Banner

Banner

Monday, November 25, 2024

CGP. KATUNGU AFANYA KIKAO NA WAKUU WA MAGEREZA YOTE TANZANIA BARA

Mkuu wa Jeshi la Magereza Nchini (CGP  Yoram Katungu Novemba 23, 2024 alifanya kikao kazi na wakuu wa Magereza  Mikoa yote Tanzania bara na kuwataka wakuu hao kutokuwa na makundi, mivutano na migongano mahala pa kazi na kuhimiza Umoja, Ushirikiano na Upendo ili kuwa na mwelekeo mmoja kama Jeshi.


CGP. Katungu, alisisitiza masuala mbalimbali ya kiutendaji ikiwemo programu za mfungwa anapoingia gerezani afanyiwe tathmini ya kina ili kugundua uwezo wake na kumpangia program ya  kumfaa katika kufanikisha suala la Urekebishaji kwa mfungwa husika na pindi anapokaribia kumaliza kifungo chake, aandaliwe kisaikolojia namna bora ya kwenda kuishi na jamii ukizingatia kwasasa Jeshi linafanya  mapitio ya Sheria ya kuwafuatilia wafungwa pindi wanapokuwa wamemaliza vifungo vyao.

Kwa upande wake Mkuu wa Divisheni ya Fedha na Mipango Kaimu Kamishna wa Magereza (DCP) Chacha Bina, alipongeza wakuu wa Magereza kwa jitihada zao za kuhakikisha maduhuli ya serikali yanapatikana kwa wakati na kuvuka malengo ya kukusanya maduhuli hayo akisisitiza kuwa maduhuli si takwa la Mkuu wa Jeshi, bali ni agizo la Serikali.


Katika kikao kazi hicho wakuu wa Divisheni, Vitengo na Sehemu waliwasilisha mada mbalimbali.