Friday, May 29, 2015

Sherehe za kufunga mafunzo ya awali ya jeshi la magereza kozi na. 27 chuo cha magereza Kiwira zafana, jijini Mbeya

Wahitimu wa Mafunzo ya Awali ya Uaskari Magereza wakipita kwa mwendo wa haraka mbele ya Mgeni rasmi, Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Bw. Mbarak Abdulwakil(hayupo pichani) leo Mei 29, 2015 katika Chuo cha Magereza, Kiwira Kilichopo Mkoani Mbeya.
Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza Nchini, John Casmir Minja akitoa maelezo mafupi kabla ya kumkaribisha Mgeni rasmi, Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi aweze kutoka hotuba ya kufunga rasmi Mafunzo ya Uaskari Magereza katika Chuo cha Magereza Kiwira, Mkoani Mbeya.
Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Bw. Mbarak Abdulwakil akipokea Salaam ya heshima akiwa jukwaan kabla ya kukagua Gwaride Maalum katika sherehe za kufunga Mafunzo ya Uaskari Magereza, Kiwira Mbeya(kushoto) ni Kamishna Jenerali wa Magereza, John Casmir Minja(kulia) ni Mkuu wa Chuo cha Magereza Kiwira, Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Magereza, Stanford Ntirundura.
 
Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Bw. Mbarak Abdulwakil akikagua Gwaride Maalum lililoandaliwa na Wahitimu wa Mafunzo ya Awali ya Uaskari Magereza leo Mei 29, 2015 Chuo cha Magereza Kiwira, Mbeya.
Katibu Mkuu akikabidhi zawadi kwa Mhitimu wa Kozi Na. 27 ya Uaskari Magereza ambaye amefanya vizuri katika Somo la Gwaride na Ukakamavu Askari Mhitimu, Ezra Kapesa leo katika sherehe za kufunga Mafunzo hayo Mkoani Mbeya(wa pili kushoto) ni Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza, John Casmir Minja.
Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza, John Casmir Minja(kulia) akimuongoza Mgeni rasmi, Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mbarak Abdulwakil(katikati) kuelekea kwenye Ukumbi wa Mihadhara kwa ajili ya kufunga rasmi Mafunzo ya Awali ya Uaskari Magereza leo Mei 29, 2015(kushoto) ni Mkuu wa Chuo cha Magereza Kiwira, Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Magereza, Stanford Ntirundura.
Gadi ya Askari wa Kike ambao ni Wahitimu wa Kozi ya Awali ya Uaskari Magereza wakila Kiapo cha Utii kwa Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama ambaye ni Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania mbele ya Mgeni rasmi, Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi(hayupo pichani) katika sherehe za ufungaji Mafunzo hayo.

(Picha zote na Lucas Mboje wa Jeshi la Magereza).