Friday, February 14, 2020

MAAFISA WASHIRIKI KUTOKA CHUO CHA ULINZI WA TAIFA(NDC) WATEMBELEA KIWANDA CHA GEREZA KUU UKONGA JIJINI DSM

Mkufunzi Mwandamizi  wa Chuo cha Taifa cha Ulinzi Tanzania, Bregedia Jenerali  Cherestino Msolla (kushoto) akisalimiana na Mkuu wa Gereza Kuu Ukonga, ACP. Nsajigwa Mwankenja walipofanya ziara ya mafunzo katika Jeshi la Magereza Februari 12, 2020.

Maafisa Washiriki kutoka Chuo cha Ulinzi wa Taifa wakitembelea sehemu mbalimbali katika Kiwanda cha Gereza Kuu Ukonga kama inavyoonekana katika picha.

Maafisa Washiriki kutoka Chuo cha Ulinzi wa Taifa wakizungumza na mfungwa ambaye amepatiwa ujuzi gerezani wa fani ya ushonaji katika Kiwanda cha Ushonaji cha Gereza Kuu Ukonga kama inavyoonekana katika picha.

Maafisa Washiriki kutoka Chuo cha Ulinzi wa Taifa wakitoka  katika Kiwanda cha Gereza Kuu Ukonga kuendelea na ziara yao ya mfunzo katika maeneo mbalimbali ya Jeshi la Magereza.

Msemaji Mkuu wa Jeshi la Magereza, SSP. Amina Kavirondo akiwasilisha andiko linalohusu majukumu ya Jeshi hilo mbele ya Maafisa Washiriki kutoka Chuo cha Ulinzi wa Taifa             (hawapo pichani).

Maafisa Washiriki kutoka Chuo cha Ulinzi wa Taifa wakifuatilia uwasilishaji wa taarifa mbalimbali nkuhusu shughuli mbalimbali zinazofanywa na Jeshi la Magereza ikiwemo program za urekebishaji, Jijini Dar es Salaam.

Kikundi cha Askari wa Kikosi Maalum cha Magereza kikionesha onesho la ukakamavu mbele ya Maafisa Washiriki kutoka Chuo cha Ulinzi wa Taifa(NDC) walipotembelea Makao Makuu ya Kikosi hicho, jijini Dar es Salaam.

Maafisa Washiriki kutoka Chuo cha Ulinzi wa Taifa cha Tanzania wakiburudika na matunda ya madafu katika ziara yao ya mafunzo katika Jeshi la Magereza.

Kamishna wa Magereza, Uwesu Ngarama(wa pili toka kulia) akiwa katika picha ya pamoja na Maafisa Washiriki waliotembelea Makao Makuu ya Jeshi la Magereza jana(waliosimama mstari wa nyuma) kutoka Chuo cha Taifa cha Ulinzi Tanzania(wa pili toka kushoto walioketi) ni Mkufunzi Mwandamizi  wa Chuo cha Taifa cha Ulinzi Tanzania, Bregedia Jenerali  Cherestino Msolla (kushoto) ni Naibu Kamishna wa Magereza, Jeremiah Katungu (Picha zote na Jeshi la Magereza).