Thursday, December 24, 2015

Mwili wa afisa wa gereza kuu Ukonga waagwa leo Ukonga jijini, Dar es Salaam

Maafisa wa Jeshi la Mageereza wameubeba mwili wa Marehemu Mkaguzi wa Magereza, Morice Peter wakiuingiza nyumbani kwake kabla ya kutoa heshima za mwisho leo Desemba 24, 2015 katika Viwanja vya Gereza Kuu Ukonga Jijini Dar es Salaam.
Mke wa Marehemu Mkaguzi wa Magereza, Morice Peter(vazi jeupe) akiwa kwenye majonzi makubwa wakati wa kuaga mwili wa mwenzi wake. Marehemu ameagwa leo katika Viwanja vya Gereza Kuu Ukonga Jijini Dar es Salaam kabla ya kusafirishwa kwa mazishi nyumbani kwao Mkoani Morogoro.
Mkaguzi wa Magereza, Seleman Sued wa Gereza Kuu Ukonga, Jijini Dar es Salaam akisoma Wasifu wa Mkaguzi wa Magereza Morice Peter aliyefariki juzi Desemba, 2015 katika Hospitali ya Dar Group, Jijini Dar es Salaam.
Baadhi ya Maofisa wa Jeshi la Magereza waliohudhuria katika hafla ya kuaga mwili wa Marehemu Mkaguzi wa Magereza, Morice Peter.
Mke wa Marehemu Mkaguzi wa Magereza, Dorice Peter(kulia) akipewa msaada ndugu wa karibu wakati wa kusindikiza mwili kuelekea kwenye gari tayari kwa safari ya kuelekea Mkoani Morogoro kwenye mazishi.
Ndugu na jamaa waliojitokeza kuuaga mwili wa Marehemu Mkaguzi wa Jeshi la Magereza, Morice Peter aliyekuwa akihudumu katika Gereza Kuu Ukonga, Jijini Dar es Salaam. Mkaguzi Morice Peter amefariki juzi Desemba 22, 2015 baada ya kuugua muda mrefu katika Hospitali ya Dar Group Jijini Dar es salaam

(Picha na Lucas Mboje wa Jeshi la Magereza).