Thursday, May 30, 2019

WAZIRI LUGOLA AZINDUA BODI MPYA YA SHIRIKA LA UZALISHAJI MALI LA MAGEREZA, AWATAKA WAJUMBE KUFANYA MAGEUZI MAKUBWA KATIKA MIRADI YA JESHI

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola akitoa maelekezo kwa wajumbe wa Bodi mpya ya Shirika la Uzalishaji Mali la Jeshi la Magereza, kabla ya kuizindua Bodi hiyo, jijini Dodoma, leo. Wapili kushoto ni Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza, Phaustine Kasike. 

Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Meja Jenerali Jacob Kingu, akizungumza kabla ya Waziri wa Wizara hiyo, Kangi Lugola (wapili kushoto) kuizindua Bodi mpya ya Shirika la Uzalishaji Mali la Jeshi la Magereza, jijini Dodoma, leo. Wapili kulia ni Kamishna Jenerali wa Magereza, Phaustine Kasike.

Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza, Phaustine Kasike, akitoa historia fupi ya Shirika la Uzalishaji Mali la Jeshi hilo, kabla ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola (kushoto) kuizindua Bodi hiyo, Jijini Dodoma, leo. Katikati ni Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Meja Jenerali Jacob Kingu.

Mwenyekiti wa Bodi Mpya ya Shirika la Uzalishaji Mali la Magereza, Meja Jenerali Mstaafu, Raphaeli Muhuga, akitoa neno la shukrani baada ya uzinduzi wa Bodi hiyo, jijini Dodoma leo. Katikati ni Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola, na kulia ni Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Meja Jenerali Jacob Kingu.

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola (wapili kushoto), Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Meja Jenerali Jacob Kingu (wapili kulia), Kamishna Jenerali wa Magereza, Phaustine Kasike (kushoto), wakiwa katika picha ya pamoja na Wajumbe wa Bodi mpya ya Shirika la Uzalishaji Mali la Jeshi la Magereza, baada ya uzinduzi wa Bodi hiyo, jijini Dodoma leo.
 Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.