Monday, November 18, 2019
CGP KASIKE AFANYA MAZUNGUMZO NA RC. MNYETI KABLA YA KUHITIMISHA ZIARA YAKE YA KIKAZI MKOANI MANYARA
3:42 PM
Mkuu wa Jeshi la Magereza nchini - CGP Phaustine Kasike akitambulisha
ujumbe alioambatanao kabla ya mazungumzo mafupi na na Mkuu wa Mkoa wa Manyara,
Mhe. Alexander Mnyeti alipomtembelea Ofisini kwake kabla ya kuendelea na ziara
yake ya kikazi Gereza Mbulu, leo Novemba 18, 2019. Mkuu huyo wa Jeshi la
Magereza amehitimisha ziara yake leo ya siku tatu Mkoani Manyara ambapo
ametembelea magereza na Kambi zote za magereza mkoani humo.
Mkuu wa Mkoa wa Manyara, Mhe. Alexander Mnyeti akizungumza na Mkuu wa
Jeshi la Magereza nchini - CGP Phaustine Kasike(hayupo pichani) alipotembelea
Ofisini kwake leo Novemba 18, 2019.
Mkuu wa Jeshi la Magereza nchini - CGP Phaustine Kasike akiteta jambo
na Mkuu wa Mkoa wa Manyara, Mhe. Alexander Mnyeti alipomtembelea Ofisi kwake
leo kabla ya kuendelea na ziara yake ya kikazi Gereza Mbulu, leo Novemba 18,
2019.
Mkuu wa Jeshi la Magereza
nchini - CGP Phaustine Kasike(kushoto) akisalimiana na Mkuu wa Gereza Mbulu,
SP. Danson Mpinga alipowasili Gereza Mbulu leo kwa ziara ya kikazi. Mkuu huyo
wa Jeshi la Magereza amehitimisha ziara yake leo ya siku tatu Mkoani Manyara
ambapo ametembelea magereza na Kambi zote za magereza mkoani humo.
Mkuu wa Jeshi la Magereza
nchini - CGP Phaustine Kasike akizungumza na wafungwa na mahabusu wa Gereza
Mbulu(hawapo pichani) leo Novemba 18, 2019 alipofanya ziara ya kikazi katika
gereza hilo(Picha zote na Jeshi la Magereza).
KAMBI YA MAGEREZA KATESH YAPEWA LENGO LA KULISHA MAGEREZA YOTE YA MKOA WA MANYARA
8:04 AM
Kamishna Jenerali wa Magereza nchini Phaustine Kasike(kushoto) akikagua
maandalizi ya awali ya shamba la mahindi alipofanya ziara ya kikazi Novemba
17, 2019 katika Kambi ya Magereza – Katesh iliyopo wilayani Hanang, Mkoa wa
Manyara. Kulia ni Mkuu wa Magereza Mkoani Manyara, ACP. Lipina Lyimo.
Kamishna Jenerali wa
Magereza nchini, Phaustine Kasike(wa pili toka kulia) akikagua moja ya trekta
linalotumika kwa shughuli za Kilimo katika Kambi ya Magereza – Katesh iliyopo
wilayani Hanang, Mkoa wa Manyara, Novemba 17, 2019 alipotembelea Kambi
hiyo.
Moja ya maghala ya
kuhifadhia mazao mbalimbali yanayozalishwa katika Kambi ya Magereza – Katesh
iliyopo wilayani Hanang, Mkoa wa Manyara.
Kamishna Jenerali wa
Magereza nchini, Phaustine Kasike akikagua mradi wa tofali za saruji ambazo
zinafyatuliwa katika Gereza la Babati tayari kwa ujenzi wa nyumba za Maafisa na
askari wa kituo hicho.(Picha zote na Jeshi la Magereza).
Thursday, November 14, 2019
KAMISHNA JENERALI WA MAGEREZA PHAUSTINE KASIKE AKAGUA UJENZI WA MAKAZI YA MAOFISA MAGEREZA UKONGA, APONGEZA HATUA KUBWA ILIYOFIKIWA TAREHE 13 NOVEMBA,2019
8:32 AM
Kamishna Jenerali wa Magereza
nchini, Phaustine Kasike akisalimiana na Maafisa wa SUMAJKT pamoja na Maafisa wa Jeshi la Magereza
alipowasili katika eneo la ujenzi Gereza Kuu Ukonga Novemba 13, 2019 katika
ziara yake ya kikazi yenye lengo la kukagua ujenzi unaoendelea wa makazi ya
Maafisa na askari wa Magereza katika eneo la Gereza Kuu Ukonga, jijini Dar es
Salaam.
Ofisa wa SUMAJKT, Meja Ashrafu Hassan akitoa taarifa fupi kwa Kamishna Jenerali wa Magereza, Phaustine Kasike
alipotembelea Novemba 13, 2019 kwa lengo la kukagua ujenzi huo.
Kamishna Jenerali wa Magereza nchini, Phaustine
Kasike akikagua ujenzi wa majengo mbalimbali ya makazi ya Maafisa na Askari wa
Magereza katika eneo la Gereza Kuu Ukonga. Kulia kwake ni Ofisa wa
SUMAJKT, Meja Ashrafu Hassan akimuonesha baadhi ya maeneo ambayo bado
yanafanyia maboresho ya miundombinu.
Kamishna
Jenerali wa Magereza nchini, Phaustine Kasike akikagua miundombinu ya mitaro ya
kupitishia maji ya mvua katika ujenzi wa majengo mbalimbali za makazi ya
Maafisa na Askari wa Magereza katika eneo la Gereza Kuu Ukonga.
Moja ya majengo ya ghorofa yaliyojengwa kwa ajili ya
makazi ya Maafisa na askari wa Magereza katika eneo la Gereza Kuu Ukonga,
jijini Dar es Salaam yakiwa tayari yamekamilika kama inavyoonekana katika picha (Picha na Jeshi la Magereza).
Thursday, November 7, 2019
KAMISHNA JENERALI WA MAGEREZA NCHINI, PHAUSTINE KASIKE ATEMBELEA MRADI WA KOKOTO GEREZA MSALATO, MKOANI DODOMA
4:38 PM
Kamishna Jenerali wa Magereza
nchini, Phaustine Kasike(aliyevaa miwani) akiongea na Wafungwa wa Gereza
Msalato(hawapo pichani) wanaofanya kazi za uzalishaji kokoto katika mradi huo
wa Gereza hilo. Kulia ni Mkuu wa Magereza Mkoani Dodoma, Kamishna Msaidizi wa
Magereza, Keneth Mwambije.
Kamishna Jenerali wa Magereza nchini, Phaustine
Kasike akikagua moja ya eneo la kulipulia mawe ya kokoto katika eneo la Gereza
Msalato leo alipofanya ziara ya kikazi.
Kamishna Jenerali wa Magereza nchini, Phaustine
Kasike(aliyevaa miwani) akiangalia mtambo wa uzalishaji katika mradi wa
uzalishaji kokoto wa Gereza Msalato, Dodoma leo alipofanya ziara ya kikazi. Shirika la Uzalishaji Mali la Magereza (SHIMA) limewekeza
mradi huo wa kokoto katika eneo
la Gereza Msalato, Mkoani Dodoma.
Kamishna Jenerali wa Magereza
nchini, Phaustine Kasike(aliyevaa miwani) akiangalia kokoto zinazozalishwa katika mradi huo wa Gereza
Msalato leo alipofanya ziara ya kikazi. Kushoto ni Mkuu wa Magereza Mkoani
Dodoma, Kamishna Msaidizi wa Magereza, Keneth Mwambije na Kulia ni Mkuu wa
Gereza Msalato, Mrakibu Mwandamizi wa Magereza, Huruma Mwalyaje.
Mkuu wa Gereza Msalato, Mrakibu Mwandamizi wa
Magereza, Huruma Mwalyaje(katikati) akimwelezea jambo Kamishna Jenerali wa
Magereza nchini, Phaustine Kasike(kulia) kabla ya kutembelea eneo la mradi wa
uzalishaji kokoto. Kushoto ni Mkuu wa Magereza Mkoani Dodoma, Kamishna Msaidizi
wa Magereza, Keneth Mwambije (Picha zote na Jeshi la Magereza).
Wednesday, November 6, 2019
SPIKA NDUGAI AKUTANA NA KUFANYA MAZUNGUMZO NA KAMISHNA JENERALI WA MAGEREZA NCHINI, PHAUSTINE KASIKE, LEO JIJINI DODOMA
2:49 PM
Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania, Mhe. Job Ndugai (kushoto)
akisalimiana na Kamishna Jenerali wa Magereza nchini, Phaustine Kasike
alipomtembelea leo Ofisini kwake Bungeni, Jijini Dodoma
Kamishna Jenerali wa Magereza nchini, Phaustine
Kasike akisaini kitabu cha Wageni
alipomtembelea Spika wa Bunge la Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania, Mhe. Job
Ndugai(hayupo pichani), leo Ofisini kwake Bungeni, Jijini Dodoma.
Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Job Ndugai (kushoto) akimsikiliza
Kamishna Jenerali wa Magereza nchini, Phaustine Kasike alipomtembelea leo Ofisini kwake Bungeni,
Jijini Dodoma kwa mazungumzo maalum.
Spika wa Bunge la
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe.
Job Ndugai (kushoto) akiagana na Kamishna Jenerali wa Magereza nchini, Phaustine Kasike mara baada ya mazungumzo alipomtembelea leo
Ofisini kwake Bungeni Jijini Dodoma.
Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania, Mhe. Job Ndugai (kushoto)
akiwa katika picha ya pamoja na Kamishna Jenerali wa Magereza nchini, Phaustine
Kasike (katikati) alipomtembelea leo Ofisini kwake Bungeni, Jijini Dodoma.
Kulia ni Mkuu wa Magereza Mkoani Dodoma, Kamishna Msaidizi wa Magereza, Keneth
Mwambije (Picha zote na Jeshi la Magereza).