Mojawapo ya Jukumu la Jeshi la Magereza ni kuwapeleka mahakamani mahabusu na kuwarudisha magerezani.

Gadi ya askari Wanawake na Wanaume wa Jeshi la Magereza katika Maadhimisho ya Sherehe za Kitaifa.

Ng'ombe bora wa Nyama na Maziwa ni sehemu ya miradi ya Uzalishaji inayoendeshwa na kusimamiwa na Jeshi la Magereza nchini.

Sehemu ya Mashamba makubwa yanayoendeshwa na Jeshi la Magereza: Shughuli za Kilimo cha Mashamba makubwa, madogo na bustani za mboga mboga ni moja ya shughuli za Magereza katika kuwafunza wafungwa namna ya kujitegemea mara wamalizapo vifungo vyao.

Baadhi wa wafungwa katika Kiwanda cha Ushonaji nguo cha Gereza Kuu Ukonga wakiwa kazini: Shughuli za Ushonaji wa nguo ni moja ya eneo ambalo wafungwa hupata huduma za urekebishwaji kwa vitendo.

Monday, December 23, 2019

KAMISHNA JENERALI WA MAGEREZA NCHINI, PHAUSTINE KASIKE AHIMIZA WAFUASI WAKE KUZINGATIA NIDHAMU JESHINI

Kamishna Jenerali wa Magereza nchini Phaustine Kasike akizungumza katika kikao na Maafisa na askari wa vituo vya Magereza Mkoa wa Dar es Salaam ambapo kikao hicho kilijadili masuala mbalimbali ikiwemo masuala ya utendaji kazi, maadili ya kazi, nidhamu na mikakati mbalimbali ya Jeshi ikiwemo ya Kilimo, viwanda na ufugaji. Kikao kazi hicho kimefanyika Bwalo Kuu la Maafisa Magereza, Ukonga jijini Dar es Salaam.

Baadhi ya Maafisa Waandamizi wa Jeshi la Magereza kutoka vituo vya Magereza Mkoa wa Dar es Salaam wakimsikiliza Kamishna Jenerali wa Magereza nchini, Phaustine Kasike(hayupo pichani) kikao hicho kilijadili masuala mbalimbali ikiwemo masuala ya utendaji kazi, maadili ya kazi, nidhamu na mikakati mbalimbali ya Jeshi ikiwemo ya Kilimo, viwanda na ufugaji.

Askari wa vyeo mbalimbali wa Jeshi la Magereza kutoka katika vituo vya Magereza Mkoa wa Dar es Salaam wakifuatilia mazungumzo ya kikao kazi na Kamishna Jenerali wa Magereza nchini Phaustine Kasike Desemba 20, 2019 (Picha zote na Jeshi la Magereza).

Saturday, December 14, 2019

UTEKELEZAJI WA ZOEZI LA KUWAACHILIA HURU WAFUNGWA WANUFAIKA WA MSAMAHA WA RAIS WAKAMILIKA NCHI NZIMA


Na ASP. Lucas Mboje, Dar es Salaam

JUMLA ya Wafungwa 5,533 katika magereza mbalimbali nchini walionufaika na msamaha wa Rais wakati wa  maadhimisho ya miaka 58 ya Uhuru wameachiliwa huru magerezani.
Akizungumza na wanahabari leo jijini Dar es Salaam, Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza, Phaustine Kasike amesema kuwa utekelezaji wa zoezi la kuwaachiliwa huru wafungwa wote walionufaika na msamaha wa Rais umekamilika nchi nzima.

“Ni matarajio yangu kuwa wafungwa walioachiliwa wamejutia makosa yao na wataacha kutenda uhalifu hivyo kujihusisha na shughuli halali kwa maendeleo yao, familia zao, jamii na taifa kwa ujumla”, amesisitiza Jenerali Kasike.

Aidha, Kamishna Jenerali Kasike ameelezea manufaa mbalimbali ya msamaha huo; mosi kupungua kwa msongamano magerezani, pili, wanufaika wa msamaha kujumuika na familia zao, tatu, kichocheo cha urekebishaji magerezani kwani msamaha huo utasaidia kuimarika kwa nidhamu na kurejesha matumaini kwa wanaobakia magerezani pamoja na wanufaika wa wamsamaha huo kupata fursa ya kujishughulisha na shughuli za maendeleo uraiani.

“Zipo changamoto zilizojitokeza katika utekelezaji wa zoezi hili ambapo baadhi ya wafungwa walionesha kuwa hawako tayari kuungana na jamii zao pamoja na waliosamehewa kurejea kutenda makosa mara baada ya kuachiwa huru. Hata hivyo nitoe wito kwa jamii nchini kuwapokea wafungwa hao na kuacha kuwanyanyapaa”, amesema Jenerali Kasike. 

Wakati huo huo, Kamishna Jenerali Kasike amemshukru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama, Dkt. John Pombe Magufuli kwa kutoa msamaha huo ambao ni wa kihistoria hapa nchini. Pia amewapongeza wanahabari wote nchini kwa namna walivyoshiriki kutoa habari za zoezi la msamaha huo katika ngazi ya Mkoa na wilaya.

Kwa mujibu wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ibara ya 45(1) (d) imempa mamlaka Rais kutoa msamaha kwa wafungwa waliopo magerezani. Kwa kutumia Ibara hiyo Rais Dkt. John Pombe Magufuli alitoa msamaha kwa wafungwa wakati wa maadhimisho ya miaka 58 ya Uhuru ambapo kilele chake kilifanyika Mkoani Mwanza Desemba 9, 2019.

Wednesday, December 11, 2019

WAFUNGWA 79 WA GEREZA KUU BUTIMBA WALIONUFAIKA NA MSAMAHA WA RAIS WAACHILIWA JIJINI MWANZA TAREHE 10 DISEMBA 2019

Mfungwa mnufaika wa Msamaha wa Rais, William Dingu akizungumza na Wanahabari(hawapo pichani) baada ya kuachiliwa huru leo. Mfungwa huyo amemshukru Rais kwa msamha huo, aidha,  amelipongeza Jeshi la Magereza kwa kumwezesha ujuzi wa wa fani ya ujenzi ambao ameupatia gerezani kupitia programu ya Urekebishaji inayosimamiwa na Jeshi hilo

Baadhi ya wafungwa wakiume wa Gereza Kuu Butimba walionufaika na Msamaha wa Rais wakitoka katika lango la Gereza Kuu Butimba tayari kwenda kuungana na familia zao. Wafungwa hao wamemshukru Rais Magufuli kwa msamaha huo wa kihistoria.


Wafungwa wa kike Gereza Kuu Butimba – Sehemu ya Wanawake wakitoka gerezani baada ya Msamaha wa Rais alioutoa jana katika maadhimisho ya miaka 58 ya uhuru. Wafungwa hao wamemshukru Rais Magufuli kwa msamaha huo na wameahidi kutokurejea katika uhalifu.

Kamati ya Ulinzi na Usalama Mkoani Mwanza pamoja na Kamishna  Jenerali wa Magereza nchini, Phaustine Kasike wakishuhudia wafungwa walionufaika na Msamaha wa Rais katika Gereza Kuu Butimba wakipewa mali zao na nauli ya kwenda kuungana na familia zao  Desemba 10, 2019 kabla ya zoezi la uachiliaji wa wafungwa husika wa msamaha huo.

Kamishna Jenerali wa Magereza nchini, CGP - Phaustine Kasike akitoa taarifa fupi ya zoezi zima la uachiliaji wa wafungwa walionufaika na msamaha wa Rais katika mikoa mbalimbali nchini mbele ya wanahabari kutoka vyombo mbalimbali vya Habari jijini Mwanza  Desemba 10, 2019.

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mhe. John Mongela ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa huo akizungumza na Wafungwa wa Gereza Kuu Butimba kabla ya zoezi la uachiliaji wa wafungwa walionufaika na Msamaha wa Rais  Desemba 10, 2019. Kushoto ni Kamishna Jenerali wa Magereza nchini, CGP - Phaustine Kasike.
(Picha zote na Jeshi la Magereza).




Tuesday, December 10, 2019

KAULI YA RAIS MAGUFULI KUHUSU MSAMAHA WA WAFUNGWA 5533 KATIKA MAADHIMISHO YA MIAKA 58 YA UHURU


Monday, November 18, 2019

CGP KASIKE AFANYA MAZUNGUMZO NA RC. MNYETI KABLA YA KUHITIMISHA ZIARA YAKE YA KIKAZI MKOANI MANYARA

Mkuu wa Jeshi la Magereza nchini - CGP Phaustine Kasike akitambulisha ujumbe alioambatanao kabla ya mazungumzo mafupi na na Mkuu wa Mkoa wa Manyara, Mhe. Alexander Mnyeti alipomtembelea Ofisini kwake kabla ya kuendelea na ziara yake ya kikazi Gereza Mbulu, leo Novemba 18, 2019. Mkuu huyo wa Jeshi la Magereza amehitimisha ziara yake leo ya siku tatu Mkoani Manyara ambapo ametembelea magereza na Kambi zote za magereza mkoani humo.
Mkuu wa Mkoa wa Manyara, Mhe. Alexander Mnyeti akizungumza na Mkuu wa Jeshi la Magereza nchini - CGP Phaustine Kasike(hayupo pichani) alipotembelea Ofisini kwake leo Novemba 18, 2019. 
Mkuu wa Jeshi la Magereza nchini - CGP Phaustine Kasike akiteta jambo na Mkuu wa Mkoa wa Manyara, Mhe. Alexander Mnyeti alipomtembelea Ofisi kwake leo kabla ya kuendelea na ziara yake ya kikazi Gereza Mbulu, leo Novemba 18, 2019. 
Mkuu wa Jeshi la Magereza nchini - CGP Phaustine Kasike(kushoto) akisalimiana na Mkuu wa Gereza Mbulu, SP. Danson Mpinga alipowasili Gereza Mbulu leo kwa ziara ya kikazi. Mkuu huyo wa Jeshi la Magereza amehitimisha ziara yake leo ya siku tatu Mkoani Manyara ambapo ametembelea magereza na Kambi zote za magereza mkoani humo.

Mkuu wa Jeshi la Magereza nchini - CGP Phaustine Kasike akizungumza na wafungwa na mahabusu wa Gereza Mbulu(hawapo pichani) leo Novemba 18, 2019 alipofanya ziara ya kikazi katika gereza hilo(Picha zote na Jeshi la Magereza).

KAMBI YA MAGEREZA KATESH YAPEWA LENGO LA KULISHA MAGEREZA YOTE YA MKOA WA MANYARA

Kamishna Jenerali wa Magereza nchini Phaustine Kasike(kushoto) akikagua maandalizi ya awali ya shamba la mahindi alipofanya ziara ya kikazi  Novemba 17, 2019 katika Kambi ya Magereza – Katesh iliyopo wilayani Hanang, Mkoa wa Manyara. Kulia ni Mkuu wa Magereza Mkoani Manyara, ACP. Lipina Lyimo.

Kamishna Jenerali wa Magereza nchini, Phaustine Kasike(wa pili toka kulia) akikagua moja ya trekta linalotumika kwa shughuli za Kilimo katika Kambi ya Magereza – Katesh iliyopo wilayani Hanang, Mkoa wa Manyara, Novemba 17, 2019 alipotembelea Kambi hiyo.

Moja ya maghala ya kuhifadhia mazao mbalimbali yanayozalishwa katika Kambi ya Magereza – Katesh iliyopo wilayani Hanang, Mkoa wa Manyara.

Kamishna Jenerali wa Magereza nchini, Phaustine Kasike akikagua mradi wa tofali za saruji ambazo zinafyatuliwa katika Gereza la Babati tayari kwa ujenzi wa nyumba za Maafisa na askari wa kituo hicho.(Picha zote na Jeshi la Magereza).

Thursday, November 14, 2019

KAMISHNA JENERALI WA MAGEREZA PHAUSTINE KASIKE AKAGUA UJENZI WA MAKAZI YA MAOFISA MAGEREZA UKONGA, APONGEZA HATUA KUBWA ILIYOFIKIWA TAREHE 13 NOVEMBA,2019

Kamishna Jenerali wa Magereza nchini, Phaustine Kasike akisalimiana na Maafisa wa SUMAJKT pamoja na Maafisa wa Jeshi la Magereza alipowasili katika eneo la ujenzi Gereza Kuu Ukonga Novemba 13, 2019 katika ziara yake ya kikazi yenye lengo la kukagua ujenzi unaoendelea wa makazi ya Maafisa na askari wa Magereza katika eneo la Gereza Kuu Ukonga, jijini Dar es Salaam.

Ofisa wa SUMAJKT, Meja Ashrafu Hassan akitoa taarifa fupi kwa Kamishna Jenerali wa Magereza, Phaustine Kasike alipotembelea  Novemba 13, 2019 kwa lengo la kukagua ujenzi huo.

Kamishna Jenerali wa Magereza nchini, Phaustine Kasike akikagua ujenzi wa majengo mbalimbali ya makazi ya Maafisa na Askari wa Magereza katika eneo la Gereza Kuu Ukonga. Kulia kwake ni Ofisa wa SUMAJKT, Meja Ashrafu Hassan akimuonesha baadhi ya maeneo ambayo bado yanafanyia maboresho ya miundombinu.

Kamishna Jenerali wa Magereza nchini, Phaustine Kasike akikagua miundombinu ya mitaro ya kupitishia maji ya mvua katika ujenzi wa majengo mbalimbali za makazi ya Maafisa na Askari wa Magereza katika eneo la Gereza Kuu Ukonga.

Moja ya majengo ya ghorofa yaliyojengwa kwa ajili ya makazi ya Maafisa na askari wa Magereza katika eneo la Gereza Kuu Ukonga, jijini Dar es Salaam yakiwa tayari yamekamilika kama inavyoonekana katika picha (Picha na Jeshi la Magereza).

Thursday, November 7, 2019

KAMISHNA JENERALI WA MAGEREZA NCHINI, PHAUSTINE KASIKE ATEMBELEA MRADI WA KOKOTO GEREZA MSALATO, MKOANI DODOMA





Kamishna Jenerali wa Magereza nchini, Phaustine Kasike(aliyevaa miwani) akiongea na Wafungwa wa Gereza Msalato(hawapo pichani) wanaofanya kazi za uzalishaji kokoto katika mradi huo wa Gereza hilo. Kulia ni Mkuu wa Magereza Mkoani Dodoma, Kamishna Msaidizi wa Magereza, Keneth Mwambije.

Kamishna Jenerali wa Magereza nchini, Phaustine Kasike akikagua moja ya eneo la kulipulia mawe ya kokoto katika eneo la Gereza Msalato leo alipofanya ziara ya kikazi.

Kamishna Jenerali wa Magereza nchini, Phaustine Kasike(aliyevaa miwani) akiangalia mtambo wa uzalishaji katika mradi wa uzalishaji kokoto wa Gereza Msalato, Dodoma leo alipofanya ziara ya kikazi.  Shirika la Uzalishaji Mali la Magereza (SHIMA)  limewekeza  mradi  huo wa kokoto katika eneo la Gereza Msalato, Mkoani Dodoma.

Kamishna Jenerali wa Magereza nchini, Phaustine Kasike(aliyevaa miwani) akiangalia kokoto  zinazozalishwa katika mradi huo wa Gereza Msalato leo alipofanya ziara ya kikazi. Kushoto ni Mkuu wa Magereza Mkoani Dodoma, Kamishna Msaidizi wa Magereza, Keneth Mwambije na Kulia ni Mkuu wa Gereza Msalato, Mrakibu Mwandamizi wa Magereza, Huruma Mwalyaje.

Mkuu wa Gereza Msalato, Mrakibu Mwandamizi wa Magereza, Huruma Mwalyaje(katikati) akimwelezea jambo Kamishna Jenerali wa Magereza nchini, Phaustine Kasike(kulia) kabla ya kutembelea eneo la mradi wa uzalishaji kokoto. Kushoto ni Mkuu wa Magereza Mkoani Dodoma, Kamishna Msaidizi wa Magereza, Keneth Mwambije (Picha zote na Jeshi la Magereza).

Wednesday, November 6, 2019

SPIKA NDUGAI AKUTANA NA KUFANYA MAZUNGUMZO NA KAMISHNA JENERALI WA MAGEREZA NCHINI, PHAUSTINE KASIKE, LEO JIJINI DODOMA

Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,  Mhe. Job Ndugai (kushoto) akisalimiana na Kamishna Jenerali wa Magereza nchini, Phaustine Kasike alipomtembelea leo Ofisini kwake Bungeni, Jijini Dodoma
Kamishna Jenerali wa Magereza nchini, Phaustine Kasike  akisaini kitabu cha Wageni alipomtembelea Spika wa Bunge la Jamhuri ya  Muungano wa Tanzania,  Mhe. Job Ndugai(hayupo pichani), leo Ofisini kwake Bungeni, Jijini Dodoma.

Spika wa Bunge la Jamhuri ya  Muungano wa Tanzania,  Mhe. Job Ndugai (kushoto) akimsikiliza Kamishna Jenerali wa Magereza nchini, Phaustine Kasike  alipomtembelea leo Ofisini kwake Bungeni, Jijini Dodoma kwa mazungumzo maalum.

Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,  Mhe. Job Ndugai (kushoto) akiagana na Kamishna Jenerali wa  Magereza nchini, Phaustine Kasike  mara baada ya mazungumzo alipomtembelea leo Ofisini kwake Bungeni Jijini Dodoma.

Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe.  Job Ndugai (kushoto) akiwa katika picha ya pamoja na Kamishna Jenerali wa Magereza nchini, Phaustine Kasike (katikati) alipomtembelea leo Ofisini kwake Bungeni, Jijini Dodoma. Kulia ni Mkuu wa Magereza Mkoani Dodoma, Kamishna Msaidizi wa Magereza, Keneth Mwambije               (Picha zote na Jeshi la Magereza).

Friday, October 25, 2019

SHEREHE ZA KUFUNGA MAFUNZO YA UONGOZI DARAJA LA PILI KATIKA JESHI LA MAGEREZA ZAFANA MKOANI MOROGORO

Kamishna Jenerali wa Magereza nchini, CGP – Phaustine Kasike akikagua Paredi Maalum lililoandaliwa na Maofisa Wahitimu wa Mafunzo ya Maafisa Wakaguzi Wasaidizi wa Magereza lililofanyika Oktoba 25, 2019 katika Viwanja vya Chuo cha Jeshi la Magereza, KPF Mkoani Morogoro.

Kamishna Jenerali wa Magereza nchini, CGP – Phaustine Kasike akiwa katika jukwaa akipokea salaam ya heshima kutoka kwa Maofisa Wahitimu wa Mafunzo ya Maafisa Wakaguzi Wasaidizi wa Magereza(hawapo pichani).

Maofisa Wahitimu wa Mafunzo ya Maafisa Wakaguzi Wasaidizi wa Magereza  wakipita mbele ya Mgeni rasmi katika Sherehe za kufunga mafunzo hayo yaliyofanyika Viwanja vya Chuo cha Jeshi la Magereza, KPF Mkoani Morogoro.

Kamishna Jenerali wa Magereza nchini, CGP Phaustine Kasike(kushoto) akimvisha cheo cha Mkaguzi Msaidizi wa Magereza mmoja wa Wahitimu wa Mafunzo ya Maafisa Wakaguzi Wasaidizi wa Magereza ambaye amefanya vizuri zaidi katika Mafunzo hayo yaliyofanyika kwa muda wa miezi minne.
Baadhi ya Maofisa wa Kike wa Jeshi la Magereza ambao ni miongoni mwa wahitimu wa Mafunzo ya Maafisa Wakaguzi Wasaidizi wa Magereza wakiwa tayari wamevishwa vyeo vipya kama wanavyoonekana katika picha.

Kamishna Jenerali wa Magereza nchini, CGP Phaustine Kasike akitoa hotuba fupi kwa Wahitimu wa Mafunzo ya Maafisa Wakaguzi Wasaidizi wa Magereza(hawapo pichani).

Baadhi ya Maafisa Waandamizi wa Jshi la Magereza wakifuatilia kwa makini hotuba ya mgeni rasmi kama wanavyoonekana katika picha.

Mhitimu wa Mafunzo ya Maafisa Wakaguzi Wasaidizi wa Magereza akisoma risala mbele ya mgeni rasmi.

Kamishna Jenerali wa Magereza nchini, CGP – Phaustine Kasike(katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Maofisa Wahitimu wa Mafunzo ya Maafisa Wakaguzi Wasaidizi wa Magereza waliosimama mstari wa nyuma(Picha zote na Jeshi la Magereza).

Thursday, October 17, 2019

“Zingatieni Maadili ya kazi katika utekelezaji wa majukumu yenu” – CGP Kasike

Kamishna Jenerali wa Magereza nchini, Phaustine Kasike akizungumza na Maafisa na askari wa Gereza Namajani lililopo Wilayani Masasi,  Oktoba 16, 2019 alipotembelea katika ziara yake ya  kikazi Mkoani Mtwara.

Baadhi ya askari wa Gereza Namajani wakimsikiliza Kamishna Jenerali wa Magereza nchini, Phaustine Kasike

Kamishna Jenerali wa Magereza nchini, Phaustine Kasike akizungumza na Maafisa na askari wa Gereza Masasi, Oktoba 16, 2019 alipotembelea katika ziara yake ya  kikazi.

Mkuu wa Gereza Masasi, Mrakibu wa Magereza, Juma Mkumba akitoa taarifa fupi ya Gereza  mbele ya Kamishna Jenerali wa Magereza nchini(hayupo pichani) alipotembelea Gereza hilo.

Kamishna Jenerali Phaustine Kasike akikagua Mifugo Katika Gereza la Wilaya Masasi.

Kamishna Jenerali wa Magereza nchini, Phaustine Kasike(katikati) akiwa katika picha ya pamoja na askari wa Gereza Namajani alipotembelea leo Oktoba 16, 2019 katika ziara yake ya  kikazi. Kulia ni Mkuu wa Magereza Mkoani Mtwara, Kamishna Msaidizi wa Magereza, Varisanga Msuya(Picha zote na Jeshi la Magereza).


Wednesday, October 16, 2019

KAMISHNA JENERALI WA MAGEREZA, PHAUSTINE KASIKE ATEMBELEA GEREZA LA WILAYA RUANGWA, LINDI TAREHE 15 OKTOBA 2019

Kamishna Jenerali wa Magereza nchini, Phaustine Kasike, akisalimiana na Msaidizi wa Mkuu wa Gereza Ruangwa, Mkaguzi wa Magereza, Alex Munga’nzo alipowasili  Oktoba 15, 2019 kwa ziara ya kikazi Gerezani hapo.

Mkuu wa Magereza Mkoani Lindi, Kamishna Msaidizi wa Magereza, Josephine Semwenda(kushoto) akisoma taarifa ya utendaji kazi ya Magereza Mkoani Lindi mbele ya Kamishna Jenerali wa Magereza, Phaustine Kasike(meza kuu) alipowasili Gereza Ruangwa  Oktoba 15, 2019.

Kamishna Jenerali wa Magereza nchini, Phaustine Kasike akikagua korosho ambayo tayari imeanza kuvunwa katika mashamba mbalimbali ya Gereza Ruangwa, lililopo Mkoani Lindi.

Ujenzi wa jengo litakalotumika kwa ajili ya mapokezi ya ndugu na jamaa wa wafungwa na mahabusu wanaofika Gereza Ruangwa kuwatembelea ndugu zao ukiendelea katika hatua mbalimbali za ujenzi.

Kamishna Jenerali wa Magereza nchini, Phaustine Kasike akiteta jambo na Mkuu wa Idara ya Uhamiaji nchini, Kamishna Jenerali wa Uhamiaji, Dkt. Anna Makakala walipokutana leo Wilayani Ruangwa ziarani (Picha zote na  Jeshi la Magereza).