Friday, July 10, 2020
KAMISHNA JENERALI WA JESHI LA MAGEREZA NCHINI MEJ.JEN. SULEIMAN MZEE,TAR. 09 JULAI 2020, AMEFUNGUA MAFUNZO YA UONGOZI NGAZI YA JUU YA JESHI LA MAGEREZA,KOZI NA.01 KATIKA CHUO CHA KPF KILICHOPO KINGOLWIRA , MOROGORO.
12:06 PM
Kamishna
Jenerali Suleima Mzee akiongea na wanafunzi wa Kozi ya Uongozi Ngazi ya Juu(
hawapo pichani), mara baada ya kuwasili katika Chuo cha KPF Morogoro
Baadhi
ya wanafunzi wa Kozi ya Uongozi Ngazi ya Juu wakimsikiliza Kamishna Jenerali
Suleiman Mzee (hayupo pichani)
Baadhi ya wakufunzi wa Kozi ya Uongozi Ngazi ya
Juu wakimsikiliza Kamishna Jenerali Suleiman Mzee (hayupo pichani)
Kamishna Jenerali Suleiman
Mzee( wa pili toka kulia) akiangalia mradi wa choo cha kisasa kinachojengwa
chuoni hapo. Wa pili toka kushoto ni Mkuu wa Chuo KPF, Kamishna Msaidizi wa
Magereza Lazaro Nyanga
Mkuu wa Chuo cha KPF, Kamishna Msaidizi wa
Magereza Lazaro Nyanga(kushoto) akimuonesha Kamishna Jenerali Suleiman Mzee
moja ya miradi inayoendelezwa chuoni hapo. ( picha na Jeshi la Magereza)
Sunday, July 5, 2020
MAKATIBU MUHTASI JESHI LA MAGEREZA WAPIGWA MSASA TAREHE 04, JULAI 2020
1:37 PM
Mgeni rasmi katika semina ya makatibu muhtasi wa jeshi
la magereza (waliokaa kushoto) kamishna wa utawala na rasmali watu
CP. Uwesu Hamidu Ngarama akiwa na wawezeshaji kutoka kikolo financial solution LTD,
maafisa waandamizi wa jeshi la Magereza pamoja na washiriki wa semina Ya makatibu muhtasi.
Muwezeshaji Akitoa Mada wakati wa semina ya Makatibu Muhtasi wa Jeshi la Magereza waliokaa ni washiriki katika semina hiyo.
Pichani ni Sgt Scolastica Ndunguru akifafanua jambo wakatyi wa semina ya makatibu Muhtasi wa Jeshi la Magereza.
Picha ya Pamoja kati ya Washiriki wa semina hiyo na wawezeshaji pamoja na Viongozi waanzamizi wa Jeshi la Magereza.
Msemaji wa Jeshi la Magereza Ssp Amina Kavirondo akitoa Mada katika Semina ya makatibu muhtasi wa Jeshi la Magereza kushoto kwake ni Viongozi waandamizi wa Jeshi la Magereza. picha na Jeshi la Magereza
Tuesday, June 23, 2020
MAFUNZO YA UHAMASISHAJI WA WAELIMISHAJI WA MTANDAO WA WANAWAKE KATIKA JESHI LA MAGEREZA NCHINI YAFUNGULIWA MKONI MOROGORO.
9:19 AM
Na
Shani Mhando, Morogoro
Kaimu
Mkurugenzi Idara ya Maendeleo ya Jinsia katika Wizara ya Afya,Maendeleo ya jamii,Wazee
na Watoto Bi.Mboni amefurahishwa kuanzishwa
kwa mtandao wa wanawake katika
jeshi a magereza nchini
akizungumza
katika ufunguzi wa mafunzo ya mtandao
huo, uliofanyika katika ukumbi wa Umwema Mkoani Morogoro,Bi Mboni amesema, hii
ni hatua nzuri sana yakupongezwa kwa Jeshi la Magereza kuhakikisha
wanawake katika Nyanja zote wanatumia
fursa mbalimbali zilizopo na zitakazojitokeza ndani ya Jeshi na Nje ya Jeshi
ili kujipatia mafanikio.
aliongeza
kuwa msingi wa kuwepo kwa mitandao ya wanawake ni nchini ni kuwawezesha na
kuwajengea uwezo wanawake katika Nyanja
za kiuchumi,mafunzo,ajira,uongozi na maamuzi ili kuweza kutimiza majukumu yao
bila kubaguliwa jinsia zao.
“Ni
matarajio yangu kuwa kuanzishwa kwa mtandao huu Jeshi la magereza litazingatia
miongozo na kanuni mbalimbali zilizotolewa na serikali kuhakikisha katika
maeneo yote yenye changamoto za usawa wa kijinsia mwanamke awezeshwe ili aweze
kukabilina nazo,”alisema Bi Monica
Aidha
Bi Mboni amewaasa washiriki wa mafunzo kuzingatia yote watakayofundishwa katika
mafunzo hayo ili wakawe wawakilishi wazuri kwa askari wote wa kike katika Jeshi
la Magereza ili kuwajengea uwezo,kukuza uelewa na kuwaunganisha waweze kufanya
kazi kw ufanisi zaidi.
“Jukumu
mlilopewa na Jeshi la Magereza la uelimshaji ni jukumu muhimu sana katika
ustawi wa mtandao wa wanawake ndani ya Jeshi la Magereza, ninahakika,mafunzo
mtakayoyapata yatawaongezea uwezo wa kutekeleza jukumu hili muhimu na kuleta
ufanisi katika utekelezaji wa majukumu ya mtando ndani Jeshi,”alisema Bi Mboni
kwa
upande wa Mkuu wa dawati la Jinsia Magereza Kamishna Msaidizi Mwandamizi Bertha
Joseph Minde amesema kuanzishwa kwa mtandao wa wanawake magereza kumewawezesha
wanawake Kushika nafasi za juu za
uongozi katika Jeshi kama kamishna mmoja,kamshna msaidizi mwandamizi mmoja na
makamishn wasaidizi 6 ingawa bado kuna upungufu mkubwa wa kinamama katika
nafasi za juu za uongozi.
naye
msemaji wa Jeshi la Magereza Mrakibu mwandamizi Amina kavirondo amemuomba
Mkurugenzi wa Idara ya Maendeleo Bi
Mboni kuwashika mkono mtandao wa wanawake
Magereza ili kuweza kufikia malengo waliyokusudia
Aidha
kamishna msaidizi mwandamizi wa mkoa wa morogoro (RPO) Ismail T.Mlawa aliwapongeza wanawake wa Jeshi
la Magereza kwa kuanzisha mtandao wa wanawake ambapo utawawezesha kupambania
haki zao
mtandao wa wanawake katika Jeshi la magereza
ulianzishwa rasmi tarehe7 Desemba,2018 baada ya mkutano wa SADC uliofanyika
Dec.2011 nchini Birchhood Johanesburg Africa ya Kusini ambapo katika kikao hicho
wazo la mtandao wa wanawake lilirasimishwa na kuwekewa mikakati(the idea of
women network consolidation and road map drawn)
Monday, June 1, 2020
KAMISHNA JENERALI WA MAGEREZA SULEIMAN MZEE AKABIDHI MALORI MATATU KATIKA SHIRIKA LA UZALISHAJI MALI LA MAGEREZA(SHIMA), LEO JIJINI DODOMA
6:00 PM
Kamishna Jenerali wa
Magereza, Suleiman Mzee(Kushoto) akikabidhi funguo za malori mapya kwa Mtendaji
Mkuu wa Shirika la Uzalishaji Mali la Magereza, SACP. Chacha Bina leo Juni 1,
2020 katika Viwanja vya Makao Makuu ya Jeshi la Magereza, jijini Dodoma.
Kamishna Jenerali wa
Magereza, Suleiman Mzee akijaribu kuliwasha moja ya lori kabla ya kukabidhi malori mapya matatu kwa Mtendaji
Mkuu wa Shirika la Uzalishaji Mali la Magereza, SACP. Chacha Bina(hayupo
pichani) leo Juni 1, 2020 katika Viwanja vya Makao Makuu ya Jeshi la Magereza,
jijini Dodoma.
Muonekano wa malori mapya matatu yaliyokabidhiwa kwa ajili ya shughuli
za Kikosi ujenzi cha Shirika la Uzalishaji Mali la Magereza, leo Juni 1, 2020
katika Viwanja vya Makao Makuu ya Jeshi la Magereza, jijini Dodoma.
Kamishna Jenerali wa
Magereza, Suleiman Mzee(wa pili toka kulia) akifanya mahojiano mafupi na wanahabari mara baada ya makabidhiano ya
malori ya Shirika la Uzalishaji mali la Magereza leo Juni 1, 2020 katika Viwanja vya Makao Makuu
ya Jeshi la Magereza, jijini Dodoma (Picha
zote na Jeshi la Magereza).
Tuesday, May 19, 2020
KAMISHNA JENERALI WA MAGEREZA AKUTANA NA MAAFISA WAANDAMIZI WA MAGEREZA WALIOHAMISHIWA MAKAO MAKUU YA JESHI HILO DODOMA HIVI KARIBUNI
3:22 PM
Kamishna Jenerali wa Magereza,
Suleiman Mzee akizungumza katika kikao kazi na Maafisa Waandamizi wa Jeshi la
Magereza ambao wamehamishiwa hivi karibuni Makao Makuu ya Jeshi la Magereza,
jijini Dodoma. Kikao hicho kimefanyika leo Mei 19, 2020 kwa lengo la kupeana
mikakati mbalimbali ya kazi sambamba na maelekezo ya utekelezaji wa mageuzi
yanaendelea ndani ya Jeshi hilo.
Baadhi ya Maafisa Waandamizi wa
Jeshi la Magereza wakifuatilia kwa makini maelekezo kutoka kwa Kamishna Jenerali
wa Magereza, Suleiman Mzee(hayupo pichani)katika kikao kazi kilichofanyika leo Mei
19, 2020 Makao Makuu ya Jeshi la Magereza, Jijini Dodoma.
Kamishna Jenerali wa Magereza, Suleiman Mzee(meza kuu) akiwa na Kamishna
wa Utawala na Rasilimali watu wa Jeshi la Magereza, Uwesu Ngarama(kulia) pamoja
na Mnadhimu Mkuu wa Jeshi la Magereza, SACP. Mzee Nyamka(kushoto) wakifuatilia
kikao kazi cha Maafisa Waandamizi wa Jeshi hilo kilichofanyika leo Mei 19, 2020,
Jijini Dodoma.
Mkuu wa Kitengo cha Rasilimali
watu katika Jeshi la Magereza, SACP. Boyd Mwambingu akiteta jambo na Kamishna
Jenerali wa Magereza, Suleiman Mzee mara baada ya kikao kazi na Maafisa
Waandamizi wa Jeshi la Magereza ambao wamehamishiwa hivi karibuni Makao Makuu
ya Jeshi la Magereza, jijini Dodoma(Picha zote na Jeshi la Magereza).
Thursday, May 14, 2020
SERIKALI YARIDHISHWA NA UTENDAJI KAZI BODI ZA PAROLE NCHINI
4:07 PM
Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya nchi, Mhe.
Hamad Masauni(Mb) akitoa hotuba katika hafla fupi ya uzinduzi wa Bodi ya Taifa
Parole Taifa, leo Mei 14, 2020 katika Ukumbi wa Chuo cha Mipango, jijini
Dodoma.
Kamishna Jenerali wa
Magereza nchini, Suleiman Mzee ambaye pia ni Katibu wa Bodi ya Taifa Parole
akitoa maelezo mafupi kuhusiana na utendaji kazi wa Bodi za Parole nchini tangu
kuanzishwa kwake mwaka 1994. Leo Mei 14, 2020 katika hafla fupi ya uzinduzi wa
Bodi ya Taifa Parole Taifa, katika Ukumbi wa Chuo cha Mipango, jijini Dodoma.
Baadhi ya Maafisa Waandamizi wa Jeshi la
Magereza wakifuatilia uzinduzi wa Bodi ya Taifa Parole leo Mei 14, 2020 jijini
Dodoma.
Mwenyekiti wa Parole Taifa, Mhe. Dkt.
Augustino Mrema akisoma taarifa fupi kabla ya kumkaribisha mgeni rasmi azindue
Bodi ya Taifa Parole leo Mei 14, 2020 jijini Dodoma.
Mjumbe wa Bodi ya Taifa Parole, Mchungaji wa
Kanisa la KKKT Dodoma, Marco Kinyau
akijitambulisha mbele ya Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya nchi, Mhe. Hamad
Masauni(Mb) kabla ya uzinduzi wa Bodi ya Taifa Parole leo Mei 14, 2020 jijini
Dodoma. Kulia kwake ni baadhi ya wajumbe wa bodi hiyo.
Meza kuu wakifuatilia utambulisho wa wajumbe
wapya wa Bodi ya Taifa Parole. Katikati ni Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya
nchi, Mhe. Hamad Masauni(kulia) ni Kamishna Jenerali wa Magereza nchini,
Suleiman Mzee(kushoto) ni Mwenyekiti wa Parole Taifa, Mhe. Augustino Mrema.
Naibu Waziri wa Mambo ya
Ndani ya nchi, Mhe. Hamad Masauni(meza kuu katikati aliyeketi) akiwa katika
picha ya pamoja na wajumbe wa Bodi ya Taifa Parole(waliosimama). Wa pili toka
kulia aliyeketi meza kuu ni Kamishna Jenerali wa Magereza nchini, Suleiman
Mzee (Wa pili toka kushoto aliyeketi meza kuu) ni Mwenyekiti wa Parole Taifa,
Mhe. Augustino Mrema.
(Picha zote na Jeshi la Magereza).
Friday, May 8, 2020
WAZIRI MAVUNDE AMWAGA MISAADA YA VIFAA VYA KUJIKINGA NA CORANA GEREZA KUU ISANGA, DODOMA
5:44 PM
Kamishna
Jenerali wa Magereza, Suleiman Mzee(kushoto) akisalimiana na Naibu Waziri, Ofisi
ya Waziri Mkuu
anayeshughulia Kazi, Vijana na Ajira Mhe. Anthony Mavunde (Mb) leo Mei
8, 2020 alipofika Makao Makuu ya Jeshi la Magereza jijini Dodoma kabla ya
kukabidhi vifaa vya kujikinga na janga la corona katika Gereza Kuu Isanga
Dodoma.
Kamishna
Jenerali wa Magereza, Suleiman Mzee (kushoto meza kuu) akizungumza jambo na Naibu Waziri, Ofisi
ya Waziri Mkuu
anayeshughulia Kazi, Vijana na Ajira Mhe. Anthony Mavunde (kulia) leo
Mei 8, 2020 alipofika Makao Makuu ya Jeshi la Magereza jijini Dodoma kabla ya
kukabidhi vifaa vya kujikinga na janga la corona katika Gereza Kuu Isanga.
Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulia Kazi, Vijana na Ajira Mhe.
Anthony Mavunde
akizungumza nje ya Gereza akikabidhi vifaa vya kujikinga na janga la corona
katika Gereza Kuu Isanga, jijini Dodoma. Mhe. Mavunde amekabidhi msaada uliojumuisha vifaa mbalimbali ikiwemo sabuni,
ndoo za maji pamoja na vitakasa mikono (Sanitizer).
Baadhi ya vifaa hivyo vilivyokabidhiwa katika Gereza
Kuu Isanga na Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulia Kazi, Vijana na Ajira Mhe.
Anthony Mavunde.
Mkuu wa Magereza Mkoani Dodoma, ACP. Keneth Mwambije
akimshukru Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulia Kazi, Vijana na Ajira Mhe.
Anthony Mavunde (kushoto) baada ya
kupokea msaada wa vifaa vya kujikinga na janga la corona.
Kamishna Jenerali wa Magereza,
Suleiman Mzee( wapili kushoto) akiagana na Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulia Kazi, Vijana na Ajira Mhe. Anthony Mavunde
mara baada ya mazungumzo katika Ofisi za Makao Makuu ya Jeshi la Magereza,
jijini Dodoma. (Picha zote na Jeshi
la Magereza).
Monday, May 4, 2020
KAMISHNA JENERALI WA MAGEREZA, SULEIMAN MZEE AWAFUNDA WAKUU WA MAGEREZA ALIOWATEUA HIVI KARIBUNI KUHAKIKISHA WANASIMAMIA AGENDA YA MABADILIKO NDANI YA JESHI LA MAGEREZA
5:28 PM
Kamishna Jenerali wa Magereza Suleiman Mzee akitoa maelekezo maalum leo
Mei 04, 2020 katika kikao kazi cha Maafisa wa Jeshi la Magereza walioteuliwa hivi karibuni kushika nyadhifa mbalimbali katika Jeshi hilo wakiwemo wakuu wa magereza,
Boharia Mkuu wa Jeshi ambapo Jenerali Mzee amewataka kuhakikisha kuwa wanasimamia ipasavyo
Agenda ya mabadiliko ndani ya Jeshi la Magereza.
Kamishna Jenerali wa Magereza,
Suleiman Mzee akiwa meza kuu pamoja na Viongozi Waandamizi wa Jeshi hilo akiwemo Kamishna wa Magereza anayeshughulika na Utawala na Rasilimali watu,
Uwesu Ngarama (kulia). Kushotoni Kamishna wa Magereza anayesimamia Divisheni ya Urekebu,
Mhandisi Tusekile Mwaisabila leo Mei 04, 2020 wakifuatilia kikao kazi cha
Maafisa wa Jeshi la
Magereza walioteuliwa hivi karibuni kushika nyadhifa mbalimbali katika Jeshi hilo wakiwemo wakuu wa magereza pamoja na Boharia Mkuu wa Jeshi hilo.
Baadhi ya Maafisa walioteuliwa kushika nyadhifa malimbali katika Jeshi
la Magereza wakiwemo wakuu wa magereza wakifuatilia kikao kazi cha maelekezo ambacho kilikuwa chini ya Uenyekiti wa Kamishna Jenerali wa Magereza, leo Mei 04,
2020 jijini Dodoma .Jenerali Mzee amewataka kuhakikisha kuwa wanasimamia ipasavyo Agenda yamabadiliko ndani ya Jeshi hilo.
Kamishna Jenerali wa Magereza,
Suleiman Mzee leo Mei 04, 2020 akizungumza na baadhi ya Maafisa wa Jeshi la
Magereza walioteuliwa hivi karibuni kushika nyadhifa mbalimbali katika Jeshi hilo wakiwemo wakuu wa magereza ,
Boharia Mkuu wa Jeshi ambapo Jenerali Mzee amewataka kuhakikisha kuwa wanasimamia ipasavyo
Agenda ya mabadiliko ndani ya Jeshi la Magereza.
Kamishna Jenerali wa Magereza,
Suleiman Mzee akizungumza na Maafisa kutoka Vyuo vya Mafunzo Zanzibar (kulia) ambao wametembelea Makao Makuu ya Jeshi
la Magereza Tanzania Bara, leo Mei 04, 2020 jijini Dodoma. (Picha zote na Jeshi la Magereza).
Thursday, March 19, 2020
Tuesday, March 17, 2020
KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE MAMBO YA NJE, ULINZI NA USALAMA (NUU) YAFANYA ZIARA YA KUTEMBELEA MRADI WA UJENZI WA KIWANDA CHA USEREMALA GEREZA MSALATO ILI KUONA HALI YA UTEKELEZAJI WA MRADI HUO LEO TAREHE 17 MACHI 2020
11:07 PM
Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi ndugu
Christopher D. Kadio(wannetokakushoto)
akimkaribisha Mkuu wa Msafara wa Kamati ya Kudumu ya Bunge Mambo ya Nje,
Ulinzi na Usalama,ambaye ni Mbungewa Zanzibar Jimbo la Uzini ndugu Salum Rehani (wannetokakulia) walipowasili eneo
la Mradi, Msalato. WatatutokakushotoniK amishna Jenerali wa Magereza Seleman Mzee.
Katibu Mkuu Wizara Ya Mambo ya Ndani ya Nchi ndugu
Christopher D. Kadio akizungumza machache kabla ya kumkaribisha Mkuu wa Msafara kuzungumza na viongozi wa Jeshi
la Magereza pamoja na Mafundi wa mradi
Mkadiriaji Mkuu wa Ujenzi Makao Makuu ya Magereza Kamishna Msaidizi Aron Lunyungu akitoa maelezo ya ramani ya mradi kwa Mkuu wa Msafara wa Kamati ya Kudumu ya
Bunge Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama,ambaye ni Mbunge wa Zanzibar Jimbo la
Uzini ndugu Salum Rehani.
Msimamizi Mkuu wa Mradi wa ujenzi wa Kiwanda cha
Useremala Gereza Msalato Mrakibu Mkandarasi Bonanza Malata akitoa maelezo kwa Kamati ya Kudumu ya
Bunge Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama( Picha zote na Jeshi la Magereza)
Friday, February 28, 2020
WAZIRI SIMBACHAWENE AWATAKA POLISI KUACHA KUZALISHA MAHABUSU MAGEREZANI
4:09 PM
Waziri
wa Mambo ya Ndani ya Nchi, George Simbachawene akitoa maelekezo kwa Kamishna
Jenerali wa Magereza nchini, Suleman Mzee(kulia) leo alipotembelea Makao Makuu
ya Jeshi la Magereza, jijini Dodoma ikiwa ni ziara yake ya kwanza tangu
ateuliwe katika Wizara hiyo.
Waziri
wa Mambo ya Ndani ya Nchi, George Simbachawene akizungumza na Maafisa na askari
wa Jeshi la Magereza(hawapo pichani)leo alipotembelea Makao Makuu ya Jeshi la
Magereza, jijini Dodoma ikiwa ni ziara yake ya kwanza tangu ateuliwe katika
Wizara hiyo. Kushoto ni Kamishna Jenerali wa Magereza nchini, Suleman Mzee(
Kulia )ni Kamishna wa Utawala na Rasilimali watu, Uwesu Ngarama.
Kamishna
Jenerali wa Magereza nchini, Suleiman Mzee akitoa taarifa fupi mbele ya Waziri
wa Mambo ya Ndani ya Nchi, George Simbachawene(meza kuu katikati) kabla ya
kuongea na Maafisa na askari wa Jeshin hilo. Kulia ni Kamishna wa Utawala na
Rasilimali watu, Uwesu Ngarama.
Baadhi
ya Maafisa na askari wa Jeshi la Magereza Mkoani Dodoma wakimsikiliza Waziri wa
Mambo ya ndani ya Nchi, George Simbachawene (hayupo pichani).
Waziri
wa Mambo ya Ndani ya Nchi, George Simbachawene(kulia) akitoa maelekezo kwa
Kamishna Jenerali wa Magereza nchini, Suleman Mzee(wa pili toka kushoto) leo
alipotembelea Makao Makuu ya Jeshi la Magereza, jijini Dodoma ikiwa ni ziara
yake ya kwanza tangu ateuliwe katika Wizara hiyo.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, George
Simbachawene(Kaunda suti) akiingia Gereza Kuu la Isanga, jijini Dodoma, leo,
tayari kwa kuzungumza na Wafungwa na Mahabusu waliopo katika Gereza hilo.
Wednesday, February 19, 2020
JESHI LA MAGEREZA KUJITEGEMEA KWA KUTUMIA RASILIMALI ZAKE
5:19 PM
Kamishna Jenerali wa Magereza,
Suleiman Mzee akiongoza Kikao kazi cha siku moja cha Maafisa Waandamizi wa
Jeshi la Magereza, Kikao hicho
kimefanyika leo Februari 19, 2020 katika
Ukumbi wa Chuo cha Mipango, Jijini Dodoma.
Baadhi ya Wakuu wa Magereza Mikoa pamoja na Maafisa Waandamizi wa Jeshi
la Magereza wakifuatilia kwa makini maelekezo kutoka kwa Kamishna Jenerali wa
Magereza, Suleiman Mzee(hayupo pichani)katika Kikao kazi kilichofanyika leo
katika Ukumbi wa Chuo cha Mipango, Jijini Dodoma.
Kamishna wa Utawala na Rasilimali
watu wa Jeshi la Magereza, Uwesu Ngarama akitoa taarifa fupi katika Kikao kazi
cha Maafisa Waandamizi wa Jeshi hilo kilichofanyika katika Ukumbi wa Chuo cha
Mipango, Jijini Dodoma.
Wajumbe wa Sekretarieti wakifuatilia kikao kazi hicho kilichoongozwa na
Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza leo Februari 19, 2020 katika Ukumbi Chuo
cha Mipango, jijini Dodoma (Picha zote na Jeshi la Magereza).