Wednesday, October 16, 2019

KAMISHNA JENERALI WA MAGEREZA, PHAUSTINE KASIKE ATEMBELEA GEREZA LA WILAYA RUANGWA, LINDI TAREHE 15 OKTOBA 2019

Kamishna Jenerali wa Magereza nchini, Phaustine Kasike, akisalimiana na Msaidizi wa Mkuu wa Gereza Ruangwa, Mkaguzi wa Magereza, Alex Munga’nzo alipowasili  Oktoba 15, 2019 kwa ziara ya kikazi Gerezani hapo.

Mkuu wa Magereza Mkoani Lindi, Kamishna Msaidizi wa Magereza, Josephine Semwenda(kushoto) akisoma taarifa ya utendaji kazi ya Magereza Mkoani Lindi mbele ya Kamishna Jenerali wa Magereza, Phaustine Kasike(meza kuu) alipowasili Gereza Ruangwa  Oktoba 15, 2019.

Kamishna Jenerali wa Magereza nchini, Phaustine Kasike akikagua korosho ambayo tayari imeanza kuvunwa katika mashamba mbalimbali ya Gereza Ruangwa, lililopo Mkoani Lindi.

Ujenzi wa jengo litakalotumika kwa ajili ya mapokezi ya ndugu na jamaa wa wafungwa na mahabusu wanaofika Gereza Ruangwa kuwatembelea ndugu zao ukiendelea katika hatua mbalimbali za ujenzi.

Kamishna Jenerali wa Magereza nchini, Phaustine Kasike akiteta jambo na Mkuu wa Idara ya Uhamiaji nchini, Kamishna Jenerali wa Uhamiaji, Dkt. Anna Makakala walipokutana leo Wilayani Ruangwa ziarani (Picha zote na  Jeshi la Magereza).