Thursday, July 2, 2015

Banda la Jeshi la Magereza lang'ara kwa bidhaa bora maonesho ya 39 ya biashara ya kimataifa 'sabasaba' 2015

Meza ya Chakula iliyotengenezwa kwa Ustadi mahiri katika Kiwanda cha Userelemala kilichopo Gereza Kuu Ukonga, Dar es Salaam. Meza hiyo ina viti vinane imetengenezwa kwa kutumia mbao ya Mninga inauzwa kwa Tsh. 2500,000/=
"Sofa set" yenye uwezo wa kukaliwa na watu saba, sofa hii imetengenezwa pia na Mafundi waliobobea kutoka Kiwanda cha Uselemala kilichopo Gereza Kuu Ukonga, Dar es Salaam kwa kutumia mbao aina ya mninga ambapo inauzwa kwa Tsh. 4,500,000/=
Meza Maalum ya Ofisi iliyotengenezwa kwa kutumia mbao ya mninga inapatikana katika Banda la Maonesho ya 39 ya Biashara ya Kimataifa, Jijini Dar es Salaam. Meza hiyo kwa pembeni ina meza ndogo kwa matumizi ya kiofisi kama ambavyo inaonekana. Aliyeketi ni Afisa Habari wa Jeshi la Magereza nchini, Mrakibu Msaidizi wa Magereza Lucas Mboje akiendelea na majukumu kama anavyoonekana katika picha.
Seti mbalimbali za kapeti za mlangoni ambazo zimetengenezwa kwa kutumia malighafi za mkonge na nazi kama zinavyoonekana katika picha. Kapeti hizo zenye ubora zinauzwa Tsh. 7000/= hadi 15,000/=
Vikoi kutoka Kiwanda cha Ushonaji cha Gereza Kuu Butimba, Mwanzaj vikiwa katika Banda la Jeshi la Magereza katika Maonesho ya 39 ya Biashara ya Kimataifa, kikoi kimoja kinauzwa kwa Tsh. 10,000/= tu
Bidhaa za mianzi zinazotengenezwa kutoka Gereza Njombe, Mkoani Njombe. Stafu Sajin wa Magereza, Shukrani wa Gereza Njombe akielezea namna bidhaa hizo zinavyotengenezwa pia namna Wafungwa wanavyonufaika kupitia Stadi hiyo ya utengenezaji wa bidhaa za mianzi Mkoani Njombe.
Vinyago vya aina mbalimbali kama vinavyoonekana katika picha ambapo vimechongwa kwa kutumia Mti wa Mpingo. Vinyago hivyo imetengenezwa katika Kiwanda cha Gereza Kuu Lilungu, Mkoani Mtwara. Wafungwa wa Gereza Kuu Lilungu wananufaika sana na Stadi hiyo ya uchongaji Vinyago hivyo kujipatia ujuzi na ajira mara wamalizapo vifungo vyao magerezani. Picha zote na Lucas Mboje wa Jeshi la Magereza.