Mojawapo ya Jukumu la Jeshi la Magereza ni kuwapeleka mahakamani mahabusu na kuwarudisha magerezani.

Gadi ya askari Wanawake na Wanaume wa Jeshi la Magereza katika Maadhimisho ya Sherehe za Kitaifa.

Ng'ombe bora wa Nyama na Maziwa ni sehemu ya miradi ya Uzalishaji inayoendeshwa na kusimamiwa na Jeshi la Magereza nchini.

Sehemu ya Mashamba makubwa yanayoendeshwa na Jeshi la Magereza: Shughuli za Kilimo cha Mashamba makubwa, madogo na bustani za mboga mboga ni moja ya shughuli za Magereza katika kuwafunza wafungwa namna ya kujitegemea mara wamalizapo vifungo vyao.

Baadhi wa wafungwa katika Kiwanda cha Ushonaji nguo cha Gereza Kuu Ukonga wakiwa kazini: Shughuli za Ushonaji wa nguo ni moja ya eneo ambalo wafungwa hupata huduma za urekebishwaji kwa vitendo.

Tuesday, December 18, 2018

MAGEREZA YAZINDUA MKAKATI WA KUMALIZA UHABA WA NYUMBA ZA WATUMISHI WA JESHI HILO, DODOMA

Kamishna Jenerali wa Magereza Phaustine Kasike akiwasili katika viwanja vya gereza Kuu Isanga Dodoma kwa ajili ya uzinduzi wa mradi wa ufyatuaji tofali za kuchoma kwa ajili ya ujenzi wa nyumba za maafisa na askari kwa njia ya kujitolea. Uzinduzi huo umefanyika Desemba 17, 2018 ikiwa ni ishara ya uzinduzi programu ya ufyatuaji na uchomaji wa tofali kitaifa ili kukabiliana na changamnto ya makazi kwa watumishi wa Jeshi la Magereza kote nchini.
Kamishna Jenerali wa Magereza Phaustine Kasike akikata utepe kuashiria  uzinduzi wa miradi ya ufyatuaji matofali za kuchoma na hydrofom kitaifa kutegemeana na hali ya udongo katika kituo husika. Zoezi la uzinduzi kitagaifa limefanyika  Desemba 16, 2018 katika viwanja vya Gereza Kuu Isanga, Dodoma. Kulia ni Kamishna wa Fedha na Mipango,Gedeon Nkana, Kamishna wa Miundombinu ya Magerezana Uzalishaji, Tusekile Mwaisabila na Mkuu wa Gereza Isanga ACP Keneth Mwambije. Kushoto ni Kamishna wa Huduma za Urekiebishaji Augostine Mboje na Mkuu wa Magereza Mkoa wa Dodoma SACP Omary Salum.

Mtaalam na msimamizi wa mradi wa ufyatuaji tofali katika Gereza Kuu Isanga Dodoma Sajin Modern Mwakialinga wa Gereza Isanga akitoa maelezo kwa viongozi mbalimbali wa Jeshi la Magereza  juu ya namna mradi huo unavyotekelezwa.

Baadhi ya wafungwa waliopo katika programu za urekebishaji ambao wanafundishwa kufyatua, kuchoma tofali na wengine kujenga nyumba wanaotumika katika mradi wa ujenzi wa nyumba za kujitolea katika Gereza Kuu Isanga mkoani Dodoma wakionesha umahiri wao wa kufyatua tofali  Desemba 17, 2018.
Baadhi ya maafisa waandamizi wa Jeshi la Magereza kutoka mikoa mbalimbali hapa nchini waliohudhuria uzinduzi wa mradi wa ufyatuaji tofali kitaifa kwa ajili ya ujenzi wa nyumba za kujitolea za maafisa na askari wa Jeshi la magereza nchini.

Kamishna Jenerali wa Magereza Phaustine Kasike akiangalia ubora wa tofali  za kuchoma alipofanya uzinduzi wa programu ya ufyatuaji tofali kitaifa kwa ajili ya ujenzi wa nyumba za maafisa na askari wa Jeshi hilo ili kukabiliana na tatizo la makazi kwa watumishi.
Muonekano wa sehemu ya tofali 100,000 moja zilizofyatuliwa na kuchomwa tayari kwa ujenzi wa nyumba 30 za maafisa na askari wa Gereza Kuu Isanga na Ofisi ya Mkuu wa Magereza wa Mkoa wa Dodoma.Nyumba hizo zitakuwa na vyumba vitatu kila moja na mambo mengine muhimu kama sebule, choo, bafu, jiko na store na zinatarajiwa kukamilika kwa mwaka 2019.

Kamishna Jenerali wa Magereza Phaustine Kasike (wa tatu kulia) akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya Makamishna, Wakuu wa Magereza wa Mikoa na Mikoa ya kiutawala ya Magereza waliohudhuria hafla ya uzinduzi wa programu ya ufyatuaji tofali kitaifa kwa ajili ya ujenzi wa nyumba za kujitolea za maafisa na askari wa Jeshi hilo. Uzinduzi huo umefanyika leo katika viwanja vya Gereza Kuu Isanga Dodoma Desemba 17, 2018.Katika hafla hiyo Kamishna Kasike amewataka Wakuu wa Magereza wa Mikoa yote nchini kwa wale ambao hawajaanza utekelezaji wa agizo la ufyatuaji tofali kuanza mara moja kwa kuzingatia hali ya udongo katika maeneo yao. Jeshi la Magereza linaupungufu wa nyumba za watumishi zaidi ya 9000 kote nchini.Picha zote na Jeshi la Magereza)

MAGEREZA SACCOS YATAO MAFUNZO KWA MAAFISA WAANDAMISHI WA JESHI LA MAGEREZA TAREHE 16 DEC,2018

Kamishna Jenerali wa Magereza Phaustine Kasike ambaye pia ni mlezi wa Magereza Saccos akisalimiana na Makamishna wa Magereza  mara alipowasili katika viwanja vya Chuo cha Mipango Dodoma kwa ajili ya mafunzo ya Ushirika yaliyoandaliwa na Chama cha Akiba na Mikopo cha Magereza (Magereza Saccos) kwa maafisa waandamizi  kutoka Makao Makuu ya Jeshi hilo pamoja na Wakuu wa Magereza wa mikoa yote ya kiutawala yaliyofanyika Desemba 16, 2018.

Baadhi ya Maafisa Waandamizi wa Jeshi la Magereza wakimpokea Kamishna Jenerali wa Magereza Phaustine Kasike (hayupo pichani) alipowasili katika ukumbi wa  mikutano katika chuo cha mipango Dodoma kwa ajili ya mafunzo ya Ushirika yaliyoandaliwa na Chama cha Akiba na Mikopo cha Magereza (Magereza Saccos) kwa maafisa waandamizi  kutoka Makao Makuu ya Jeshi hilo pamoja na Wakuu wa Magereza wa mikoa yote ya kiutawala yaliyofanyika  Desemba 16, 2018.
Kamishna Jenerali wa Magereza Phaustine Kasike (katikati) akiwa meza kuu na Makamishna wa Magereza pamoja Mwenyekiti wa Bodi ya Magereza Saccos  Kamishna wa Fedha na Utawala wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Mbaraka Semwanza ambaye hivi karibuni aliteuliwa kushika wadhifa huo akitokea Jeshi la Magereza.
Mwenyekiti wa Bodi ya Magereza Saccos  Kamishna wa Fedha na Utawala wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Mbaraka Zemwanza akitoa mada katika ya mafunzo ya Ushirika yaliyoandaliwa na Chama cha Akiba na Mikopo cha Magereza (Magereza Saccos) kwa maafisa waandamizi  kutoka Makao Makuu ya Jeshi hilo pamoja na Wakuu wa Magereza wa mikoa yote ya kiutawala yaliyofanyika  Desemba 16, 2018.
Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Magereza (SACP) Ramadhan Nyamka  akichangia hoja katika  ya mafunzo ya Ushirika yaliyoandaliwa na Chama cha Akiba na Mikopo cha Magereza (Magereza Saccos) kwa maafisa waandamizi  kutoka Makao Makuu ya Jeshi hilo pamoja na Wakuu wa Magereza wa mikoa yote ya kiutawala yaliyofanyika Desemba 16, 2018.

Kamishna Msaidizi wa Magereza (ACP) Hasseid Mkwanda  akichangia hoja katika  ya mafunzo ya Ushirika yaliyoandaliwa na Chama cha Akiba na Mikopo cha Magereza (Magereza Saccos) kwa maafisa waandamizi  kutoka Makao Makuu ya Jeshi hilo pamoja na Wakuu wa Magereza wa mikoa yote ya kiutawala yaliyofanyika Desemba 16, 2018.
Baadhi ya Washiriki wa mafunzo Ushirika yaliyoandaliwa na Chama cha Akiba na Mikopo cha Magereza (Magereza Saccos) kwa maafisa waandamizi  kutoka Makao Makuu ya Jeshi hilo pamoja na Wakuu wa Magereza wa mikoa yote ya kiutawala yaliyofanyika  Desemba 16, 2018.(Picha zote na Jeshi la Magereza)

Friday, December 7, 2018

JESHI LA MAGEREZA LAFANYA MAANDALIZI YA UZINDUZI WA DAWATI LA JINSIA JIJINI DAR TAREHE 6 DEC, 2018

Kamishna Jenerali wa Magereza Phaustine Kasike akitoa hotuba  katika ufunguzi wa mafunzo ya siku moja  kuhusu mambo ya Dawati la Jinsia kwa Waratibu na Watendaji  wa Dawati hilo kutoka  Magereza yote nchini leo Desemba 06, 2018  ikiwa ni maandalizi ya uzinduzi wa Dawati la Jinsia ndani ya Jeshi la Magereza utakaofanyika  Desemba  07, 2018 katika viwanja vya Karimjee jijini  Dar es salaam.
Mwenyekiti  wa Taifa wa Dawati la Jinsia katika Jeshi la Magereza Kamishna wa Magereza Tusekile Mwaisabila akichangia jambo wakati wa ufunguzi wa mafunzo ya siku moja  kuhusu mambo ya Dawati la Jinsia kwa Waratibu na Watendaji  wa Dawati hilo kutoka  Magereza yote nchini  ikiwa ni maandalizi ya uzinduzi wa Dawati la Jinsia ndani ya Jeshi la Magereza yatakayofanyika  Desemba  07, 2018.
Meneja Huduma na Mikopo Binafsi kutoka Benki ya NMB Bw. Emmanuel Mahodaga akitoa mada kuhusu huduma za NMB hasa kwa watumishi wa Umma. NMB ni mmoja wa wadhamini wa shughuli za Uzinduzi wa Dawati la jinsia katika Jeshi la Magereza unaotarajiwa kufanyika kesho tarehe 07 Desemba, 2018 katika viwanja vya Karimjee, Dar es salaam.
Mtendaji Mkuu wa Chama cha Wanasheria Wanawake (TAWLA) Bi. Tike Mwambipile akichangia mada katika mafunzo  kuhusu mambo ya Dawati la Jinsia kwa Waratibu na Watendaji  wa Dawati hilo wa Magereza yote nchini  yaliyofanyika leo Desemba 06, 2018 katika Bwalo Kuu la Magereza ikiwa ni maandalizi ya uzinduzi wa Dawati la Jinsia ndani ya Jeshi la Magereza utakaofanyika Desemba  07, 2018 katika viwanja vya Karimjee jijini  Dar es salaam.
Baadhi ya washiriki wakifuatilia  mafunzo  kuhusu mambo ya Dawati la Jinsia kwa Waratibu na Watendaji  wa Dawati hilo kutoka  Magereza yote nchini yanayofanyika katika Bwalo Kuu la Magereza Ukonga, Dar es salaam  ikiwa ni maandalizi ya uzinduzi wa Dawati la Jinsia ndani ya Jeshi hilo. Uzinduzi huo utafanyika Desemba  07, 2018 katika viwanja vya Karimjee jijini  Dar es salaam.

Baadhi ya askari  ambao ni Waratibu na Watendaji  wa Dawati kutoka  Magereza mbalimbali nchini wakifuatilia  mafunzo  kuhusu mambo ya Dawati la Jinsia yaliyofanyika katika Ukumbi wa Bwalo Kuu la Magereza Ukonga, Dar es salaam  Desemba 06, 2018  ikiwa ni maandalizi ya uzinduzi wa Dawati la Jinsia ndani ya Jeshi la Magereza  utakaofanyika Desemba  07, 2018 katika viwanja vya Karimjee jijini  Dar es salaam.
Mtoa Mada kutoka Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Bw. Mapunda  John ambaye ni Afisa Maendeleo ya Jamii akifafanua jambo wakati wa mafunzo ya jinsia kwa Waratibu na Watendaji  wa Dawati la Jinsia kutoka  Magereza yote nchini yaliyofanyika leo Desemba 06, 2018 katika Ukumbi wa Bwalo Kuu la Magereza Ukonga, Dar es salaam.
Kamishna Jenerali wa Magereza Phaustine Kasike (katikati waliokaa) akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya maafisa na askari wa kike kutoka magereza mabalimbali hapa nchini ambao ni waratibu wa Dawati la Jinsia waliohudhuria mafunzo kuhusu Dawati la Jinsia yaliyofanyika leo Desemba 06, 2018 katika Ukumbi wa Bwalo Kuu la Magereza Ukonga, Dar es salaam.

Kamishna Jenerali wa Magereza Phaustine Kasike (katikati waliokaa) akiwa katika picha ya pamoja na maafisa wenye cheo cha Mkaguzi Msaidizi wa Magereza waliohudhuria mafunzo kuhusu Dawati la Jinsia yaliyofanyika leo Desemba 06, 2018 katika Ukumbi wa Bwalo Kuu la Magereza Ukonga, Dar es salaam.
Baadhi ya watoa mada na wafadhili  wakiwa katika picha ya pamoja na  Kamishna Jenerali wa Magereza Phaustine Kasike (katikati waliokaa) wakati wa ufunguzi wa mafunzo ya Dawati la Jinsia kwa Waratibu na Watendaji wa Dawati hilo kutoka magereza yote nchini yaliyofanyika leo Desemba 06, 2018. Kushoto ni Mkuu wa Magereza wa Mkoa wa Pwani ACP Rehema Songelaeli,  Mratibu wa Dawati la Jinsia Makao Makuu ya Magereza SACP Betha Minde na Mwenyekiti waTaifa wa Dawati la Jinsia ndani ya Magereza Kamishna wa Magereza Tusekile Mwaisabila. Kulia ni Afisa Mnadhimu wa Magereza Mkoa wa Morogoro ACP Elizaberth Mbezi, Mkuu wa Magereza wa Mkoa wa Lindi ACP Josephine Semwenda na Mkuu wa Magereza Mkoa wa Dar es Salaam SACP Julius Ntambala. (Picha zote na Jeshi la Magereza)

Tuesday, December 4, 2018

CGP KASIKE AFUNGUA MKUTANO WA WANGANGA WAKUU WA VITUO VYA AFYA VYA MAGEREZA NCHINI LEO DESEMBA 4, 2018.


Na ASP Deodatus Kazinja, Dodoma.

Wataalam wa  afya wa vituo vya magereza nchini wameaswa kufanya kazi kwa weledi na juhudi kubwa ili kutimiza malengo yanayotarajiwa na jeshi la magereza na taifa kwa ujumla.

Hayo yamesemwa na Kamishna Jenerali wa Magereza nchini (CGP) Phaustine Kasike wakati wa ufunguzi wa mkutano wa siku moja wa waganga wakuu wa vituo vya afya vya Jeshi la Magereza uliofanyika katika Ukumbi wa Morena Hoteli leo jijini Dodoma.

Aidha, CGP Kasike amemuagiza Mganga Mkuu wa Jeshi la Magereza kufuatilia kwa ukaribu utendaji wa kituo kimoja kimoja na kuhakikisha wataalam waliopo jeshini wanafanya kazi zao kwa uweledi ikiwa ndiyo matarajio ya jeshi.

Wakati huo huo CGP amewatolea wito wataalam hao wa afya magerezani kuhakikisha wanatekeleza muongozo wa serikali unaoagiza kuwaanzishia dawa watu wote wanaogundulika kuwa na maambukizi ya VVU na kuhakikisha wanakuwa na ufuasi mzuri wa dawa.

Waganga wakuu wa vituo vya afya katika Jeshi la magereza wapo katika mkutano huo  unaofadhiliwa na Asasi isiyo ya kiserikali ya JSI AIDS Free  ukiwa na lengo la kufanya tathmini ya mwenendo wa Mradi wa Uimarishaji wa Huduma za Ukimwi katika vituo vya afya vya polisi na magereza kwa mwaka 2017/18.

Asasi ya JSI AIDS Free chini ya serikali ya Marekani kwa kushirikiana na Wizara ya Mambo ya Ndani na Wziara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa miaka minne sasa imekuwa ikishirikia na Jeshi la Magereza katika kuboresha Huduma za Afya hasa mapambano ya Ukimwi.
Kamishna Jenerali wa Magereza  (CGP) Phaustine Kasike akisalimiana na baadhi ya wajumbe na viongozi wa Asasi ya kiraia ya JSI AIDS Free mara alipowasili leo Desemba 4, 2018  katika viwanja vya Morena Hotel jijini Dodoma kwa ajili ya ufunguzi wa kikao cha siku moja cha kutathmini ya mwenendo  wa  Mradi wa Uimarishaji wa Huduma za Ukimwi katika vituo vya afya vya polisi na magereza kwa mwaka 2017/18.
Kamishna Jenerali wa Magereza  (CGP) Phaustine Kasike akitoa hotuba katika mkutano wa waganga wakuu wa vituo vya afya vya magereza yote nchini kilichoandaliwa na Asasi isiyo ya kiserikali ya JSI AIDS Free  kwa ajili ya kutathmini ya mwenendo wa Mradi Uimarishaji wa Huduma za Ukimwi katika vituo vya afya vya polisi na magereza kwa mwaka 2017/18 leo Desemba 4, 2018 Morena Hoteli jijini Dodoma.  Kushoto ni Mkuu wa Magereza Mkoa wa Dodoma SACP Omary Salum, Mtendaji Mkuu wa AIDS Free Tanzania Dkt. Deogratias Kakiziba. Kutoka kulia ni Mwakilishi wa Mganga Mkuu wa Jeshi la Magereza INSP Adili Kachima na wapili kulia  ni SSP Dkt. Richard Mwakina kutoka kituo cha afya chama magereza Ukonga, Dar es salaam.

Washiriki wa kikao wakifuatilia hotuba ya Kamishna Jenerali wa Magereza Phaustine Kasike (hayupo pichani) katika kikao cha waganga wakuu wa vituo vya afya vya magereza nchini kilichoandaliwa na Asasi isiyo ya kiserikali ya JSI AIDS Free  kwa ajili ya ufuatiliaji wa mwenendo  wa Mradi Uimarishaji wa Huduma za Ukimwi katika vituo vya afya vya polisi na magereza kwa mwaka 2017/18 kilichofanyika leo tarehe 04 Desemba, 2018 jijini Dodoma.
Mganga Mkuu wa Kituo cha Afya cha Gereza Kuu Butimba Mwanza ASP. Dkt.  Alex Lukuba akipokea cheti kutoka kwa mgeni rasmi (CGP Kasike) ikiwa ni utambuzi wa kufanya vizuri kwa kituo anachokisimamia katika kusimamia masuala yahusuyo Ukimwi katika kituo chake.

Kamishna Jenerali wa Magereza  (CGP) Phaustine Kasike (katikati waliokaa) akiwa katika picha ya pamoja na waganga wakuu wa vituo vya afya vya magereza kote nchini na watendaji wakuu wa Asasi ya isiyo ya kiserikali ya JSI AIDS Free ambayo ndiyo wafadhili wa Mradi Uimarishaji wa Huduma za Ukimwi katika vituo vya afya vya Magereza na polisi nchini. (Picha zote na Jeshi la Magereza)

Sunday, November 18, 2018

KATIBU MKUU WA MAMBO YA NDANI, MEJA JENERALI JACOB KINGU AKAGUA MABORESHO YA KIWANDA CHA VIATU GEREZA KUU KARANGA MOSHI

Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Ndani, Meja Jenerali Jacob Kingu akisalimiana na Maafisa wa Jeshi la Magereza Mkoani Kilimanjaro mara baada ya kuwasili katika ziara Maalum ya kukagua maboresho mbalimbali katika Kiwanda cha Viatu cha Gereza Kuu Karanga Moshi jana  Novemba 17, 2018. Kushoto kwake ni Kamishna Jenerali wa Magereza, Phaustine Kasike.

Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Ndani ya nchi, Meja Jenerali Jacob Kingu(meza kuu) akitoa maelekezo kwa Kaimu Mkuu wa Kiwanda hicho, Mrakibu Msaidizi wa Magereza, Hamis Nyaku(aliyesimama). Kushoto ni Kamishna Jenerali wa Magereza, Phaustine Kasike
Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Ndani ya nchi, Meja Jenerali Jacob Kingu na Kamishna Jenerali wa Magereza, Phaustine Kasike wakiangalia Buti za aina mbalimbali za Jeshi zinazotengenezwa katika Kiwanda cha Viatu Karanga Moshi.
Sehemu ya viatu aina mbalimbali ikiwemo viatu vya maafisa na Buti za Jeshi zinazotengenezwa katika Kiwanda cha Viatu Karanga Moshi kwa ajili ya Jeshi la Polisi nchini. Jeshi la Polisi limetengenezewa viatu aina ya buti pea elfu kumi (10,000) na pea elfu tano (5,000) za viatu vya maafisa zenye thamani ya Tsh. 1, 237, 666, 600/=, tayari buti zimekabidhiwa kwa Jeshi hilo na hivi sasa kiwanda kinamalizia utengenezaji wa viatu vya maafisa wa Jeshi la Polisi.

Maafisa Masoko wa Kiwanda cha viatu Karanga Moshi wakivipanga viatu vya kiraia aina mbalimbali vinavyotengenezwa katika kiwanda hicho kama inavyoonekana katika picha.

Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Ndani ya nchi, Meja Jenerali Jacob Kingu akipata maelezo ya kitaalam juu ya utengenezaji wa Buti za Jeshi kutoka kwa Mtaalam wa utengenezaji viatu wa Jeshi la Magereza
(Picha zote na Jeshi la Magereza).

KATIBU MKUU MAMBO YA NDANI NA CGP KASIKE WATEMBELEA KIWANDA CHA SAMANI CHA JESHI LA MAGEREZA CHA ARUSHA KILICHOTEKETEA KWA MOTO


Na Lucas Mboje, Arusha
KATIBU Mkuu Wizara ya Mambo ya  Ndani ya Nchi, Meja Jenerali Jacob Kingu pamoja na Kamishna Jenerali wa Magereza nchini, Phaustine Kasike leo wametembelea Kiwanda cha Samani cha Arusha, mali ya Jeshi la Magereza ili kujionea athari mbalimbali iliyosababishwa na ajali ya moto iliyotokea juzi Novemba 16, 2018.
Akizungumza eneo la tukio Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Meja Jenerali Jacob Kingu amesema kuwa ni vyema taasisi mbalimbali nchini pamoja na wananchi wakachukua tahadhali za majanga ya moto ili kuepusha hasara zinazoweza kujitokeza kufuatia majanga hayo.
Amesema kuwa Wizara yake itaendelea kuliwezesha Jeshi la Zimamoto na Uokoaji vifaa vya kisasa ili liweze kukabiliana na majanga ya moto pindi yanapojitokeza.
Aidha, Katibu Mkuu huyo, Meja Jenerali Kingu amelitaka Jeshi la Magereza kuhakikisha kuwa linafanya jitihada za haraka za kurejesha shughuli za uzalishaji katika kiwanda hicho ikiwemo kufanyia matengenezo baadhi  ya mashine zilizoteketezwa na moto.
Kwa upande wake, Kamishna Jenerali wa Magereza nchini, Phaustine Kasike amevishukru vyombo vya ulinzi na usalama ikiwemo Jeshi la Zimamoto na Uokoaji pamoja na Jeshi la Polisi Mkoani Arusha sambamba na wananchi waliojitokeza kusaidia katika uzimaji wa moto huo ambao umeunguza sehemu ya kiwanda hicho.
“Nawashukru sana Jeshi la zimamoto na uokoaji Mkoani Arusha, Jeshi la Polisi pamoja na wananchi kwa kazi kubwa waliyoifanya siku ya tukio kwani niliarifiwa kuwa moto ulikuwa mkubwa lakini tunashukuru Mungu hatimaye uzimaji ulifanikiwa pamoja na hasara iliyojitokeza”. Alisema Jenerali Kasike.
Akizungumzia chanzo cha moto huo na hasara iliyojitokeza, Kamishna Jenerali Kasike amesema kuwa taarifa za awali zinaonesha kuwa moto huo ulisababishwa na hitilafu ya umeme ambayo ilisababisha kuteketea kwa baadhi ya mashine za kiwanda hicho pamoja na uharibu wa nyaraka mbalimbali za ofisi katika jengo la utawala.
Wakati huo huo, Kamishna Jenerali Phaustine Kasike ameunda Kamati maalum ya Maafisa watano kutoka Makao Makuu ya Jeshi la Magereza ambayo itachunguza chanzo cha moto huo pamoja na kuwasilisha taarifa kamili ya hasara iliyojitokeza. Tume hiyo itaongozwa na Kamishna wa Fedha na Mipango wa Jeshi hilo, Kamishna wa Magereza, Gideon Nkana.
Kiwanda cha samani cha Magereza Arusha kilimikishwa rasmi kwa Jeshi la Magereza mwaka 1973 baada ya Azimio la Arusha mwaka 1967 ambapo tangu kipindi hicho kiwanda hicho kinajishughulisha na utengenezaji wa samani mbalimbali za ofisi na samani za majumbani. Pia kiwanda hiki hutumika kuwafundisha na kuwarekebisha wafungwa ili wamalizapo vifungo vyao waweze kujitegemea kupitia ujuzi waliojifunza.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Meja Jenerali Jacob Kingu akiwasili Novemba 17, 2018 katika Kiwanda cha samani cha Magereza Arusha kukagua sehemu mbalimbali ambazo moto umeteketeza sehemu ya kiwanda hicho. Kushoto kwake ni Kamishna Jenerali wa Magereza, Phaustine Kasike.

Mkuu wa Magereza Mkoa huo, ACP Anderson Kamtiaro akisoma taarifa ya janga la moto mbele ya Katibu Mkuu Mambo ya ndani ya nchi, Meja Jenerali Jacob Kingu aliwasili kiwandani kujionea uhabribu mbalimbali uliojitokeza.

Kamishna Jenerali wa Magereza nchini, Phaustine Kasike akitoa taarifa kwa Katibu Mkuu Mambo ya ndani ya nchi, Meja Jenerali Jacob Kingu kuhusu hatua mbalimbali ambazo amezichukua ikiwemo kuunda kamati maalum ya watu watano ambayo itachunguza tukio la moto katika kiwanda hicho.

Kamishna Jenerali wa Magereza nchini, Phaustine Kasike (wa pili toka kulia) pamoja na Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Meja Jenerali Jacob Kingu (kulia kwake), wakiangalia moja ya mashine mbalimbali ambazo zimeteketezwa na moto katika kiwanda cha Samani cha Magereza Arusha. Chanzo cha moto huo inasemekana ni hitilafu ya umeme ndani ya kiwanda hicho.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Meja Jenerali Jacob Kingu (wa kwanza kushoto) akitoa maelekezo mbalimbali kwa Kamishna Jenerali wa Magereza, Phaustine Kasike(katikati). Kulia ni Kamishna wa Fedha na Mipango, Kamishna wa Magereza, Gideon Nkana ambaye ni Kiongozi wa Kamati Maalum ya kuchunguza tukio hilo.

Jengo la kiwanda cha samani cha Magereza Arusha ambalo limeteketea kwa moto.

Muonekano wa baadhi ya mashine pamoja na vifaa mbalimbali na nyaraka nyinginezo za ofisi zilizoungua kufuatia janga la moto.

Samani mbalimbali zinazotengenezwa katika kiwanda cha samani cha Magereza Arusha kama inavyoonekana katika picha zikiwa tayari kwenda sokoni(Picha na Jeshi la Magereza).

Friday, November 16, 2018

MKUU WA JESHI LA MAGEREZA AKUTANA NA RC NJOMBE KABLA YA KUHITIMISHA ZIARA YAKE TAREHE 15/11/2018

Mkuu wa Mkoa wa Njombe, Mhe. Christopher Ole Sendeka akisalimiana na Mkuu wa Jeshi la Magereza nchini (CGP) Phaustine Kasike  alipotembelea Ofisi za Mkuu wa Mkoa kabla ya kuhitimisha ziara yake ya kikazi, Novemba 15, 2018.

Mkuu wa Mkoa wa Njombe, Mhe. Christopher Ole Sendeka akitoa taarifa fupi ya Mkoa wake alipotembelewa na Mkuu wa Jeshi la Magereza Ofsini kwake.
Kamishna Jenerali wa Magereza Nchini (CGP) Phaustine Kasike akielezea malengo ya ziara yake ya kikazi mbele ya Mkuu wa Mkoa wa Njombe alipotembelea Ofisi za Mkoa huo.


Mkuu wa Jeshi la Magereza, CGP. Phaustine Kasike akiagana na baadhi ya askari wa Gereza Njombe baada ya kuhitimisha ziara yake ya kikazi Mkoani Njombe.

Mkuu wa Mkoa wa Njombe, Mhe. Christopher Ole Sendeka (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na  Kamishna Jenerali wa Magereza nchini, Phaustine Kasike(wa pili toka kulia) pamoja na wajumbe wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa wa Njombe. Wa pili toka kushoto ni Katibu Tawala Mkoa wa Njombe, Bw. Erick Shitindi ( Picha na Jeshi la Magereza).

Thursday, November 15, 2018

ZIARA YA CGP KASIKE GEREZA LA WILAYA MAKETE, MKOANI JOMBE



Mkuu wa Jeshi la Magereza Nchini (CGP) Phaustine Kasike akizungumza jambo alipotembelea Ofisi za Mkuu wa Wilaya Makete Novemba 14, 2018. Wengine ni Maafisa Waandamizi wa Jeshi hilo.
Baadhi ya Askari wa kike wa Jeshi la Magereza wakiteta jambo na Kamishna Jenerali wa Magereza nchini, Phaustine Kasike ambapo askari hao wamempongeza Mkuu wa Jeshi hilo kwa uamuzi wake wa kutembelea magereza mbalimbali hapa nchini.
Mkuu wa Jeshi la Magereza nchini (CGP) Phaustine Kasike akiwasili Gereza Makete tayari kwa ziara yake ya kikazi Mkoani Njombe, Novemba 14,  2018.

 Kamishna Jenerali wa Magereza, Phaustine Kasike akikagua maandalizi ya mashamba ya kilimo cha mahindi katika eneo la Gereza Ludewa mapema leo asbuhi Novemba 14, 2018  kabla ya kuelekea Gereza Makete kuendelea na ziara yake ya kikazi.
Mkuu wa Gereza Makete, SP. Aloyce Kayera(kushoto) akisoma taarifa ya Gereza mbele ya Kamishna Jenerali wa Magereza Nchini (CGP) Phaustine Kasike(kulia) alipotembelea gereza hilo leo Novemba 14, 2018.
. Mkuu wa Wilaya ya Makete, Mhe. Veronica Kessy akiagana na Kamishna Jenerali wa Magereza, Phaustine Kasike alipotembelea Ofisi za Mkuu wa Wilaya Makete.