Wednesday, January 20, 2021

TANZIA: NAIBU KAMISHNA WA MAGEREZA JULIUS SANG'UDI AFARIKI DUNIA JIJINI DODOMA.

 

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI

(Jeshi la Magereza)

TANZIA

 

 

 

Kamishna Jenerali wa Jeshi Magereza Mej. Jen Suleiman M. Mzee anasikitika kutangaza kifo cha Naibu Kamishna wa Magereza Julius Mayenga Sang’udi kilichotokea Hospitali ya Benjamin Mkapa, Jijini Dodoma leo tarehe 20 Januari, 2021.

Aidha anatoa pole kwa Familia ya Marehemu, Watumishi wote wa Jeshi la Magereza Nchini, Ndugu, Jamaa na Marafiki wote walioguswa na msiba huu.

Jeshi  la Magereza kwa kushirikiana na familia ya Marehemu inaendelea kuratibu taratibu za Mazishi nyumbani kwake Kisasa nyumba 300, Dodoma.

Mwili wa Marehemu unatarajiwa kusafirishwa Ijumaa tarehe 22 Januari,2021 na Mazishi yatafanyika Mkoani Simiyu Kijiji cha Ikulilo – Mwandete Jumamosi tarehe 23 Januari,2021.

Mwenyezi Mungu ailaze Roho ya Marehemu mahala pema peponi, Amen.

 

Imetolewa na Msemaji wa Jeshi la Magereza,

Kitengo cha Habari na Mawasiliano ya Umma,

Dodoma.