Monday, September 23, 2019
KAMISHNA JENERALI PHAUSTINE KASIKE ARIDHISHWA NA UJENZI WA NYUMBA ZA GHARAMA NAFUU, GEREZA KUU ISANGA TAREHE 21 SEPT 2019
10:28 AM
Kamishna Jenerali wa Magereza, Phaustine
Kasike akisalimiana na Maafisa wa Jeshi la Magereza mkoani Dodoma alipowasili kwenye ukaguzi wa mradi wa ujenzi
wa nyumba za makazi ya Maafisa na askari katika Gereza Kuu Isanga, Septemba
21, 2019.
Kamishna Jenerali wa Magereza, Phaustine Kasike(mwenye
miwani) akikagua mradi wa ujenzi wa nyumba za makazi ya Maafisa na askari katika
Gereza Kuu Isanga, Septemba 21, 2019. Kulia kwake ni Mkuu wa Magereza
mkoani Dodoma, ACP. Keneth Mwambije.
Muonekano wa nyumba takribani 20 ambazo tayari zimejengwa katika mradi wa ujenzi wa nyumba za makazi ya Maafisa
na askari katika Gereza Kuu Isanga zikiwa katika hatua mbalimbali ya ujenzi.
Tofali
za kuchoma zikiwa tayari katika mradi
wa ujenzi wa nyumba za makazi ya Maafisa na askari katika Gereza Kuu Isanga.
Wafungwa wa Gereza Kuu
Isanga wakiendelea na kazi ya ujuenzi katika mradi wa ujenzi wa nyumba za makazi ya Maafisa
na askari katika Gereza Kuu Isanga ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa program ya
Urekebishaji magerezani.
Kamishna
Jenerali wa Magereza, Phaustine Kasike(mwenye miwani) akiangalia mbao zinazotumika katika hatua
mbalimbali za ujenzi wa mradi wa nyumba za makazi ya Maafisa na askari katika Gereza Kuu Isanga, alipotembelea eneo hilo la ujenzi, Septemba 21, 2019. (Picha zote na Jeshi la Magereza).
Tuesday, September 10, 2019
Monday, September 2, 2019
MAKAMISHNA WASTAAFU WA JESHI LA MAGEREZA WALIOSTAAFU UTUMISHI WAO KWA MUJIBU WA SHERIA, WAAGWA JIJINI DAR TAREHE 31/09/2019
12:01 PM
Kamishna Mstaafu wa Magereza, Gedion
Nkana(kushoto) na Kamishna Mstaafu wa Magereza, Augustine Mboje(kulia) wakiwa
kwenye gari maalum wakipita katikati ya Gwaride likiwa katika umbo la OMEGA
ikiwa ni ishara ya kuwaaga rasmi baada ya kustaafu utumishi wao Jeshini. Hafla
hiyo imefanyika katika Viwanja vya Chuo cha Taaluma ya Urekebishaji Tanzania, Ukonga
jijini Dar es Salaam Agosti 30, 2019.
Makamishna
Wastaafu wa Magereza wakipita katika gari maalum wakiwapungia mikono Maafisa na
askari pamoja na Wageni mbalimbali waliofika katika hafla ya kuwaaga wastaafu
hao iliyofanyika katika Viwanja vya Chuo
cha Taaluma ya Urekebishaji Tanzania, Ukonga jijini Dar es salaam Agosti 30,
2019
Kamishna
Jenerali wa Magereza nchini, Phaustine Kasike(wa pili toka kushoto) akiwa na
Maafisa Waandamizi kutoka Vyombo vya Ulinzi na Usalama nchini wakiwapungia
mikono Makamishna Wastaafu wa Jeshi la
Magereza(hawapo pichani) katika hafla ya kuwaaga wastaafu hao iliyofnyika katika Viwanja vya Chuo cha Taaluma ya
Urekebishaji Tanzania, Ukonga jijini Dar es salaam Agosti 30, 2019.
Kamishna
Mstaafu wa Magereza, Gedion Nkana akikagua Gwaride maalum lililoandaliwa na
Maofisa na askari wa Jeshi la Magereza kwa ajili ya kuwaaga wastaafu wa Jeshi
hilo leo
Agosti 30, 2019.
Gwaride maalum
lililoundwa na Maafisa na Askari wa Jeshi la Magereza likipita kwa mwendo wa
haraka mbele ya Makamishna Wastaafu wa Jeshi hilo ambao wamestaafu utumishi wao
kwa mujibu wa Sheria.
Kamishna Mstaafu wa Magereza, Gedion
Nkana(kushoto) na Kamishna Mstaafu wa Magereza, Augustine Mboje(kulia) wakiwa
katika jukwaa kuu wakipokea salaam ya heshima kutoka kwa Gwaride maalum la
kuwaaga leo Agosti 30, 2019 katika Viwanja vya Chuo cha Taaluma ya Urekebishaji Tanzania, Ukonga jijini
Dar es salaam.
Kamishna
Jenerali wa Magereza nchini, Phaustine Kasike akiteta jambo na Kamishna
Jenerali Mstaafu wa Magereza, John Casmir Minja mara baada ya gwaride maalum la
kuwaaga Makamishna wastaafu wa Jeshi hilo ambao wamestaafu utumishi wao Jeshini
kwa mujibu wa Sheria. Hafla hiyo imefanyika katika Viwanja vya Chuo cha Taaluma ya Urekebishaji Tanzania,
Ukonga jijini Dar es Salaam leo Agosti 30, 2019.
Kamishna
Jenerali wa Magereza nchini, Phaustine Kasike(wa tatu toka kulia) akiwa katika picha ya
pamoja na Makamishna Jenerali Wastaafu wa Jeshi la Magereza(walioketi) pamoja
na Makamishna Waliopo wa Jeshi Magereza, Makamishna Wastaafu wa Magereza na
Maafisa Waandamizi wastaafu wa Jeshi la Magereza(waliosimama mstari wa nyuma) mara
baada ya ya Gwaride rasmi la kuwaaga Makamishna Wastaafu wa Jeshi hilo leo
Agosti 30, 2019(Picha zote na
Jeshi la Magereza).