Banner

Banner

Wednesday, August 7, 2019

KAMISHNA JENERALI WA MAGEREZA, PHAUSTINE KASIKE AWAVISHA VYEO MAAFISA MAGEREZA WA MKOA WA DAR ES SALAAM NA PWANI WALIOPANDISHWA VYEO HIVI KARIBUNI

Kamishna Jenerali wa Magereza nchini, Phaustine Kasike(kulia) akimvalisha cheo   Mrakibu Mwandamizi wa Magereza, Lipina Lyimo kuwa Kamishina Msaidizi  wa Magereza katika hafla fupi iliyofanyika kwenye viwanja wa Chuo cha Taaluma ya Urekebishaji, Ukonga jijini Dar es salaam, jana Agosti 6, 2019.

Kamishna Jenerali wa Magereza nchini, Phaustine Kasike(kulia) akimvalisha cheo  Mrakibu Msaidizi wa Magereza, Merkiory Komba kuwa Mrakibu wa Magereza katika hafla fupi iliyofanyika kwenye viwanja wa Chuo cha Taaluma ya Urekebishaji, Ukonga jijini Dar es salaam, jana Agosti 6, 2019. Mrakibu wa Magereza, Merkiory Komba ni Msaidizi wa Mkuu wa Jeshi hilo.
Baadhi ya Maafisa waliopandishwa vyeo katika ngazi mbalimbali wakiwa timamu kabla ya Kamishna Jenerali wa Magereza nchini, Phaustine Kasike kuwasili kwa zoezi la uvishaji vyeo , jana Agosti 6, 2019 kwenye viwanja wa Chuo cha Taaluma ya Urekebishaji, Ukonga jijini Dar es salaam.

Kamishna Jenerali wa Magereza nchini, Phaustine Kasike(kulia) akikagua Gwaride maalum  kabla ya zoezi la uvishaji vyeo kwa Maafisa wa Mkoa wa Dr es Salaam na Mkoa wa Pwani  waliopandishwa vyeo hivyo hivi karibuni.
Gwaride maalum likipita kwa mwendo wa pole mbele ya Kamishna Jenerali wa Magereza nchini(hayupo pichani) kwenye hafla ya uvishaji vyeo kwa maafisa wa Mkoa wa Dar es Salaam na Mkoa wa Pwani jana Agosti 6, 2019.
Kamishna Jenerali wa Magereza nchini, Phaustine Kasike(katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Maofisa wa ngazi mbalimbali wa Jeshi la Magereza waliopandishwa vyeo (waliosimama)baada ya hafla uvishaji vyeo iliyofanyika katika viwanja vya Chuo cha Taaluma ya Urekebishaji, Ukonga jijini Dar es salaam, jana Agosti 6, 2018(Picha zote na Jeshi la Magereza).

Friday, July 12, 2019

KAMISHNA JENERALI WA MAGEREZA, PHAUSTINE KASIKE AKAGUA SHAMBA LA KIMKAKATI LA MAHINDI KATIKA GEREZA LA KILIMO NA MIFUGO KITENGULE, MKOANI KAGERA

Kamishna Jenerali wa Magereza( wa Kwanza kulia) akikagua shamba la mahindi ambalo liko katika hatua za mwisho za kuvunwa la gereza Kitengule.

 Kamishna Jenerali wa Magereza nchini, Phaustine Kasike(kushoto) akikagua ghala la kuhifadhia chakula cha wafungwa Gereza Kitengule alipotembelea gereza hilo leo Julai 11, 2019.

Kamishna Jenerali wa Magereza nchini, Phaustine Kasike(wa pili toka kulia) akiangalia moja ya mashine maalum inayotumika katika upandaji wa mbegu katika mashamba ya Gereza Kitengule alipotembelea gereza hilo leo Julai 11, 2019(Picha zote na Jeshi la Magereza)

ZAIDI YA WAFUNGWA 640 WAMENUFAIKA NA MPANGO WA BODI YA PAROLE NCHINI KATIKA KIPINDI CHA MIAKA MITATU


                      


 
Kaimu Kamishna Jenerali wa Magereza, Kamishna wa Magereza, Uwesu Ngarama(kulia) ambaye pia ni Kaimu Katibu wa Sekretarieti ya Bodi ya Taifa ya Parole akitoa taarifa fupi kabla ya kumkaribisha Mgeni rasmi Mwenyekiti wa Bodi ya Taifa ya Parole, Mhe. Augustino Mrema(kushoto) afungue rasmi Kikao cha 41 cha kujadili Wafungwa waliopendekezwa kunufaika/kutonufaika katika mpango wa Parole. Kikao hicho cha siku moja kimefanyika leo Julai 12, 2019, katika Bwalo la Maafisa Magereza, lililopo Ukonga,  Jijini Dar es Salaam.


           Baadhi ya Wajumbe Sekretarieti wakifuatilia kwa makini majadiliano katika kikao hicho.


Mwenyekiti wa Bodi ya Taifa ya Parole, Mhe. Augustino Mrema(hayupo pichani) akifungua kikao cha 41 cha kujadili Wafungwa waliopendekezwa kunufaika/kutonufaika katika mpango wa Parole.

      Mwenyekiti wa Bodi ya Taifa ya Parole, Mhe. Augustino Mrema(meza kuu) akiongoza Kikao cha 41 cha Bodi hiyo.

Wajumbe wa Bodi ya Taifa ya Parole wakifuatilia majadiliano ya wafungwa waliopendekezwa kunufaika/kutonufaika katika mpango wa Parole leo Julai 12, 2019, katika Bwalo la Maafisa Magereza, lililopo Ukonga, Jijini Dar es Salaam.(Picha zote na Jeshi la Magereza).