Mojawapo ya Jukumu la Jeshi la Magereza ni kuwapeleka mahakamani mahabusu na kuwarudisha magerezani.

Gadi ya askari Wanawake na Wanaume wa Jeshi la Magereza katika Maadhimisho ya Sherehe za Kitaifa.

Ng'ombe bora wa Nyama na Maziwa ni sehemu ya miradi ya Uzalishaji inayoendeshwa na kusimamiwa na Jeshi la Magereza nchini.

Sehemu ya Mashamba makubwa yanayoendeshwa na Jeshi la Magereza: Shughuli za Kilimo cha Mashamba makubwa, madogo na bustani za mboga mboga ni moja ya shughuli za Magereza katika kuwafunza wafungwa namna ya kujitegemea mara wamalizapo vifungo vyao.

Baadhi wa wafungwa katika Kiwanda cha Ushonaji nguo cha Gereza Kuu Ukonga wakiwa kazini: Shughuli za Ushonaji wa nguo ni moja ya eneo ambalo wafungwa hupata huduma za urekebishwaji kwa vitendo.

Sunday, January 29, 2017

KAIMU KAMISHNA JENERALI WA MAGEREZA DR. JUMA MALEWA AHITIMISHA ZIARA MAGEREZA MKOANI MOROGORO NA PWANI

Kaimu Mkuu wa Magereza Mkoa wa Morogoro  Kamishna Msaidizi wa Magereza (ACP)Mzee Nyamka akitoa taarifa ya utendaji katika mkoa wake kwa Kaimu Kamishna Magereza Dr. Juma Malewa (hayupo pichani) mwishoni mwa juma hili alipofanya ziara ya kiutendaji katika baadhi ya Magereza mkoani humo.
Baadhi ya Maafisa na askari wa Gereza Mbigiri Mkoani Morogoro wakifuatilia ufafanuzi wa hoja mbalimbali walizozitoa mbele ya Kaimu Kamishna Jenerali wa Magereza Dr. Juma Malewa (hayupo pichani) alipofanya ziara kituoni hapo na kufanya Baraza la watumishi hao ili kusikiliza kero, hoja na mapendekezo yote ikiwa ni kuboresha utendaji kazi wa siku kwa siku.
Baadhi ya Maafisa na askari wa Gereza  Wami Kuu pamoja na Wami Vijana Mkoani Morogoro kwa pamoja  kwa makini wakifuatilia ufafanuzi wa hoja mbalimbali walizozitoa kwa Kaimu Kamishna Jenerali wa Magereza Dr. Juma Malewa (hayupo pichani) katika Baraza la pamoja alipowatembelea hivi karibuni kuona utendaji kazi katika vituo vyao lakini pia kuwapa hamasa ya utendaji kazi.
Kaimu Kamishna Jenerali wa Magereza Dr. Juma Malewa (wa kwanza kulia) akitembelea jengo la Karakana ya Ufundi ya Gereza Wami Vijana.  Jengo hilo pamoja na kuendelea kutumika lakini bado linahitaji kukamilishwa kujengwa na kuwekewa miundombinu ili liweze kutoa huduma kama ilivyokusudiwa.
Kaimu Kamishna Jenerali wa Magereza Dr. Juma Malewa (katikati) akipata maelezo mafupi ya kiutendaji kutoka kwa Mkuu wa Gereza la Mahabusu Mrakibu wa Magereza (SP) Zephania Neligwa (aliyesimama) ofisini kwake wakati wa ziara ya Kaimu Kamishna Jenerali Mkoani Morogoro aliyoifanya mwishoni  mwa juma.
Kaimu Kamishna Jenerali wa Magereza Dr. Juma Malewa (wa kwanza kushoto) akitolea ufafanuzi hoja mbalimbali zilizotolewa na baadhi ya Maafisa na Askari katika kikao kilichojumuisha askari wa Ofisi ya Mkuu wa Magereza  Mkoa wa Morogoro na Gereza Mahabusu. 
Kaimu Kamishna Jenerali wa Magereza Dr. Juma Malewa (katikati)akisisitiza jambo wakati wa kikao  kikao chake kilichojumuisha askari wa Ofisi ya Mkuu wa Magereza  Mkoa wa Morogoro na Gereza Mahabusu. Kushoto ni Kaimu Mkuu wa Magereza Mkoa wa Morogoro Kamishna Msaidizi wa Magereza (ACP) Mzee R.Nyamka. Na kulia Mkuu wa Shirika la Magereza (Corporation Sole) Kamishna Msaidizi wa Magereza (ACP) Joel Bukuku na nawa mwisho ni Mkuu wa Kitengo cha Uwekezaji na Ujasiliamari wa Jeshi la Magereza Mrakibu Mwandamizi wa Magereza (SSP) Uswege Mwakahesya.
Kaimu Kamishna Jenerali wa Magereza Dr. Juma Malewa akisaini kitabu cha wageni ofisini kwa Mkuu wa Gereza Kihonda mara alipowasili kituoni hapo kujionea shughuli mbalimbali kituoni hapo  sanjari na kuongea na maafisa na askari wa kituo hicho mwishoni mwa Juma hili.
Kaimu Kamishna Jenerali wa Magereza Dr. Juma Malewa (wa kwanza kushoto) akikagua maendeleo ya jengo jipya la ofisi ya Mkuu wa Gereza Kihonda. Jengo hilo linashengwa kwa jitihada za Mkuu wa Gereza hilo kwa kushirikiana na maafisa na askari wa kituo hicho. Viongozi wengine hapo ni Kaimu Mkuu wa Magereza Mkoa wa Morogoro, Kamishna Msaidizi wa Magereza (ACP) Mzee Nyamka, Mkuu wa Shirika la Magereza (Corporation Sole) Kamishna Msaidizi wa Magereza (ACP) Joel Bukuku na Mkuu wa Gereza Kihonda Kamishna Msaidizi wa Magereza Ben Mwansasu.
Kaimu Kamishna Jenerali wa Magereza Dr. Juma Malewa akiendelea kusikiliza hoja mbalimbali za maafisa na askari wa Gereza Kihonda wakati wa ziara ya kikazi kituoni hapo. Aliyesimama ni Mkaguzi Msaidizi wa Magereza (A/Insp) Amani Moses akichangia jambo wakati wa kikao hicho.
Kaimu Kamishna Jenerali wa Magereza Dr. Juma Malewa akisalimiana na baadhi ya maafisa wa gereza Kihonda mara alipowasili akiwa tayari kufanya kikao na watendaji wa gereza hilo.
Mmoja wa askari wa gereza Kihonda akiwa na sura ya bashasha baada ya kupata fursa ya kusalimiana na Kaimu Kamishna Jenerali wa Magereza mara baada ya kikao wakati wa ziara ya Kaimu Kamishna Jenerali katika baadhi ya vituo mkoani Morogoro ikiwemo gereza Kihonda, mwishoni wa juma hili
Kaimu Kamishna Jenerali wa Magereza Dr. Juma Malewa akikagua maendeleo ya moja ya nyumba za zinazojengwa kwa mtindo wa kujitolea katika gereza la Wanawake Kingolwira mkoani Morogoro ikiwa ni jitihada za kukabiliana na tatizo la uhaba wa nyumba kituoni hapo. Aliyefuatana naye ni Mkuu wa Gereza la Wanawake Kamishna Msaidizi wa Magereza (ACP) Loyce Luhembe
Kaimu Kamishna Jenerali wa Magereza Dr. Juma Malewa (katikati) akitolea ufafanuzi wa jambo katika kikao chake na watumishi wa gereza Kihonda alipofanya ziara ya kiutendaji katika baadhi ya Magereza ya mkoa wa Morogoro. Kushoto ni Kaimu Mkuu wa Magereza mkoa wa Morogoro, Kamishna Msaidizi wa Magereza (ACP) Mzee Nyamka na kulia Mkuu wa Gereza la Kihonda, Kamishna Msaidizi wa Magereza (ACP) Ben Mwansasu.
Baadhi ya Maafisa na askari wa Kingolwira Complex inayojumuisha Chuo cha Uhunzi na Udereva, Gereza Mtego wa Simba, Gereza Mkono wa Mara na Gereza la Wanawake Kingolwira katika kikao cha pamoja na Kaimu Kamishna Jenerali wa Magereza Dr. Juma Malewa alipofanya ziara katika vituo hivyo kujionea shughuli mbalimbali za kila siku.
Sehemu ya Maafisa na askari wa vituo vya Bwawani Sekondari (inayomilikiwa na Jeshi la Magereza) na Gereza Ubena mkoani Pwani wakiwa katika kikao cha pamoja na Kaimu Kamishna Jenerali wa Magereza Dr. Juma Malewa (hayupo pichani) alipofanya ziara vituoni hapo ili kujionea shughuli za vitu hivyo lakini pia kusiliza shida na maoni ya watumishi katika vituo hivyo jana tarehe 28.01. 2017.
Mkuu wa Magereza Mkoa wa Pwani (RPO), Kamishna Msaidizi wa Magereza (ACP) Boyd Mwambingu akitolea ufafanuzi moja ya hoja zilizoibuka katika kikao cha Kaimu Kamishna Jenerali wa Magereza Dr. Juma Malewa na wafanyakazi wa vituo hivyo alichofanya mwishoni mwa juma.
Kaimu Kamishna Jenerali wa Magereza Dr. Juma Malewa (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya maafisa na askari wa gereza Wami Kuu na Vijana alipifanya ziara ya kikazi vituoni hapo.
Kaimu Kamishna Jenerali wa Magereza Dr. Juma Malewa (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya maafisa na askari wa Gereza la Mahabusu Morogoro alipofanya ziara mkoani humo mwishoni mwa juma.
Kaimu Kamishna Jenerali wa Magereza Dr. Juma Malewa (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya maafisa na askari wa gereza Kihonda alipofanya ziara ya kikazi kituoni hapo Ijumaa, 27.01.2017.
Kaimu Kamishna Jenerali wa Magereza Dr. Juma Malewa (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya maafisa na askari wa Kingolwira Complex mara baada ya kikao kilicholenga kusikiliza kero na hoja mbalimbali za watumishi hao, tarehe 28.01.2017.
Picha zote na ASP Deodatus Kazinja, PHQ 


Kaimu Kamishna Jenerali wa Magereza Dr. Juma Malewa katika hali ya kuamsha hari na morali ya kufanya kazi kwa watendaji wa Jeshi la Magereza amefanya ziara ya kikazi katika baadhi ya Magereza ya Mkoa wa Morogoro na Pwani mwishoni juma hili.
 
Ziara hiyo imejumuisha Magereza ya Mbigiri, Wami Kuu, Wami Vijna, Mahabusu, Kihonda, Kingolwira Complex yote ya mkoa wa Morogoro na Shule ya Sekondari Bwawani na gereza Ubena vya mkoani Pwani.
 
Kutoka kwa Kaimu Jenerali maafisa na askari aliwapata taarifa fupi ya Uwekezaji wa Ubia katika kiwanda cha sukari cha gereza Mbigiri Mkoani Morogoro kati ya Jeshi la Magereza na Mifuko ya Hifadhi ya Jamii ya PPF na NSSF. Alisema uwekezaji huu ni kwa faida ya Jeshi kama Taasisi hivyo ni vizuri kila askari akalifahamu hilo.
 
Katika ziara hiyo pia alipata wasaa wa kufanya vikao na watendaji ambapo maafsa, askari na watumishi raia walipata fursa ya kuuliza maswali moja kwa moja kutoka kwa Mtendaji mkuu wa Jeshi la Magereza ambapo baadhi ya mambo yalipatiwa majibu ya papo hapo na mengine kupewa ahadi ya kutatuliwa katika siku za usoni hasa yenye uhusiano na masuala ya kibajeti.
 
Miongoni mwa masuala yaliyoonekana kuwa ni tatizo sugu ni pamoja na huduma za maji, usafiri, matibabu kwa wafungwa na mahabusu, sare za askari, posho mbalimbali kulingana na stahiki ya kila askari  na mambo mengine madogo madogo ambayo yote kimsingi yanagusia suala la fedha.
 
Katika vikao hivyo Kaimu Kamishna Jenerali wa Magereza Dr. Juma Malewa alitolea maelekezo baadhi ya mambo yaliyohitaji kauli ya Makao Makuu ya Jeshi lakini pia aliwahakikishia kuwa ofisi yake itaendelea kushughulikia kero zote na kusaidia kwa haraka pale inapohitaji kwa kutegemeana na hali ya fedha kwa wakati huo.
 
Kaimu Kamishna Jenerali aliwaasa maafisa askari kuwa waangalifu wanapotumia mitandao ya kijamii hasa kwa kuzingatia viapo vya utumishi wao.
 
“Ninyi ni askari wenye viapo vya utii wa mamlaka zilizopo, jiepusheni na mijadala ya mitandaoni kwani mingine iko kinyume na maadili ya kazi zetu. Ukipokea ujumbe usiofaa futa kabisa badala ya kuusambaza” alisisitiza Dr. Malewa
 
Aidha Dr. Malewa aliwataarifu watumishi hao adhma yake kuu ya kuona Jeshi linakuwa na hospitali kubwa nayakisasa ili kuondoa kero na aibu inayowapata askari na familia zao wanapokuja kutibiwa Jijini Dar es salaam.
 
Ni dhamira yangu kuona tunaanzisha ujenzi wa hospitali hivi karibuni ili kuondoka na adha ambayo wote mnaifahamu, na hospitali hii tutaijenga kwa kutumia vyanzo mbali mbali ikiwemo na sisi kama askari kujitolea. Naomba mtuunge mkono mara wazo hili litakapoletwa kwenu” alisisitiza Kaimu Jenerali.
 
Mwisho aliwataka maafisa na askari kudumisha nidhamu kazini ikiwa ndiyo msingi mkuu wa mafanikio hasa katika kazi za majeshi.

Friday, January 27, 2017

JESHI LA MAGEREZA, PPF NA NSSF KUITIKIA TANZANIA YA VIWANDA KWA VITENDO

Kaimu Kamishna Jenerali wa Magereza Dkt. Juma Malewa (mwenye miwani) na ujumbe wake wakiwasili Gereza Mbigiri Mkoani Morogoro jana tarehe 26.01.2017 tayari kwa kukagua eneo la uwekezaji wa Kilimo cha Miwa na Uzalishaji wa Sukari. Wa kwanza nyuma yake ni Mkurugenzi Mkuu wa NSSF Prof.Godius  Kahyarara, mshauri mwelekezi katika mradi huo ndugu  Seleman Karanga akifuatiwa na Mkurugenzi Mkuu wa PPF ndugu William Erio
Ujumbe wa Uwekezaji wa Ubia katika kiwanda cha sukari cha Mbigiri kati ya  Mifuko ya Jamii ya NSSF, PPF na Jeshi la Magereza  kupitia Shirika la Magereza (Corporation Sole) wakikagua baadhi ya maeneo ya ndani ya kiwanda cha zamani cha sukari cha Gereza hilo kilichosimamisha uzalisha zaidi ya miaka 10 iliyopita.
Ujumbe wa Uwekezaji wa Ubia katika kiwanda cha sukari cha Mbigiri kati ya  Mifuko ya Jamii ya NSSF, PPF na Jeshi la Magereza wakipata  maelezo kutoka kwa Mrakibu Msaidizi wa Magereza (ASP) Angolwise Pilla (wa pili kushoto) ambaye ni mfanyakazi wa zamani kilichokuwa kiwanda cha sukari cha Gereza Mbigiri kilicho simamisha uzalisha zaidi ya miaka 10 iliyopita.
Viongozi waandamizi kutoka Jeshi la Magereza, PPF na NSSF wakipata maelezo ya namna kiwanda cha sukari cha Gereza Mbigiri mkoani Morogoro kilivyokuwa kikifanya kazi kutoka kwa mfanyakazi wa zamani wa kiwanda hicho  Mrakibu Msaidizi wa Magereza (ASP) Angolwise Pilla (wa nne kushoto). Viongonzi hao walitembelea kiwanda hicho jana ikiwa ni hatua za awali za uwekezaji wa ubia katika uzalishaji wa sukari nchini kati ya Taasisi hizo tatu.
Kaimu Kamishna Jenerali wa Magereza Dkt. Juma Malewa (wa pili kushoto) akisikiliza kwa makini maelezo na namna kiwanda cha zamani cha sukari cha Gereza Mbigiri mkoani Morogoro kilivyokuwa kikifanya kazi kutoka kwa mmoja wa wafanyakazi wa zamani wa kiwanda hicho Mrakibu Msaidizi wa Magereza (ASP) Angolwise Pilla (wa pili kuli). Nyuma ya Dr. Malewa ni Mkurugenzi Mkuu wa PPF William Erio na  wa tatu ni Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa NSSF Prof. Godius Kahyarara.
Mwonekano wa baadhi ya majengo ya kilichokuwa kiwanda cha sukari cha Gereza Mbigiri Mkoani Morogoro. Kiwanda hicho kilisimamisha uzalishaji tangu mwaka 1996 kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo uchakavu wa mitambo. Mifuko ya PPF, NSSF na Jeshi la Magereza wako katika hatua za awali za kuingia ubia wa kufufua Kiwanda hicho ili kuitikia kauli mbiu ya serikali ya Awamu ya Tano inayotilia msisitizo wa ujenzi wa viwanda.
Msafara wa wawekezaji wa ubia kati ya Mifuko ya PPF, NSSF na Jeshi la Magereza katika Kiwanda cha Sukari katika Gereza la Mbigiri Mkoani Morogoro wakikagua eneo la mashamba yatakayolimwa miwa kwa ajili ya kiwanda hicho. Eneo la ekari 12,000 zimetengwa kwa ajili ya kuanza kilimo cha miwa.
Mkuu wa Gereza la Mbigiri Kamishna Msaidizi wa Magereza (ACP) Charlez Kimbi (aliyeinua mkono juu) akitoa ufafanuzi wa jambo katika ziara ya kukagua shamba la hekari 12,000 zilizotayari kwa kilimo cha miwa kwa ajili ya uzalishaji wa sukari.
Maafisa wa Jeshi la Magereza, PPF na NSSF wakipiga kambi polini ili kuteta jambo wakati wa ziara ya kukagua shamba linalotarajiwa kulimwa miwa kwa ajili ya kiwanda cha sukari cha Gereza Mbigiri kinachotarajiwa kuendeshwa kwa ubia wa Taasisi hizo tatu.
Kaimu Kamishna Jenerali wa Magereza Dkt. Juma Malewa akifafanua jambo kwa waandishi wa habari wakati wa ziara ya kutembelea eneo la uwekezaji wa Kilimo cha Miwa na Uzalishaji wa sukari mradi utakaoendeshwa kwa ubia kati ya Jeshi la Magereza kupitia Shirika la Magereza (Corporation Sole), Mifuko ya Hifadhi ya Jamii ya PPF na NSSF katika eneo la Gereza Mbigiri Mkoani Morogoro, jana tarehe 26. 01. 2017
Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Jamii wa PPF ndugu William Erio akisisitiza jambo kwa waandishi wa habari wakati wa ziara ya kutembelea eneo la uwekezaji wa Kilimo cha Miwa na Uzalishaji wa sukari mradi utakaoendeshwa kwa ubia kati ya Jeshi la Magereza kupitia Shirika la Magereza (Corporation Sole), Mifuko ya Hifadhi ya Jamii ya PPF na NSSF katika eneo la Gereza Mbigiri Mkoani Morogoro, jana tarehe 26. 01. 2017
Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Jamii wa NSSF Prof.Godius Kahyarara akitoa maelezo ya ziada  kwa waandishi wa habari wakati wa ziara ya kutembelea eneo la uwekezaji wa Kilimo cha Miwa na Uzalishaji wa sukari mradi utakao endeshwa kwa ubia kati ya Jeshi la Magereza kupitia Shirika la Magereza (Corporation Sole), Mifuko ya Hifadhi ya Jamii ya PPF na NSSF katika eneo la Gereza Mbigiri Mkoani Morogoro, jana tarehe 26. 01. 2017

(Picha zote na ASP Deodatus Kazinja, PHQ) 

Na ASP Deodatus Kazinja, Magereza Makao Makuu
Katika kuitikia wito wa serikali ya Awamu ya Tano wa Kujenga Tanzania ya Viwanda Jeshi la Magereza kupitia Shirika la Magereza (Corporation Sole) limeingia ubia na Mifuko ya Jamii ya PPF na NSSF wa kufufua kilichokuwa kiwanda cha Sukari kilichopo Gereza Mbigiri Mkoani Morogoro.
 
Kiwanda cha sukari cha Mbigiri kilisimisha uzalishaji tangu mwaka 1996 kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo uchakavu wa mitambo. Lakini kutokana na kuwa eneo zuri kimkakati yaani uwepo wa raslimali ardhi ya kutosha, nguvu kazi ya baadhi ya wataalam wa zamani wa kiwanda hicho, chanzo cha maji kuwezesha kuendesha kilimo cha umwagiliaji kumezishawishi taasisi zingine kushirikiana na Jeshi la Magereza kuwekeza katika eneo hili.
 
Akiongea na waandishi wa habari katika ziara ya kukagua eneo la Uwekezaji Kaimu Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza Dkt. Juma Malewa amesema uwekezaji huu utakuwa na faida nyingi ikiwa ni pamoja na kuongeza ajira, upatikanaji wa sukari ya kutosha nchini lakini pia wakulima  wa eneo hilo watapata soko la uhakika la kuuza miwa katika kiwanda hicho.
 
Aidha Kaimu Kamishna huyo ametoa wito kwa wananchi kutovamiwa maeneo ya majeshi kwani mengi yamehifadhiwa kwa shughuli za baadae zenye maslahi mapana kwa taifa.
 
Naye Mkurugenzi Mkuu wa PPF William Erio amesema matarajio yao ni kuona kiwanda kinaanza mapema iwezekanavyo hivyo, ametoa wito kwa wananchi wa maeneo jirani kuchangamkia fursa ya kulima zao la miwa kwa maana sasa watakuwa na uhakika wa soko lililo karibu nao.
 
Kwa upande wake Mkurugenzi Mkuu wa NSSF Prof. Godius Kyaharara amesema kuwa kiwanda hicho kitakuwa na uwezo wa kuzalisha tani 30,000 kwa mwaka na kitahitaji tani 500,000 za miwa hivyo ni fursa nzuri kwa wananchi wa maeneo jirani.
 
“Ni matarajio yetu kuwa kiwanda hiki kitaongeza ajira, kitainua uchumi kwa wafanyakazi na wanakijiji, tutapata wanachama wengi zaidi lakini pia tutakuwa tumeongeza uwezo wetu vizuri zaidi wa kuwahudumia wanachama wetu kupitia uwekezaji huu” Alihitimisha Prof. Kahyarara.
 

Friday, January 13, 2017

VIDEO: ASKARI WAHITIMU WA MAFUNZO YA KIKOSI MAALUM WAKIONESHA UWEZO WAO MBELE YA WAZIRI NCHEMBA



Askari Wahitimu wa Mafunzo Maalum ya Kikosi Maalum cha Jeshi la Magereza Kozi Namba 11 wakitoa maonesho mbalimbali ya Ukakamavu na ujasiri mbele ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe. Mwigulu Nchemba(Mb) alipofunga rasmi mafunzo ya kikosi hicho leo Januari 13, 2017 katika Viwanja vya Kikosi Maalum cha Kutuliza Ghasia Magerezani kilichopo Ukonga, Jijini Dar es Salaam.

Video kwa hisani ya Ayo TV

WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI MWIGULU NCHEMBA AFUNGA RASMI MAFUNZO YA KIKOSI MAALUM CHA MAGEREZA JIJINI DAR

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe. Mwigulu Nchemba(Mb)  akipokea Salaam ya heshima kutoka Gwaride Maalum la heshima lililoandaliwa na askari wahitimu wa Mafunzo Maalum ya Kikosi Maalum cha Jeshi la Magereza Kozi Namba 11. Hafla ya hiyo imefanyika leo Januari 13, 2017 katika Viwanja vya Kikosi Maalum cha Kutuliza Ghasia Magerezani kilichopo Ukonga, Jijini Dar es Salaam(kushoto) ni Kaimu Kamishna Jenerali wa Jeshi hilo Dkt. Juma Malewa.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe. Mwigulu Nchemba(Mb) akikagua Gwaride Maalum la heshima lililoandaliwa na Askari wahitimu wa Mafunzo Maalum ya Kikosi Maalum cha Jeshi la Magereza Kozi Namba 11 kama inavyoonekana katika picha.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe. Mwigulu Nchemba(Mb) akimtunuku cheti cha sifa Mmoja wa askari wahitimu wa Mafunzo Maalum ya Kikosi Maalum cha Jeshi la Magereza Kozi Namba 11 ambapo Mafunzo hayo yamefungwa rasmi leo Januari 13, 2017 katika Viwanja vya Kikosi Maalum cha Kutuliza Ghasia Magerezani kilichopo Ukonga, Jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe. Mwigulu Nchemba(Mb) akimvisha nembo ya kijani Mmoja wa askari wahitimu wa Mafunzo Maalum ya Kikosi Maalum cha Jeshi la Magereza Kozi Namba 11 kwa niaba ya wahitimu wenzake. Mafunzo hayo Maalum yamefungwa rasmi leo Januari 13, 2017 katika Viwanja vya Kikosi Maalum cha Kutuliza Ghasia Magerezani kilichopo Ukonga, Jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe. Mwigulu Nchemba(Mb) akitoa hotuba fupi kwa Wahitimu wa Mafunzo Maalum ya Kikosi Maalum cha Jeshi la Magereza Kozi Namba 11 kabla ya kuyafunga rasmi leo Januari 13, 2017.
Kaimu Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza nchini Dkt. Juma Malewa akitoa maelezo mafupi kabla ya kumkaribisha Mgeni rasmi kufunga Mafunzo hayo.
Askari Wahitimu wa Mafunzo hayo Maalum wakionesha umahiri wao wa kuvuka vikwazo mbalimbali kwa kutumia kamba kama inavyoonekana katika picha.
Onesho Maalum la Ukakamavu na ujasiri kama inavyoonekana katika picha Askari wa Kikosi Maalum akihimiri kipigo cha nyundo katika mwili wake kwa ujasiri wa hali ya juu.
Askari Wahitimu wa Mafunzo Maalum ya Kikosi Maalum cha Jeshi la Magereza Kozi Namba 11 wakiingia uwanjani kwa ajili ya kutoa maonesho mbalimbali ya Ukakamavu na ujasiri.
Wahitimu wa Mafunzo Maalum wakifuatilia kwa umakini hotuba ya Mgeni rasmi kama inavyoonekana katika picha

(Picha zote na Jeshi la Magereza).

Saturday, January 7, 2017

KAIMU KAMISHNA JENERALI WA MAGEREZA DKT JUMA MALEWA AFANYA MABADILIKO YA UONGOZI KWA MAAFISA WAANDAMIZI WA MAGEREZA

Kaimu Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza nchini, Dkt. Juma Ally Malewa(pichani) amefanya Mabadiliko ya Uongozi kwa baadhi ya Wakuu wa Magereza Mikoa na vituo mbalimbali hapa nchini.

Mabadiliko hayo ni pamoja na aliyekuwa Mkuu wa Magereza Mkoa wa Morogoro Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Magereza SACP Katos Rugainunura amehamishiwa Makao Makuu ya Magereza sehemu ya Utawala na nafasi yake inakaimiwa na Kamishna Msaidizi wa Magereza ACP Mzee Nyamka aliyekuwa Mkuu wa Utawala Magereza Mkoani Morogoro. Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Magereza SACP Antonino Kilumbi  aliyekuwa Mkuu wa Magereza Mkoa wa Dodoma amehamishwa kwenda Makao Makuu ya Magereza kuwa Mkuu wa Kikosi cha Ujenzi na nafasi yake inachukuliwa na Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Magereza SACP Julius Sang’udi aliyekuwa Mkuu wa Magereza Mkoa wa Mbeya.

Aliyekuwa Mkuu wa Magereza Mkoa wa Kilimanjaro Kamishna Msaidizi wa Magereza ACP Anderson Kamtiaro anaenda kuwa Afisa Mnadhimu Magereza Mkoani Arusha na nafasi yake inachukuliwa na Kamishna Msaidizi wa Magereza ACP Hassan Mkwiche ambaye alikuwa ni Mkuu wa Gereza Kuu Karanga, Moshi. Aliyekuwa Mkuu wa Gereza Same Kamishna Msaidizi wa Magereza ACP Evarist Katego anakwenda kuwa Mkuu wa Gereza Kuu Karanga, Moshi. Aliyekuwa Mkuu wa Magereza Mkoa wa Mwanza Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Magereza SACP Uwesu Ngarama amehamishiwa Makao Makuu kuwa Boharia Mkuu wa Jeshi na nafasi yake inachukuliwa na aliyekuwa Afisa Mipango wa Jeshi ACP Athuman Kitiku.  

Aidha,  aliyekuwa Mkuu wa Magereza Mkoani Mtwara,  Kamishna Msaidizi wa Magereza ACP Musa Kaswaka anakwenda Makao Makuu Kitengo cha Ukaguzi  na nafasi yake kuchukuliwa na Kamishna Msaidizi wa Magereza ACP Ismail Mlawa aliyekuwa Mkuu wa Kiwanda cha Samani Gereza Kuu Ukonga. Aliyekuwa Afisa Mdhibiti wa Fedha wa Jeshi Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Magereza SACP Gideon Nkana anakwenda kuwa Mkuu wa Chuo cha Taaluma ya Urekebishaji, Ukonga, Dar es Salaam na nafasi yake kuchukuliwa na Kamishna Msaidizi wa Magereza ACP Chacha Jakson.

Wengine ni pamoja na aliyekuwa Afisa Mnadhimu wa Magereza Mkoa wa Mbeya ACP Kijida Mwakingi anakaimu nafasi ya Mkuu wa Magereza Mkoa wa Mbeya, Kamishna Msaidizi wa Magereza ACP Abdalah Misanga anayetoka Gereza Mgumu kwenda kuwa Mkuu wa Gereza Msalato, Kamishna Msaidizi wa Magereza ACP  John Itambu anayetoka Gereza Kilosa kwenda kuwa Mkuu wa Kiwanda cha Samani Gereza Kuu Ukonga.

Kamishna Msaidizi wa Magereza ACP Erasmus Kundy anayetoka Chuo cha Taaluma ya Urekebishaji Ukonga kwenda Makao Makuu Kitengo cha Habari, Kamishna Msaidizi wa Magereza ACP Julius Ntambala aliyekuwa Mkuu wa Kitengo cha Ujenzi Makao Makuu anabakia Makao Makuu Kitengo cha ujenzi kuwa Msaidizi wa Mkuu wa Kitengo, Kamishna Msaidizi wa Magereza ACP Sylivester Mrema  anayetoka Gereza Idete kwenda Gereza Ubena kuwa Mkuu wa Gereza.

Aliyekuwa Mkuu wa Gereza Ubena Kamishna Msaidizi wa Magereza ACP Shaba Zephania anakwenda Magereza Mkoa wa Pwani kuwa Afisa Mnadhimu, Kamishna Msaidizi wa Magereza ACP Solomon Urio anayetoka Makao Makuu kwenda Magereza Mkoa wa Dar es Salaam kuwa Afisa Mnadhimu pamoja na aliyekuwa Boharia Mkuu wa Jeshi la Magereza Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Magereza SACP George Kiria amehamishiwa Makao Makuu Kitengo cha Uhasibu .

Mabadiliko hayo ni ya kawaida na yanalenga kuboresha utendaji kazi na ufanisi wa Jeshi la Magereza.

Imetolewa na:

Lucas Mboje - ASP
Ofisa Habari wa Jeshi la Magereza
Makao Makuu ya Magereza Tanzania Bara
07 Januari, 2017.

Wednesday, January 4, 2017

MASAUNI AFANYA ZIARA MAGEREZA, AAGIZA SARE ZOTE ZA JESHI LA ZIMAMOTO NA IDARA YA UHAMIAJI KUANZIA SASA ZISHONWE KIWANDA CHA MAGEREZA UKONGA, JIJINI DAR ESA SALAAM

Naibu Waziri wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni akikagua gwaride la heshima lililoandaliwa na maafisa na askari wa Jeshi la Magereza, Makao Makuu, jijini Dar es Salaam wakati kiongozi huyo alipofanya ziara ya kikazi katika Jeshi hilo leo. Masauni mara baada ya kumaliza ziara yake aliagiza Jeshi la Zimamoto na Uokoaji na Idara ya Uhamiaji nchini, kuanzia sasa sare zote za askari na maafisa wa Idara hizo zitashonwa katika Kiwanda cha Magereza, Ukonga, jijini Dar es Salaam. 
Naibu Waziri wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni akimpa maelekezo Mratibu wa Mradi wa Ujenzi wa Nyumba za Makazi ya Askari wa Jeshi la Magereza, Julius Chego (kulia), wakati kiongozi huyo alipofanya ziara katika eneo la Ujenzi wa nyumba hizo 320, Ukonga, jijini Dar es Salaam leo, ambazo Rais Dk. John Magufuli ametoa Shilingi Bilioni kumi kwa ajili ya ujenzi wa nyumba hizo. Katikati ni Kaimu Kamishna Jenerali wa Jeshi hilo, Dk Juma Malewa.
Naibu Waziri wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni (aliyevaa suti) akiiikagua moja ya nyumba za askari wa Jeshi la Magereza zinazojengwa Ukonga, jijini Dar es Salaam. Jumla ya nyumba 320 zinatarajiwa kujengwa katika eneo hilo mara baada ya Rais Dk John Magufuli kutoa shilingi Bilioni Kumi kwa ajili ya ujenzi wa nyumba hizo. Masauni alifanya ziara ya kikazi katika maeneo mbalimbali ya Jeshi hilo, na alitoa agizo kwa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji pamoja na Idara ya Uhamiaji, kuhakikisha kuwa, sare za idara hizo kuanzia sasa zitakuwa zinashonwa katika Kiwanda cha Magereza, Ukonga. Mbele kushoto ni Kaimu Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza nchini, Dk Juma Malewa.
Naibu Waziri wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni (katikati) akitoka katika Jengo la Useremala mara baada ya kukagua mashine mbalimbali zinazotumika kuranda na kuchana mbao kwa ajili ya utengenezaji wa samani katika Kiwanda cha Magereza Ukonga, jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Kaimu Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza nchini, Dk Juma Malewa, na kulia ni Mkuu wa Kiwanda hicho, Ismail Mlawa. 
Naibu Waziri wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni (kulia) akiviangalia viti vilivyotengenezwa na wafungwa katika Kiwanda cha Magereza Ukonga, jijini Dar es Salaam, huku Mkuu wa Kiwanda hicho, Ismail Mlawa akitoa maelezo ya utengenezaji wa viti hivyo. Masauni alifanya ziara katika kiwanda hicho na kujionea vitu mbalimbali vinavyotengenezwa na wafungwa kiwandani hapo.
Naibu Waziri wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni (aliyevaa suti) akikiangalia kitanda kilichotengenezwa na wafungwa katika Kiwanda cha Magereza Ukonga, jijini Dar es Salaam, huku Mkuu wa Kiwanda hicho, Ismail Mlawa (kushoto) akitoa maelezo ya utengenezaji wa kitanda hicho.
Naibu Waziri wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni akikiangalia kikapu kilichoshonwa na wafungwa katika Kiwanda cha Magereza Ukonga, jijini Dar es Salaam. Masauni alifanya ziara katika kiwanda hicho na kujionea vitu mbalimbali vinavyotengenezwa na wafungwa kiwandani hapo. Watatu kulia ni Kaimu Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza nchini, Dk Juma Malewa, kulia ni Mkuu wa Kiwanda hicho, Ismail Mlawa.  

Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.