Wahitimu wa Mafunzo ya Awali ya Uaskari Magereza wakipita kwa mwendo wa
haraka mbele ya Mgeni rasmi, Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Ndani ya
Nchi, Bw. Mbarak Abdulwakil(hayupo pichani) leo Mei 29, 2015 katika Chuo
cha Magereza, Kiwira Kilichopo Mkoani Mbeya.
Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza Nchini, John Casmir Minja akitoa
maelezo mafupi kabla ya kumkaribisha Mgeni rasmi, Katibu Mkuu Wizara ya
Mambo ya Ndani ya Nchi aweze kutoka hotuba ya kufunga rasmi Mafunzo ya
Uaskari Magereza katika Chuo cha Magereza Kiwira, Mkoani Mbeya.
Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Bw. Mbarak Abdulwakil
akipokea Salaam ya heshima akiwa jukwaan kabla ya kukagua Gwaride Maalum
katika sherehe za kufunga Mafunzo ya Uaskari Magereza, Kiwira
Mbeya(kushoto) ni Kamishna Jenerali wa Magereza, John Casmir
Minja(kulia) ni Mkuu wa Chuo cha Magereza Kiwira, Kamishna Msaidizi
Mwandamizi wa Magereza, Stanford Ntirundura.
Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Bw. Mbarak Abdulwakil
akikagua Gwaride Maalum lililoandaliwa na Wahitimu wa Mafunzo ya Awali
ya Uaskari Magereza leo Mei 29, 2015 Chuo cha Magereza Kiwira, Mbeya.
Katibu Mkuu akikabidhi zawadi kwa Mhitimu wa Kozi Na. 27 ya Uaskari
Magereza ambaye amefanya vizuri katika Somo la Gwaride na Ukakamavu
Askari Mhitimu, Ezra Kapesa leo katika sherehe za kufunga Mafunzo hayo
Mkoani Mbeya(wa pili kushoto) ni Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza,
John Casmir Minja.
Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza, John Casmir Minja(kulia)
akimuongoza Mgeni rasmi, Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi,
Mbarak Abdulwakil(katikati) kuelekea kwenye Ukumbi wa Mihadhara kwa
ajili ya kufunga rasmi Mafunzo ya Awali ya Uaskari Magereza leo Mei 29,
2015(kushoto) ni Mkuu wa Chuo cha Magereza Kiwira, Kamishna Msaidizi
Mwandamizi wa Magereza, Stanford Ntirundura.
Gadi ya Askari wa Kike ambao ni Wahitimu wa Kozi ya Awali ya Uaskari
Magereza wakila Kiapo cha Utii kwa Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi
na Usalama ambaye ni Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania mbele ya
Mgeni rasmi, Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi(hayupo
pichani) katika sherehe za ufungaji Mafunzo hayo.
(Picha
zote na Lucas Mboje wa Jeshi la Magereza).