Tuesday, December 8, 2015

Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza nchini aongoza kikao maalumu cha kupitia rasimu ya mpango wa Jeshi la Magereza kujitosheleza chakula, Jijini Dar

Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza, John Casmir Minja akifungua Kikao Maalum cha Wadau kutoka nje ya Magereza(hawapo pichani) cha kujadili rasimu ya Mpango wa Jeshi la Magereza wa kujitosheleza kwa chakula cha Wafungwa waliopo Magerezani. Kikao hicho kimefanyika leo Desemba 8, 2015 katika Ofisi za Makao Makuu ya Jeshi hilo Jijini Dar es Salaam.

Mshauri Mwelekezi kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Prof. Beatus Kundy(aliyesimama) akiwasilisha rasimu ya Mpango wa Jeshi la Magereza wa kujitosheleza kwa chakula cha Wafungwa waliopo Magerezani. Jeshi la Magereza limeandaa rasimu hiyo ili kuipunguzia Serikali gharama za kuwalisha wafungwa waliopo magerezani.
Maafisa Waandamizi wa Jeshi la Magereza wakifuatilia kwa makini uwasilishaji wa Andiko hilo(wa kwanza kulia) ni Kamishna wa Huduma za Urekebishaji, Eng. Deonice Chamulesile(wa pili kulia) ni Kamishna wa Sheria na Uendeshaji wa Magereza, Dkt. Juma Malewa(wa pili kushoto) ni Kamishna wa Fedha na Utawala wa Magereza, Gaston Sanga.
Mwakilishi kutoka Wizara ya Kilimo, Chakula na Ushirika, Bw. Hashim Kimmwe akitoa mchango wake wakati wa kujadili rasimu ya Mpango wa Jeshi la Magereza wa kujitosheleza kwa chakula cha Wafungwa waliopo Magerezani.
Wataalam wa Jeshi la Magereza walioshiriki kikamilifu katika maandalizi ya Andiko la Mpango wa Jeshi la Magereza kujitosheleza kwa chakula kwa kushirikiana na Mshauri Mwelekezi kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam wakifuatilia majadiliano ya rasimu hiyo.

(Picha zote na Lucas Mboje wa Jeshi la Magereza).