Monday, November 18, 2019

CGP KASIKE AFANYA MAZUNGUMZO NA RC. MNYETI KABLA YA KUHITIMISHA ZIARA YAKE YA KIKAZI MKOANI MANYARA

Mkuu wa Jeshi la Magereza nchini - CGP Phaustine Kasike akitambulisha ujumbe alioambatanao kabla ya mazungumzo mafupi na na Mkuu wa Mkoa wa Manyara, Mhe. Alexander Mnyeti alipomtembelea Ofisini kwake kabla ya kuendelea na ziara yake ya kikazi Gereza Mbulu, leo Novemba 18, 2019. Mkuu huyo wa Jeshi la Magereza amehitimisha ziara yake leo ya siku tatu Mkoani Manyara ambapo ametembelea magereza na Kambi zote za magereza mkoani humo.
Mkuu wa Mkoa wa Manyara, Mhe. Alexander Mnyeti akizungumza na Mkuu wa Jeshi la Magereza nchini - CGP Phaustine Kasike(hayupo pichani) alipotembelea Ofisini kwake leo Novemba 18, 2019. 
Mkuu wa Jeshi la Magereza nchini - CGP Phaustine Kasike akiteta jambo na Mkuu wa Mkoa wa Manyara, Mhe. Alexander Mnyeti alipomtembelea Ofisi kwake leo kabla ya kuendelea na ziara yake ya kikazi Gereza Mbulu, leo Novemba 18, 2019. 
Mkuu wa Jeshi la Magereza nchini - CGP Phaustine Kasike(kushoto) akisalimiana na Mkuu wa Gereza Mbulu, SP. Danson Mpinga alipowasili Gereza Mbulu leo kwa ziara ya kikazi. Mkuu huyo wa Jeshi la Magereza amehitimisha ziara yake leo ya siku tatu Mkoani Manyara ambapo ametembelea magereza na Kambi zote za magereza mkoani humo.

Mkuu wa Jeshi la Magereza nchini - CGP Phaustine Kasike akizungumza na wafungwa na mahabusu wa Gereza Mbulu(hawapo pichani) leo Novemba 18, 2019 alipofanya ziara ya kikazi katika gereza hilo(Picha zote na Jeshi la Magereza).