Mojawapo ya Jukumu la Jeshi la Magereza ni kuwapeleka mahakamani mahabusu na kuwarudisha magerezani.

Gadi ya askari Wanawake na Wanaume wa Jeshi la Magereza katika Maadhimisho ya Sherehe za Kitaifa.

Ng'ombe bora wa Nyama na Maziwa ni sehemu ya miradi ya Uzalishaji inayoendeshwa na kusimamiwa na Jeshi la Magereza nchini.

Sehemu ya Mashamba makubwa yanayoendeshwa na Jeshi la Magereza: Shughuli za Kilimo cha Mashamba makubwa, madogo na bustani za mboga mboga ni moja ya shughuli za Magereza katika kuwafunza wafungwa namna ya kujitegemea mara wamalizapo vifungo vyao.

Baadhi wa wafungwa katika Kiwanda cha Ushonaji nguo cha Gereza Kuu Ukonga wakiwa kazini: Shughuli za Ushonaji wa nguo ni moja ya eneo ambalo wafungwa hupata huduma za urekebishwaji kwa vitendo.

Friday, May 29, 2015

Sherehe za kufunga mafunzo ya awali ya jeshi la magereza kozi na. 27 chuo cha magereza Kiwira zafana, jijini Mbeya

Wahitimu wa Mafunzo ya Awali ya Uaskari Magereza wakipita kwa mwendo wa haraka mbele ya Mgeni rasmi, Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Bw. Mbarak Abdulwakil(hayupo pichani) leo Mei 29, 2015 katika Chuo cha Magereza, Kiwira Kilichopo Mkoani Mbeya.
Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza Nchini, John Casmir Minja akitoa maelezo mafupi kabla ya kumkaribisha Mgeni rasmi, Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi aweze kutoka hotuba ya kufunga rasmi Mafunzo ya Uaskari Magereza katika Chuo cha Magereza Kiwira, Mkoani Mbeya.
Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Bw. Mbarak Abdulwakil akipokea Salaam ya heshima akiwa jukwaan kabla ya kukagua Gwaride Maalum katika sherehe za kufunga Mafunzo ya Uaskari Magereza, Kiwira Mbeya(kushoto) ni Kamishna Jenerali wa Magereza, John Casmir Minja(kulia) ni Mkuu wa Chuo cha Magereza Kiwira, Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Magereza, Stanford Ntirundura.
 
Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Bw. Mbarak Abdulwakil akikagua Gwaride Maalum lililoandaliwa na Wahitimu wa Mafunzo ya Awali ya Uaskari Magereza leo Mei 29, 2015 Chuo cha Magereza Kiwira, Mbeya.
Katibu Mkuu akikabidhi zawadi kwa Mhitimu wa Kozi Na. 27 ya Uaskari Magereza ambaye amefanya vizuri katika Somo la Gwaride na Ukakamavu Askari Mhitimu, Ezra Kapesa leo katika sherehe za kufunga Mafunzo hayo Mkoani Mbeya(wa pili kushoto) ni Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza, John Casmir Minja.
Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza, John Casmir Minja(kulia) akimuongoza Mgeni rasmi, Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mbarak Abdulwakil(katikati) kuelekea kwenye Ukumbi wa Mihadhara kwa ajili ya kufunga rasmi Mafunzo ya Awali ya Uaskari Magereza leo Mei 29, 2015(kushoto) ni Mkuu wa Chuo cha Magereza Kiwira, Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Magereza, Stanford Ntirundura.
Gadi ya Askari wa Kike ambao ni Wahitimu wa Kozi ya Awali ya Uaskari Magereza wakila Kiapo cha Utii kwa Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama ambaye ni Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania mbele ya Mgeni rasmi, Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi(hayupo pichani) katika sherehe za ufungaji Mafunzo hayo.

(Picha zote na Lucas Mboje wa Jeshi la Magereza).

Wednesday, May 27, 2015

Kikao cha maafisa waandamizi wa Jeshi la Magereza nchini chaanza leo mkoani Morogoro

Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mbarak Abdulwakil akitoa hotuba ya ufunguzi leo Mei 26, 2015 kwenye Kikao cha Maafisa Waandamizi wa Jeshi la Magereza nchini kinachofanyika katika Ukumbi wa Hoteli ya Edema, Mkoani Morogoro.
Wajumbe wa Kikao ambao ni  Maafisa Waandamizi wa Jeshi la Magereza nchiniwa kifuatilia kwa makini hotuba ya Mgeni rasmi, Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mbarak Abdulwakil(wa kwanza kushoto) ni Mkuu wa Magereza Mkoa wa Dar es Salaam, Kamishna Msaidizi wa Magereza Joel Bukuku.
Mshauri Mwelekezi katika Maboresho ndani ya Jeshi la Magereza Nchini, Dkt. Haji Semboja kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam akiwasilisha Mada ya Maboresho ndani ya Jeshi la Magereza kwa Maafisa Waandamizi wa Jeshi la Magereza nchini.
Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza nchini, John Casmir Minja(kushoto) akiteta jambo na Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mbarak Abdulwakil kwenye kikao  cha Maafisa Waandamizi wa Jeshi la Magereza nchini kinachofanyika katika Ukumbi wa Hoteli ya Edema, Mkoani Morogoro.
Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mbarak Abdulwakil(shati jeupe) akiwa kwenye picha ya pamoja na Maafisa Waandamizi wa Jeshi la Magereza nchini waliosimama nyuma(wa sita kushoto) ni Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza nchini, John Casmir Minja(wa tano kushoto) ni Kamishna wa Fedha na Utawala wa Magereza, Gaston Sanga(wa tatu kulia) ni Kamanda wa Polisi Mkoa wa Morogoro, Leonard Paul.

(Picha zote na Lucas Mboje wa Jeshi la Magereza).

Monday, May 25, 2015

Katibu mkuu wizara ya mambo ya ndani ya nchi afungua kikao cha bajeti ya shirika la Magereza kwa mwaka 2015/2016 leo mkoani Morogoro

Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Bw. Mbarak Abdulwakil(suti nyeusi) akisalimiana na Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza, John Casmir Minja mara baada ya kuwasili leo Mei 25, 2015 katika Ukumbi wa Mikutano wa Edema, Mkoani Morogoro kwa ajili ya ufunguzi wa Kikao cha Bajeti ya Shirika la Magereza kwa Mwaka 2015/2016(wa pili kulia) ni Kamishna wa Huduma za Urekebishaji, Deonice Chamulesile.
Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza, John Casmir Minja akitoa maelezo mafupi kabla ya kumkaribisha Mgeni rasmi, Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Bw. Mbarak Abdulwakil(hayupo pichani) kutoa hotuba ya ufunguzi wa Kikao cha Bajeti ya Shirika la Magereza kwa Mwaka 2015/2016.
Wajumbe wa Kikao cha Bajeti ya Shirika la Magereza kwa Mwaka 2015/2016 wakifuatilia kwa makini hotuba ya mgeni rasmi leo Mei 25, 2015 katika Ukumbi wa Mikutano wa Edema, Mkoani Morogoro.
Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza, John Casmir Minja akimkabidhi Begi lenye makabrasha ya Kikao cha Bajeti ya Shirika la Magereza, Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Bw. Mbarak Abdulwakil(wa kwanza kulia) ni  Kamishna wa Huduma za Urekebishaji, Deonice Chamulesile.
Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Bw. Mbarak Abdulwakil(katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Wajumbe wa Kikao cha Bajeti ya Shirika la Magereza kwa Mwaka 2015/2016 waliosimama(wa tatu kushoto) ni Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza, John Casmir Minja(wa tatu kulia) ni  Kamishna wa Huduma za Urekebishaji, Deonice Chamulesile(wa pili kulia) ni Kamishna wa Fedha na Utawala, Gaston Sanga

(Picha zote na Lucas Mboje wa Jeshi la Magereza).