Mojawapo ya Jukumu la Jeshi la Magereza ni kuwapeleka mahakamani mahabusu na kuwarudisha magerezani.

Gadi ya askari Wanawake na Wanaume wa Jeshi la Magereza katika Maadhimisho ya Sherehe za Kitaifa.

Ng'ombe bora wa Nyama na Maziwa ni sehemu ya miradi ya Uzalishaji inayoendeshwa na kusimamiwa na Jeshi la Magereza nchini.

Sehemu ya Mashamba makubwa yanayoendeshwa na Jeshi la Magereza: Shughuli za Kilimo cha Mashamba makubwa, madogo na bustani za mboga mboga ni moja ya shughuli za Magereza katika kuwafunza wafungwa namna ya kujitegemea mara wamalizapo vifungo vyao.

Baadhi wa wafungwa katika Kiwanda cha Ushonaji nguo cha Gereza Kuu Ukonga wakiwa kazini: Shughuli za Ushonaji wa nguo ni moja ya eneo ambalo wafungwa hupata huduma za urekebishwaji kwa vitendo.

Wednesday, May 31, 2017

BODI YA KWANZA YA CHUO CHA TAALUMA YA UREKEBISHAJI TANZANIA YAZINDULIWA

Kamishna Jenerali wa Magereza Dkt. Juma Malewa akitoa hotuba ya ufunguzi wa Bodi ya Chuo cha Mafunzo ya Taaluma ya Urekebishaji Tanzania katika Ukumbi wa Bwalo Kuu la Maafisa Magereza Ukonga, Dar es salaam leo Mei 31, 2017
Baadhi ya Maafisa Waandamizi wa Jeshi la Magereza wakifuatilia hotuba ya Mgeni rasmi katika hafla ya uzinduzi wa Bodi ya Chuo cha Mafunzo ya Taaluma ya Urekebishaji Tanzania katika Ukumbi wa Bwalo Kuu la Maafisa Magereza Ukonga, Dar es salaam leo Mei 31, 2017
Mkuu wa Chuo cha Mafunzo ya Taaluma ya Urekebishaji Tanzania ambaye pia ni Katibu wa Bodi hiyo Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Magereza – SACP. Gideon Nkana akitoa historia fupi ya Chuo.
 Baadhi ya Wajumbe wa Bodi hiyo wakifuatilia hotuba ya Mgeni rasmi.
Mwenyekiti wa Bodi ya Chuo cha Mafunzo ya Taaluma ya Urekebishaji Tanzania, Dkt. James Jesse akitoa neno la shukrani baada ya hotuba ya Mgeni rasmi.
Wajumbe wa Sekretarieti ya Bodi ya Chuo cha Mafunzo ya Taaluma ya Urekebishaji Tanzania wakitekeleza majukumu yao katika hafla ya uzinduzi wa Bodi hiyo.
Kamishna Jenerali wa Magereza Dkt. Juma Malewa(wa kwanza kulia) akiteta jambo na baadhi ya Wajumbe wa Bodi kabla ya uzinduzi rasmi uliofanyika Bwalo Kuu la Maafisa Magereza Ukonga, Dar es salaam leo Mei 31, 2017.
Wajumbe wa Bodi ya Chuo cha Mafunzo ya Taaluma ya Urekebishaji Tanzania wakiongozwa na mwenyeji wao Mkuu wa Chuo cha Mafunzo ya Taaluma ya Urekebishaji Tanzania, SACP. Gideon Nkana(wa kwanza kulia) kutembelea mazingira ya chuo hicho.
 Muonekano wa mbele wa Chuo cha Mafunzo ya Taaluma ya Urekebishaji Tanzania.
Mgeni rasmi Kamishna Jenerali wa Magereza Dkt. Juma Malewa (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Wajumbe wa Bodi ya Chuo cha Mafunzo ya Taaluma ya Urekebishaji Tanzania. Walioketi kutoka kulia ni SACP. Gideon Nkana, Godfrey Semango na Dkt. Zena Mabeho. Kutoka kushoto ni DCP. Ally Lugendo, Bi. Catherine Jorome na Dkt. James Jesse. Waliosimama(kushoto) ni SACP. Dkt. Kato Rugainunura(katikati) ACP. Charles Novart na wa kwanza kulia ni SACP. Uwesu Ngarama.

(Picha zote na Kitengo cha Habari na Mawasiliano – Jeshi la Magereza)