Banner

Banner

Thursday, October 24, 2024

DKT. MPANGO AFUNGUA MKUTANO WA MWAKA WA MAAFISA WAANDAMIZI WA JESHI LA MAGEREZA

Na. SP. Kilian Ngalla - DODOMA


Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh. Dkt. Philip Isidor Mpango, leo tarehe 24 Oktoba, 2024 amefungua Mkutano Mkuu wa Mwaka wa Maafisa Waandamizi wa Jeshi la Magereza ambapo Mkutano huo wa siku mbili unalenga kufanya tathmini ya utekelezaji wa majukumu ya Jeshi la Magereza na kuweka mikakati ya kuboresha utendaji kazi. 

Akizungumza wakati wa ufunguzi wa Mkutano huo Dkt. Mpango amesema, Jeshi la Magereza lishirikiane na Jeshi la Polisi pamoja na Bodi ya Taifa ya Parole ili kuweka utaratibu wa pamoja wa kuwatambua na kuwafuatilia wale wote wanaotoka Magerezani baada ya kumaliza vifungo vyao ili wawezeshwe kwa kupewa mikopo kutoka kwa Halmashauri zinazowazunguka itakayowasaidia kufanya biashara na kujikimu kimaisha ili kuwaepusha kurudi tena Magerezani.

Dkt. Mpango pia amesema, mchakato wa marekebisho ya Sheria ya Magereza ni mchakato muhimu lakini hautakua na maana iwapo Maafisa na askari hawatabadilika kimtazamo kuendana na mazingira, kwa kuwa Sheria na mifumo ya Magereza tuliyo nayo tumeirithi kutoka kwa wakoloni hivyo ameitaka Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi kuharakisha marekebisho ya Sheria hiyo yanafanyika haraka na yazingatie mapendekezo ya Tume ya Haki Jinai. 

Makamu wa Rais aliendelea kusisitiza kuwa mkutano huu usaidie kuleta mitazamo chanya ndani ya Jeshi la Magereza kuhusu mabadiliko na kujitosheleza kwa chakula ikiwa ni pamoja na kuzalisha miche na mbegu bora za mazao tofauti ya kimkakati ili kuondokana na utegemezi kutoka nje ya Nchi huku akisisitiza kuwa Viwanda vyetu vya ndani na vile vya ubia vinazalisha na kukidhi masoko ya ndani ya Nchi. 

“Ili kuendelea kuboresha kilimo na kujitosheleza kwa chakula Jeshi halina budi kununua au kukopa zana bora za kilimo kutoka taasisi binafsi ili kuzalisha chakula kwa aajili ya Wafungwa na Mahabusu” Alisema Dkt. Mpango.

Aidha Dkt. Mpango amelitaka Jeshi la Magereza lishirikiane na Wakala wa Misitu Tanzania ili kuweza kuzalisha miche ya miti na matunda ili liwe kielelezo cha utunzaji wa Mazingira.

Kwa upande wake Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Mh. Mhandisi Hamad Masauni amesema,ndoto ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh. Dkt. Samia Suluhu Hassan ni kuona Jeshi la Magereza linatumia rasilimali zake kikamilifu ikiwemo ardhi ili kuzalisha kwa tija na kujitosheleza kwa chakula na kutoa mchango kwa Taifa ili kutatua changamoto ndani ya Jeshi na kuipunguzia mzigo Serikali.

Naye Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza (CGP) Jeremiah Yoram Katungu amesema, mwelekeo wa Jeshi la Magereza ni kuhakikisha tunaboresha Programu za Urekebishaji wa Wafungwa ili ziendane na wakati uliopo na kwa kuzingatia Sheria za nchi, Kikanda na Kimataifa.

Aidha CGP. Katungu ameishukuru Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Mh. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa jinsi inavyoliwezesha Jeshi la Magereza kutekeleza majukumu yake kwa kuliongezea bajeti, kuajiri askari wapya na kuwapandisha vyeo maafisa na askari katika ngazi mbalimbali wapatao 11,880 kwa kipindi cha kuanzia mwaka 2020/2021 hadi mwaka 2023/2024.

Hafla ya ufunguzi wa mkutano wa Maafisa Waandamizi wa Jeshi la Magereza imehudhuriwa na Viongozi mbalimbali wa Chama na Serikali.

Wednesday, October 9, 2024

CGP. KATUNGU AMTEMBELEA MAKAMU WA RAIS DKT. MPANGO, OFISINI KWAKE

Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza (CGP) Jeremiah Yoram Katungu, Oktoba 07, 2024 amemtembelea Dkt. Philip Isdor Mpango, Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Ofisini kwake jijini Dodoma, kwaajili ya kujitambulisha ikiwa ni mara ya kwanza tangu alipoteuliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, kuliongoza Jeshi la Magereza hivi karibuni.




Friday, October 4, 2024

WAZIRI MASAUNI AFANYA ZIARA MAGEREZA MAKAO MAKUU, AKUTANA NA MENEJIMENTI YA SHIMA.

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Mhe. Mhandisi Hamad Masauni (Mb), Oktoba 04, 2024 amefanya ziara ya kikazi Makao Makuu ya Magereza Msalato jijini Dodoma na kufanya Kikao na Menejimenti ya Shirika la Uzalishaji Mali Jeshi la Magereza (SHIMA) Pamoja na Wakuu wa Magereza Mikoa na Wakuu wa Vituo vya Magereza vinavyo tekeleza Miradi mbalimbali ya Shirika hilo.


Katika kikao hicho yamejadiliwa mambo mbalimbali ikiwemo utendaji wa Shirika na mikakati ya kulifanya lizalishe zaidi kwa manufaa ya Jeshi la Magereza na Taifa kwaujumla, 


Kikao hicho pia kimedhuriwa na Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Mhe. Danniel Sillo, Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi Dkt. Maduhu Kazi, Kamishna Jenerali wa Magereza (CGP) Jeremiah Yoram Katungu na Maafisa Waandamizi wa Magereza Makao Makuu.

TCTA YAKABIDHIWA GARI MPYA KWA SHUGHULI ZA UTAWALA.

Na. A/insp. Nurdin Nanyanga.


Mkuu wa Chuo cha Taaluma ya Sayansi ya  Urekebishaji Tanzania (TCTA) kilichopo Ukonga jijini Dar es salaam, Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Magereza (SACP) Willington Kahumuza, Mapema leo Oktoba 04, 2024 amekabidhiwa gari mpya aina ya Toyota Land Cruiser Hard top na Mkuu Msaidizi  wa Kitengo cha Usafirishaji cha Jeshi la Magereza Mrakibu wa   Magereza (SP) Adam Kipalamoto, kwaniaba ya Kamishna Jenerali wa Magereza Jeremiah Yoram Katungu.


Akizungumza wakati wa makabidhiano ya gari hilo , Mkuu wa Chuo SACP. Kahumuza amemshukuru Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzani Dk Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kuliwezesha Jeshi la Magereza vitendea kazi.


Aidha amemshukuru Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Mhandisi Hamad Masauni (MB) na Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza (CGP) Jeremiah Yoram Katungu kwa kuwapa kipaumbele kwa Chuo TCTA katika Mgao wa gari

Aidha amewataka Watumishi wa Chuo kulitunza gari hilo ili liweze kudumu na kufanya kazi zilizokusudiwa.



CGP. KATUNGU AFANYA KIKAO NA WATENDAJI WA SHIMA JIJINI DODOMA.


Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza (CGP) Jeremiah Katungu,  Oktoba 03, 2024 amekutana na Watendaji wa Shirika la Uzalishaji Mali Jeshi la Magereza (SHIMA) wakiongozwa na Kaimu Mkurugenzi wa Shirika hilo, Kamishna Msaidizi wa Magereza (ACP) Omary Msepwa, kwaajili kujadili masuala mbalimbali ya kiutendaji wa Shirika hilo ili liweze kuleta tija zaidi katika Uzalishaji.




DPP. MWAKITALU ATEMBELEA MAGEREZA MAKAO MAKUU, AFANYA MAZUNGUMZO NA CGP. KATUNGU.


Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza (CGP) Jeremiah Katungu, amekutana na kuzungumza na Mkurugenzi wa Mashtaka Nchini (DPP) Silvester Mwakitalu, alipotembelea Makao Makuu ya Magereza Msalato, jijini Dodoma, Oktoba 03, 2024.


CGP. KATUNGU AKUTANA NA KUZUNGUMZA NA WAZIRI WA FEDHA DKT. MWIGULU NCHEMBA.


Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza (CGP) Jeremiah Yoram Katungu, Oktoba 03, 2024 ambetembelea Ofisi za Wizara ya Fedha zilizopo Jijini Dodoma, ambapo amekutana na kufanya mazungumzo na Waziri wa Fedha, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb).


Lengo la ziara hiyo ni kujitambulisha na kujadili masuala mbalimbali ikiwemo mipango ya maendeleo ya Jeshi la Magereza.

Kamishna Jenerali wa Magereza Jeremiah Yoram Katungu, akiagana na Waziri wa Fedha Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba, mara baada ya mazungumzo yao, jijini Dodoma, Octoba 03, 2024


KATIBU MKUU WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI AFANYA ZIARA MAGEREZA MAKAO MAKUU, AZINDUA MAGARI MAPYA 11

 Na. Sgt. Geofrey Jacka - DODOMA


Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Ndg. Ally Senga Gugu, akikata utepe kuashiria Uzinduzi wa Magari 11 ya Jeshi la Magereza.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Ndg. Ally Senga Gugu, leo Oktoba 02, 2024 ametembelea Makao Makuu ya Jeshi la Magereza eneo la Msalato Jijini Dodoma na  kupokelewa na Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza, Jeremiah Y Katungu, pamoja na maafisa wa ngazi mbalimbali.


Akizungumza na Maafisa, Askari na Watumishi wasio Askari Katibu Mkuu Gugu amesema, lengo la ziara hiyo ni kujitambulisha ili kufahamiana na kupeana Miongozo ya kiutendaji wa kazi huku akiahidi Ushirikiano na Viongozi wa Jeshi la Magereza katika kutatua changamoto zinazowakabili watumishi na kusisitiza umoja na ushirikiano miongoni mwa watendaji. 


Aidha Ndg. Gugu ameutaka Uongozi wa Jeshi la Magereza kutumia falsa ya 4R ya Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambayo inabeba  Ujumbe wa Maridhiano (Reconcilation)  Ustahamiliivu (Resilience) Mabadiliko (Reforms) na Kujenga Upya yaani Rebuilding, ambayo imeonesha mafanikio  makubwa pale inapotekelezwa kikamilifu.


Kabla ya kumkaribisha Katibu Mkuu kuzungumza, Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza (CGP) Jeremiah Katungu alitoa maelezo ya kina kuhusu shughuli mbalimbali zinazofanywa na Jeshi la Magereza nchini na kumshukuru Katibu Mkuu Kwa kutenga muda wake kufanya ziara ndani ya Jeshi la Magereza.


Katibu Mkuu Ndg. Ally Senga Gugu pia alipata fursa ya kuzindua Magari 11 ya Jeshi la Magereza yatakayo tumika katika shughuli za kiutawala, pamoja na gari moja la kubebea wagonjwa (Ambulance ) ambalo litapelekwa Hospitali Kuu ya Jeshi la Magereza iliyopo Ukonga, Jijini Dar es Salaam.