Tuesday, September 29, 2015
Taarifa kwa umma kuhusu ajira katika Jeshi la Magereza zilizosambazwa kwenye baadhi ya mitandao ya kijamii
3:44 PM
Hii ni taarifa ya kukanusha kuhusiana na tangazo la ajira katika Jeshi la
Magereza ambayo imekuwa ikisambazwa kwenye baadhi ya mitandao ya kijamii
hivyo kusababisha usumbufu mkubwa kwa wananchi na Uongozi wa Jeshi kwa
ujumla.
Bofya hapa kupata taarifa kamili
Friday, September 18, 2015
Katibu mkuu wizara ya mambo ya ndani ya nchi azindua huduma za "Duty Free Shop" magereza mkoani Arusha
5:54 PM
Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe. Mbarak Abdulwakil(wa
pili kushoto)akikata utepe kuashiria uzinduzi rasmi wa Huduma za
Magereza Duty free shop Mkoani Arusha leo Septemba 18, 2015 katika
Viwanja vya Gereza Kuu Arusha(wa kwanza kulia) ni Kamishna Jenerali wa
Jeshi la Magereza, John Casmir Minja(wa pili kulia) ni Mkurugenzi
Mtendaji wa Dar Smart LTD, Bw. Mohamed Panjwani.
Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe. Mbarak
Abdulwakil(kulia)akisoma jiwe la Msingi kwenye hafla ya uzinduzi wa Duty
free shop ya Magereza Mkoani Arusha(kushoto) ni Kamishna Jenerali wa
Magereza, John Casmir Minja.
Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza Nchini, John Casmir Minja akitoa
maelezo mafupi wakati wa kumkaribisha Mgeni rasmi katika hafla ya
uzinduzi wa Huduma za Duty free shop ya Magereza Mkoani Arusha.
Askari wa Jeshi la Magereza kutoka Magereza mbalimbali yaliyopo Mkoani
Arusha wakifuatilia kwa makini hotuba ya Mgeni Katibu Mkuu Wizara ya
Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe. Mbaraka Abdulwakil(hayupo pichani).
Bidhaa za majumbani zinazopatikana katika Duty free shop ya Magereza Mkoani Arusha
Mgeni rasmi Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe. Mbarak
Abdulwakil(katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Kamati ya Ulinzi na
Usalama Mkoani Arusha waliosimama mara tu baada ya kuzindua Huduma za
Duty free shop ya Magereza Mkoani Arusha(wa pili kushoto) ni Kamishna
Jenerali wa Magereza, John Casmir Minja(wa pili kulia) ni Mkuu wa
Magereza Mkoani Arusha, SACP. Hamis Nkubasi(wa kwanza kushoto) ni Mkuu
wa Magereza Mkoani Kilimanjaro, SACP. Venant Kayombo(wa kwanza kulia) ni
Mkurugenzi Mtendaji wa Dar Mart LTD, Bw. Mohamed Panjwani
Na Lucas Mboje, Arusha
Katibu
Mkuu Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe. Mbarak Abdulwakil
amepongeza kasi ya Utendaji kazi wa Kamishna Jenerali wa Magereza
nchini, John Casmir Minja pamoja na Uongozi wote wa Jeshi hilo kwa
kutekeleza kwa mafanikio makubwa mpango wa Serikali ya Awamu ya Nne wa
kuwasogezea huduma za bidhaa muhimu na zenye manufaa Maafisa, askari
Magereza na familia zao katika maeneo yao ya kazi hususani huduma za
"Duty free shops".
Mhe. Mbarak
Abdulwakil ameyasema hayo wakati wa uzinduzi rasmi wa "Duty free shop"ya
Magereza Mkoani Arusha iliyofanyika leo Septemba 18, 2015 katika
Viwanja vya Gereza Kuu Arusha ambapo baadhi ya Viongozi mbalimbali wa
Kiserikali na Binafsi wa Mkoa wa Arusha walihudhuria hafla hiyo.
"Nampongeza
kwa dhati Kamishna Jenerali wa Magereza John Casmir Minja kwa jitihada
hizi ambapo matunda yake yanaonekana na amethibitisha kwamba azma ya
kusambaza huduma hii nchi nzima ipo pale pale na jitihada zinaonekana".
Alisema Abdulwakil.
Ameongeza kuwa lengo la Mpango huu ni kuhakikisha kuwa ustawi wa maisha ya Maafisa na Askari wa Majeshi yote ya Ulinzi na Usalama unatekelezwa ipasavyo kwa kuwapatia bidhaa zenye bei nafuu ili kuwapunguzia ukali wa maisha.
Aidha, Mhe. Abdulwakil amewaasa Maafisa na askari watakaotumia huduma husika kuzingatia Sheria, Kanuni na taratibu pamoja na maadili ya uendeshaji wa maduka hayo ili kuhakikisha kuwa adhima ya Serikali ya kuwapunguzia makali ya maisha Maafisa, askari pamoja na familia zao wananufaika ipasavyo na si vinginevyo.
Awali akimkaribisha Mgeni rasmi,Kamishna Jenerali wa Magereza nchini, John Casmir Minja alisema kuwa Jeshi la Magereza kwa kushirikiana na Kampuni ya Dar Mart LTD limeazimia kusambaza huduma za Duty Free Shop nchi nzima kwa ajili ya kutoa huduma kwa Maafisa na askari.
Kamishna Jenerali Minja alimhakikishia Mgeni rasmi kuwa maduka hayo yataendeshwa kwa kuzingatia Sheria, Kanuni na taratibu za "Duty Free Shop" na akasema kuwa hata sita kuchukua hatua kali za kinidhamu kwa Maafisa na askari watakao kwenda kinyume na uendeshaji wa huduma hizo.
Hivi sasa Jeshi la Magereza limefanikiwa kuzindua jumla ya "Duty Free Shops" tisa(09) ikiwemo Gereza Kuu Ukonga na Keko - Dar es Salaam, Gereza Isanga - Dodoma, Gereza Kuu Karanga - Moshi, Gereza Butimba - Mwanza, Gereza Ruanda - Mbeya, Gereza Lilungu - Mtwara, Gereza Uyui - Tabora, Chuo KPF - Morogoro na duka la tisa(09) ni Gereza Kuu Arusha.
Ameongeza kuwa lengo la Mpango huu ni kuhakikisha kuwa ustawi wa maisha ya Maafisa na Askari wa Majeshi yote ya Ulinzi na Usalama unatekelezwa ipasavyo kwa kuwapatia bidhaa zenye bei nafuu ili kuwapunguzia ukali wa maisha.
Aidha, Mhe. Abdulwakil amewaasa Maafisa na askari watakaotumia huduma husika kuzingatia Sheria, Kanuni na taratibu pamoja na maadili ya uendeshaji wa maduka hayo ili kuhakikisha kuwa adhima ya Serikali ya kuwapunguzia makali ya maisha Maafisa, askari pamoja na familia zao wananufaika ipasavyo na si vinginevyo.
Awali akimkaribisha Mgeni rasmi,Kamishna Jenerali wa Magereza nchini, John Casmir Minja alisema kuwa Jeshi la Magereza kwa kushirikiana na Kampuni ya Dar Mart LTD limeazimia kusambaza huduma za Duty Free Shop nchi nzima kwa ajili ya kutoa huduma kwa Maafisa na askari.
Kamishna Jenerali Minja alimhakikishia Mgeni rasmi kuwa maduka hayo yataendeshwa kwa kuzingatia Sheria, Kanuni na taratibu za "Duty Free Shop" na akasema kuwa hata sita kuchukua hatua kali za kinidhamu kwa Maafisa na askari watakao kwenda kinyume na uendeshaji wa huduma hizo.
Hivi sasa Jeshi la Magereza limefanikiwa kuzindua jumla ya "Duty Free Shops" tisa(09) ikiwemo Gereza Kuu Ukonga na Keko - Dar es Salaam, Gereza Isanga - Dodoma, Gereza Kuu Karanga - Moshi, Gereza Butimba - Mwanza, Gereza Ruanda - Mbeya, Gereza Lilungu - Mtwara, Gereza Uyui - Tabora, Chuo KPF - Morogoro na duka la tisa(09) ni Gereza Kuu Arusha.
(Picha zote na
Lucas Mboje wa Jeshi la Magereza).
Friday, September 4, 2015
Kamishna wa sheria na uendeshaji wa magereza afunga rasmi kongamano la wasaidizi wa kisheria magerezani mkoani Morogoro
9:35 PM
Kamishna wa Sheria na Uendeshaji wa Magereza, Dkt. Juma Malewa akitoa
hotuba kwa Maofisa Wasaidizi wa Kisheria Magerezani kwenye hafla ya
ufungaji wa Kongamano la Wasaidizi wa Sheria lililofadhiliwa na Shirika
la Envirocare ambapo Kongamano hilo limefanyika kwa siku tatu kuanzia
Septemba 2, 2015 Mkoani Morogoro.
Washiriki wa Kongamano hilo ambao ni Maofisa wa Jeshi la Magereza kutoka
Mikoa Mitano Tanzania Bara(Dar es Salaam, Tanga, Arusha, Kilimanjaro na
Morogoro) wakifuatilia kwa makini hotuba ya ufungaji wa Kongamano hilo.
Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Envirocare, Bi. Loyce Lema akitoa neno
la shukrani kwa Washiriki kabla ya kumkaribisha Kamishna wa Sheria na
Uendeshaji wa Magereza kufunga Kongamano hilo.
Kamishna wa Sheria na Uendeshaji wa Magereza, Dkt. Juma Malewa(kulia)
akiwa ameongozana na mwenyeji wake Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la
Envirocare, Bi. Loyce Lema(kushoto) tayari kwa ufungaji rasmi wa
Kongamano la Wasaidizi wa Kisheria ambalo limefanyika Mkoani Morogoro
kuanzia Septemba 02 - 04, 2015
(Picha zote na Lucas Mboje wa Jeshi la
Magereza).
Thursday, September 3, 2015
Jeshi la Magereza nchini kushirikiana na asasi za kiraia katika kupunguza msongamano magerezani
1:19 PM
Washiriki
wa Kongamano la Wasaidizi wa Kisheria Magerezani kutoka Magereza Mkoani
tanga wakiendelea na majadiliano katika Kongamano hilo linalofanyika
Mkoani Morogoro kwa siku tatu.
Na, Lucas Mboje, Morogoro
Jeshi la Magereza nchini limeahidi kuendelea kushirikiana na Asasi ya Envirocare katika kuimarisha Madawati ya Msaada wa Kisheria Magerezani ili kuleta tija katika utatuzi wa changamoto ya Msongamano wa Mahabusu inayolikabili Jeshi hilo.
Kauli hiyo imetolewa jana Mkoani Morogoro na Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza, John Casmir Minja alipokuwa Mgeni rasmi wakati wa hafla ya ufunguzi wa Kongamano la Wasaidizi wa Kisheria Magerezani na Mahabusi za Watoto.
Jenerali Minja amesema kuwa Serikali imeendelea kuchukulia kwa uzito stahiki suala la Msongamano wa Mahabusu Magerezani ikiwemo kushirikiana na Wadau wa Haki Jinai katika kupunguza changamoto ya Msongamano wa Mahabusu Magerezani.
"Napenda kutoa rai kwa Asasi zingine zenye malengo yanayofanana na Asasi hii nazikaribisha kuja kufanya kazi na Jeshi la Magereza kwani mwelekeo wa Jeshi kwa sasa ni Urekebishaji wa Wafungwa(From Prisons to Corrections) ambapo Jeshi la Magereza watafanya kazi kwa karibu na Asasi za Kiraia na Jamii kwa ujumla". Alisema Jenerali Minja.
Awali akimkaribisha Mgeni rasmi Mkurugenzi Mtendaji wa Envirocare, Bi. Loyce Lema amesema kuwa imekuwa ni faraja kwao kupata ushirikiano kama huo kutoka Jeshi la Magereza kwani umewezesha kutekelezwa kwa mradi huo wa kutoa Msaada wa Kisheria kwa Mahabusu waliopo Magerezani kwa matokeo chanya kwa muda mufupi.
Bi. Lema alisema kuwa mradi huo umetekelezwa kwa miaka mitatu(2012 - 2015) na umetekelezwa kwenye Magereza 20 na Mahabusu 04 za Watoto katika Mikoa 05 ambayo ni Mkoa wa Kilimanjaro, Arusha, Tanga, Morogoro na Dar es Salaam.
Asasi ya Envirocare kwa kushirikiana na Jeshi la Magereza ilifanya utafiti wa awali wa kuangalia hali halisi ya Msongamano katika Magereza yaliyopo katika Mikoa mitano ya mradi. Matokeo ya jumla ya utafiti huo yalionesha kuwa kuna tatizo kubwa la Msongamano ambao unasababishwa na idadi kubwa ya Mahabusu katika Magereza ya Mikoa hiyo.
Jeshi la Magereza nchini limeahidi kuendelea kushirikiana na Asasi ya Envirocare katika kuimarisha Madawati ya Msaada wa Kisheria Magerezani ili kuleta tija katika utatuzi wa changamoto ya Msongamano wa Mahabusu inayolikabili Jeshi hilo.
Kauli hiyo imetolewa jana Mkoani Morogoro na Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza, John Casmir Minja alipokuwa Mgeni rasmi wakati wa hafla ya ufunguzi wa Kongamano la Wasaidizi wa Kisheria Magerezani na Mahabusi za Watoto.
Jenerali Minja amesema kuwa Serikali imeendelea kuchukulia kwa uzito stahiki suala la Msongamano wa Mahabusu Magerezani ikiwemo kushirikiana na Wadau wa Haki Jinai katika kupunguza changamoto ya Msongamano wa Mahabusu Magerezani.
"Napenda kutoa rai kwa Asasi zingine zenye malengo yanayofanana na Asasi hii nazikaribisha kuja kufanya kazi na Jeshi la Magereza kwani mwelekeo wa Jeshi kwa sasa ni Urekebishaji wa Wafungwa(From Prisons to Corrections) ambapo Jeshi la Magereza watafanya kazi kwa karibu na Asasi za Kiraia na Jamii kwa ujumla". Alisema Jenerali Minja.
Awali akimkaribisha Mgeni rasmi Mkurugenzi Mtendaji wa Envirocare, Bi. Loyce Lema amesema kuwa imekuwa ni faraja kwao kupata ushirikiano kama huo kutoka Jeshi la Magereza kwani umewezesha kutekelezwa kwa mradi huo wa kutoa Msaada wa Kisheria kwa Mahabusu waliopo Magerezani kwa matokeo chanya kwa muda mufupi.
Bi. Lema alisema kuwa mradi huo umetekelezwa kwa miaka mitatu(2012 - 2015) na umetekelezwa kwenye Magereza 20 na Mahabusu 04 za Watoto katika Mikoa 05 ambayo ni Mkoa wa Kilimanjaro, Arusha, Tanga, Morogoro na Dar es Salaam.
Asasi ya Envirocare kwa kushirikiana na Jeshi la Magereza ilifanya utafiti wa awali wa kuangalia hali halisi ya Msongamano katika Magereza yaliyopo katika Mikoa mitano ya mradi. Matokeo ya jumla ya utafiti huo yalionesha kuwa kuna tatizo kubwa la Msongamano ambao unasababishwa na idadi kubwa ya Mahabusu katika Magereza ya Mikoa hiyo.
Wednesday, September 2, 2015
Kamishna Jenerali wa Magereza afungua rasmi kongamano la wasaidizi wa kisheria magerezani mkoani Morogoro
3:07 PM
Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza, John Casmir Minja akitoa hotuba
kwa Maofisa Wasaidizi wa Kisheria Magerezani kwenye ufunguzi wa
Kongamano la Wasaidizi wa Sheria lililofadhiliwa na Shirika la
Envirocare ambapo Kongamano hilo litafanyika kwa siku tatu kuanzia leo
Septemba 2, 2015 Mkoani Morogoro.
Baadhi ya Washiriki wa Kongamano hilo ambao ni Maofisa wa Jeshi la
Magereza kutoka Mikoa Mitano Tanzania Bara(Dar es Salaam, Tanga, Arusha,
Kilimanjaro na Morogoro) wakifuatilia kwa makini hotuba ya Mgeni rasmi
ambaye ni Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza, John Casmir
Minja(hayupo pichani).
Meza Kuu wakimsikiliza Mwakilishi kutoka Wizara ya Mambo ya Ndani -
Jeshi la Polisi, Kamisheni ya Upelelezi, Mrakibu wa Polisi Emmy
Mkonyi(hayupo pichani). Kutoka kulia ni Mkurugenzi wa Huduma za Kisheria
kwa Umma kutoka Wizara ya Sheria na Katiba, Bw. Joseph
Ndunguru(kushoto) ni Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Envirocare, Bi.
Loyce Lema(katikati) ni Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza, John
Casmir Minja.
Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Envirocare, Bi. Loyce Lema akitoa
maelezo mafupi ya lengo la Kongamano hilo ambalo ni kutoa msaada wa
Kisheria Magerezani ili kupunguza Msongamano Magerezani.
Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza, John Casmir Minja akimpongeza
baada ya kukabidhi cheti cha kuhitimu Mafunzo ya Wasaidizi wa Kisheria
Magerezani kwa mmoja wa Washiriki wa Kongamano hilo linalofanyika Mkoani
Morogoro.
Mwandishi wa Habari wa ITV, Bi. Devotha Minja akiteta jambo na Kamishna
Jenerali wa Jeshi la Magereza, John Casmir Minja mara baada ya ufunguzi
rasmi wa Kongamano la Wasaidizi wa Kisheria katika Viwanja vya Ukumbi wa
CCT uliopo Mkoani Morogoro(wa pili kulia) ni Mkurugenzi Mtendaji wa
Shirika la Envirocare, Bi. Loyce Lema(kulia) ni Mwakilishi kutoka Wizara
ya Mambo ya Ndani ya Nchi - Jeshi la Polisi, Mrakibu wa Polisi Emmy
Mkonyi.
Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza, John Casmir Minja(katikati)
walioketi akiwa katika picha ya pamoja na Washiriki wa Kongamano la
Wasaidizi wa Kisheria kutoka Mikoa Mitano ya Magereza Tanzania Bara(wa
kwanza kulia) ni Mkuu wa Magereza Mkoani Morogoro, Kamishna Msaidizi
Mwandamizi wa Magereza, Dkt. Kato Rugainunula(wa pili kulia) ni
Mkurugenzi wa Huduma za Kisheria kwa Umma, Wizara ya Katiba na Sheria,
Bw. Joseph Ndunguru(wa kwanza kushoto) ni Mwakilishi kutoka Wizara ya
Mambo ya Ndani ya Nchi - Jeshi la Polisi, Mrakibu wa Polisi, Emmy
Mkonyi(wa pili kushoto) ni Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Envirocare,
Bi. Loyce Lema(Picha zote na Lucas Mboje wa Jeshi la Magereza).