Mojawapo ya Jukumu la Jeshi la Magereza ni kuwapeleka mahakamani mahabusu na kuwarudisha magerezani.

Gadi ya askari Wanawake na Wanaume wa Jeshi la Magereza katika Maadhimisho ya Sherehe za Kitaifa.

Ng'ombe bora wa Nyama na Maziwa ni sehemu ya miradi ya Uzalishaji inayoendeshwa na kusimamiwa na Jeshi la Magereza nchini.

Sehemu ya Mashamba makubwa yanayoendeshwa na Jeshi la Magereza: Shughuli za Kilimo cha Mashamba makubwa, madogo na bustani za mboga mboga ni moja ya shughuli za Magereza katika kuwafunza wafungwa namna ya kujitegemea mara wamalizapo vifungo vyao.

Baadhi wa wafungwa katika Kiwanda cha Ushonaji nguo cha Gereza Kuu Ukonga wakiwa kazini: Shughuli za Ushonaji wa nguo ni moja ya eneo ambalo wafungwa hupata huduma za urekebishwaji kwa vitendo.

Friday, July 10, 2020

KAMISHNA JENERALI WA JESHI LA MAGEREZA NCHINI MEJ.JEN. SULEIMAN MZEE,TAR. 09 JULAI 2020, AMEFUNGUA MAFUNZO YA UONGOZI NGAZI YA JUU YA JESHI LA MAGEREZA,KOZI NA.01 KATIKA CHUO CHA KPF KILICHOPO KINGOLWIRA , MOROGORO.

    Kamishna Jenerali Suleima Mzee akiongea na wanafunzi wa Kozi ya Uongozi Ngazi ya Juu( hawapo pichani), mara baada ya kuwasili katika Chuo cha KPF Morogoro

Baadhi ya wanafunzi wa Kozi ya Uongozi Ngazi ya Juu wakimsikiliza Kamishna Jenerali Suleiman Mzee (hayupo pichani)

Baadhi ya wakufunzi wa Kozi ya Uongozi Ngazi ya Juu wakimsikiliza Kamishna Jenerali Suleiman Mzee (hayupo pichani)

Kamishna Jenerali Suleiman Mzee( wa pili toka kulia) akiangalia mradi wa choo cha kisasa kinachojengwa chuoni hapo. Wa pili toka kushoto ni Mkuu wa Chuo KPF, Kamishna Msaidizi wa Magereza Lazaro Nyanga

Mkuu wa Chuo cha KPF, Kamishna Msaidizi wa Magereza Lazaro Nyanga(kushoto) akimuonesha Kamishna Jenerali Suleiman Mzee moja ya miradi inayoendelezwa chuoni hapo. ( picha na Jeshi la Magereza)

Sunday, July 5, 2020

MAKATIBU MUHTASI JESHI LA MAGEREZA WAPIGWA MSASA TAREHE 04, JULAI 2020

Mgeni rasmi katika semina ya makatibu muhtasi wa jeshi la magereza (waliokaa kushoto) kamishna wa utawala na rasmali watu CP. Uwesu Hamidu Ngarama akiwa na wawezeshaji kutoka kikolo financial solution LTD, maafisa waandamizi wa jeshi la Magereza pamoja na washiriki wa semina Ya makatibu muhtasi.

Muwezeshaji Akitoa Mada wakati wa semina ya Makatibu Muhtasi wa Jeshi la Magereza waliokaa ni washiriki katika semina hiyo.


Pichani ni Sgt Scolastica Ndunguru akifafanua jambo wakatyi wa semina ya makatibu Muhtasi wa Jeshi la Magereza.

Picha ya Pamoja kati ya Washiriki wa semina hiyo na wawezeshaji pamoja na Viongozi waanzamizi wa Jeshi la Magereza.

Msemaji wa Jeshi la Magereza Ssp Amina Kavirondo akitoa Mada katika Semina ya makatibu muhtasi wa Jeshi la Magereza kushoto kwake ni Viongozi waandamizi wa Jeshi la Magereza. picha na Jeshi la Magereza


Tuesday, June 23, 2020

MAFUNZO YA UHAMASISHAJI WA WAELIMISHAJI WA MTANDAO WA WANAWAKE KATIKA JESHI LA MAGEREZA NCHINI YAFUNGULIWA MKONI MOROGORO.



Na Shani Mhando, Morogoro

Kaimu Mkurugenzi Idara ya Maendeleo ya Jinsia katika Wizara ya Afya,Maendeleo ya jamii,Wazee na Watoto Bi.Mboni amefurahishwa kuanzishwa   kwa mtandao wa wanawake katika jeshi a magereza nchini
akizungumza katika ufunguzi wa mafunzo ya  mtandao huo, uliofanyika katika ukumbi wa Umwema Mkoani Morogoro,Bi Mboni amesema, hii ni hatua nzuri sana yakupongezwa kwa Jeshi la Magereza kuhakikisha wanawake  katika Nyanja zote wanatumia fursa mbalimbali zilizopo na zitakazojitokeza ndani ya Jeshi na Nje ya Jeshi ili kujipatia mafanikio.
aliongeza kuwa msingi wa kuwepo kwa mitandao ya wanawake ni nchini ni kuwawezesha na kuwajengea uwezo  wanawake katika Nyanja za kiuchumi,mafunzo,ajira,uongozi na maamuzi ili kuweza kutimiza majukumu yao bila kubaguliwa jinsia zao.
“Ni matarajio yangu kuwa kuanzishwa kwa mtandao huu Jeshi la magereza litazingatia miongozo na kanuni mbalimbali zilizotolewa na serikali kuhakikisha katika maeneo yote yenye changamoto za usawa wa kijinsia mwanamke awezeshwe ili aweze kukabilina nazo,”alisema Bi Monica
Aidha Bi Mboni amewaasa washiriki wa mafunzo kuzingatia yote watakayofundishwa katika mafunzo hayo ili wakawe wawakilishi wazuri kwa askari wote wa kike katika Jeshi la Magereza ili kuwajengea uwezo,kukuza uelewa na kuwaunganisha waweze kufanya kazi kw ufanisi zaidi.
“Jukumu mlilopewa na Jeshi la Magereza la uelimshaji ni jukumu muhimu sana katika ustawi wa mtandao wa wanawake ndani ya Jeshi la Magereza, ninahakika,mafunzo mtakayoyapata yatawaongezea uwezo wa kutekeleza jukumu hili muhimu na kuleta ufanisi katika utekelezaji wa majukumu ya mtando ndani Jeshi,”alisema Bi Mboni
kwa upande wa Mkuu wa dawati la Jinsia Magereza Kamishna Msaidizi Mwandamizi Bertha Joseph Minde amesema kuanzishwa kwa mtandao wa wanawake magereza kumewawezesha wanawake  Kushika nafasi za juu za uongozi katika Jeshi kama kamishna mmoja,kamshna msaidizi mwandamizi mmoja na makamishn wasaidizi 6 ingawa bado kuna upungufu mkubwa wa kinamama katika nafasi za juu za uongozi.
naye msemaji wa Jeshi la Magereza Mrakibu mwandamizi Amina kavirondo amemuomba Mkurugenzi wa Idara ya Maendeleo Bi  Mboni  kuwashika mkono mtandao wa wanawake Magereza ili kuweza kufikia malengo waliyokusudia
Aidha kamishna msaidizi mwandamizi wa mkoa wa morogoro (RPO)  Ismail T.Mlawa aliwapongeza wanawake wa Jeshi la Magereza kwa kuanzisha mtandao wa wanawake ambapo utawawezesha kupambania haki zao
 mtandao wa wanawake katika Jeshi la magereza ulianzishwa rasmi tarehe7 Desemba,2018 baada ya mkutano wa SADC uliofanyika Dec.2011 nchini Birchhood Johanesburg Africa ya Kusini ambapo katika kikao hicho wazo la mtandao wa wanawake lilirasimishwa na kuwekewa mikakati(the idea of women network consolidation and road map drawn)


Monday, June 1, 2020

KAMISHNA JENERALI WA MAGEREZA SULEIMAN MZEE AKABIDHI MALORI MATATU KATIKA SHIRIKA LA UZALISHAJI MALI LA MAGEREZA(SHIMA), LEO JIJINI DODOMA

Kamishna Jenerali wa Magereza, Suleiman Mzee(Kushoto) akikabidhi funguo za malori mapya kwa Mtendaji Mkuu wa Shirika la Uzalishaji Mali la Magereza, SACP. Chacha Bina leo Juni 1, 2020 katika Viwanja vya Makao Makuu ya Jeshi la Magereza, jijini Dodoma.

Kamishna Jenerali wa Magereza, Suleiman Mzee akijaribu kuliwasha moja ya lori kabla ya kukabidhi malori mapya matatu kwa Mtendaji Mkuu wa Shirika la Uzalishaji Mali la Magereza, SACP. Chacha Bina(hayupo pichani) leo Juni 1, 2020 katika Viwanja vya Makao Makuu ya Jeshi la Magereza, jijini Dodoma.

Muonekano wa malori mapya matatu yaliyokabidhiwa kwa ajili ya shughuli za Kikosi ujenzi cha Shirika la Uzalishaji Mali la Magereza, leo Juni 1, 2020 katika Viwanja vya Makao Makuu ya Jeshi la Magereza, jijini Dodoma.

Kamishna Jenerali wa Magereza, Suleiman Mzee(wa pili toka kulia) akifanya mahojiano mafupi  na wanahabari mara baada ya makabidhiano ya malori ya Shirika la Uzalishaji mali la Magereza leo Juni 1, 2020 katika Viwanja vya Makao Makuu ya Jeshi la Magereza, jijini Dodoma                            (Picha zote na Jeshi la Magereza).

Tuesday, May 19, 2020

KAMISHNA JENERALI WA MAGEREZA AKUTANA NA MAAFISA WAANDAMIZI WA MAGEREZA WALIOHAMISHIWA MAKAO MAKUU YA JESHI HILO DODOMA HIVI KARIBUNI

Kamishna Jenerali wa Magereza, Suleiman Mzee akizungumza katika kikao kazi na Maafisa Waandamizi wa Jeshi la Magereza ambao wamehamishiwa hivi karibuni Makao Makuu ya Jeshi la Magereza, jijini Dodoma. Kikao hicho kimefanyika leo Mei 19, 2020 kwa lengo la kupeana mikakati mbalimbali ya kazi sambamba na maelekezo ya utekelezaji wa mageuzi yanaendelea ndani ya Jeshi hilo.

Baadhi ya Maafisa Waandamizi wa Jeshi la Magereza wakifuatilia kwa makini maelekezo kutoka kwa Kamishna Jenerali wa Magereza, Suleiman Mzee(hayupo pichani)katika kikao kazi kilichofanyika leo Mei 19, 2020 Makao Makuu ya Jeshi la Magereza, Jijini Dodoma.

Kamishna Jenerali wa Magereza, Suleiman Mzee(meza kuu) akiwa na Kamishna wa Utawala na Rasilimali watu wa Jeshi la Magereza, Uwesu Ngarama(kulia) pamoja na Mnadhimu Mkuu wa Jeshi la Magereza, SACP. Mzee Nyamka(kushoto) wakifuatilia kikao kazi cha Maafisa Waandamizi wa Jeshi hilo kilichofanyika leo Mei 19, 2020, Jijini Dodoma.

Mkuu wa Kitengo cha Rasilimali watu katika Jeshi la Magereza, SACP. Boyd Mwambingu akiteta jambo na Kamishna Jenerali wa Magereza, Suleiman Mzee mara baada ya kikao kazi na Maafisa Waandamizi wa Jeshi la Magereza ambao wamehamishiwa hivi karibuni Makao Makuu ya Jeshi la Magereza, jijini Dodoma(Picha zote na Jeshi la Magereza).

Thursday, May 14, 2020

SERIKALI YARIDHISHWA NA UTENDAJI KAZI BODI ZA PAROLE NCHINI

Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya nchi, Mhe. Hamad Masauni(Mb) akitoa hotuba katika hafla fupi ya uzinduzi wa Bodi ya Taifa Parole Taifa, leo Mei 14, 2020 katika Ukumbi wa Chuo cha Mipango, jijini Dodoma.

Kamishna Jenerali wa Magereza nchini, Suleiman Mzee ambaye pia ni Katibu wa Bodi ya Taifa Parole akitoa maelezo mafupi kuhusiana na utendaji kazi wa Bodi za Parole nchini tangu kuanzishwa kwake mwaka 1994. Leo Mei 14, 2020 katika hafla fupi ya uzinduzi wa Bodi ya Taifa Parole Taifa, katika Ukumbi wa Chuo cha Mipango, jijini Dodoma.

Baadhi ya Maafisa Waandamizi wa Jeshi la Magereza wakifuatilia uzinduzi wa Bodi ya Taifa Parole leo Mei 14, 2020 jijini Dodoma.

Mwenyekiti wa Parole Taifa, Mhe. Dkt. Augustino Mrema akisoma taarifa fupi kabla ya kumkaribisha mgeni rasmi azindue Bodi ya Taifa Parole leo Mei 14, 2020 jijini Dodoma.

Mjumbe wa Bodi ya Taifa Parole, Mchungaji wa Kanisa la KKKT  Dodoma, Marco Kinyau akijitambulisha mbele ya Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya nchi, Mhe. Hamad Masauni(Mb) kabla ya uzinduzi wa Bodi ya Taifa Parole leo Mei 14, 2020 jijini Dodoma. Kulia kwake ni baadhi ya wajumbe wa bodi hiyo.

Meza kuu wakifuatilia utambulisho wa wajumbe wapya wa Bodi ya Taifa Parole. Katikati ni Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya nchi, Mhe. Hamad Masauni(kulia) ni Kamishna Jenerali wa Magereza nchini, Suleiman Mzee(kushoto) ni Mwenyekiti wa Parole Taifa, Mhe. Augustino Mrema.

Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya nchi, Mhe. Hamad Masauni(meza kuu katikati aliyeketi) akiwa katika picha ya pamoja na wajumbe wa Bodi ya Taifa Parole(waliosimama). Wa pili toka kulia aliyeketi meza kuu ni Kamishna Jenerali wa Magereza nchini, Suleiman Mzee (Wa pili toka kushoto aliyeketi meza kuu) ni Mwenyekiti wa Parole Taifa, Mhe. Augustino Mrema.
 (Picha zote na Jeshi la Magereza).

Friday, May 8, 2020

WAZIRI MAVUNDE AMWAGA MISAADA YA VIFAA VYA KUJIKINGA NA CORANA GEREZA KUU ISANGA, DODOMA

Kamishna Jenerali wa Magereza, Suleiman Mzee(kushoto) akisalimiana na Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulia Kazi, Vijana na Ajira Mhe. Anthony Mavunde (Mb) leo Mei 8, 2020 alipofika Makao Makuu ya Jeshi la Magereza jijini Dodoma kabla ya kukabidhi vifaa vya kujikinga na janga la corona katika Gereza Kuu Isanga Dodoma.

Kamishna Jenerali wa Magereza, Suleiman Mzee (kushoto meza kuu) akizungumza jambo na Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulia Kazi, Vijana na Ajira Mhe. Anthony Mavunde (kulia) leo Mei 8, 2020 alipofika Makao Makuu ya Jeshi la Magereza jijini Dodoma kabla ya kukabidhi vifaa vya kujikinga na janga la corona katika Gereza Kuu Isanga.

Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulia Kazi, Vijana na Ajira Mhe. Anthony Mavunde akizungumza nje ya Gereza akikabidhi vifaa vya kujikinga na janga la corona katika Gereza Kuu Isanga, jijini Dodoma. Mhe. Mavunde amekabidhi msaada uliojumuisha vifaa mbalimbali ikiwemo sabuni, ndoo za maji pamoja na  vitakasa mikono (Sanitizer).

Baadhi ya vifaa hivyo vilivyokabidhiwa katika Gereza Kuu Isanga na Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulia Kazi, Vijana na Ajira Mhe. Anthony Mavunde.

Mkuu wa Magereza Mkoani Dodoma, ACP. Keneth Mwambije akimshukru Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulia Kazi, Vijana na Ajira Mhe. Anthony Mavunde (kushoto) baada ya kupokea msaada wa vifaa vya kujikinga na janga la corona.

Kamishna Jenerali wa Magereza, Suleiman Mzee( wapili kushoto) akiagana na Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulia Kazi, Vijana na Ajira Mhe. Anthony Mavunde mara baada ya mazungumzo katika Ofisi za Makao Makuu ya Jeshi la Magereza, jijini Dodoma.                                              (Picha zote na Jeshi la Magereza).

Monday, May 4, 2020

KAMISHNA JENERALI WA MAGEREZA, SULEIMAN MZEE AWAFUNDA WAKUU WA MAGEREZA ALIOWATEUA HIVI KARIBUNI KUHAKIKISHA WANASIMAMIA AGENDA YA MABADILIKO NDANI YA JESHI LA MAGEREZA

Kamishna Jenerali wa Magereza Suleiman Mzee akitoa maelekezo maalum leo Mei 04, 2020 katika kikao kazi cha Maafisa wa Jeshi la Magereza walioteuliwa hivi karibuni kushika nyadhifa mbalimbali katika Jeshi hilo wakiwemo wakuu wa magereza, Boharia Mkuu wa Jeshi ambapo Jenerali Mzee amewataka kuhakikisha kuwa wanasimamia ipasavyo Agenda ya mabadiliko ndani ya Jeshi la Magereza.

Kamishna Jenerali wa Magereza, Suleiman Mzee akiwa meza kuu pamoja na Viongozi Waandamizi wa Jeshi hilo akiwemo Kamishna wa Magereza anayeshughulika na Utawala na Rasilimali watu, Uwesu Ngarama (kulia). Kushotoni Kamishna wa Magereza anayesimamia Divisheni ya Urekebu, Mhandisi Tusekile Mwaisabila leo Mei 04, 2020 wakifuatilia kikao kazi cha Maafisa wa Jeshi la Magereza walioteuliwa hivi karibuni kushika nyadhifa mbalimbali katika Jeshi hilo wakiwemo wakuu wa magereza pamoja na Boharia Mkuu wa Jeshi hilo.

Baadhi ya Maafisa walioteuliwa kushika nyadhifa malimbali katika Jeshi la Magereza wakiwemo wakuu wa magereza wakifuatilia kikao kazi cha maelekezo ambacho kilikuwa chini ya Uenyekiti wa Kamishna Jenerali wa Magereza, leo Mei 04, 2020 jijini Dodoma .Jenerali Mzee amewataka kuhakikisha kuwa wanasimamia ipasavyo  Agenda yamabadiliko ndani ya Jeshi hilo.

Kamishna Jenerali wa Magereza, Suleiman Mzee leo Mei 04, 2020 akizungumza na baadhi ya Maafisa wa Jeshi la Magereza walioteuliwa hivi karibuni kushika nyadhifa mbalimbali katika Jeshi hilo wakiwemo wakuu wa magereza , Boharia Mkuu wa Jeshi ambapo Jenerali Mzee amewataka kuhakikisha kuwa wanasimamia ipasavyo Agenda ya mabadiliko ndani ya Jeshi la Magereza.

Kamishna Jenerali wa Magereza, Suleiman Mzee akizungumza na Maafisa kutoka Vyuo vya Mafunzo Zanzibar (kulia) ambao wametembelea Makao Makuu ya Jeshi la Magereza Tanzania Bara, leo Mei 04, 2020 jijini Dodoma. (Picha zote na Jeshi la Magereza).

Thursday, March 19, 2020

TAARIFA KWA UMMA


TAARIFA KWA UMMA


Tuesday, March 17, 2020

KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE MAMBO YA NJE, ULINZI NA USALAMA (NUU) YAFANYA ZIARA YA KUTEMBELEA MRADI WA UJENZI WA KIWANDA CHA USEREMALA GEREZA MSALATO ILI KUONA HALI YA UTEKELEZAJI WA MRADI HUO LEO TAREHE 17 MACHI 2020

Katibu Mkuu Wizara ya  Mambo ya Ndani ya Nchi ndugu Christopher D. Kadio(wannetokakushoto) akimkaribisha Mkuu wa Msafara wa Kamati ya Kudumu ya Bunge Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama,ambaye ni  Mbungewa Zanzibar Jimbo la Uzini ndugu Salum Rehani (wannetokakulia) walipowasili eneo la Mradi, Msalato. WatatutokakushotoniK amishna Jenerali wa Magereza Seleman Mzee.

Katibu Mkuu Wizara Ya Mambo ya Ndani ya Nchi ndugu Christopher D. Kadio akizungumza machache kabla ya kumkaribisha Mkuu wa Msafara kuzungumza na viongozi wa Jeshi la Magereza pamoja na Mafundi wa mradi

    Mkadiriaji Mkuu wa Ujenzi Makao Makuu ya Magereza Kamishna Msaidizi  Aron Lunyungu akitoa maelezo ya ramani ya mradi kwa Mkuu wa Msafara wa Kamati ya Kudumu ya Bunge Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama,ambaye ni Mbunge wa Zanzibar Jimbo la Uzini ndugu Salum Rehani.

Msimamizi Mkuu wa Mradi wa ujenzi wa Kiwanda cha Useremala Gereza Msalato Mrakibu Mkandarasi Bonanza Malata akitoa maelezo kwa Kamati ya Kudumu ya Bunge Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama( Picha zote na Jeshi la Magereza)


Friday, February 28, 2020

WAZIRI SIMBACHAWENE AWATAKA POLISI KUACHA KUZALISHA MAHABUSU MAGEREZANI

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, George Simbachawene akitoa maelekezo kwa Kamishna Jenerali wa Magereza nchini, Suleman Mzee(kulia) leo alipotembelea Makao Makuu ya Jeshi la Magereza, jijini Dodoma ikiwa ni ziara yake ya kwanza tangu ateuliwe        katika Wizara hiyo.

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, George Simbachawene akizungumza na Maafisa na askari wa Jeshi la Magereza(hawapo pichani)leo alipotembelea Makao Makuu ya Jeshi la Magereza, jijini Dodoma ikiwa ni ziara yake ya kwanza tangu ateuliwe katika Wizara hiyo. Kushoto ni Kamishna Jenerali wa Magereza nchini, Suleman Mzee( Kulia )ni Kamishna wa Utawala na Rasilimali watu, Uwesu Ngarama.

Kamishna Jenerali wa Magereza nchini, Suleiman Mzee akitoa taarifa fupi mbele ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, George Simbachawene(meza kuu katikati) kabla ya kuongea na Maafisa na askari wa Jeshin hilo. Kulia ni Kamishna wa Utawala na Rasilimali watu, Uwesu Ngarama.

Baadhi ya Maafisa na askari wa Jeshi la Magereza Mkoani Dodoma wakimsikiliza Waziri wa Mambo ya ndani ya Nchi, George Simbachawene (hayupo pichani).

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, George Simbachawene(kulia) akitoa maelekezo kwa Kamishna Jenerali wa Magereza nchini, Suleman Mzee(wa pili toka kushoto) leo alipotembelea Makao Makuu ya Jeshi la Magereza, jijini Dodoma ikiwa ni ziara yake ya kwanza tangu ateuliwe katika Wizara hiyo.

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, George Simbachawene(Kaunda suti) akiingia Gereza Kuu la Isanga, jijini Dodoma, leo, tayari kwa kuzungumza na Wafungwa na Mahabusu waliopo katika Gereza hilo.


Wednesday, February 19, 2020

JESHI LA MAGEREZA KUJITEGEMEA KWA KUTUMIA RASILIMALI ZAKE

Kamishna Jenerali wa Magereza, Suleiman Mzee akiongoza Kikao kazi cha siku moja cha Maafisa Waandamizi wa Jeshi la Magereza,  Kikao hicho kimefanyika leo Februari 19, 2020  katika Ukumbi wa Chuo cha Mipango, Jijini Dodoma.

Baadhi ya Wakuu wa Magereza Mikoa pamoja na Maafisa Waandamizi wa Jeshi la Magereza wakifuatilia kwa makini maelekezo kutoka kwa Kamishna Jenerali wa Magereza, Suleiman Mzee(hayupo pichani)katika Kikao kazi kilichofanyika leo katika Ukumbi wa Chuo cha Mipango, Jijini Dodoma.

Kamishna wa Utawala na Rasilimali watu wa Jeshi la Magereza, Uwesu Ngarama akitoa taarifa fupi katika Kikao kazi cha Maafisa Waandamizi wa Jeshi hilo kilichofanyika katika Ukumbi wa Chuo cha Mipango, Jijini Dodoma.

Wajumbe wa Sekretarieti wakifuatilia kikao kazi hicho kilichoongozwa na Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza leo Februari 19, 2020 katika Ukumbi Chuo cha Mipango, jijini Dodoma         (Picha zote na Jeshi la Magereza).