Mojawapo ya Jukumu la Jeshi la Magereza ni kuwapeleka mahakamani mahabusu na kuwarudisha magerezani.

Gadi ya askari Wanawake na Wanaume wa Jeshi la Magereza katika Maadhimisho ya Sherehe za Kitaifa.

Ng'ombe bora wa Nyama na Maziwa ni sehemu ya miradi ya Uzalishaji inayoendeshwa na kusimamiwa na Jeshi la Magereza nchini.

Sehemu ya Mashamba makubwa yanayoendeshwa na Jeshi la Magereza: Shughuli za Kilimo cha Mashamba makubwa, madogo na bustani za mboga mboga ni moja ya shughuli za Magereza katika kuwafunza wafungwa namna ya kujitegemea mara wamalizapo vifungo vyao.

Baadhi wa wafungwa katika Kiwanda cha Ushonaji nguo cha Gereza Kuu Ukonga wakiwa kazini: Shughuli za Ushonaji wa nguo ni moja ya eneo ambalo wafungwa hupata huduma za urekebishwaji kwa vitendo.

Sunday, December 31, 2017

KAMISHNA JENERALI WA MAGEREZA DKT. JUMA MALEWA AHUTUBIA BARAZA LA KUFUNGA MWAKA 2017 NA KUUKARIBISHA MWAKA MPYA 2018 JIJINI MBEYA

Kamishna Jenerali wa Magereza, Dkt. Juma Malewa akiongoza Baraza Maalum la kufunga mwaka 2017 na kuukaribisha mwaka mpya 2018. Baraza hilo limehudhuriwa na Maafisa na Askari kutoka vituo mbalimbali vya Magereza Mkoani Mbeya, Chuo cha Magereza Kiwira na Chuo cha Ufundi Mbeya ambapo Baraza hilo limefanyika leo Desemba 31, 2017 katika Viwanja  vya Magereza Mkoani Mbeya.
Baadhi ya Askari wa kike wa Jeshi la Magereza kutoka vituo mbalimbali vya Magereza ya Mkoa wa Mbeya wakisikiliza hotuba ya Kamishna Jenerali wa Magereza, Dkt. Juma Malewa(hayupo pichani) katika Baraza Maalum la kufunga mwaka 2017 na kuukaribisha mwaka mpya 2018.
Wakuu wa Magereza yaliyopo Mkoani Mbeya wakifuatilia kwa umakini mkubwa maelekezo ya Kamishna Jenerali wa Magereza aliyoyatoa katika Baraza Maalum la kufunga mwaka 2017 na kuukaribisha mwaka mpya 2018.
Mkuu wa Magereza Mkoani Mbeya, Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Magereza, Kijida Mwakingi akitoa taarifa fupi ya Mkoa wake katika Baraza Maalum la kufunga mwaka 2017 na kuukaribisha mwaka mpya 2018.
Naibu Kamishna wa Magereza, Tusekile Mwaisabila akitoa ufafanuzi wa masuala yahusuyo Divisheni ya Huduma za Urekebishaji mbele ya  Kamishna Jenerali wa Magereza, Dkt. Juma Malewa(wa pili kulia) katika Baraza la kufunga mwaka 2017 na kuukaribisha mwaka mpya 2018 (wa kwanza kushoto) ni Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Magereza, Mbaraka Semwanza. Baraza hilo limefanyika katika Viwanja  vya Magereza Mkoani Mbeya.
Mkuu wa Kitengo cha Fedha na Uhasibu katika Jeshi la Magereza, Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Magereza, Chacha Binna akitolea ufafanuzi kuhusiana na masuala ya madeni ya watumishi yaliyoulizwa na Maafisa na Askari wa Jeshi hilo Mkoani Mbeya(hawapo pichani) katika Baraza hilo.
Kamishna Jenerali wa Magereza, Dkt. Juma Malewa akipokea salaam ya heshima kutoka kwa gwaride maalum alipowasili katika Viwanja vya Magereza Mkoani Mbeya kabla ya kuhutubia Baraza la Maalum la Maafisa na Askari kutoka vituo mbalimbali vya Magereza Mkoani Mbeya, Chuo cha Magereza Kiwira na Chuo cha Ufundi Mbeya ambapo Baraza hilo limefanyika Desemba 31, 2017.
Kamishna Jenerali wa Magereza, Dkt. Juma Malewa akikagua gwaride la Maafisa na Askari wa Jeshi la Magereza kabla ya kuhutubia Baraza Maalum la Maafisa na Askari wa Jeshi hilo lililofanyika katika Viwanja vya Magereza Mkoani Mbeya leo Desemba 31, 2017

(Picha zote na Lucas Mboje wa Jeshi la Magereza).