Thursday, November 14, 2019

KAMISHNA JENERALI WA MAGEREZA PHAUSTINE KASIKE AKAGUA UJENZI WA MAKAZI YA MAOFISA MAGEREZA UKONGA, APONGEZA HATUA KUBWA ILIYOFIKIWA TAREHE 13 NOVEMBA,2019

Kamishna Jenerali wa Magereza nchini, Phaustine Kasike akisalimiana na Maafisa wa SUMAJKT pamoja na Maafisa wa Jeshi la Magereza alipowasili katika eneo la ujenzi Gereza Kuu Ukonga Novemba 13, 2019 katika ziara yake ya kikazi yenye lengo la kukagua ujenzi unaoendelea wa makazi ya Maafisa na askari wa Magereza katika eneo la Gereza Kuu Ukonga, jijini Dar es Salaam.

Ofisa wa SUMAJKT, Meja Ashrafu Hassan akitoa taarifa fupi kwa Kamishna Jenerali wa Magereza, Phaustine Kasike alipotembelea  Novemba 13, 2019 kwa lengo la kukagua ujenzi huo.

Kamishna Jenerali wa Magereza nchini, Phaustine Kasike akikagua ujenzi wa majengo mbalimbali ya makazi ya Maafisa na Askari wa Magereza katika eneo la Gereza Kuu Ukonga. Kulia kwake ni Ofisa wa SUMAJKT, Meja Ashrafu Hassan akimuonesha baadhi ya maeneo ambayo bado yanafanyia maboresho ya miundombinu.

Kamishna Jenerali wa Magereza nchini, Phaustine Kasike akikagua miundombinu ya mitaro ya kupitishia maji ya mvua katika ujenzi wa majengo mbalimbali za makazi ya Maafisa na Askari wa Magereza katika eneo la Gereza Kuu Ukonga.

Moja ya majengo ya ghorofa yaliyojengwa kwa ajili ya makazi ya Maafisa na askari wa Magereza katika eneo la Gereza Kuu Ukonga, jijini Dar es Salaam yakiwa tayari yamekamilika kama inavyoonekana katika picha (Picha na Jeshi la Magereza).