Mojawapo ya Jukumu la Jeshi la Magereza ni kuwapeleka mahakamani mahabusu na kuwarudisha magerezani.

Gadi ya askari Wanawake na Wanaume wa Jeshi la Magereza katika Maadhimisho ya Sherehe za Kitaifa.

Ng'ombe bora wa Nyama na Maziwa ni sehemu ya miradi ya Uzalishaji inayoendeshwa na kusimamiwa na Jeshi la Magereza nchini.

Sehemu ya Mashamba makubwa yanayoendeshwa na Jeshi la Magereza: Shughuli za Kilimo cha Mashamba makubwa, madogo na bustani za mboga mboga ni moja ya shughuli za Magereza katika kuwafunza wafungwa namna ya kujitegemea mara wamalizapo vifungo vyao.

Baadhi wa wafungwa katika Kiwanda cha Ushonaji nguo cha Gereza Kuu Ukonga wakiwa kazini: Shughuli za Ushonaji wa nguo ni moja ya eneo ambalo wafungwa hupata huduma za urekebishwaji kwa vitendo.

Monday, November 18, 2019

CGP KASIKE AFANYA MAZUNGUMZO NA RC. MNYETI KABLA YA KUHITIMISHA ZIARA YAKE YA KIKAZI MKOANI MANYARA

Mkuu wa Jeshi la Magereza nchini - CGP Phaustine Kasike akitambulisha ujumbe alioambatanao kabla ya mazungumzo mafupi na na Mkuu wa Mkoa wa Manyara, Mhe. Alexander Mnyeti alipomtembelea Ofisini kwake kabla ya kuendelea na ziara yake ya kikazi Gereza Mbulu, leo Novemba 18, 2019. Mkuu huyo wa Jeshi la Magereza amehitimisha ziara yake leo ya siku tatu Mkoani Manyara ambapo ametembelea magereza na Kambi zote za magereza mkoani humo.
Mkuu wa Mkoa wa Manyara, Mhe. Alexander Mnyeti akizungumza na Mkuu wa Jeshi la Magereza nchini - CGP Phaustine Kasike(hayupo pichani) alipotembelea Ofisini kwake leo Novemba 18, 2019. 
Mkuu wa Jeshi la Magereza nchini - CGP Phaustine Kasike akiteta jambo na Mkuu wa Mkoa wa Manyara, Mhe. Alexander Mnyeti alipomtembelea Ofisi kwake leo kabla ya kuendelea na ziara yake ya kikazi Gereza Mbulu, leo Novemba 18, 2019. 
Mkuu wa Jeshi la Magereza nchini - CGP Phaustine Kasike(kushoto) akisalimiana na Mkuu wa Gereza Mbulu, SP. Danson Mpinga alipowasili Gereza Mbulu leo kwa ziara ya kikazi. Mkuu huyo wa Jeshi la Magereza amehitimisha ziara yake leo ya siku tatu Mkoani Manyara ambapo ametembelea magereza na Kambi zote za magereza mkoani humo.

Mkuu wa Jeshi la Magereza nchini - CGP Phaustine Kasike akizungumza na wafungwa na mahabusu wa Gereza Mbulu(hawapo pichani) leo Novemba 18, 2019 alipofanya ziara ya kikazi katika gereza hilo(Picha zote na Jeshi la Magereza).

KAMBI YA MAGEREZA KATESH YAPEWA LENGO LA KULISHA MAGEREZA YOTE YA MKOA WA MANYARA

Kamishna Jenerali wa Magereza nchini Phaustine Kasike(kushoto) akikagua maandalizi ya awali ya shamba la mahindi alipofanya ziara ya kikazi  Novemba 17, 2019 katika Kambi ya Magereza – Katesh iliyopo wilayani Hanang, Mkoa wa Manyara. Kulia ni Mkuu wa Magereza Mkoani Manyara, ACP. Lipina Lyimo.

Kamishna Jenerali wa Magereza nchini, Phaustine Kasike(wa pili toka kulia) akikagua moja ya trekta linalotumika kwa shughuli za Kilimo katika Kambi ya Magereza – Katesh iliyopo wilayani Hanang, Mkoa wa Manyara, Novemba 17, 2019 alipotembelea Kambi hiyo.

Moja ya maghala ya kuhifadhia mazao mbalimbali yanayozalishwa katika Kambi ya Magereza – Katesh iliyopo wilayani Hanang, Mkoa wa Manyara.

Kamishna Jenerali wa Magereza nchini, Phaustine Kasike akikagua mradi wa tofali za saruji ambazo zinafyatuliwa katika Gereza la Babati tayari kwa ujenzi wa nyumba za Maafisa na askari wa kituo hicho.(Picha zote na Jeshi la Magereza).

Thursday, November 14, 2019

KAMISHNA JENERALI WA MAGEREZA PHAUSTINE KASIKE AKAGUA UJENZI WA MAKAZI YA MAOFISA MAGEREZA UKONGA, APONGEZA HATUA KUBWA ILIYOFIKIWA TAREHE 13 NOVEMBA,2019

Kamishna Jenerali wa Magereza nchini, Phaustine Kasike akisalimiana na Maafisa wa SUMAJKT pamoja na Maafisa wa Jeshi la Magereza alipowasili katika eneo la ujenzi Gereza Kuu Ukonga Novemba 13, 2019 katika ziara yake ya kikazi yenye lengo la kukagua ujenzi unaoendelea wa makazi ya Maafisa na askari wa Magereza katika eneo la Gereza Kuu Ukonga, jijini Dar es Salaam.

Ofisa wa SUMAJKT, Meja Ashrafu Hassan akitoa taarifa fupi kwa Kamishna Jenerali wa Magereza, Phaustine Kasike alipotembelea  Novemba 13, 2019 kwa lengo la kukagua ujenzi huo.

Kamishna Jenerali wa Magereza nchini, Phaustine Kasike akikagua ujenzi wa majengo mbalimbali ya makazi ya Maafisa na Askari wa Magereza katika eneo la Gereza Kuu Ukonga. Kulia kwake ni Ofisa wa SUMAJKT, Meja Ashrafu Hassan akimuonesha baadhi ya maeneo ambayo bado yanafanyia maboresho ya miundombinu.

Kamishna Jenerali wa Magereza nchini, Phaustine Kasike akikagua miundombinu ya mitaro ya kupitishia maji ya mvua katika ujenzi wa majengo mbalimbali za makazi ya Maafisa na Askari wa Magereza katika eneo la Gereza Kuu Ukonga.

Moja ya majengo ya ghorofa yaliyojengwa kwa ajili ya makazi ya Maafisa na askari wa Magereza katika eneo la Gereza Kuu Ukonga, jijini Dar es Salaam yakiwa tayari yamekamilika kama inavyoonekana katika picha (Picha na Jeshi la Magereza).

Thursday, November 7, 2019

KAMISHNA JENERALI WA MAGEREZA NCHINI, PHAUSTINE KASIKE ATEMBELEA MRADI WA KOKOTO GEREZA MSALATO, MKOANI DODOMA





Kamishna Jenerali wa Magereza nchini, Phaustine Kasike(aliyevaa miwani) akiongea na Wafungwa wa Gereza Msalato(hawapo pichani) wanaofanya kazi za uzalishaji kokoto katika mradi huo wa Gereza hilo. Kulia ni Mkuu wa Magereza Mkoani Dodoma, Kamishna Msaidizi wa Magereza, Keneth Mwambije.

Kamishna Jenerali wa Magereza nchini, Phaustine Kasike akikagua moja ya eneo la kulipulia mawe ya kokoto katika eneo la Gereza Msalato leo alipofanya ziara ya kikazi.

Kamishna Jenerali wa Magereza nchini, Phaustine Kasike(aliyevaa miwani) akiangalia mtambo wa uzalishaji katika mradi wa uzalishaji kokoto wa Gereza Msalato, Dodoma leo alipofanya ziara ya kikazi.  Shirika la Uzalishaji Mali la Magereza (SHIMA)  limewekeza  mradi  huo wa kokoto katika eneo la Gereza Msalato, Mkoani Dodoma.

Kamishna Jenerali wa Magereza nchini, Phaustine Kasike(aliyevaa miwani) akiangalia kokoto  zinazozalishwa katika mradi huo wa Gereza Msalato leo alipofanya ziara ya kikazi. Kushoto ni Mkuu wa Magereza Mkoani Dodoma, Kamishna Msaidizi wa Magereza, Keneth Mwambije na Kulia ni Mkuu wa Gereza Msalato, Mrakibu Mwandamizi wa Magereza, Huruma Mwalyaje.

Mkuu wa Gereza Msalato, Mrakibu Mwandamizi wa Magereza, Huruma Mwalyaje(katikati) akimwelezea jambo Kamishna Jenerali wa Magereza nchini, Phaustine Kasike(kulia) kabla ya kutembelea eneo la mradi wa uzalishaji kokoto. Kushoto ni Mkuu wa Magereza Mkoani Dodoma, Kamishna Msaidizi wa Magereza, Keneth Mwambije (Picha zote na Jeshi la Magereza).

Wednesday, November 6, 2019

SPIKA NDUGAI AKUTANA NA KUFANYA MAZUNGUMZO NA KAMISHNA JENERALI WA MAGEREZA NCHINI, PHAUSTINE KASIKE, LEO JIJINI DODOMA

Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,  Mhe. Job Ndugai (kushoto) akisalimiana na Kamishna Jenerali wa Magereza nchini, Phaustine Kasike alipomtembelea leo Ofisini kwake Bungeni, Jijini Dodoma
Kamishna Jenerali wa Magereza nchini, Phaustine Kasike  akisaini kitabu cha Wageni alipomtembelea Spika wa Bunge la Jamhuri ya  Muungano wa Tanzania,  Mhe. Job Ndugai(hayupo pichani), leo Ofisini kwake Bungeni, Jijini Dodoma.

Spika wa Bunge la Jamhuri ya  Muungano wa Tanzania,  Mhe. Job Ndugai (kushoto) akimsikiliza Kamishna Jenerali wa Magereza nchini, Phaustine Kasike  alipomtembelea leo Ofisini kwake Bungeni, Jijini Dodoma kwa mazungumzo maalum.

Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,  Mhe. Job Ndugai (kushoto) akiagana na Kamishna Jenerali wa  Magereza nchini, Phaustine Kasike  mara baada ya mazungumzo alipomtembelea leo Ofisini kwake Bungeni Jijini Dodoma.

Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe.  Job Ndugai (kushoto) akiwa katika picha ya pamoja na Kamishna Jenerali wa Magereza nchini, Phaustine Kasike (katikati) alipomtembelea leo Ofisini kwake Bungeni, Jijini Dodoma. Kulia ni Mkuu wa Magereza Mkoani Dodoma, Kamishna Msaidizi wa Magereza, Keneth Mwambije               (Picha zote na Jeshi la Magereza).