Monday, June 3, 2019

WAZIRI MKUU, KASSIM MAJALIWA AFUNGUA RASMI GEREZA JIPYA LA WILAYA YA RUANGWA, LEO MKOANI LINDI

Waziri Mkuu, Mhe. Kassim Majaliwa akisalimiana na Kamishna Jenerali wa Magereza, Phaustine Kasike alipowasili kwenye hafla ya ufunguzi wa Gereza la Wilaya ya Ruangwa leo Juni 3, 2019.

Kamishna Jenerali wa Magereza, Phaustine Kasike akitoa historia fupi ya ujenzi wa Gereza la Wilaya Ruangwa kabla ya kumkaribisha Waziri Mkuu, Mhe. Kassim Majaliwa kufungua rasmi Gereza hilo, leo Juni 3, 2019.
Waziri Mkuu, Mhe. Kassim Majaliwa akitoa hotuba fupi kabla ya ufunguzi wa Gereza la Wilaya ya Ruangwa. Kushoto ni Waziri wa Mambo ya Ndani ya nchi, Mhe. Kangi Lugola. 
Waziri Mkuu, Mhe. Kassim Majaliwa(kulia) akisoma jiwe la msingi kabla ya ufunguzi wa Gereza la Wilaya ya Ruangwa leo Juni 3, 2019. Kushoto ni Waziri wa Mambo ya Ndani ya nchi, Mhe. Kangi Lugola.

Baadhi ya Askari wa Gereza Ruangwa wakifuatilia hotuba ya Waziri Mkuu, Mhe. Kassim Majaliwa katika hafla ya ufunguzi wa Gereza hilo, leo Juni 3, 2019.

Waziri Mkuu, Mhe. Kassim Majaliwa akiongea na wafungwa na mahabusu wa Gereza Ruangwa(hawapo pichani) baada ya uzinduzi wa Gereza hilo leo.

Muonekano wa nje wa Gereza la Wilaya ya Ruangwa  (Picha zote na Kitengo cha Habari na Mawasiliano – Jeshi la Magereza).