Mojawapo ya Jukumu la Jeshi la Magereza ni kuwapeleka mahakamani mahabusu na kuwarudisha magerezani.

Gadi ya askari Wanawake na Wanaume wa Jeshi la Magereza katika Maadhimisho ya Sherehe za Kitaifa.

Ng'ombe bora wa Nyama na Maziwa ni sehemu ya miradi ya Uzalishaji inayoendeshwa na kusimamiwa na Jeshi la Magereza nchini.

Sehemu ya Mashamba makubwa yanayoendeshwa na Jeshi la Magereza: Shughuli za Kilimo cha Mashamba makubwa, madogo na bustani za mboga mboga ni moja ya shughuli za Magereza katika kuwafunza wafungwa namna ya kujitegemea mara wamalizapo vifungo vyao.

Baadhi wa wafungwa katika Kiwanda cha Ushonaji nguo cha Gereza Kuu Ukonga wakiwa kazini: Shughuli za Ushonaji wa nguo ni moja ya eneo ambalo wafungwa hupata huduma za urekebishwaji kwa vitendo.

Wednesday, September 13, 2017

FOMU ZA UN AFRIKA YA KATI

Maafisa waliopewa maelekezo ya kujaza fomu za UN Afrika ya kati wajaze fomu hizo hapa chini na wazitume kama walivyoelekezwa.

  1. Annex 1: United Nations Personal History Profile for Government Provided Corrections Personnel
  2. Entry Medical Examination
  3. MINUSCA P5 Senior Corrections Officer

Friday, September 8, 2017

KAMISHNA JENERALI WA MAGEREZA, DKT JUMA MALEWA APOKEA MISAADA YA KIBINADAMU YA WAFUNGWA, MKOANI KILIMANJARO

Mwenyekiti wa New Life In Christ Mkoani Kilimanjaro, Bi. Elly Makyao (kulia) akikabidhi misaada ya kibinadamu ya Wafungwa waliopo Magerezani nchini kwa Kamishna Jenerali wa Magereza Nchini, Dkt. Juma Malewa. Hafla fupi ya Makabidhiano ya Misaada hiyo imefanyika leo Septemba 08, 2017 katika Viwanja vya Gereza Kuu Karanga – Moshi, Mkoani Kilimanjaro.
Kamishna Jenerali wa Magereza Nchini, Dkt. Juma Malewa akitoa hotuba fupi wakati wa hafla ya kupokea misaada ya kibinadamu kwa Wafungwa waliopo Magerezani iliyotolewa na Asasi ya "New Life In Christ" leo Septemba 08, 2017 katika Viwanja vya Gereza Kuu Karanga - Moshi, Mkoani Kilimanjaro.
Mkurugenzi wa Doricas Aide International - Tawi la Tanzania, Bi. Lilian Urasa akitoa maelezo mafupi namna Shirika linavyoshirikiana na Serikali katika Nyanja mbalimbali hapa nchini.
Aina mbalimbali ya misaada ya kibinadamu iliyotolewa kwa Wafungwa waliopo Magerezani nchini na Asasi ya "New Life In Christ". Hafla ya Makabidhiano ya misaada hiyo imefanyika leo Septemba 08, 2017 katika Viwanja vya Gereza Kuu Karanga, Moshi ambapo Mgeni rasmi alikuwa ni Kamishna Jenerali wa Magereza nchini, Dkt. Juma Malewa.
Kamishna Jenerali wa Magereza nchini, Dkt. Juma Malewa akiwakabidhi cheti cha shukrani Viongozi wa Asasi ya "New Life In Christ" kwa kutambua mchango wao kwa niaba ya Jeshi la Magereza Tanzania na Serikali kwa ujumla.
Kamishna Jenerali wa Magereza nchini, Dkt. Juma Malewa akimsukuma askari ambaye ameketi kwenye Baiskeli Maalum ya kubebea wagonjwa wasiojiweza ambayo ni miogoni mwa vifaa mbalimbali vilivyotolewa kama msaada kwa Jeshi la Magereza na Asasi ya "New Life In Christ"(kushoto) ni Mkurugenzi wa Doricas Aide International anayeshughulikia Miradi ya Afya katika nchi za Africa, Bi. Mirjam Verwij.
Baadhi ya Wakuu wa Magereza waliohudhuria hafla hiyo wakifuatilia kwa umakini hafla ya tukio hilo kama inavyoonekana katika picha.
Mkuu wa Magereza Mkoani Dodoma, Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Magereza, Julius Sangu’udi(wa kwanza kushoto) akiteta jambo na Mkuu wa Magereza Mkoa Tanga, Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Magereza, John Masunga na Mkuu wa Magereza Mkoani Morogoro, Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Magereza, Ramadhani Nyamka kama inavyoonekana katika picha.
Wafungwa wa Kike wa Gereza Kuu Karanga, moshi wakionesha mikate na skonsi zinazotengenezwa na wafungwa wa Kike katika gereza hilo ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa programu mbalimbali za urekebishaji magerezani.
Kamishna Jenerali wa Magereza Nchini, Dkt. Juma Malewa(katikati) akiwa katika picha ya pamoja Askari wa Magereza Mkoani Kilimanjaro(waliosimama) pamoja na Viongozi Wawakilishi wa Asasi ya "New Life In Christ" mara baada ya kupokea misaada ya kibinadamu ya Wafungwa waliopo Magerezani nchini (wa kwanza kushoto) ni Mwenyekiti wa New Life In Christ Mkoani Kilimanjaro, Bi. Elly Makyao(wa pili kushoto) ni Mratibu wa Huduma za Magereza toka Asasi ya "New Life In Christ", Bw. Charles Shang'aa (wa pili kulia) ni Mkuu wa Magereza Mkoani Arusha, Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Magereza, Khamis Nkubasi( wa tatu kulia) ni Mkuu wa Magereza Mkoani Kilimanjaro, Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Magereza, Hassan Mkwiche. 

(Picha zote na Lucas Mboje wa Jeshi la Magereza).

Tuesday, September 5, 2017

KAMISHNA WA FEDHA NA UTAWALA GHASTON K. SANGA APOKEA VIFAA NYA KUHIFADHIA TAKATAKA KUTOKA KWA TAASISI YA MIKOPO YA FAIDIKA.

KAMISHNA WA FEDHA NA UTAWA WA JESHI LA MAGEREZA GHASTON K. SANGA AKIPOKEA BAADHI YA VIFAA VYA KUHIFADHIA TAKATAKA KUTOKA KWA MKURUGENZI WA HUDUMA ZA WATEJA WA FAIDIKA BW. MBUSO DLIMIN ALIPO TEMBELEA OFISI ZA MAKAO MAKUU YA MAGEREZA.
KAMISHNA WA FEDHA NA UTAWALA WA JESHI LA MAGEREZA GHASTAN K. SANGA AKIWASHUKURU TAASISI YA MUKOPO YA FAIDIKA KWA KULIUNGA MKONO JESHI LA MAGEREZA  KWA KUTUZA MAZINGIRA  AMBAPO FAIDIKA IMETOA MSAA WA VIFAA VYA KUDIFADHIA TAKATAKA.
BAADHI YA MAAFISA WA MAGEREZA WAKIANGALIA KWA MAKINI MAKABIDIANO YA VIFAA VYA KUHIFADHIA TAKATAKA VILIVYO TOLEWA NA TAASISI YA MIKOPO YA FAIDIKA.
BAADHI YA MAAFISA WA MAGEREZA WAKIANGALIA KWA MAKINI MAKABIDIANO YA VIFAA VYA KUHIFADHIA TAKATAKA VILIVYO TOLEWA NA TAASISI YA MIKOPO YA FAIDIKA.
KAMISHNA WA FEDHA NA UTAWALA WA JESHI LA MAGEREZA AKIWA NA BAADI YA MAAFISA WA MAGEREZA NA MAAFISA WA TAASISI YA MIKOPO YA FAIDIKA NA LETSHEGO WALIPOKUJA MAKAO MAKUU YA MAGEREZA KUTOA MSAADA WA VIFAA VYA KUHIFADHIA TAKATAKA.

Saturday, September 2, 2017

WAZIRI MKUU MAJALIWA ATEMBELEA MRADI WA KIWANDA CHA SUKARI, GEREZA MBIGIRI MKOANI MOROGORO

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa(Mb)  akisalimiana na Kamishna Jenerali wa Magereza, Dkt. Juma Malewa alipofanya ziara ya kikazi ya kukagua maandalizi ya kufufua Kiwanda cha Sukari na Kilimo cha miwa katika Gereza la Mbigiri Mkoani Morogoro Septemba 2, 2017. Jeshi la Magereza kwa kushirikiana na Mifuko ya Jamii ya PPF na NSSF limeingia ubia katika mradi huo wa uchumi wa viwanda chini ya Kampuni ya MKULAZI.
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa(Mb) akiangalia mbegu za miwa kabla ya kuzipanda katika eneo la Shamba la miwa alipowasili Gereza Mbigiri katika ziara ya kikazi ya kukagua maandalizi ya kufufua Kiwanda cha Sukari na Kilimo cha miwa katika Gereza la Mbigiri Mkoani Morogoro Septemba 2, 2017. Kulia ni Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Ajira na Watu wenye ulemavu) Mhe. Jenista Mhagama.
Shamba la miwa katika mradi wa Kiwanda cha Sukari na Kilimo cha miwa - MKULAZI katika eneo la Gereza la Mbigiri Mkoani Morogoro likiwa limestawi kama inavyoonekana katika picha.
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa akitoa hotuba fupi kwa  Maafisa na askari wa Jeshi la Magereza Mkoani Morogoro, Watendaji wa Kampuni ya MKULAZI pamoja na Wananchi wanaoishi jirani na Gereza Mbigiri katika ziara ya kikazi ya kukagua maandalizi ya kufufua Kiwanda cha Sukari na Kilimo cha miwa katika Gereza la Mbigiri Mkoani Morogoro Septemba 2, 2017.
Kamishna Jenerali wa Magereza, Dkt. Juma Malewa akitoa maelezo mafupi kwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim(hayupo pichani) namna Jeshi hilo lilivyojipanga katika kuhakikisha kuwa ufufuaji wa Kiwanda cha Sukari na Kilimo cha miwa katika Gereza la Mbigiri Mkoani Morogoro unakamilika kama ilivyopangwa ambapo matarijio ni kuwa Kiwanda hicho kitakuwa na uwezo wa kuzalisha sukari tani 50,000 kwa mwaka.
Maafisa Waandamizi wa PPF na NSSF wakifuatilia kwa makini hotuba ya Waziri Mkuu, Mhe. Kassim Majaliwa(hayupo pichani).
Baadhi ya Maafisa Waandamizi wa Jeshi la Magereza pamoja na Wakuu wa Vyombo vya Ulinzi na Usalama wa Mkoani Morogoro wakimsikiliza Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa alipofanya ziara ya kikazi ya kukagua maandalizi ya kufufua Kiwanda cha Sukari na Kilimo cha miwa katika Gereza la Mbigiri Mkoani Morogoro Septemba 2, 2017.
Mkurugenzi Mkuu wa NSSF Prof. Godius Kyaharara akitoa maelezo mafupi kwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa alipofanya ziara ya kikazi ya kukagua maandalizi ya kufufua Kiwanda cha Sukari na Kilimo cha miwa katika Gereza la Mbigiri Mkoani Morogoro Septemba 2, 2017.
Kamishna Jenerali wa Magereza, Dkt. Juma Malewa(kushoto) akiteta jambo na Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Mhe. Charles Mwijage(kulia) mara baada ya ziara ya Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa ambapo amekagua maandalizi ya kufufua Kiwanda cha Sukari na Kilimo cha miwa katika Gereza la Mbigiri Mkoani Morogoro Septemba 2, 2017.
Mkurugenzi Mkuu wa PPF William Erio akitoa neno la shukurani mbele ya Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa alipofanya ziara ya kikazi ya kukagua maandalizi ya kufufua Kiwanda cha Sukari na Kilimo cha miwa katika Gereza la Mbigiri Mkoani Morogoro Septemba 2, 2017.
Ujenzi wa maghala ya kuhifadhia sukari katika mradi wa Kiwanda cha Sukari cha MKULAZI kilichopo Gereza Mbigiri ukiendelea katika hatua mbalimbali kama inavyoonekana katika picha
Wataalam wazalendo ambao wanajitolea katika ujenzi wa mradi wa Kiwanda cha Sukari – MKULAZI Mbigiri wakitambulishwa mbele ya Waziri Mkuu, Mhe. Kassim Majaliwa(hayupo pichani.

(Picha zote na Lucas Mboje wa Jeshi la Magereza).