Mojawapo ya Jukumu la Jeshi la Magereza ni kuwapeleka mahakamani mahabusu na kuwarudisha magerezani.

Gadi ya askari Wanawake na Wanaume wa Jeshi la Magereza katika Maadhimisho ya Sherehe za Kitaifa.

Ng'ombe bora wa Nyama na Maziwa ni sehemu ya miradi ya Uzalishaji inayoendeshwa na kusimamiwa na Jeshi la Magereza nchini.

Sehemu ya Mashamba makubwa yanayoendeshwa na Jeshi la Magereza: Shughuli za Kilimo cha Mashamba makubwa, madogo na bustani za mboga mboga ni moja ya shughuli za Magereza katika kuwafunza wafungwa namna ya kujitegemea mara wamalizapo vifungo vyao.

Baadhi wa wafungwa katika Kiwanda cha Ushonaji nguo cha Gereza Kuu Ukonga wakiwa kazini: Shughuli za Ushonaji wa nguo ni moja ya eneo ambalo wafungwa hupata huduma za urekebishwaji kwa vitendo.

Monday, January 29, 2018

JESHI LA MAGEREZA LASHIRIKI VYEMA MAADHIMISHO YA WIKI YA SHERIA NCHINI, JIJINI DAR

Naibu Kamishna wa Magereza Tusekile Mwaisabila(wa pili toka kushoto) akiwa na Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Magereza, Mussa Kaswaka(wa tatu toka kulia) pamoja na Maafisa wa Jeshi la Magereza  wakishiriki maandamando ya Maadhimisho ya wiki ya sheria. Maandamano hayo yalfanyika jana Januari 28, 2018 yakianzia katika Viwanja vya Mahakama ya Kisutu na kuishia katika Viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es salaam.
Baadhi ya askari wa Jeshi la Magereza wakishiriki katika maandamano hayo jana ambapo yaliongoozwa na Jaji Mkuu wa Tanzania Mhe. Profesa. Ibrahim Juma.
Baadhi ya Wananchi waliotembela Banda la Jeshi la Magereza wakipata ufafanuzi wa mambo mbalimbali kutoka kwa Maafisa Magereza kuhusiana na Uendeshaji wa Jeshi la Magereza kama inavyoonekana katika picha.

Mrakibu wa Magereza, Amina Kavirondo ambaye ni Mwanasheria kutoka Kitengo cha Sheria Makao Makuu ya Magereza akitoa ufafanuzi kwa kisheria kwa Mwananchi aliyetembelea katika Banda la Magereza katika Viwanja vya Mnazi Mmoja kwenye Maonesho ya wiki ya Sheria hapa nchini.
(Picha zote na Cpl. Mfaume wa  Jeshi la Magereza).

Sunday, January 28, 2018

KAMISHNA JENERALI WA MAGEREZA, DKT. JUMA MALEWA ATETA NA MAHABUSU GEREZA KEKO MAADHIMISHO YA WIKI YA SHERIA NCHINI

Kamishna Jenerali wa Magereza nchini Dkt. Juma Malewa akiwasili katika Gereza la Mahabusu Keko jijini Dar es salaam katika ziara yake ya kikazi kukagua gereza hilo leo Januari 28, 2018 ikiwa ni sehemu ya Maadhimisho ya Wiki ya Sheria hapa nchini. Jeshi la Magereza ni moja ya wadau muhimu katika sekta ya Sheria hapa nchini. 
Kamishna Jenerali wa Magereza nchini Dkt. Juma Malewa akisalimiana na Mkuu wa Gereza la Mahabusu Keko, Kamishna Msaidizi wa Magereza, Kiangi Abdallah alipowasili katika ziara yake ya kikazi kukagua gereza hilo ikiwa ni sehemu ya Maadhimisho ya Wiki ya Sheria hapa nchini. Wengine ni Maafisa Waandamizi wa Jeshi hilo.
Mkuu wa Gereza la Mahabusu Keko, Kamishna Msaidizi wa Magereza, Kiangi Abdallah akitoa taarifa fupi mbele ya Kamishna Jenerali wa Magereza nchini Dkt. Juma Malewa kabla ya kumkaribisha kuongea na Mahabusu wa Gereza Keko(hawapo pichani).
Kamishna Jenerali wa Magereza nchini Dkt. Juma Malewa akiongea na Mahabusu wa Gereza Keko(awapo pichani) leo Januari 28, 2018 alipotembelea gereza hilo ikiwa ni sehemu ya Maadhimisho ya Wiki ya Sheria hapa nchini
Kamishna Jenerali wa Magereza nchini Dkt. Juma Malewa akimsikiliza Mahabusu ambaye ni raia wa kigeni mara baada ya kuongea na Mahabusu wa Gereza Keko.
Kamishna Jenerali wa Magereza nchini Dkt. Juma Malewa akikagua jiko la gesi katika Gereza la Mahabusu Keko. Jeshi la Magereza tayari limeanza kutekeleza maelekezo ya Serikali ya kuachana na matumizi ya kuni kwa kutumia nishati ya gesi katika baadhi ya magereza nchini hivyo kutunza mazingira.
Maafisa Waandamizi wa Jeshi la Magereza wakiwa katika chumba Maalum, Gereza Keko ambapo chumba hicho kitatumika katika Uendeshaji wa Mashauli mbalimbali kwa kutumia njia ya TEHAMA. Uwepo wa mfumo huu utalipunguzia gharama Jeshi la Magereza katika kuwasafirisha Mahabusu mahakamani na kuwarejesha magerezani.
Kamishna Jenerali wa Magereza nchini, Dkt. Juma Malewa(katikati) akiwa katika Chumba Maalum ambacho kitatumika katika uendeshaji wa mashauli kwa kutumia njia ya  TEHAMA(wa kwanza kushoto) ni  Kaimu Mkuu wa Magereza Mkoa wa Dar es Salaam, Kamishna Msaidizi wa Magereza, Noel James(wa kwanza kulia) ni Mkuu wa Gereza Keko, Kamishna Msaidizi wa Magereza, Kiangi Abdallah 

(Picha zote na Lucas Mboje wa Jeshi la Magereza).

Monday, January 1, 2018

KAMISHNA JENERALI WA MAGEREZA, DKT. JUMA MALEWA ATETA NA VIONGOZI WA KIMILA JIJINI MBEYA

Kamishna Jenerali wa Magereza, Dkt. Juma Malewa akiagana na Kiongozi Mkuu wa kimila kabila la Wasafa lililopo Mkoani Mbeya, Rocket Mwashinga mara baada ya mazungumzo mafupi walipokutana katika viwanja vya Magereza Mkoani Mbeya, leo Desemba 31, 2017. Kamishna Jenerali wa Magereza nchini yupo Jijini Mbeya kwa ziara ya kikazi ya siku nne ambapo hadi jana amefanya ukaguzi katika Magereza ya Ruanda, Kyela, Tukuyu pamoja na Chuo cha Mafunzo ya Magereza, Kiwira kilichopo Wilaya ya Rungwe Mkoani Mbeya. 

Kamishna Jenerali wa Magereza, Dkt. Juma Malewa akiwa katika picha ya pamoja na Viongozi wa Kimila Mkoani Mbeya(kushoto) ni Kiongozi Mkuu wa kimila kabila la Wasafa lililopo Mkoani Mbeya, Rocket Mwashinga(kulia) ni Kiongozi wa Pili wa Wasafa Mkoani Mbeya, George Joto mara baada ya mazungumzo mafupi na Kamishna Jenerali wa Magereza walipokutana katika viwanja vya Magereza Mkoani Mbeya, leo Desemba 31, 2017

(Picha zote na Lucas Mboje wa Jeshi la Magereza).