Wednesday, April 27, 2016
Kamishna jenerali wa magereza nchini afunga rasmi mafunzo ya maafisa wateule daraja la kwanza, mkoani Morogoro
5:00 PM
Kamishna Jenerali wa Magereza nchini, CGP John Casmir Minja akikagua Gadi Maalum iliyoandaliwa na Maofisa Wahitimu wa Mafunzo ya Maafisa Wateule Daraja la Kwanza yalifanyika Aprili 27, 2016 katika Viwanja vya chuo cha Jeshi la Magereza, KPF Mkoani Morogoro.
Kamishna Jenerali wa Magereza nchini, CGP John Casmir Minja katika jukwaa akipokea salaam ya heshima kutoka Gadi Maalum iliyoandaliwa na Maofisa Wahitimu wa Mafunzo ya Maafisa Wateule Daraja la Kwanza(hawapo pichani).
Maofisa Wahitimu wa Mafunzo ya Maafisa Wateule Daraja la Kwanza wakipita mbele ya Mgeni rasmi katika sherehe za kufunga mafunzo hayo yaliyofanyika Viwanja vya chuo cha Jeshi la Magereza, KPF Mkoani Morogoro.
Kamishna Jenerali wa Magereza nchini, CGP John Casmir Minja(kushoto) akimvisha cheo cha RSM mmoja wa Wahitimu wa Mafunzo ya Maafisa Wateule Daraja la Kwanza ambaye amefanya vizuri zaidi katika Mafunzo hayo yaliyofanyika kwa muda wa miezi miwili.
Baadhi ya Maofisa wa Kike wa Jeshi la Magereza ambao ni miongoni mwa wahitimu wa Mafunzo ya Maafisa Wateule Daraja la Kwanza kama wanavyoonekana katika picha.
Kamishna Jenerali wa Magereza nchini, CGP John Casmir Minja akitoa hotuba fupi kwa Wahitimu wa Mafunzo ya Maafisa Wateule Daraja la Kwanza(hawapo pichani).
Maofisa Wahitimu wa Mafunzo ya Maafisa Wateule Daraja la Kwanza wakifuatilia kwa makini hotuba ya mgeni kama wanavyoonekana katika picha.
Kamishna Jenerali wa Magereza nchini, CGP John Casmir Minja akifanya mahojiano na baadhi ya Wawakilishi wa Vyombo vya Habari, Mkoani Morogoro.
Kamishna Jenerali wa Magereza nchini, CGP John Casmir Minja(katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Maofisa Wahitimu wa Mafunzo ya Maafisa Wateule Daraja la Kwanza waliosimama mstari wa nyuma
(Picha zote na Lucas Mboje wa Jeshi la Magereza).
Friday, April 22, 2016
Wahitimu Bwawani Sekondari waaswa kuwa waadilifu na wazalendo kwa Taifa
4:18 PM
Mgeni rasmi Kamishna wa Fedha na Utawala wa Magereza, Gaston Sanga
akitoa cheti kwa mwanafunzi mhitimu wa kidato cha sita katika mahafali
ya kwanza ya kidato cha sita Bwawani Sekondari, yaliyofanyika leo Aprili
22, 2016.
Mkuu wa shule ya Bwawani Sekondari, ACP. Emmanuel Lwinga akitoa maelezo mafupi ya maendeleo ya shule kabla ya kumkaribisha mgeni rasmi kutoa hotuba yake.
Wanafunzi wahitimu wa Kidato cha sita Bwawani Sekondari wakiimba wimbo wa shule kwenye mahafali hayo yaliyofanyika leo Aprili 22, 2016, Mkoani Pwani.
Kamishna wa Utawala na Fedha, Gaston Sanga akiwasalimu wahitimu na wazazi kabla ya kutoa hotuba fupi kwa wahitimu wa kidato cha sita Bwawani Sekondari(hawapo pichani).
Wazazi wa wahitimu wa kidato cha sita shule ya Bwawani Sekondari wakifuatilia kwa makini hotuba ya Mgeni rasmi
Ujenzi wa Bweni la Wasichana katika shule ya Bwawani Sekondari ukiwa katika hatua mbalimbali za ujenzi kama inavyoonekana katika picha.
Mgeni rasmi Kamishna wa Fedha na Utawala wa Magereza, Gaston Sanga(katikati)akiwa katika picha ya pamoja na wanafunzi wahitimu kidato cha sita Bwawani Sekondari(waliosimama mstari wa nyuma)mahafali hayo yamefanyika leo Aprili 22, 2016
(Picha zote na lucas mboje wa Jeshi la Magereza).
Na Lucas Mboje, Pwani
WAHITIMU wa Kidato cha sita nchini wameaswa kuwa waadilifu na wazalendo ili hatimaye taifa liweze kupata viongozi bora na raia wema katika jamii.
Rai hiyo imetolewa na Kamishna wa Fedha na Utawala wa Magereza Gaston Sanga akiongea kwa niaba ya Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza nchini katika mahafali ya kwanza ya Kidato cha sita ya Shule ya Bwawani Sekondari iliyopo Mkoani Pwani.
“Nadhani wote ni mashahidi kwa namna Serikali ya Awamu ya Tano inavyowahudumia wananchi kwa kasi na kiwango cha kuridhisha. Hivyo mkipata kazi nawasihi mkawajibike kwa kasi, uadilifu na mkawe wazalendo kwa taifa”. Alisema Kamishna Sanga.
Kamishna Sanga ameongeza kuwa kwa kufanya hivyo watakuwa wameunga mkono kwa vitendo juhudi mbalimbali zinazofanywa na Serikali ya Awamu ya Tano chini ya Rais Dkt. John Pombe Magufuli.
Aidha, Afande Sanga ameahidi kuwa Uongozi wa Jeshi la Magereza kwa kushirikiana na Bodi ya shule hiyo utaendelea kuzitafutia ufumbuzi changamoto mbalimbali zinazozikabili shule hiyo kadri uwezo wa kifedha unavyopatikana.
Kwa upande wake Mkuu wa shule ya Sekondari Bwawani, Kamishna Msaidizi wa Magereza, Emmanuel Lwinga alipokuwa akitoa taarifa fupi kwa mgeni rasmi katika mahafali hayo amesema kuwa shule yake ni miongoni mwa shule bora nchini ambazo zinafanya vizuri kitaaluma na masuala mengineyo yasiyoyakitaaluma.
Aliongeza kuwa katika mitihani mbalimbali waliyofanya wanafunzi hao wa kidato cha sita wamekuwa na matokeo mazuri kutokana na mazingira mazuri ya kujisomea, ushirikiano mzuri wa walimu pamoja na kuimarishwa kwa miundombinu muhimu ya kujifunzia.
"Afande mgeni rasmi wanafunzi wahitimu 13 wa leo tuna hakika kuwa watatuletea matunda mazuri kutokana na mwelekeo waliouonesha katika mitihani ya ndani na nje ya shule waliyoifanya". Alisema Mkuu wa Shule Lwinga.
Shule ya Sekondari Bwawani inamilikiwa na Jeshi la Magereza, ilianzishwa Mwaka 1978 kwa lengo la kutoa elimu ya Sekondari kwa Watumishi wa Magereza ambapo hivi sasa shule hiyo inatoa elimu kwa vijana wa kike na kiume kutoka maeneo mbalimbali hapa nchini kuanzia kidato cha kwanza hadi cha Sita.
WAHITIMU wa Kidato cha sita nchini wameaswa kuwa waadilifu na wazalendo ili hatimaye taifa liweze kupata viongozi bora na raia wema katika jamii.
Rai hiyo imetolewa na Kamishna wa Fedha na Utawala wa Magereza Gaston Sanga akiongea kwa niaba ya Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza nchini katika mahafali ya kwanza ya Kidato cha sita ya Shule ya Bwawani Sekondari iliyopo Mkoani Pwani.
“Nadhani wote ni mashahidi kwa namna Serikali ya Awamu ya Tano inavyowahudumia wananchi kwa kasi na kiwango cha kuridhisha. Hivyo mkipata kazi nawasihi mkawajibike kwa kasi, uadilifu na mkawe wazalendo kwa taifa”. Alisema Kamishna Sanga.
Kamishna Sanga ameongeza kuwa kwa kufanya hivyo watakuwa wameunga mkono kwa vitendo juhudi mbalimbali zinazofanywa na Serikali ya Awamu ya Tano chini ya Rais Dkt. John Pombe Magufuli.
Aidha, Afande Sanga ameahidi kuwa Uongozi wa Jeshi la Magereza kwa kushirikiana na Bodi ya shule hiyo utaendelea kuzitafutia ufumbuzi changamoto mbalimbali zinazozikabili shule hiyo kadri uwezo wa kifedha unavyopatikana.
Kwa upande wake Mkuu wa shule ya Sekondari Bwawani, Kamishna Msaidizi wa Magereza, Emmanuel Lwinga alipokuwa akitoa taarifa fupi kwa mgeni rasmi katika mahafali hayo amesema kuwa shule yake ni miongoni mwa shule bora nchini ambazo zinafanya vizuri kitaaluma na masuala mengineyo yasiyoyakitaaluma.
Aliongeza kuwa katika mitihani mbalimbali waliyofanya wanafunzi hao wa kidato cha sita wamekuwa na matokeo mazuri kutokana na mazingira mazuri ya kujisomea, ushirikiano mzuri wa walimu pamoja na kuimarishwa kwa miundombinu muhimu ya kujifunzia.
"Afande mgeni rasmi wanafunzi wahitimu 13 wa leo tuna hakika kuwa watatuletea matunda mazuri kutokana na mwelekeo waliouonesha katika mitihani ya ndani na nje ya shule waliyoifanya". Alisema Mkuu wa Shule Lwinga.
Shule ya Sekondari Bwawani inamilikiwa na Jeshi la Magereza, ilianzishwa Mwaka 1978 kwa lengo la kutoa elimu ya Sekondari kwa Watumishi wa Magereza ambapo hivi sasa shule hiyo inatoa elimu kwa vijana wa kike na kiume kutoka maeneo mbalimbali hapa nchini kuanzia kidato cha kwanza hadi cha Sita.
Thursday, April 14, 2016
Monday, April 11, 2016
Jeshi la Magereza na Suma-JKT wakabidhiwa jukumu la kutengeneza madawati yenye thamani ya bilioni 6, jijini Dar
8:50 PM
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Joseph
Magufuli akionesha mfano wa hundi aliyokabidhiwa na Ofisi ya Bunge leo
Ikulu, Jijini Dar es Salaam ambapo fedha hizo ameelekeza zitumike
kutengenezea madawati ya shule hapa nchini(kulia)ni Naibu Spika wa Bunge
la Tanzania, Dkt. Tulia Ackson.
Muonekano wa Madawati ambayo yanatarajiwa kutengenezwa na yaliyoidhinishwa na Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi kama yanavyoonekana katika picha.
Kamishna Jenerali wa Magereza nchini, CGP John Casmir Minja(kushoto) akiwa na Mkuu wa Jeshi la Kujenga Taifa, Bregedia Jenerali, Michael Isamuhyo(katikati) wakifuatilia hotuba ya Rais Magufuli(kulia) ni Mtendaji Mkuu wa SUMA - JKT, Bregedia Jenerali C.Yateri.
Kamishna Jenerali wa Magereza nchini, CGP John Casmir Minja akiongea na Wandishi wa Habari kuhusu namna Jeshi hilo lilivyojipanga kutekeleza jukumu lililopewa.
Kamishna Jenerali wa Magereza nchini, CGP John Casmir Minja akisalimiana na Katibu wa Bunge, Dkt. Thomas Kashilila wakipokutana katika Viwanja vya Ikulu, Jijini Da es Salaam(Picha zote na Lucas Mboje wa Jeshi la Magereza).
Na; Lucas Mboje wa Jeshi la Magereza,
JESHI LA MAGEREZA nchini pamoja na Jeshi la Kujenga Taifa limepewa jukumu la kutengeneza madawati yenye thamani ya Bilioni 6 ambayo yatasambazwa katika Mikoa yote ya Tanzania Bara na Zanzibar.
JESHI LA MAGEREZA nchini pamoja na Jeshi la Kujenga Taifa limepewa jukumu la kutengeneza madawati yenye thamani ya Bilioni 6 ambayo yatasambazwa katika Mikoa yote ya Tanzania Bara na Zanzibar.
Jukumu
hilo kwa Vyombo vya Ulinzi na Usalama limetolewa leo Aprili 11, 2016 na
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Joseph
Magufuli, katika hafla fupi ya makabidhiziano ya mfano wa hundi ya
Bilioni 6 za pesa ya kitanzania kutoka Sekretarieti ya Bunge ya Jamuhuri
ya Muungano wa Tanzania pesa ambazo zimepatikana kufuatia kubana
matumizi ya uendeshaji wa Ofisi hiyo.
Rais
Magufuli amesema kuwa Ofisi ya Bunge pamoja na Watendaji wake
wameonesha moyo wa kizalendo kwa Taifa lao kwani wametekeleza kwa
vitendo maelekezo ya kubana matumizi ya fedha za Serikali hivyo kuokoa
kiasi hicho cha Bilioni 6 ambazo wamezikabidhi ili zitumike katika
kutatua changamoto ya uhaba wa Madawati katika shule nyingi hapa nchini.
“Nikupongeze
sana Dkt. Thomas Kashilila, Watendaji wote wa Ofisi ya Bunge kwa moyo
wenu wa upendo, uzalendo mkaamua kiasi hiki cha fedha Bilioni 6
zikafanye kazi ya maendeleo kwani mngeweza kuzitumia fedha hizi katika
matumizi mengine hata Mhe. Spika asingejua". Alisema Rais Magufuli.
Aidha,
Rais Magufuli amewataka Makatibu Wakuu wote wa Wizara pamoja na
Watendaji Wakuu wote wa Taasisi za Umma/Serikali kuiga mfano huo wa
kizalendo aliouonesha Katibu wa Bunge,
Dkt. Thomas Kashilila kwani huo
ndio mwelekeo anaoutaka katika Serikali yake ya Awamu ya Tano.
Awali
akiongea kabla ya Makabidhiano ya hundi hiyo Naibu Spika wa Bunge la
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Tulia Ackson amesema kuwa
kiasi hicho cha fedha kimepatikana kufuatia kubana matumizi katika
maeneo mbalimbali ikiwemo kupunguza safari za nje, gharama za machapisho
mbalimbali, gharama za viburudisho na chakula, matibabu kwa wabunge,
mafuta na uendeshaji wa mitambo nk.
Akizungumzia
utekelezaji wa jukumu la utengenezaji wa madawati hayo Kamishna
Jenerali wa Jeshi la Magereza Nchini, John Casmir Minja amesema kuwa
Jeshi la Magereza lipo tayari kutekeleza agizo la Rais na amejipanga
kutumia nguvu kazi ya Wafungwa waliopo magerezani pamoja na Maafisa na
Askari wa Jeshi hilo ili kukamilisha kazi hiyo kwa wakati kama
ilivyokusudiwa.
"Mhe. Rais ametoa maelekezo ya kwenda kufanya kazi hiyo kama operesheni maalum hivyo sisi kwa upande wa Jeshi letu tupo tayari kuifanya kazi hiyo kama ilivyoelekezwa kwa kuzingatia maelekezo ya Mhe. Rais". Alisema Jenerali Minja.
"Mhe. Rais ametoa maelekezo ya kwenda kufanya kazi hiyo kama operesheni maalum hivyo sisi kwa upande wa Jeshi letu tupo tayari kuifanya kazi hiyo kama ilivyoelekezwa kwa kuzingatia maelekezo ya Mhe. Rais". Alisema Jenerali Minja.
Jeshi la Magereza
Tanzania limepiga hatua kubwa ya Maboresho juu ya utengenezaji wa bidhaa
bora za Samani hivyo kupelekea kuibuka mara kwa mara Mshindi wa kwanza
katika Maonesho mbalimbali ya Kibiashara hapa nchini.
Tuesday, April 5, 2016
Majina ya walioongezwa kujiunga na Jeshi la Magereza Tanzania Bara
11:22 AM
S/N | JINA | KAMBI ATOKAKO |
1 | WALES YOHANA MNKAI | MAFINGA |
2 | VICTOR ROBERT JACOB | NACHINGWEA |
3 | RASHID JABU ISSA | OLJORO |
4 | GILBERT HONESPHORY GEREVAZI | BULOMBORA |
5 | ELISHA FAUSTIN MAHANDAKI | MBWENI |
6 | UPENDO CHARLES HIZZA | RWAMKOMA |
7 | TABITHA PAUL STEPHANO | KANEMBWA |
8 | YONNIE WILFRED MWAILAFU | MGULANI |