Mojawapo ya Jukumu la Jeshi la Magereza ni kuwapeleka mahakamani mahabusu na kuwarudisha magerezani.

Gadi ya askari Wanawake na Wanaume wa Jeshi la Magereza katika Maadhimisho ya Sherehe za Kitaifa.

Ng'ombe bora wa Nyama na Maziwa ni sehemu ya miradi ya Uzalishaji inayoendeshwa na kusimamiwa na Jeshi la Magereza nchini.

Sehemu ya Mashamba makubwa yanayoendeshwa na Jeshi la Magereza: Shughuli za Kilimo cha Mashamba makubwa, madogo na bustani za mboga mboga ni moja ya shughuli za Magereza katika kuwafunza wafungwa namna ya kujitegemea mara wamalizapo vifungo vyao.

Baadhi wa wafungwa katika Kiwanda cha Ushonaji nguo cha Gereza Kuu Ukonga wakiwa kazini: Shughuli za Ushonaji wa nguo ni moja ya eneo ambalo wafungwa hupata huduma za urekebishwaji kwa vitendo.

Thursday, May 30, 2019

WAZIRI LUGOLA AZINDUA BODI MPYA YA SHIRIKA LA UZALISHAJI MALI LA MAGEREZA, AWATAKA WAJUMBE KUFANYA MAGEUZI MAKUBWA KATIKA MIRADI YA JESHI

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola akitoa maelekezo kwa wajumbe wa Bodi mpya ya Shirika la Uzalishaji Mali la Jeshi la Magereza, kabla ya kuizindua Bodi hiyo, jijini Dodoma, leo. Wapili kushoto ni Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza, Phaustine Kasike. 

Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Meja Jenerali Jacob Kingu, akizungumza kabla ya Waziri wa Wizara hiyo, Kangi Lugola (wapili kushoto) kuizindua Bodi mpya ya Shirika la Uzalishaji Mali la Jeshi la Magereza, jijini Dodoma, leo. Wapili kulia ni Kamishna Jenerali wa Magereza, Phaustine Kasike.

Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza, Phaustine Kasike, akitoa historia fupi ya Shirika la Uzalishaji Mali la Jeshi hilo, kabla ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola (kushoto) kuizindua Bodi hiyo, Jijini Dodoma, leo. Katikati ni Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Meja Jenerali Jacob Kingu.

Mwenyekiti wa Bodi Mpya ya Shirika la Uzalishaji Mali la Magereza, Meja Jenerali Mstaafu, Raphaeli Muhuga, akitoa neno la shukrani baada ya uzinduzi wa Bodi hiyo, jijini Dodoma leo. Katikati ni Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola, na kulia ni Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Meja Jenerali Jacob Kingu.

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola (wapili kushoto), Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Meja Jenerali Jacob Kingu (wapili kulia), Kamishna Jenerali wa Magereza, Phaustine Kasike (kushoto), wakiwa katika picha ya pamoja na Wajumbe wa Bodi mpya ya Shirika la Uzalishaji Mali la Jeshi la Magereza, baada ya uzinduzi wa Bodi hiyo, jijini Dodoma leo.
 Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.

Friday, May 17, 2019

KATIBU MKUU WA MAMBO YA NDANI, MEJA JENERALI JACOB KINGU AFUNGUA KIKAO KAZI CHA WAKUU WA MAGEREZA YOTE TANZANIA BARA, LEO MKOANI MOROGORO

Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Ndani ya nchi, Meja Jenerali, Jacob Kingu (kushoto) akiwasili katika Viwanja vya NaneNane, Mkoani Morogoro tayari kwa Ufunguzi wa Kikao Kazi cha Wakuu wa Magereza yote Tanzania Bara kinachofanyika kwa siku mbili kuanzia leo Mei 17 – 18, 2019 katika Ukumbi wa Magereza Mkoani Morogoro. Kulia ni Kamishna Jenerali wa Magereza, Phaustine Kasike

Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Ndani ya nchi, Meja Jenerali, Jacob Kingu akihutubia katika Kikao Kazi cha Wakuu wa Magereza yote Tanzania Bara kinachofanyika kwa siku mbili kuanzia leo Mei 17 – 18, 2019 katika Ukumbi wa Magereza Mkoani Morogoro.  Kushoto ni Kamishna Jenerali wa Magereza, Phaustine Kasike.

Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Ndani ya nchi, Meja Jenerali, Jacob Kingu akihutubia katika Kikao Kazi cha Wakuu wa Magereza yote Tanzania Bara kinachofanyika kwa siku mbili kuanzia leo Mei 17 – 18, 2019 katika Ukumbi wa Magereza Mkoani Morogoro.  Kushoto ni Kamishna Jenerali wa Magereza, Phaustine Kasike.


. Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge, Ulinzi na Usalama, Mhe. Salum Rehani(vazi la kiraia) akiongea katika Kikao Kazi cha Wakuu wa Magereza yote Tanzania Bara, leo Mei 17, 2019 katika Ukumbi wa Magereza Mkoani Morogoro. Kushoto  ni Kamishna Jenerali wa Magereza Nchini, Phaustine Kasike
Baadhi ya Wakuu wa Magereza wakifuatilia kwa makini hotuba ya Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Ndani ya nchi, Meja Jenerali, Jacob Kingu(hayupo pichani).


Kamishna Jenerali wa Magereza Nchini, Phaustine Kasike akiteta jambo na Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Ndani ya nchi, Meja Jenerali, Jacob Kingu baada ya ufunguzi wa Kikao kazi cha Wakuu wa Magereza yote Tanzania Bara.