Wednesday, March 9, 2016

Tangazo la kuitwa chuoni

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI

(Jeshi la Magereza)
TANGAZO LA KUITWA CHUONI
Kamishna Jenerali wa Magereza Tanzania Bara anawatangazia wafuatao kuwa wamechaguliwa kujiunga na Jeshi la Magereza baada ya Usaili kufanyika katika kambi mbalimbali za JKT.  Usaili huu ulihusu vijana waliohitimu Shahada ya Kwanza, Stashahada, Astashahada, Kidato cha Sita na Kidato cha Nne.

Wahusika wote wanatakiwa kuripoti katika Ofisi za Wakuu wa Magereza Mikoa mara wapatapo taarifa hii tayari kwa safari ya kwenda Chuo cha Mafunzo ya Awali kilichopo Kiwira Tukuyu Mkoani Mbeya.

Mafunzo yanategemewa kuanza tarehe 12 Machi, 2016 hivyo mwisho wa kuripoti chuoni ni tarehe 14 Machi, 2016.  Yeyote atakayeshindwa kuripoti kwa tarehe iliyotamkwa kwenye tangazo hili hatapokelewa.

Wahusika wanatakiwa kuzingatia mambo yafuatayo:-

1.          Walete vyeti halisi vya masomo na vya kuzaliwa, vikiwa na pamoja na nakala 5 za kila cheti.

2.          Picha (Passport size) za rangi 5 za hivi karibuni.

3.         Chandarua cheupe cha duara ft 31/2, shuka nyeupe mbili, mto wenye foronya nyeupe zisizo na maua/maandishi.

4.           Fedha taslimu Tshs.90,000/=.

5.           Kalamu za wino,  za risasi na madaftari ya kutosha.

6.           Cheti cha afya kutoka kwa hospitali ya Serikali.

7.           Nguo za kiraia za kutosha sweta, raba (Brown au nyeusi) na soksi

8.           Kwa wale wenye kadi za Bima waje nazo na

9.           Kila mwanafunzi atajitegemea kwa nauli ya kwenda.

Tangazo hili linapatikana kwenye mbao za matangazo zilizopo Ofisi za Magereza, tovuti ya Magereza kwa anwani ya www.magereza.go.tz sanjari na blog ya Magereza kwa anwani ya www.magereza.blogspot.com

Imetolewa na Kamishna Jenerali wa Magereza.

SIGNED
Dr. J. A. Malewa  -  CP
Kny:  KAMISHNA JENERALI WA MAGEREZA