Mojawapo ya Jukumu la Jeshi la Magereza ni kuwapeleka mahakamani mahabusu na kuwarudisha magerezani.

Gadi ya askari Wanawake na Wanaume wa Jeshi la Magereza katika Maadhimisho ya Sherehe za Kitaifa.

Ng'ombe bora wa Nyama na Maziwa ni sehemu ya miradi ya Uzalishaji inayoendeshwa na kusimamiwa na Jeshi la Magereza nchini.

Sehemu ya Mashamba makubwa yanayoendeshwa na Jeshi la Magereza: Shughuli za Kilimo cha Mashamba makubwa, madogo na bustani za mboga mboga ni moja ya shughuli za Magereza katika kuwafunza wafungwa namna ya kujitegemea mara wamalizapo vifungo vyao.

Baadhi wa wafungwa katika Kiwanda cha Ushonaji nguo cha Gereza Kuu Ukonga wakiwa kazini: Shughuli za Ushonaji wa nguo ni moja ya eneo ambalo wafungwa hupata huduma za urekebishwaji kwa vitendo.

Thursday, April 9, 2015

Kamishna Jenerali wa Magereza nchini Tanzania Bw. John Casmir Minja ashiriki mahafali ya kumaliza mafunzo ya awali ya uaskari magereza nchini Uganda

Kamishna Jenerali wa Magereza Nchini Tanzania Bwn.John .C.Minja akiwaongoza Wakuu wa Magereza wanachama wa ACSA (Umoja wa Nchi zinazoshughulika na Urekebishaji/Magereza Barani Afrika wakati wakiingia Viwanja vya Kololo Jijini Kampala,Uganda kabla ya kuanza kwa ratiba ya kumaliza Mafunzo ya Awali ya Uaskari Magereza Nchini Uganda.Shughuli zilizofanyika leo tarehe 9 April,2015 katika Viwanja Kololo Kampala.Aliyeongozana nae ni Mkuu wa Magereza Nchini Angola.
Kamishna Jenerali wa Magereza Nchini Tanzania Bw. John .C. Minja aliyekaa katikati,amevaa nguo za kijana akiwa amekaa na Wakuu Wengine wa Magereza Wanachama wa ACSA wakimsubiri Mgeni rasmi katika Mahafali hayo Mhe. Yoweri Kaguta Mseveni Rais wa Jamhuri ya Uganda,hata hivyo hakuweza kuja na badala yake aliwakilishwa na Makamu wa Rais Nchini Uganda Mhe. Edward Sekand