Banner

Banner

Friday, October 4, 2024

WAZIRI MASAUNI AFANYA ZIARA MAGEREZA MAKAO MAKUU, AKUTANA NA MENEJIMENTI YA SHIMA.

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Mhe. Mhandisi Hamad Masauni (Mb), Oktoba 04, 2024 amefanya ziara ya kikazi Makao Makuu ya Magereza Msalato jijini Dodoma na kufanya Kikao na Menejimenti ya Shirika la Uzalishaji Mali Jeshi la Magereza (SHIMA) Pamoja na Wakuu wa Magereza Mikoa na Wakuu wa Vituo vya Magereza vinavyo tekeleza Miradi mbalimbali ya Shirika hilo.


Katika kikao hicho yamejadiliwa mambo mbalimbali ikiwemo utendaji wa Shirika na mikakati ya kulifanya lizalishe zaidi kwa manufaa ya Jeshi la Magereza na Taifa kwaujumla, 


Kikao hicho pia kimedhuriwa na Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Mhe. Danniel Sillo, Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi Dkt. Maduhu Kazi, Kamishna Jenerali wa Magereza (CGP) Jeremiah Yoram Katungu na Maafisa Waandamizi wa Magereza Makao Makuu.