Monday, August 31, 2015

Kamishna Jenerali wa Magereza ashiriki hafla ya uwekaji jiwe la msingi la ujenzi wa makao makuu ya ulinzi wa Taifa, Lugalo jijini Dar

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama, Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akitoa hotuba fupi kwenye hafla ya kuweka Jiwe la Msingi la Ujenzi wa Makao Makuu ya Ulinzi wa Taifa, Lugalo Jijini Dar es Salaam leo Agosti 31, 2015.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama, Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akiweka jiwe la Msingi la Ujenzi wa Makao Makuu ya Ulinzi wa Taifa, Lugalo Jijini Dar es Salaam leo Agosti 31, 2015.

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama, Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akiangalia ramani/mchoro wa Ujenzi wa Makao Makuu ya Ulinzi wa Taifa, Lugalo Jijini Dar es Salaam leo Agosti 31, 2015(kushoto) ni Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Tanzania, Jenerali Davis Mwamunyange.

 Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Tanzania, Jenerali Davis Mwamunyange akitoa maelezo mafupi ya mradi huo wa Ujenzi wa Makao Makuu ya Ulinzi wa Taifa, Lugalo Jijini Dar es Salaam leo Agosti 31, 2015 kabla ya kumkaribisha Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Dkt. Hussein Mwinyi(hayupo pichani).
 Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza nchini, John Casmir Minja akiteta jambo na Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini, Ernest Jumbe Mangu kwenye hafla ya kuweka Jiwe la Msingi la Ujenzi wa Makao Makuu ya Ulinzi wa Taifa, Lugalo Jijini Dar es Salaam leo Agosti 31, 2015.

Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza nchini, John Casmir Minja akiteta jambo na Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Mhe. Paul Makonda(Picha zote na Lucas Mboje wa Jeshi la Magereza.
 Baadhi ya Maafisa wa Ngazi za Juu wa Jeshi la Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa wakifuatilia kwa umakini mkubwa hotuba ya Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama  kwenye hafla ya kuweka Jiwe la Msingi la Ujenzi wa Makao Makuu ya Ulinzi wa Taifa, Lugalo Jijini Dar es Salaam leo Agosti 31, 2015.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama, Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete(katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Viongozi mbalimbali wa Serikali na Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Tanzania, Jenerali Davis Mwamunyange(wa nne kulia) walioketi. wa pili kulia waliosimama) ni Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza nchini, John Casmir Minja(wa tatu kulia waliosimama) ni Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini, Ernest Jumbe Mangu na wa kwanza kulia ni Kamishna Mkuu wa Idara ya Uhamiaji, Sylvester Ambokile.