Friday, December 2, 2016

ZIARA YA RAIS MAGUFULI MAGEREZA MKOA WA DAR ES SALAAM

Amiri Jeshi Mkuu Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt John Pombe Joseph Magufuli akiweka saini kitabu cha wageni akiwa na  Kamishna Jenerali wa Magereza John Casmir Minja kabla ya kuongea na Maafisa na askari wa Jeshi la Magereza Mkoa wa Dar es Salaam alipofanya ziara ya kustukiza katika Jiji la Dar es Salaam Novemba 29, 2016.
Kamishna Jenerali Magereza, John Casmir Minja(Kushoto) akiteta jambo na Amiri Jeshi Mkuu Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt John Pombe Joseph Magufuli katika Bwalo Kuu la Maafisa Magereza Ukonga kabla ya kuongea na Maafisa na askari wa Jeshi la Magereza Mkoani Dar es Salaam alipofanya ziara ya kustukiza katika Jiji la Dar es Salaam Novemba 29, 2016.
Amiri Jeshi Mkuu Rais Dkt John Pombe Joseph Magufuli akiongea na baadhi ya Maafisa na askari wa Jeshi la Magereza Mkoani Dar es Salaam alipofanya ziara ya kustukiza katika Jiji la Dar es salaam Novemba 29, 2016.
Kamishna Jenerali wa Magereza John Casmir Minja akimkaribisha Amiri Jeshi Mkuu Rais Dkt John Pombe Joseph Magufuli ili aongee  na Maafisa na askari wa Jeshi la Magereza alipofanya ziara ya kustukiza Jijini Dar es salaam Novemba 29, 2016
Amiri Jeshi Mkuu Rais Dkt John Pombe Joseph Magufuli akichukua maelezo kutoka kwa  Maafisa na askari wa Jeshi la Magereza alipofanya ziara ya kustukiza Jijini Dar es Salaam Novemba 29, 2016.
Baadhi ya Maafisa na askari wa Jeshi la Magereza wakimsikiliza Amiri Jeshi Mkuu Rais Dkt. John Pombe Magufuli alipofanya ziara ya kustukiza jijini Dar es salaam  Novemba 29, 2016.
Amiri Jeshi Mkuu Rais Dkt John Pombe Joseph Magufuli akiwa katika picha ya pamoja na Maafisa Waandamizi wa Jeshi la Magereza alipofanya ziara ya kustukiza Jijini Dar es salaam  Novemba 29, 2016.

(Picha zote na Lucas Mboje wa Jeshi la Magereza)