Monday, December 19, 2016

JESHI LA MAGEREZA NA WAKALA WA MAJENGO - TBA WAINGIA MAKUBALIANO UJENZI WA NYUMBA 320 ZA ASKARI MAGEREZA MKOA WA DAR ES SALAAM

Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Majengo – TBA, Arch. Elius Mwakalinga akimkabidhi Mkataba wa Makubaliano ya mradi wa ujenzi wa nyumba 320 Kaimu Kamishna Jenerali wa Magereza, Dkt. Juma Malewa. Hafla hiyo ya uwekaji saini makubaliano hayo ya ujenzi wa nyumba za askari wa Jeshi la Magereza Mkoani Dar es Salaam imefanyika leo Desemba 19, 2016 Jijini, Dar es Salaam katika Ukumbi wa TBA. Ujenzi wa nyumba hizo ni agizo la Rais Magufuli kufuatia ziara yake hivi karibuni ambapo alitoa kiasi cha bilioni 10 kwa ajili ya ujenzi wa nyumba za makazi ya askari wa Jeshi hilo.
Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Majengo – TBA, Arch. Elius Mwakalinga (kushoto) na Kaimu Kamishna Jenerali wa Magereza, Dkt. Juma Malewa(kulia) kwa pamoja wakisaini Mkataba wa Makubaliano ya ujenzi wa nyumba 320 za Askari wa Jeshi la Magereza Mkoa wa Dar es Salaam katika Ukumbi wa Mikutano wa TBA, leo Desemba 19, 2016 Jijini, Dar es Salaam.
Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Majengo – TBA, Arch. Elius Mwakalinga na Kaimu Kamishna Jenerali wa Magereza, Dkt. Juma Malewa(kulia) wakionesha nyaraka mbalimbali baada ya hafla fupi ya uwekaji saini wa Mkataba wa Makubaliano ya mradi wa ujenzi wa nyumba 320 za askari wa Jeshi la Magereza Mkoani Dar es Salaam.
Maafisa Waandamizi wa Wakala wa Majengo - TBA wakifuatilia majadiliano kabla ya uwekaji saini wa Mkataba wa Makubaliano ya ujenzi wa nyumba 320 za Askari wa Jeshi la Magereza Mkoa wa Dar es Salaam katika Ukumbi wa Mikutano wa TBA, leo 19 Desemba, 2016 Jijini Dar es Salaam.
Kamishna wa Fedha na Utawala wa Jeshi la Magereza, Gaston Sanga(wa kwanza kushoto) akiwa pamoja na Maafisa Waandamizi wa Jeshi la Magereza wakishuhudia uwekaji saini wa Makubaliano ya ujenzi wa nyumba 320 za Askari wa Jeshi la Magereza Mkoa wa Dar es Salaam katika Ukumbi wa Mikutano wa TBA, leo 19 Desemba, 2016 Jijini Dar es Salaam.

(Picha zote na Lucas Mboje wa Jeshi la Magereza)