Sunday, November 18, 2018

KATIBU MKUU WA MAMBO YA NDANI, MEJA JENERALI JACOB KINGU AKAGUA MABORESHO YA KIWANDA CHA VIATU GEREZA KUU KARANGA MOSHI

Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Ndani, Meja Jenerali Jacob Kingu akisalimiana na Maafisa wa Jeshi la Magereza Mkoani Kilimanjaro mara baada ya kuwasili katika ziara Maalum ya kukagua maboresho mbalimbali katika Kiwanda cha Viatu cha Gereza Kuu Karanga Moshi jana  Novemba 17, 2018. Kushoto kwake ni Kamishna Jenerali wa Magereza, Phaustine Kasike.

Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Ndani ya nchi, Meja Jenerali Jacob Kingu(meza kuu) akitoa maelekezo kwa Kaimu Mkuu wa Kiwanda hicho, Mrakibu Msaidizi wa Magereza, Hamis Nyaku(aliyesimama). Kushoto ni Kamishna Jenerali wa Magereza, Phaustine Kasike
Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Ndani ya nchi, Meja Jenerali Jacob Kingu na Kamishna Jenerali wa Magereza, Phaustine Kasike wakiangalia Buti za aina mbalimbali za Jeshi zinazotengenezwa katika Kiwanda cha Viatu Karanga Moshi.
Sehemu ya viatu aina mbalimbali ikiwemo viatu vya maafisa na Buti za Jeshi zinazotengenezwa katika Kiwanda cha Viatu Karanga Moshi kwa ajili ya Jeshi la Polisi nchini. Jeshi la Polisi limetengenezewa viatu aina ya buti pea elfu kumi (10,000) na pea elfu tano (5,000) za viatu vya maafisa zenye thamani ya Tsh. 1, 237, 666, 600/=, tayari buti zimekabidhiwa kwa Jeshi hilo na hivi sasa kiwanda kinamalizia utengenezaji wa viatu vya maafisa wa Jeshi la Polisi.

Maafisa Masoko wa Kiwanda cha viatu Karanga Moshi wakivipanga viatu vya kiraia aina mbalimbali vinavyotengenezwa katika kiwanda hicho kama inavyoonekana katika picha.

Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Ndani ya nchi, Meja Jenerali Jacob Kingu akipata maelezo ya kitaalam juu ya utengenezaji wa Buti za Jeshi kutoka kwa Mtaalam wa utengenezaji viatu wa Jeshi la Magereza
(Picha zote na Jeshi la Magereza).