Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza (CGP) Jeremiah Yoram Katungu, Oktoba 07, 2024 amemtembelea Dkt. Philip Isdor Mpango, Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Ofisini kwake jijini Dodoma, kwaajili ya kujitambulisha ikiwa ni mara ya kwanza tangu alipoteuliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, kuliongoza Jeshi la Magereza hivi karibuni.