFUNGWA 79 WA GEREZA KUU BUTIMBA WALIONUFAIKA NA MSAMAHA WA RAIS WAACHILIWA JIJINI MWANZA TAREHE 10 DISEMBA 2019

Mfungwa mnufaika wa Msamaha wa Rais, William Dingu akizungumza na Wanahabari(hawapo pichani) baada ya kuachiliwa huru leo. Mfungwa huyo amemshukru Rais kwa msamha huo, aidha,  amelipongeza Jeshi la Magereza kwa kumwezesha ujuzi wa wa fani ya ujenzi ambao ameupatia gerezani kupitia programu ya Urekebishaji inayosimamiwa na Jeshi hilo

Baadhi ya wafungwa wakiume wa Gereza Kuu Butimba walionufaika na Msamaha wa Rais wakitoka katika lango la Gereza Kuu Butimba tayari kwenda kuungana na familia zao. Wafungwa hao wamemshukru Rais Magufuli kwa msamaha huo wa kihistoria.


Wafungwa wa kike Gereza Kuu Butimba – Sehemu ya Wanawake wakitoka gerezani baada ya Msamaha wa Rais alioutoa jana katika maadhimisho ya miaka 58 ya uhuru. Wafungwa hao wamemshukru Rais Magufuli kwa msamaha huo na wameahidi kutokurejea katika uhalifu.

Kamati ya Ulinzi na Usalama Mkoani Mwanza pamoja na Kamishna  Jenerali wa Magereza nchini, Phaustine Kasike wakishuhudia wafungwa walionufaika na Msamaha wa Rais katika Gereza Kuu Butimba wakipewa mali zao na nauli ya kwenda kuungana na familia zao  Desemba 10, 2019 kabla ya zoezi la uachiliaji wa wafungwa husika wa msamaha huo.

Kamishna Jenerali wa Magereza nchini, CGP - Phaustine Kasike akitoa taarifa fupi ya zoezi zima la uachiliaji wa wafungwa walionufaika na msamaha wa Rais katika mikoa mbalimbali nchini mbele ya wanahabari kutoka vyombo mbalimbali vya Habari jijini Mwanza  Desemba 10, 2019.

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mhe. John Mongela ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa huo akizungumza na Wafungwa wa Gereza Kuu Butimba kabla ya zoezi la uachiliaji wa wafungwa walionufaika na Msamaha wa Rais  Desemba 10, 2019. Kushoto ni Kamishna Jenerali wa Magereza nchini, CGP - Phaustine Kasike.
(Picha zote na Jeshi la Magereza).




Tuesday, December 10, 2019

KAULI YA RAIS MAGUFULI KUHUSU MSAMAHA WA WAFUNGWA 5533 KATIKA MAADHIMISHO YA MIAKA 58 YA UHURU