Kamishna Jenerali wa Magereza
nchini, Phaustine Kasike akisalimiana na Maafisa wa SUMAJKT pamoja na Maafisa wa Jeshi la Magereza
alipowasili katika eneo la ujenzi Gereza Kuu Ukonga Novemba 13, 2019 katika
ziara yake ya kikazi yenye lengo la kukagua ujenzi unaoendelea wa makazi ya
Maafisa na askari wa Magereza katika eneo la Gereza Kuu Ukonga, jijini Dar es
Salaam.
Ofisa wa SUMAJKT, Meja Ashrafu Hassan akitoa taarifa fupi kwa Kamishna Jenerali wa Magereza, Phaustine Kasike
alipotembelea Novemba 13, 2019 kwa lengo la kukagua ujenzi huo.
Kamishna Jenerali wa Magereza nchini, Phaustine
Kasike akikagua ujenzi wa majengo mbalimbali ya makazi ya Maafisa na Askari wa
Magereza katika eneo la Gereza Kuu Ukonga. Kulia kwake ni Ofisa wa
SUMAJKT, Meja Ashrafu Hassan akimuonesha baadhi ya maeneo ambayo bado
yanafanyia maboresho ya miundombinu.
Kamishna
Jenerali wa Magereza nchini, Phaustine Kasike akikagua miundombinu ya mitaro ya
kupitishia maji ya mvua katika ujenzi wa majengo mbalimbali za makazi ya
Maafisa na Askari wa Magereza katika eneo la Gereza Kuu Ukonga.
Moja ya majengo ya ghorofa yaliyojengwa kwa ajili ya
makazi ya Maafisa na askari wa Magereza katika eneo la Gereza Kuu Ukonga,
jijini Dar es Salaam yakiwa tayari yamekamilika kama inavyoonekana katika picha (Picha na Jeshi la Magereza).