Thursday, May 19, 2016

Katibu mkuu wizara ya mambo ya ndani ya nchi kufunga mafunzo ya uongozi daraja la pili kwa maafisa wa jeshi la magereza, jijini Mbeya


Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Meja Jenerali Projest Rwegasira kesho tarehe 20 Mei, 2016 saa 3:00
asubuhi anatarajia kufunga Mafunzo ya Uongozi Daraja la Pili katika Chuo cha Magereza, Kiwira Mkoani Mbeya.

Mafunzo hayo ambayo yamechukua muda wa miezi mitatu yalilenga kuwaandaa Maafisa(pichani) kuwa viongozi wa kati katika vituo vya Magereza nchini. Jumla ya wahitimu ni 327, kati yao Wanaume 246 na Wanawake 81, Aidha Wanaume 08 na Wanawake 02 wanatoka Vyuo vya Mafunzo Zanzibar. 

Sherehe hizo, zitajumuisha mambo yafuatayo:- 
* Mgeni Rasmi kukagua Gwaride rasmi lililoandaliwa na wahitimu hao; 
* Mgeni Rasmi kutoa vyeti kwa Wanafunzi waliofanya vizuri katika Mafunzo ya darasani na
  Mafunzo ya mbinu za medani; 
* Mgeni Rasmi kuvisha cheo cha Mkaguzi Msaidizi wa Magereza kwa wahitimu wawili kwa niaba
  ya wahitimu wengine na; 
* Mgeni Rasmi kutoa Hotuba. 

Sherehe za ufungaji wa Mafunzo hayo zinatarajia kukamilika saa 8:00 mchana. Vyombo vya Habari vinakaribishwa 
kwenye sherehe hizo siku ya Ijumaa  tarehe 20 Mei, 2016 kuanzia saa 3:00 asubuhi. 


IMETOLEWA NA KITENGO CHA HABARI NA MAWASILIANO 
MAKAO MAKUU YA JESHI LA MAGEREZA 
Mei 19, 2016