Sunday, February 9, 2020

WAZIRI MHAGAMA ARIDHISHWA NA KASI YA UJENZI WA KIWANDA KIPYA CHA NGOZI KARANGA, MOSHI

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Kazi, Ajira na Uwekezaji) Jenista Mhagama (wa tatu toka kushoto) pamoja na Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Ajira, Vijana na Wenye Ulemavu) Andrew Massawe (wa pili toka kushoto) wakiongozana na Makamanda Waandamizi wa Jeshi la Magereza Nchini wakati wa ziara yake ya kukagua ujenzi wa mradi wa kiwanda cha Ngozi cha Karanga kinachojengwa kwa Ubia baina ya Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF) na Gereza la Karanga lilolopo Moshi Mkoani Kilimanjaro, Februari 8, 2020.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Kazi, Ajira na Uwekezaji) Jenista Mhagama (wa pili toka kulia) akitoa maelekezo leo kwa watendaji mbalimbali Naibu Kamishna wa Magereza, Afwilile Mwakijungu(kushoto) ambaye ni Mtendaji Mkuu wa Shirika la Uzalishaji Mali la Magereza wakati wa ziara yake ya kukagua ujenzi wa mradi wa kiwanda cha Ngozi cha Karanga kinachojengwa kwa Ubia baina ya Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF)
 na Jeshi la Magereza.

Moja ya majengo katika mradi wa ujenzi wa kiwanda cha Ngozi cha Karanga kinachojengwa kwa Ubia baina ya Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF) na Jeshi la Magereza likiwa limefikia hatua mbalimbali za ujenzi kama inavyoonekana katika picha. Jengo hilo litatumika kuhifadhia mashine ambazo tayari zimewasili bandarini

Mhandisi wa Mradi wa ujenzi wa Kiwanda kipya cha bidhaa za ngozi, Mrakibu wa Magereza, Julius Sukambi (kulia) akisoma taarifa ya ujenzi mbele ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Kazi, Ajira na Uwekezaji) Jenista Mhagama (kushoto).

Mafundi wakiendelea na ujenzi wa majengo ya kiwanda hicho (Picha zote na Jeshi la Magereza).