Mojawapo ya Jukumu la Jeshi la Magereza ni kuwapeleka mahakamani mahabusu na kuwarudisha magerezani.

Gadi ya askari Wanawake na Wanaume wa Jeshi la Magereza katika Maadhimisho ya Sherehe za Kitaifa.

Ng'ombe bora wa Nyama na Maziwa ni sehemu ya miradi ya Uzalishaji inayoendeshwa na kusimamiwa na Jeshi la Magereza nchini.

Sehemu ya Mashamba makubwa yanayoendeshwa na Jeshi la Magereza: Shughuli za Kilimo cha Mashamba makubwa, madogo na bustani za mboga mboga ni moja ya shughuli za Magereza katika kuwafunza wafungwa namna ya kujitegemea mara wamalizapo vifungo vyao.

Baadhi wa wafungwa katika Kiwanda cha Ushonaji nguo cha Gereza Kuu Ukonga wakiwa kazini: Shughuli za Ushonaji wa nguo ni moja ya eneo ambalo wafungwa hupata huduma za urekebishwaji kwa vitendo.

Friday, March 18, 2016

Orodha ya nyongeza ya majina ya waliochaguliwa kujiunga na jeshi la magereza


S/N JINA KAMBI YA JKT ATOKAYO
1 RAPHAEL STEPHANO MWAMBASHI ITENDE
2 RASHID MUSTAPHA MRAMBA ITENDE
3 HAMZA MOHAMED MAKAIKA ITENDE
4 SULTAN ABDALLAH MASSANJA ITENDE
5 SALIMA BAKARI MAVUKILO ITENDE
6 SALEHE ABBAS SALEHE ITENDE
7 MOHAMED ADAM LUKWELLE ITENDE
8 ALLY IAN BUGOYA ITENDE
9 SIMON DAUDI REGATA ITENDE
10 RAYMOND RAPHAEL NAKEI ITENDE
11 PROSPER MATHIAS ASENGA ITENDE
12 NICHOLAUS GODWIN MWAMBEBULE ITENDE/RUVU
13 RASHID ABDALLAH MZIRAY MGAMBO
14 REAGAN OCTAVIAN NGOWI RUVU
15 ANDREW VITUS JOPHN RUVU
16 YONA JOTHAM MWANGOKA RUVU
17 PASCHAL CLEMENCE MTENGA BULOMBORA
18 ISACK RICHARD HOYANGA BULOMBORA
19 REBECCA SALIM GUMBO BULOMBORA
20 JACKLINE AGRICOLA LIHIRU BULOMBORA
21 MASOKA KITWARA ELLY BULOMBORA
22 KAMSON FREDRICK MWANDAGONE BULOMBORA
23 ALEX LEOPOLD ULAYA BULOMBORA
24 SEIF RAMADHANI IDDI BULOMBORA
25 NELSON GERALD MUNYI BULOMBORA
26 FRANK NELSON TITO BULOMBORA
27 NOVATUS JEREMIA MASUNZU KANEMBWA
28 JUVENALI AMEDEUS TARIMO MAFINGA
29 WAISAKA CHACHA KICHELE MAKUTUPORA
30 PIUS SIMON HONGOA MAKUTUPORA
31 MICHAEL ALEX MWAKIHABA MAKUTUPORA
32 WANSAMA KENYUNKO EDWARD MAKUTUPORA
33 HIDAYA YOELI MBWAMBO MAKUTUPORA
34 GETRUDA SIMON YANSEBO MBWENI
35 AZIZI RAMADHANI MNG'ALI MBWENI
36 ANDREW MATHEW MAYUNGU MBWENI
37 BARAKA NGALILWA MBWENI
38 MIDIAN CHARLES MJUNGU MBWENI
39 JOSEPH DAMAS MHAGAMA MLALE
40 HAMISI SAID ONGOLOMA MLALE
41 ELIBARIKI MESIAKI SELEO MLALE
42 ZABRON GEORGE MLALE
43 NYOTA SEBASTIAN LUKUWI MLALE
44 VICENT THEOPHIL SHAGI MLALE
45 AMOS PASCHAEL BINAMUNGU MSANGE
46 FRANK FAUSTUS KAILI NACHINGWEA
47 GLORIUS OBERLIN MASAWE NACHINGWEA
48 WILFRED ASAGWILE MWALINGO NACHINGWEA
49 DAVID MATHIAS KAHYOLO RWAMKOMA
50 EUNICE PEJIWA SIMANDO RWAMKOMA
51 MAKENE ELIAS NYANKORO RWAMKOMA
52 MERINDA ALLOYCE MASIGE MGULANI
53 MARY SOSTENES BUGALAMA OLJORO
54 BERENADETHER ELIZEUS DOMINICK OLJORO
55 JACKSON DEOGRATIUS MICHAEL MTABILA
56 LILIAN DEOGRATIUS NYANYIGE MARAMBA

Monday, March 14, 2016

Waziri mkuu Kassim Majaliwa ampongeza kamishna jenerali wa magereza kwa namna anavyosimamia utendaji kazi mzuri wa jeshi hilo nchini

Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza nchini, CGP John Casmir Minja akisalimiana na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa(MB) alipotembelea Kambi Maalum ya Mwisa inayohifadhi Wakimbizi kutoka nchini Burundi leo Machi 14, 2016
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa(MB)akitoa hotuba yake fupi kwa Maafisa na askari wa  wa Jeshi la Magereza(hawapo pichani) kutoka vituo mbalimbali vya Magereza yaliyopo Mkoa wa Kagera alipotembelea Kambi ya Utenganisho ya Mwisa leo Machi 14, 2016.
Maafisa Waandamizi wa Jeshi la Magereza wakifuatilia kwa umakini mkubwa hotuba ya Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa(hayupo pichani).
Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza nchini, CGP John Casmir Minja akitoa taarifa fupi ya Hali ya Magereza nchini mbele ya Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa(hayupo pichani).
Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe. Hamad Masauni akitoa neno fupi kabla ya kumkaribisha rasmi Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa kutoa hotuba yake fupi.
Mkuu wa Magereza Mkoa wa Kagera, SACP. Omari (aliyesimama kushoto)  taarifa fupi ya Wambizi kwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa.
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa akiongea na Wakimbizi(walioketi chini) katika Kambi ya Mwisa inayosimamiwa na Jeshi la Magereza kwa kushirikiana na Shirika la kuwahudumia Wakimbizi Duniani(UNHCR).
Msafara wa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa ukiondoka katika Kambi ya Mwisa iliyopo Mkoani Kagera


WAZIRI MKUU  wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa amempongeza Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza, John Casmir Minja kwa utendaji wake mzuri wa kazi kwa namna anavyosimamia kikamilifu utekelezaji wa majukumu wa Jeshi hilo.

Pongezi hizo zimetolewa na Waziri Mkuu  kwenye ziara yake  Mkoani Kagera aliyoifanya katika Kambi ya Utenganisho ya Mwisa inayoendeshwa na Jeshi la Magereza kwa kushirikiana na Shirika la kuhudumia Wakimbizi Duniani(UNHCR).

"Nampongeza sana Kamishna Jenerali Minja hususani kwa kazi nzuri anayoifanya ya kuhakikisha kuwa  Jeshi la Magereza linaendelea kutekeleza kikamilifu majukumu yake kwa kuzingatia Sheria za Magereza mbali na changamoto kadhaa zinazolikabili Jeshi hilo ikiwemo Msongamano mkubwa uliopo Magerezani." Alisema Waziri Mkuu Majaliwa.

Aidha, ameongeza kuwa Serikali ya Awamu ya Tano imedhamilia kutatua baadhi ya changamoto mbalimbali zinazokabili Jeshi hilo ili kuwezesha ufanisi zaidi wa utekelezaji wa majukumu yake. 

Awali akitoa maelezo mafupi kwa Waziri Mkuu  kwenye ziara yake  Mkoani Kagera aliyoifanya katika Kambi ya Utenganisho ya Mwisa, Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza nchini, John Casmir Minja alisema kuwa Jshi la Magereza linakabiliwa na changamoto mbalimbali ambazo kwa kiasi fulani zinaathiri utekelezaji wa majukumu yake.
 
Jenerali Minja alizitaja baadhi ya changamoto hizo ni pamoja na Msongamano wa wafungwa Magerezani, ufinyu wa bajeti, makazi duni ya Maafisa n askari, uhaba wa vitendea kazi, uhaba na uchakavu wa vyombo vya usafiti na mawasiliano, ukosefu wa pembejeo, ukosefu  wa Magereza katika baadhi ya Wilaya mpya zinazoanzishwa kiutawala. 

Aidha,  Jenerali Minja amesema kuwa katika kukabiliana na changamoto hizo, Jeshi la Magereza limekuwa likifanya jitihada mbalimbali na za makusudi kwa kufanya maboresho katika maeneo kadhaa ili kujiongezea tija na ufanisi katika utekelezaji wa majukumu yake ya kila siku.

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa yupo Mkoani Kagera kwa lengo la kukagua miradi mbalimbali ya maendeleo Mkoani humo ambapo katika ziara yake pia ameweza kuitembelea Kambi ya Mwisa inayohifadhi Wakimbizi kutoka nchini Burundi.



(Picha na Lucas Mboje wa Jeshi la Magereza).
                                                                                                                             

    Sunday, March 13, 2016

    Kamishna Jenerali Minja atembelea kambi maalum ya wakimbizi kutoka Burundi inayosimamiwa na jeshi la Magereza pamoja na shamba la mifugo gereza Kitengule, mkoani Kagera

    Kamishna Jenerali wa Magereza, CGP John Casmir Minja akisalimiana na Mkuu wa Kambi ya Utenganisho Mwisa, SP. S. Lubinza alipotembelea katika Kambi hiyo Machi 12, 2016 kisha kuongea na Wakimbizi kutoka Burundi ambao wanazuiliwa katika Kambi hiyo kwa mujibu wa Sheria.
     Kamishna Jenerali wa Magereza, CGP John Casmir Minja pamoja na ujumbe wake aliofuatana nao akikagua sehemu mbalimbali za Kambi hiyo ili kuona kama zinakidhi viwango vinavyokubalika katika kuwahifadhi Wakimbizi hao ambao wanahifadhiwa katika Kambi hiyo.
    Askari Mlinzi kutoka Kikosi Maalum cha Jeshi la Magereza akiwa timamu kiulinzi kama anavyoonekana katika eneo lake la kazi ili kuhakikisha Ulinzi na Usalama wa Kambi hiyo Maalum iliyopo Mkoani Kagera.
    Kamishna Jenerali wa Magereza, CGP John Casmir Minja(katikati) akiongea na Wakimbizi kutoka nchini Burundi(hawapo pichani) ambao wanahifadhiwa katika Kambi hiyo Maalum kwa sababu za kiusalama.
    Sehemu ya kundi la ngo'mbe wa maziwa na nyama wakiwa zizini katika Shamba la Mifugo linalomilikiwa na Jeshi la Magereza katika Gereza la Kilimo Kitengule lililopo Mkoani Kagera.
    Kamishna Jenerali wa Magereza, CGP John Casmir Minja akikagua ujenzi unaoendelea wa Jengo la Banda la ndama katika  Shamba la Mifugo linalomilikiwa na Jeshi la Magereza katika Gereza la Kilimo Kitengule lililopo Mkoani Kagera alipotembelea katika ziara yake ya kikazi Machi 12, 2016.
    Kundi la ndama wakiwa zizini katika Shamba la Mifugo linalomilikiwa na Jeshi la Magereza katika Gereza la Kilimo Kitengule.

    (Picha zote na Lucas Mboje wa Jeshi la Magereza)

    Friday, March 11, 2016

    Ziara ya Kamishna Jenerali wa Magereza nchini mkoani Kagera

    Kamishna Jenerali wa Magereza John C. Minja( wa pili kushoto) akikagua maeneo mbalimbali ya Gereza Bukoba alipofanya ziara ya kikazi leo Machi 11, 2016 (wa kwanza kushoto) ni Mkuu wa Magereza Mkoa wa Kagera, SACP. Omari Mtiga (wa pili kulia) ni Mkuu wa Gereza Bukoba, ACP. Benizeth Bisibe.
    Kamishna Jenerali wa Magereza John C. Minja (wa nne kushoto) akiwa katika picha ya pamoja na Maofisa Waandamizi wa Jeshi la Magereza Mkoani Kagera mara baada ya kutembelea Gereza la Wilaya ya Bukoba 
    Mkuu wa Mkoa wa Kagera Mhe. John Mongella akiongea ofisini kwake na Kamishna Jenerali wa Magereza John C. Minja na ujumbe wake (hawapo pichani)
    Mkuu wa Mkoa wa Kagera Mhe. John Mongella akiongea ofisini kwake na Kamishna Jenerali wa Magereza John C. Minja na ujumbe wake kama inavyoonekana katika picha.
    Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu Kanda ya Bukoba Mhe. Sivangilwa Mwangesi Akisalimiana na Kamishna Jenerali wa Magereza John C. Minja alipomtembelea ofisini kwake

    (Picha na Lucas Mboje wa Jeshi la Magereza).


    Kamishina Jenerali wa Mageraza nchini John Carmir Minja afanya ziara ya kikazi  Mkoani Kagera yenye lengo la kutembelea na kukagua Magereza ya Mkoa wa Kagera pamoja na kujionea miradi ya uzalishaji inayosimamiwa na Jeshi hilo.

    Akiwa Mkoani hapa Kamishna Jenerali Minja alifika ofisini kwa Mkuu wa Mkoa wa Kagera Mhe. John Mongella na kufanya naye mazungumzo kuhusu utendaji kazi na ufanisi wa Jeshi la Magereza Mkoani hapa katika kuimarisha ulinzi na usalama.

    Aidha katika mazungumzo hayo walizungumzia  changamoto ya  msongamano wa Mahabusu katika Gereza la Wilaya ya Muleba ambalo hivi sasa linatumika kuhifadhi Mahabusu wa Wilaya ya Muleba na Wilaya ya Chato Mkoani Geita ambayo haina Gereza la Wilaya.

    Kamishna Jenerali wa Mageraza nchini John Carmir Minja pia alitembelea Mahakama Kuu Kanda ya Bukoba na kufanya mazungumzo na Jaji Mfawidhi wa Mahakama hiyo Mhe. Sivangilwa Mwangesi juu ya namna ya kuongeza kasi ya usikilizwaji wa kesi mbalimbali za watuhumiwa ili kuondoa msongamano Magerezani.

    Vilevile Kamishna Jenerali Minja alitembelea Gereza la Wilaya la Bukoba na kuongea na wafungwa na Mahabusu wa Gereza  hilo pia na kukagua mradi wa ujenzi wa jengo la zahanati ambalo lipo katika hatua za mwisho kukamilishwa ili liweze kutoa huduma za afya kwa wafungwa na watumishi wa Jeshi hilo pamoja na wananchi wanaoishi jirani na zahanati hiyo.

    Kamishna Jenerali Minja yupo Mkoani Kagera kwa siku 7 kuanzia tarehe 10 hadi 16 Machi, 2016 ambapo lengo la ziara hiyo ni kutembelea na kukagua Magereza ya Mkoa wa Kagera pamoja na kujionea miradi ya uzalishaji inayosimamiwa na jeshi hilo.


    Thursday, March 10, 2016

    Kamishna Jenerali wa Magereza atembelea gereza Biharamulo pamoja na eneo linakojengwa gereza la wiliya ya Chato mkoani Geita

    Kamishna Jenerali wa Magereza - CGP John Casmir Minja akisalimiana na Mkuu wa Gereza Kuu Butimba, Mwanza Kamishna Msaidizi wa Magereza, Jaili Mwamugunda alipowasili katika Uwanja wa Ndege wa Mwanza kabla ya kuanza ziara yake ya kikazi Mkoani Kagera ambapo leo Machi 10, 2016 ametembelea eneo kunakojengwa Gereza la Wilaya ya Chato lililopo Mkoani Geita pamoja na Gereza la Wilaya ya Biharamulo(wengine) ni Maofisa wa Jeshi la Magereza kutoka Ofisi ya Magereza Mkoani Mwanza.
    Kamishna Jenerali wa Magereza, John Casmir Minja akifurahia jambo pamoja na Luteni Jenerali Mstaafu Samuel Ndomba walipokutana katika Kivuko cha Busisi kabla ya kuendelea na safari kuekelea Mkoani Kagera(kulia) ni Mkuu wa Magereza Mkoani Mwanza, Goleha Masunzu.
    Mkuu wa Wilaya ya Chato, Mhe. Shaban Ntarambe(kushoto) akiwa na Kamati yake ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya wakielekea eneo linakojengwa Gereza la Wilaya ya Chato mara baada ya Kamishna Jenerali wa Magereza kuwasili Wilayani Chato kabla ya kuelekea Mkoani Kagera.
    Mkuu wa Magereza Mkoani Kagera, Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Magereza, Omar Mtiga(wa pili kushoto) akimuonesha Kamishna Jenerali wa Magereza, John Casmir Minja(wa tatu kulia) nyumba mbili za Askari wa Jeshi la Magereza ambazo tayari zimekamilika katika eneo linakojengwa Gereza la Wilaya ya Biharamulo(wa pili kulia) ni Mkuu wa Wilaya ya Chato, Mhe. Shaaban Ntarambe.
    Kamishna Jenerali wa Magereza, John Casmir Minja(suti nyeusi) akiwa na Wajumbe wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya ya Chato wakiaangalia moja ya Bweni la kulala Wafungwa/Mahabusu ambalo tayari limekamilika katika eneo linakojengwa Gereza la Wilaya ya Chato Mkoani Geita. Kukamilika kwa Gereza hilo kutasaidia kutatua tatizo la Msongamano wa Wafungwa na Mahabusu katika Magereza ya Biharamulo na Gereza Muleba.
    Kamishna Jenerali wa Magereza John Casmir Minja akisaini katika kitabu cha Wageni alipotembelea Gereza la Wilaya ya Biharamulo katika ziara yake ya kikazi leo Machi 10, 2016.
    Mkuu wa Gereza la Biharamulo, Mrakibu Mwandamizi wa Magereza, Gidion Kakulu akimuonesha Kamishna Jenerali wa Magereza maeneo mbalimbali ya Gereza hilo katika ziara yake ya Kikazi leo Machi 10, 2016. Wengine ni Maafisa Waandamizi wa Jeshi hilo ambao wameambatana na Kamishna Jenerali wa Magereza katika ziara yake ya kikazi.




    Wednesday, March 9, 2016

    Tangazo la kuitwa chuoni

    JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
    WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI

    (Jeshi la Magereza)
    TANGAZO LA KUITWA CHUONI
    Kamishna Jenerali wa Magereza Tanzania Bara anawatangazia wafuatao kuwa wamechaguliwa kujiunga na Jeshi la Magereza baada ya Usaili kufanyika katika kambi mbalimbali za JKT.  Usaili huu ulihusu vijana waliohitimu Shahada ya Kwanza, Stashahada, Astashahada, Kidato cha Sita na Kidato cha Nne.

    Wahusika wote wanatakiwa kuripoti katika Ofisi za Wakuu wa Magereza Mikoa mara wapatapo taarifa hii tayari kwa safari ya kwenda Chuo cha Mafunzo ya Awali kilichopo Kiwira Tukuyu Mkoani Mbeya.

    Mafunzo yanategemewa kuanza tarehe 12 Machi, 2016 hivyo mwisho wa kuripoti chuoni ni tarehe 14 Machi, 2016.  Yeyote atakayeshindwa kuripoti kwa tarehe iliyotamkwa kwenye tangazo hili hatapokelewa.

    Wahusika wanatakiwa kuzingatia mambo yafuatayo:-

    1.          Walete vyeti halisi vya masomo na vya kuzaliwa, vikiwa na pamoja na nakala 5 za kila cheti.

    2.          Picha (Passport size) za rangi 5 za hivi karibuni.

    3.         Chandarua cheupe cha duara ft 31/2, shuka nyeupe mbili, mto wenye foronya nyeupe zisizo na maua/maandishi.

    4.           Fedha taslimu Tshs.90,000/=.

    5.           Kalamu za wino,  za risasi na madaftari ya kutosha.

    6.           Cheti cha afya kutoka kwa hospitali ya Serikali.

    7.           Nguo za kiraia za kutosha sweta, raba (Brown au nyeusi) na soksi

    8.           Kwa wale wenye kadi za Bima waje nazo na

    9.           Kila mwanafunzi atajitegemea kwa nauli ya kwenda.

    Tangazo hili linapatikana kwenye mbao za matangazo zilizopo Ofisi za Magereza, tovuti ya Magereza kwa anwani ya www.magereza.go.tz sanjari na blog ya Magereza kwa anwani ya www.magereza.blogspot.com

    Imetolewa na Kamishna Jenerali wa Magereza.

    SIGNED
    Dr. J. A. Malewa  -  CP
    Kny:  KAMISHNA JENERALI WA MAGEREZA