Friday, June 20, 2014

Maadhimisho ya siku ya Magereza (Magereza Day) yafana jijini Dar es Salaam

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe. Mathias Chikawe(MB) akipokea Salaam ya heshima toka kwa Gwaride Maalum lililoandaliwa na Maafisa wa Jeshi la Magereza(hawapo pichani) katika maadhimisho ya Siku ya Magereza(Magereza Day). Kushoto katika picha ni Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza, John Casmir Minja (kulia) ni Mkuu wa Chuo cha Maafisa wa Magereza Ukonga, Kamishna Msaidizi wa Magereza, Erasmus Kundy
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe. Mathias Chikawe (MB) akikagua Gadi ya Wanawake inayoundwa na Maafisa na Askari wa Jeshi la Magereza katika Maadhimisho ya Magereza Day yaliyofanyika leo Juni 20, 2014 katika Viwanja vya Chuo cha Maafisa wa Magereza Ukonga, Jijini Dar es Salaam.
Gadi ya Wanaume iliyoundwa na Maafisa na Askari wa Jeshi la Magereza wakipita mbele ya Mgeni rasmi katika mwendo wa haraka wakati wa kutoa heshima katika Maadhimisho ya Magereza Day yaliyofanyika katika Viwanja vya Chuo cha Maafisa Magereza Ukonga kilichopo Jijini Dar es Salaam.
Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza Nchini, John Casmir Minja(aliyesimama) akitoa maelezo mafupi kuhusu Madhumuni ya Maadhimisho ya Siku ya Magereza(Magereza Day). Maadhimisho haya ya siku ya Magereza yanafanyika hapa nchini kwa mara ya pili ambapo leo yamefanyika katika Chuo cha Maafisa wa Magereza Ukonga, Jijini Dar es Salaam(wa Nne kulia katika vazi la suti nyeusi) ni Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe. Mathias Chikawe(wa pili kulia) ni Kamishna Jenerali wa Magereza Nchini Namibia, Raphael Tuhaferi.
Baadhi ya Maafisa wa Jeshi la Magereza Nchini wakitoa heshima ya Utii wakati Kikosi cha Bendera kikipita mbele ya Mgeni rasmi(hayupo pichani) katika Maadhimisho ya Siku ya Magereza(Magereza Day) yaliyofanyika leo Juni 20, 2014 katika Viwanja vya Chuo cha Maafisa Magereza Ukonga, Jijini Dar es Salaam.
Mkuu wa Kitengo cha Kilimo na Mifugo Ndani ya Jeshi la Magereza, Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Magereza, Mlasan Kimaro(wa pili kushoto) akitoa maelezo mafupi kwa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe. Mathias Chikawe (suti nyeusi) kuhusu uzalishaji wa mafuta ya mawese ambayo hutumika kwa matumizi ya Wafungwa Magerezani alipotembelea Banda la Kilimo na Mifugo (wa pili kulia kwa Waziri) ni Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza Nchini, John Casmir Minja.
Msanii Nguza Viking anayetumikia Kifungo chake Gerezani akiwa na Bendi ya Wafungwa(anayepiga gitaa) akiimba Wimbo Maalum kuhusu Urekebishaji wa Wafungwa unavyofanyika Magerezani(wa pili kulia) ni Jonson Nguza Maarufu kwa jina la Papii Kocha wakitumbuiza katika Maadhimisho ya Magereza Day yaliyofanyika leo Juni 20, 2014 katika Viwanja vya Chuo cha Maafisa Magereza Ukonga.